Tukumbuke majina ya utani kwa walimu shule tulikotoka

Tukumbuke majina ya utani kwa walimu shule tulikotoka

Mwalimu Mamba, Tabora boys alikuwa akifundisha history. Domo kubwa akilifumba na kufunua 'mmwaaaa' akisema, 'yes, that is thaaat'
 
Mwalimu Ruba Mara Sec... alikuwa akifundisha Kiswahili. Mfupi na mkorofi au akiigiza kutojua kiingereza vizuri, kandambili anaziita two zones, kuruka kichura akiita jump frog frog. Kila mara utamsikia, 'ntakuganda kama ruba.'
 
Kuna bwana wa kuitwa singo muvabo puli au bwana savimbi Taqwa pale mwanza alikuwa ana ndevu kama savimbi hatumii fimbo,anaweza kutia makonzi darasa zima!
 
Mkwele alikua mkuu islamiya sec school mwz akiitwa hivo kutokana na kumfanana sana mkwele wa mizengwe kwa kila kitu
 
Mwalimu Kijo

Mzee wa kununa darasani
Ukicheka tu anakutoa kwenye kipindi...

Mzee yule sijui bado yupo hai!
 
Mwl therefore alinifundisha mhangu primary school aliitwa hivo kutokana na kulitajataja sana neno hilo akitufundisha kiinglish
 
MBIA: mwalimu wa English tulimpa jina kutoka katika kitabu cha three sweeters one husband alikua anakipenda sana hiki kitabu
 
Nakumbuka baadhi ya majina ya walimu waliyopewa na wanafunzi kama ifuatavyo:

1. Solar system - mwalimu wa geograph form 1 au 2 alifundisha solar system akapatiwa jina hapohapo

2. Bambabay - mwalimu wa commerce form 3 alikua akielezea transport system,akaitaja bambabay ndio ikawa jina lake.

3.magazijuto - mwalimu wa hisabati darasa la saba alifundisha magazijuto na yeye ndio ikawa jina lake la utani au aka

4. Chonya of chilimwa - mwalimu wa kiswahili secondary alisoma habari za chonya of chilomwa akawa ndio jina lake

tupeni majina zaidi

Magma - mwalimu wa Kidachi nguli wa hesabu aliyesemekana alikuwa rubani vita vya 2 vya dunia kabla ya kuwa buruda.

Mwingine - "Babu Jeff" mwalimu wa Useremala, raia wa Ushelisheli
 
Intellectuals
Alikuwa hawezi kusema na mwanafunzi/wanafunzi bila kuwasisitiza kuwa wao ni intellectuals.

Tulimbatiza Anko B.
Kama ilivyo kwa mkulu Anko M.

Kwasasa ni mkuu wa wilaya SIHA.
 
basuba-mwalimu wa english tulimfuma kona anacheza wimbo mmoja hivi wa kikongo uliokuwa na kikorombwezo basubaaaa
Huu wimbo, ulikua na neno kama 'chukuru-chukuru-chu' halafu wanaitikia 'baasuba' unasikia tena 'okaye' basuba

Sijui muimbaji ni nani.
 
Kuna ticha tulikuwa tunafundisha naye shule x alikuwa wa history, sasa yeye alikuwa anafundisha topic ya African resistance kidato cha tatu,kwenye kipengere cha Nama and Herero resistance,basi watoto wakawa wanamwita Mwalimu Herero,nikiwa mgeni shuleni pale nikiwa na three months ,sijui hili wala lile ,na huyo ticha alikuwa mshikaji wangu sana,basi akaja mwanafunzi tukiwa na walimu wengine anataka kuchukua chaki ,basi akaulizwa na moja ya walimu nani kakuagiza chaki ,mtoto akijibu mwl Herero,duh likawa jina geni kwa walimu,bahati mbaya hata mtoto mwenyewe alikuwa hajui jina sahihi la mwalimu,akabidi amuelezee kwa phiscal appearance ndo tukamuelewa,staff mzima ilibaki kucheka tu



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna ticha tulikuwa tunafundisha naye shule x alikuwa wa history, sasa yeye alikuwa anafundisha topic ya African resistance kidato cha tatu,kwenye kipengere cha Nama and Herero resistance,basi watoto wakawa wanamwita Mwalimu Herero,nikiwa mgeni shuleni pale nikiwa na three months ,sijui hili wala lile ,na huyo ticha alikuwa mshikaji wangu sana,basi akaja mwanafunzi tukiwa na walimu wengine anataka kuchukua chaki ,basi akaulizwa na moja ya walimu nani kakuagiza chaki ,mtoto akijibu mwl Herero,duh likawa jina geni kwa walimu,bahati mbaya hata mtoto mwenyewe alikuwa hajui jina sahihi la mwalimu,akabidi amuelezee kwa phiscal appearance ndo tukamuelewa,staff mzima ilibaki kucheka tu



Sent using Jamii Forums mobile app
Umefika hadi sekondari unaandika hovyo mamna hii. Habari nzima hamna nukta umejaza mikato tuu.
Halafu ni kipengele sio Kipengere.
Ni physical sio Phiscal.
Umechezea ada ya baba yako.
 
Back
Top Bottom