Tukumbuke Zamani: Historia ya Taifa letu katika picha

Tukumbuke Zamani: Historia ya Taifa letu katika picha

Mkuu Jasusi,

Heshima mbele sana, nimewahi kuongea na mkulu mmoja aliyehudhuruia hicho kikako OAU, kule Adis ambako Nkurumah alikuwa amepania sana kuanzisha huo muungano wa Afrika na jinsi alivyokuwa akumuona Mwalimu kama ni tatizo katika hiyo ndoto yake ya kuwa rais wa kwanza wa huo muungano,

Nkurumah alifanya mambo mengi ya aibu sana kwenye hicho kikao, akijaribu kummshusha hadi Mwalimu, lakini Mwalimu hakuonyesha kuwa na wasi wasi naye wala kugombea hiyo power kama Nkurumah alivyofikiri, mkulu aliniambia kuwa katika hiyo kiu ya power Nkurumah alisafiri sana kuonana na Wareno, watawala wa Then Mozambique, katika kutafuta njia za kuiua EAA,

Anyways, ninakushukuru sana mkuu kwa kuweka habari hii sawa, kwa kweli tunakula elimu nzito sana hapa.

Hilo la Nkurumah kupinga alichokiita "Balkanization of Africa" na kutaka Africa nzima iungane kuunda United States of Africa ni la kweli na limekuwa documented sawasawa, na Nyerere aliwahi kuliongelea mara nyingi sana katika hotuba zake. Vile vile ile tamaa yake ya kutaka kuwa George Washington wa United States of Africa linajulikana sana ingawa hilo halikuwa documented nadhani ili kumtunzia heshima. Nilikuwa sifahamu kuwa ndiye alikwamisha juhudi za Nyerere za kuchelewesha uhuru wa Tanganyika kuwasubiri ndugu zetu wa Kenya na Uganda kusdi tuunde Shirikisho la Afrika ya Mashariki, na nawashukuru sana FMES na Jasusi kwa kulileta. Nilichopinga hapo nyuma ni hii EAC ambayo iliundwa mwaka 1967 baada ya yeye kuwa alishafukuzwa huko kwao.


Hata mimi nimewahi kusimuliwa kuwa wakati wa mkutano wa kuundwa kwa OAU mwaka 1963 kule Ethiopia, baadaye Nkrumah alimwomba Nyerere samahani baada ya kugundua kuwa katika mkutano ule , Nyerere aliokena kuwa more intellectual na alionekana kusikilizwa zaidi na viongozi wengine wengi hasa Mfalme Haile Selassie, ambaye alikuwa anaheshimiwa na viongozi wote wakati huo, na Gamal Abdul Nasser.


Charter ya OAU iliyosainiwa na viongozi hao siku hiyo ni hii hapa, kwa wale ambao walikuwa hawajaiona:
 

Attachments

akhwari1.gif
John Steven Akhwari akimaliza mbio za marathon katika olimpiki ya mwaka 1968 Mexico City, saa moja baada ya washiriki wote kumaliza mbio hizo.

John anakumbukwa dunia nzima kwa kauli yake hii
"My country did not send me 7000 miles away to start the race. They sent me 7000 miles to finish it."
 
View attachment 2149

...Enzi hizo za vita vya kagera tulijifwaudu kule mbarara, masaka, entebbe na 'kujipongeza' kwa kuchukua hizo Mig-21 za nduli, joka kuu Idi Amin dada, Big Dadi, aka the last king of scotland!...

...The Tanzanian Army captured seven MiG-21MFs and one MiG-21U trainer from the Ugandan Air Force, as well as a considerable amount of spare parts. All of these were flown out to Mwanza AB, to enter service with the TPDF/AW...

....Sssshhhhh....
(The TPDF/AW MiG-21MFs are now confirmed to have carried serials - in black or green - underneath the cockpit, but no details about these are known)...
...siri-kali!
 
Hiyo picha ya Yanga ilipigwa mwanzoni mwa mwaka 1974 Yanga ilipokwenda Brazili na Simba kwenda Poland na ziliporudi zikaenda moja kwa moja Mwanza kushiriki michuano ya klabu bingwa ya Tanzania ambapo zilifanikiwa kufika fainal kwenye uwanja wa Nyamagana na Yanga kuilaza Simba 2-1 wafungaji wakiwa Sunday Manara na marehemu Gibson Sembuli.
Katika kikosi hicho cha Yanga kilichokwenda Brazil Tenga alikuwa hajajiunga na Yanga kwa sababu yeye alijiunga mwaka 1974 mwishoni akiwa pamoja na Muhaji Mukhi, Juma Matokeo, Patrick Nyaga, Juma Shabaan na Jellah Mtagwa wote wakitokea Morogoro baada ya michuano ya Taifa Cup ya mwaka huo.
Pia Sunday Manara alikwenda Austria mwanzoni mwa mwaka 1976.

Timu ya Yanga ilicheza na timu ya Enugu Rangers International mwezi May mwaka 1975 ukiwa ni mchezo wa pili wa raundi ya pili wa kombe la klabu bingwa Afrika baada ya kutoka sare ya 1-1 wiki mbili kabla huko Nigeria. Yanga ilitakiwa kutoa draw tu ya kutofungana isonge mbele lakini dakika za mwanzo tu za kipindi cha kwanza wakapigwa kimoja kilichokaa hadi mwisho wa mchezo na kuacha umati mkubwa wa watanzania ukibubujikwa na machozi. naunga mkono mchangiaji mmoja kuwa huu ulikuwa miongoni mwa michezo ya kusisimua sana iliyopatwa kuchezwa Uwanja wa taifa.

naomba kuwakilisha.

Wazee wa michezo,
Nasikia kuna mchezaji mmoja wa Simba alichelewa ndege na hivyo kusafiri peke yake kwenda Poland. Kufika pale akasema ameifuata timu yake. Timu ipi? Akasema "Lions Sports Club", wakamwambia "hamna timu kama hiyo iliyokuja kutoka Tanzania". Ndege iliyofuata wakamrudisha. Je hii story ni kweli au ndiyo zile story za miaka hiyo nikiwa Secondary?
Pia juu ya Enugu Rangers, nasikia Emanuel Okala alikuja kuwa kocha wa timu hiyo. Nakumbuka leo kumsikia redioni kuwa "anadaka mpira na kuurudisha kwa forward......... na jamaa akapiga shuti, Okala akaudaka tena." Miaka kadhaa baadaye wakaja wale ndugu Wazambia, sijui Dickson Nkwasa???
Enugu Rengers :- http://en.wikipedia.org/wiki/Enugu_Rangers
 
Hiyo picha ya Yanga ilipigwa mwanzoni mwa mwaka 1974 Yanga ilipokwenda Brazili na Simba kwenda Poland na ziliporudi zikaenda moja kwa moja Mwanza kushiriki michuano ya klabu bingwa ya Tanzania ambapo zilifanikiwa kufika fainal kwenye uwanja wa Nyamagana na Yanga kuilaza Simba 2-1 wafungaji wakiwa Sunday Manara na marehemu Gibson Sembuli.

Katika kikosi hicho cha Yanga kilichokwenda Brazil Tenga alikuwa hajajiunga na Yanga kwa sababu yeye alijiunga mwaka 1974 mwishoni akiwa pamoja na Muhaji Mukhi, Juma Matokeo, Patrick Nyaga, Juma Shabaan na Jellah Mtagwa wote wakitokea Morogoro baada ya michuano ya Taifa Cup ya mwaka huo. Pia Sunday Manara alikwenda Austria mwanzoni mwa mwaka 1976.

Timu ya Yanga ilicheza na timu ya Enugu Rangers International mwezi May mwaka 1975 ukiwa ni mchezo wa pili wa raundi ya pili wa kombe la klabu bingwa Afrika baada ya kutoka sare ya 1-1 wiki mbili kabla huko Nigeria. Yanga ilitakiwa kutoa draw tu ya kutofungana isonge mbele lakini dakika za mwanzo tu za kipindi cha kwanza wakapigwa kimoja kilichokaa hadi mwisho wa mchezo na kuacha umati mkubwa wa watanzania ukibubujikwa na machozi. naunga mkono mchangiaji mmoja kuwa huu ulikuwa miongoni mwa michezo ya kusisimua sana iliyopatwa kuchezwa Uwanja wa taifa.

1. Kama ninakumbuka vizuri ni kwamba Yanga ilichukua wachezaji wawili toka Mlimani, nao ni Leodgar Tenga, na Edward Hizza, wote walikuwa benchi kwa sababu Tenga, alikuwa akimsaidia Hassan Gobbos, Hizza hakuweza hata kucheza mechi kubwa,

However, Yanga wakiwa wanajitayarisha kwa safari ya Brazil, Tenga na Hizza, waliitwa kwenye timu ya Mlimani, ili kuiwakilisha kwenye michezo ya Vyuo Vikuu iliyokuwa inafanyika Mexico, hivyo wote wawili wakashindwa kwenda Brazil na Yanga,

2. kwa sababu ninakumbuka vizuri sana kwamba baada tu ya mechi ya Nyamagana, ambapo Sunday na Sembuli waliifunga Simba, timu hizi ziilirudiana tena kwenye Uwanja Wa Tartan wa Zanzibar, kwenye finali ya Kombe la Ubingwa wa East and Central Afrika, ambako kwa mara nyingine tena Yanga waliishinda Simba kwa magoli mawili kwa moja, yaliyofungwa na wale wale Sunday Manara na Sembuli na this time Tenga alikuwemo ndani ya ile mechi upande wa Yanga, mechi mabayo kwa mara ya kwanza katika historia ya michezo bongo ilichezwa usiku.

Kipindi kati ya cha mechi ya Nyamagana na Zanzibar, kilikuwa ni kifupi sana kwamba Tenga ndio alijiunga na kuweza kucheza mechi kubwa namna ile, lakini I colud be wrong pia.

3. Wachezaji waliojiunga na Yanga kutokea Morogoro, baada ya kombe la Taifa, kwenye ngwe ya kwanza alikuwa ni Sembuli peke yake,

Ngwe iliyofuatia walikuwa ni kipa Patric Nyaga, Juma shaabani, Jella Mtagwa, na Juma Matokeo, Muhaji Mukhi, naamini alitokea timu ya mkoa wa Kigoma kama Makumbi Juma.

Ngwe ya mwisho ya wachezaji wa Morogoro kuingia Yanga, ilimalizwa na Ahmed Jongo na Omar Hussein. Otherwise, wakuu heshima mbele kwa historia na marekebisho, nia na madhumuni ni kuelimishana.
 
baadaye wakaja wale ndugu Wazambia, sijui Dickson Nkwasa???

1. Walikuja wa-Zambia, wawili ambao wote walikuwa kwenye timu yao ya taifa nao ni Dick Chama (Greeen Buffaloes), na Dick Makwaza (Kabwe Worriors).

2. Timu zote hizo zilitolewa na Simba, kwenye ubingwa wa Afrika in fact mwaka Simba walipowatoa Buffaloes, waliweza kwenda mpaka Nusu Finali kwa mara ya kwanza na kutolewa na wale wahuni wa Mehala-El Kubra, kutoka Egypt, ambao waliwafanyia vitimbi vingi sana vya kihuni kwenye hiyo mechi.
 
1. Kama ninakumbuka vizuri ni kwamba Yanga ilichukua wachezaji wawili toka Mlimani, nao ni Leodgar Tenga, na Edward Hizza, wote walikuwa benchi kwa sababu Tenga, alikuwa akimsaidia Hassan Gobbos, Hizza hakuweza hata kucheza mechi kubwa,

However, Yanga wakiwa wanajitayarisha kwa safari ya Brazil, Tenga na Hizza, waliitwa kwenye timu ya Mlimani, ili kuiwakilisha kwenye michezo ya Vyuo Vikuu iliyokuwa inafanyika Mexico, hivyo wote wawili wakashindwa kwenda Brazil na Yanga,


2. kwa sababu ninakumbuka vizuri sana kwamba baada tu ya mechi ya Nyamagana, ambapo Sunday na Sembuli waliifunga Simba, timu hizi ziilirudiana tena kwenye Uwanja Wa Tartan wa Zanzibar, kwenye finali ya Kombe la Ubingwa wa East and Central Afrika, ambako kwa mara nyingine tena Yanga waliishinda Simba kwa magoli mawili kwa moja, yaliyofungwa na wale wale Sunday Manara na Sembuli na this time Tenga alikuwemo ndani ya ile mechi upande wa Yanga, mechi mabayo kwa mara ya kwanza katika historia ya michezo bongo ilichezwa usiku.

Kipindi kati ya cha mechi ya Nyamagana na Zanzibar, kilikuwa ni kifupi sana kwamba Tenga ndio alijiunga na kuweza kucheza mechi kubwa namna ile, lakini I colud be wrong pia.

3. Wachezaji waliojiunga na Yanga kutokea Morogoro, baada ya kombe la Taifa, kwenye ngwe ya kwanza alikuwa ni Sembuli peke yake,

Ngwe iliyofuatia walikuwa ni kipa Patric Nyaga, Juma shaabani, Jella Mtagwa, na Juma Matokeo, Muhaji Mukhi, naamini alitokea timu ya mkoa wa Kigoma kama Makumbi Juma.

Ngwe ya mwisho ya wachezaji wa Morogoro kuingia Yanga, ilimalizwa na Ahmed Jongo na Omar Hussein. Otherwise, wakuu heshima mbele kwa historia na marekebisho, nia na madhumuni ni kuelimishana.

Ndiyo Mkuu, kumbukumbu yanko ni sahihi kabisa, umenikumbusha hilo. Wakati huo Tenga alikuwa akijulikana pia kama "msomi."
 
FMES,

..umesahau timu ya Mufulira Wonderers ambao waliwafunga simba 40--0 nationala stadium.

..mechi ya marudiano Simba waliwachabanga Mufulira bao 5 -- 0 !!

..nadhani baada ya mechi hiyo walicheza na Rakka Rovers ya Nigeria. Simba ilimpata msiba wa mchezaji wake Hussein Tindwa kufariki uwanjani.

..Prof.James Shaba alipochunguza mwili wa Hussein Tindwa aligundua kwamba moyo wake ulikuwa na matatizo. Prof alidai ilikuwa ni kitu cha ajabu sana kwa Hussein Tindwa kushiriki michezo ukizingatia hali ya moyo wake.

..Hussein Tindwa alikuwa akicheza beki namba tano.

..Wachezaji wa Zambia ninaowakumbuka mimi, walikuja na timu mbalimbali ni kama ifuatavyo: Pele Kaimana, Jani Simulambo, Blackwell Chalwe, Jones Chilengi, Peter Kaumba[namba saba hatari], Alex Chola "mosquito" [namba 11 hatari], Chabala [ he was a golie].

..Halafu kulikuwa na Vita FC ya Zaire ambao walicheza na Simba na baadaye Pan African.

..Pan African kutokana na ufadhili wa Shiraz Sharrif na Sammy Mdee waliamua kuchezea mechi zao za kombe la washindi uwanja wa Sheikh Amri Abeid Arusha.

..Vita ilikuwa na wachezaji hatari kama Mayanga Maku, Lofombo [namba 9 aliyependelea kunyoa kipara], Lobilo [namba 5 anayejiamini kupita kiasi], Mbuya Mpaka [golikipa].

..Halafu walikuja Harambee Stars ambao walianza kama vijana. Hawa walifungwa 3 -- 1 na Taifa Stars lakini walipopata uzoefu walikuja kutesa sana Afrika Mashariki na Kati.

..Harambee Stars ninayoikumbuka mimi ni hii hapa: 1.Mahamoud Abbas "Kenya One" 2. Mike Weche 3. Peter Otieno "Basanga" 4. John Bobby Ogolla "simba" 5.Josephat Mulira "controler" 6.Hussein Heri 7.Francis Kadenge 8.Wilberforce Mulamba 9.Joe Masiga "Dr.JJ -- he was a dental surgeon by proffesion" 10.??? 11.Sammy Onyango "jogoo"

Sikonge,

..goalkeeper aliyeacha historia kuliko wote ni Robert Mensah wa Ghana.

..Mensah ndiyo alidaka mpira kwa maajabu katikati ya miguu yake, kama mtu aliyetaka kupitishwa tobo, baada ya kubaki yeye na Dilunga. hili mimi nimehadithiwa sikuliona.

..Juma Pondamali ameiga vituko na style ya udakaji wa Robert Mensah.

..Pondamali alikuwa anavuta watu wakamwangalia yeye badala ya kufuatilia mechi inakwenda vipi.

..hata nje ya Tanzania, washabiki wa Zambia na Nigeria, wanamsifia na kumtaja kama mmoja wa magolikipa wenye kipaji.

..now, Pondamali aliwahi kufanya kituko cha kudaka mpira na 'kumrudishia' mshambuliaji Mustafa Naggar wa Sudan. lakini siyo kama alimrudishia bali alifanya kama kumbabua na mpira ukamrudia yeye Pondamali. Mustafa Naggar naye hakutegemea kama Pondamali angafanya kitu kama hicho.

..Pondamali aliponzwa na uzalendo alipokataa offer ya kwenda UAE, yeye na Mohamed Salim, kucheza mpira wa kulipwa. leo hii nadhani Mohamed Salim ana maisha yake mazuri tu tofauti na Juma Pondamali "Mensah."

..Mahamoud Abbas wa Kenya alikuja kuiga udakaji na mbwembwe za Juma Pondamali!!
 
..Hussein Tindwa alikuwa akicheza beki namba tano.

List ya Simba wakati huo ilikuwa,

1. Omar Mahadhi/Idd Pazi "Father"
2. Shabaan Baraza.
3. Mohamed Kajole "Machela"
4. Aloo Mwitu/Athumani Juma.
5. Omar Choggo "Choggo Chemba"
6. Khalid Abeid.
7. Abbas Dilunga.
8. Haidari Abeid "Muchacho"
9. Adam Sabu.
10. Abdallah Kibadeni "King"
11. Hussein Tindwa.
 
FMES,

..Hussein Tindwa hakuwa mshambuliaji.

..nadhani Hussein Tindwa ndiye mrithi wa Omar Chogo.

..halafu Mohamed Bakari "Tall" alikuja kumrithi Tindwa[r.i.p].

..Baada ya Omar Mahadhi alifuata Athumani Mambosasa.

..sina uhakika kama Moses Mkandawile alicheza kabla au baada ya Iddi Pazi.

..nina uhakika Iddi Pazi hakucheza na Mohamed Kajole. Pazi amecheza miaka ya kina Raphael Paul, Mussa Kiwelu, na Lila Shomari.

..Halafu Willy Mwaijibe,Abdalah Mwinyimkuu, na Ezekiel Greyson "juju man," walicheza miaka ipi?
 
FMES,

..Hussein Tindwa hakuwa mshambuliaji.

..nadhani Hussein Tindwa ndiye mrithi wa Omar Chogo.

..halafu Mohamed Bakari "Tall" alikuja kumrithi Tindwa[r.i.p].

..Baada ya Omar Mahadhi alifuata Athumani Mambosasa.

..sina uhakika kama Moses Mkandawile alicheza kabla au baada ya Iddi Pazi.


..nina uhakika Iddi Pazi hakucheza na Mohamed Kajole. Pazi amecheza miaka ya kina Raphael Paul, Mussa Kiwelu, na Lila Shomari.

..Halafu Willy Mwaijibe,Abdalah Mwinyimkuu, na Ezekiel Greyson "juju man," walicheza miaka ipi?


Katika historia ya Simba, ninadhani kuwa Iddi Pazi ni wa juzi tu. Mwanzoni mwa miaka ya sabini alikuwapo mambosasa aliyedumu takriban miaka minne hivi halafu nafasi yake ikachukuliwa na Mahadhi akitokea Tanga, ambaye aliendelea hadi mwishoni mwa miaka ya sabini akifuatiwa na Mkandawile mwanzoni mwa miaka themanini ndipo akaja Pazi katikati ya miaka ya themanini.


Nilisoma na Ezekiel Greyson Primary School: alichezea Simba mwishoni mwa miaka ya sabini hadi mwanzoni mwa miaka ya themanini. Kwa mfano mwaka 1983, timu ya Simba ilikuwa na wachezaji wafuatao: Moses Mkandawile, Thobias Nkoma, Shabani Mussa, Lilla Shomari, Ezekiel Greyson "Jujuman", Ibrahim Malekano (alisoma Kazima Sec. wakati nikiwa Tabora Boys' Sec.), Nico Njohole, Zamoyoni Mogela, Malota Soma, Abdalah Mwinyimkuu, na Sunday Juma.
 
... kwenye list ya wana msimbazi nawakumbukia hawa, ila sijui kama kuna wengine nimewachanganya (?), ...siisahau siku ile Bernard madale alipokwenda wavuni mara sita kuokota mipira😀!!!

1.Omar Mahadhi Bin Jabbir/Athuman Mambosasa
2.Daud Salum "Bruce Lee"
3.Mohammed Kajole Machela
4.Athuman Juma
5.Mohammed Bakari Tall
6.Willy Mwaijibe/Ezekiel Greyson "Juju Man"
7.Nico Demus Njohole
8.George "Best" Kulagwa
9.Thuwein Ally
10.Abdalla King Kibaden
11.Adam Sabu/Abdallah Mwinyimkuu

hawa nao vipi, mnakumbuka "Peter Tino anatupeleka Lagos!" ...sijui alikuwa Dominic Chilambo yule, au Mikidadi Mahmoud RTD enzi hizoooo!!!...


View attachment 2157

...kikosi kilichokuwa na kina Zamoyoni mogella, Ahmad Amasha, Charles Boniface Mkwasa, Athuman Chama, etc chini ya kocha Rudi Gutendorf, au huyu mzungu ndiye yule muingereza aliyeliboronga?
 
1. Kama ninakumbuka vizuri ni kwamba Yanga ilichukua wachezaji wawili toka Mlimani, nao ni Leodgar Tenga, na Edward Hizza, wote walikuwa benchi kwa sababu Tenga, alikuwa akimsaidia Hassan Gobbos, Hizza hakuweza hata kucheza mechi kubwa,

However, Yanga wakiwa wanajitayarisha kwa safari ya Brazil, Tenga na Hizza, waliitwa kwenye timu ya Mlimani, ili kuiwakilisha kwenye michezo ya Vyuo Vikuu iliyokuwa inafanyika Mexico, hivyo wote wawili wakashindwa kwenda Brazil na Yanga,

2. kwa sababu ninakumbuka vizuri sana kwamba baada tu ya mechi ya Nyamagana, ambapo Sunday na Sembuli waliifunga Simba, timu hizi ziilirudiana tena kwenye Uwanja Wa Tartan wa Zanzibar, kwenye finali ya Kombe la Ubingwa wa East and Central Afrika, ambako kwa mara nyingine tena Yanga waliishinda Simba kwa magoli mawili kwa moja, yaliyofungwa na wale wale Sunday Manara na Sembuli na this time Tenga alikuwemo ndani ya ile mechi upande wa Yanga, mechi mabayo kwa mara ya kwanza katika historia ya michezo bongo ilichezwa usiku.

Kipindi kati ya cha mechi ya Nyamagana na Zanzibar, kilikuwa ni kifupi sana kwamba Tenga ndio alijiunga na kuweza kucheza mechi kubwa namna ile, lakini I colud be wrong pia.

3. Wachezaji waliojiunga na Yanga kutokea Morogoro, baada ya kombe la Taifa, kwenye ngwe ya kwanza alikuwa ni Sembuli peke yake,

Ngwe iliyofuatia walikuwa ni kipa Patric Nyaga, Juma shaabani, Jella Mtagwa, na Juma Matokeo, Muhaji Mukhi, naamini alitokea timu ya mkoa wa Kigoma kama Makumbi Juma.

Ngwe ya mwisho ya wachezaji wa Morogoro kuingia Yanga, ilimalizwa na Ahmed Jongo na Omar Hussein. Otherwise, wakuu heshima mbele kwa historia na marekebisho, nia na madhumuni ni kuelimishana.

FMES,

I was there in Nyamagana, a kid enjoying my first Yanga na Simba match and that is the day I wore Kandambili forever!

Kama yule jamaa wa nyumbani, ukikata mwili, ni kandambili tupu, CCM wametuibia rangi!
 
Katika historia ya Simba, ninadhani kuwa Iddi Pazi ni wa juzi tu. Mwanzoni mwa miaka ya sabini alikuwapo mambosasa aliyedumu takriban miaka minne hivi halafu nafasi yake ikachukuliwa na Mahadhi akitokea Tanga, ambaye aliendelea hadi mwishoni mwa miaka ya sabini akifuatiwa na Mkandawile mwanzoni mwa miaka themanini ndipo akaja Pazi katikati ya miaka ya themanini.


Nilisoma na Ezekiel Greyson Primary School: alichezea Simba mwishoni mwa miaka ya sabini hadi mwanzoni mwa miaka ya themanini. Kwa mfano mwaka 1983, timu ya Simba ilikuwa na wachezaji wafuatao: Moses Mkandawile, Thobias Nkoma, Shabani Mussa, Lilla Shomari, Ezekiel Greyson "Jujuman", Ibrahim Malekano (alisoma Kazima Sec. wakati nikiwa Tabora Boys' Sec.), Nico Njohole, Zamoyoni Mogela, Malota Soma, Abdalah Mwinyimkuu, na Sunday Juma.

Mwalimu,

Mambosasa na Mahadhi walipokezana hata baada ya Mahadhi kuanza kuachia ngazi.

Mkandawire na Pazi walipokezana pamoja na Nemes (Khadija Kopa).

Yanga nayokumbuka ni ile ya Bernard Madale, kisha akaja Dunia Adonis, kisha kuja nafikiri Hamisi Kinye. Kama sikosei, hata Steven Nemes alidakia Yanga kwa muda mfupi na alipomrithi Pazi, ndipo tulipoanza kumuita Khadija Kopa.

Pondamali alikuja mrithi Kinye, kisha akaja yule kipa kutoka Pamba, i am not sure kama alikuwa ni Lubigisa, but a cycle ya makipa wazuri walikuja Yanga huku Mwameja akishikilia usukani Simba kwa muda (possibly the longest Simba GK)

Je mwamkumbuka Paul Ssali wa KCC na Uganda Cranes?
 
Waliowengi na hasa Makuhani na Askari walioshiriki kumsurubisha YESU hawakuamini kama alikuwa mwana wa MUNGU mpaka pale alipokataa roho na giza likaifunika nchi mnamo mida ya saa sita mchana ndipo walipoamini kuwa alikuwa ndiye.

Nimefika Butiama kwa Mwalimu, kweli ndio utajua Jamaa hakuwa fisadi, utakachokiona ni cha kawaida tu ambacho yeyote anaweza kuwa nacho. Swali langu la kwanza niliuliza ile mizawadi (ng'ombe, magari na n.k.) aliyopewa wakati amestaafu iko wapi? Maana sikuiona pale. Majibu ni kwamba magari yote aliyopewa aliamuru zipewe idara za serikali na taasisi ambazo hazikuwa na magari. Kuhusu mifugo aliamua ipelekwe kwenye ranchi za taifa. Mmmmmmm kweli alikuwa msafi.

Je, tujiulize tukienda kwenye ranchi za taifa masalia ya mifugo aliyoipeleka Mwl bado ipo au mafisadi wamefisadi yote? viongozi wetu wa sasa wajifunze tabia aliyokuwa nayo Mwl ya kuridhika na kile walichonacho na kupenda kuwainua wanyonge. Itakufaa nini ukiupata ulimwengu wote? wakumbuke wanaofisadi wanaumri unaoanzia miaka 50 na kuendelea, ukiwapigia hesabu wamebakisha miaka mingapi ya kuishi labda walioowengi 10, 5, 2 maana wengi wana visukari na pressure. Sasa unaiba billioni uziweke wapi? unaendelea kujenga mahekalu nani aishi humo? Nawashauri bora wawasaidie wanyonge ili wawe na 'grounds' za kujitetea baada ya kufaa kwao ambako ni karibu sana.
 
..Halafu Willy Mwaijibe,Abdalah Mwinyimkuu, na Ezekiel Greyson "juju man," walicheza miaka ipi?

Mkuu uko sawa-

1. Willy Mwaijibe - alikuwepo Mwanza, lakini akielekea ukingoni kwa sababu hata Chitete alikuwepo Nyamgana lakini ndio waliokuwa wakielkea mwishoni mwa career zao.

Ni kweli Idd Pazi "Father" Alikuwa hajaingia hapa ananikumbusha mbali sana huyu mkulu, ambaye niliwahi kucheza naye mpira utotoni, na mpaka leo ni jirani yangu kule Kinyerezi, maana huyu alikuwa kile kitu kinaitwa multi-talented, originally alikuwa mshambuliaji akitumia mguu wa kushoto nilicheza naye timu moja ya mabaharia Jangwani (MS. Stella Maris) au Muungano Sports Club,

Baadaye nilicheza naye tena kwenye timu ya kiwanda cha nguo cha Sungura-Tex, ambako mara kwa mara tulikuwa tukipambana na Kurugenzi ya Kisarawe timu ya Ezekieli Greyson "Jujuman", kabla hajachukuliwa na Yanga, baadaye Simba. Nilipoamua seriously ku-stick na ubaharia, Idd Pazi na wachezaji wengine niliocheza nao pale kama Hamzuruni, na Makobe, wao walienda Nyota ya Mtwara, baadaye Idd alichukuliwa na Simba, Hamzuruni alichukuliwa na Yanga, Makobe naye alikuja Ummangani kwenye Meli.

Sasa hivi Idd ambaye ninawasiliana naye mara kwa mara, yupo Thailand ambako ni mfanya biashara mkubwa sana. wadogo zake Idd yaani Omar na Muhidini, nao pia waliwahi kuchezea Simba na Yanga, lakini hawakuwa na talent kama ya kaka yao Idd, the guy was just phenominal ninakumbuka kuna wakati wa mechi zetu za utotoni timu za adui zilikuwa zikimkataa kabisa kushiriki kwa sababu akiwa mdogo sana tayari alikuwa akichukuliwa kucheza timu za watu wazima, kwa hiyo maadui walidai kuwa asiruhusiwe kushiriki, off course sasa it sound like a joke, lakini I wish ungewepo uone how serious hii ishu ilikuwa.

2. Abdallah Mwinyimkuu "Carlos" na Ezekiel Greyson "Jujuman", hawa walikuwemo katika miaka ya kati kati ya 70s, kwa sababu nakumbuka sana ile mechi ya Simba na AS Vita ya Zaire, pale Uwanja wa Taifa, hawa wawili walikuwemo na kwenye lists ya zamani aliyekuwemo siku ile alikuwa ni Kibadeni,

Maana hizi zilikuwa enzi za kina Daudi Salum "Bruce Lee", unakumbuka Simba walikuwa na huyu mchezaji aliyetokea Tabora?
 
ninakumbuka,kama kuna wakati a clandestine radio,ilikuwa inaipinga serikali,sijui ilikuwa inaitwa sauti huru or something like that,wengine walisema stesheni zake zilikuwa baharini,sijui iliishia wapi ,lakini ilikuwa inaipinga sana serikali,anyone remembers this?
 
attachment.php

Baada ya Picha hii ndipo upepo mkali ulipokipiga chombo, nacho kimekuwa hakiendi sawa toka wakati huo. Kimekuwa kikiyumba karibu kuvunjika. Mabaharia walipoamua kupunguza shehena yao kwa kutupa baadhi ya mizigo bharini, nao wakakubaliana kupiga kura ya kumtafuta nani aliyesababisha tatizo hili. Kura ikawaangukia mafisadi, wakawauliza mafisadi tuwafanyaje, nao wakajibu tupeleke Ukonga. Kwa mshangao wa walio wengi, Nahodha akatangaza Msamaha, Chombo kingali baharini, Upepo ni Mkali, Tunaomba msaada Rescue scuad.

sorry nasikia eti mkapa alihusika moja kwa moja na kifo chake naomba anayeyajua vizuri haya mambo anielimishe wakuu maana nasikia baada ya kufa makaburu waliangusha pati ya nguvu kule south africa na baada ya hapo mkapa akawaita Tanzania na kuwapa kila kitu bure
 
sorry nasikia eti mkapa alihusika moja kwa moja na kifo chake naomba anayeyajua vizuri haya mambo anielimishe wakuu maana nasikia baada ya kufa makaburu waliangusha pati ya nguvu kule south africa na baada ya hapo mkapa akawaita Tanzania na kuwapa kila kitu bure

Leelee leelele ambaa!
 
Back
Top Bottom