Tukumbuke Zamani: Historia ya Taifa letu katika picha

.DJ Mc hope[makop]....CAVE DISCO TQ -arusha...........or arusha by nite ..late 70"s To early 90"s [RIP]

KURUGENZI JAZZ BAND....msimbe and bonzo...

nyerere alikuwa bomba sana enzi zake tulikuwa na band kila mkoa zikiburudisha....tulikuwa na ligi za ushindani[tena bila wadhamini ]..kila mkoa......timu za mashirika....arusha na moshi...

KILTEX
MOULBADOW-karatu
mbuni...
AICC
NDOVU
USHIRIKA -MOSHI
CCP
TPC
AFRICAN SPORT[WANA KIMANU MANU]
COASTAL UNION

DODOMA....

KURUGENZI
CDA
MTO - SINGIDA

ZIWA..

RTC KAGERA
RTC - SHINYANGA
RTC MWANZA-----DANNY MUHOJA...
PAMBA - WAANA KAWEKAMO...
RTC KIGOMA
RELI KIGOMA...

DUU jamani unaweza kulia.....hatukuwa na pesa lakini tulikuwa tunapata entertainment..........
 
Nchi zilizo Mstari wa Mbele katika Ukombozi wa Nchi za Kusini mwa Afrika.... Pichani chini ni mojawapo wa Viongozi waliopata kunufaika na nafasi ya Tanzania katika front line states...

Mkuu Kibunango,

Heshima mbele sana, hapo nimewaona Sam Nujoma(SWAPO-Namibia), Samora Machel (Frelimo-Mozambique), Kaunda (ex-Rais Zambia), na Mugabe (ZANU-PF Zimbabwe).

Wallahi enzi hizi wananchi tulikuwa hatulazimishwi na viongozi kwenda Airport kuwapokea hawa viongozi, yaani it was so good a history in the making kwamba hakuna aliyetaka kuikosa kuiona ikitengenezwa na Mwalimu.

Ahsante sana Mkuu Kibunango.
 
MAJI MAJI-SONGEA...wappi shafie bora..
KATAVI RANGERS - RUKWA
LIPULI-IRINGA
MECCO-MBEYA
TUKUYU STARS...wapi KAKA..
UFUNDI-MBEYA[PRISONS?]
TRM-MUHEZA[now TANROADS]
MWADUI - SHINYANGA
BANDARI-MTWARA
LINDI[?]
RELI-MORO..wapi JUMA LIMONGA 'stop engine"..WAPI ..dr madundo mtambo...
TUMBAKU
MSETO....

dar WAPI...

PILSNER...
KILIMANJARO HOTEL..wapi nico kiondo,maliro...
..BOOM ...RIP...amir ali bamchawi..mlezi wa wana...,mzee wa pilau mbuzi..mtaalamu wa mvua..simba dume..
FARU DUME..
SIGARA..
WAZO..
........................
 
field marshall,dj kalikali ni marehemu,baadaye akaibuka mdogo wake katika fani ya reggae kwa jina kalikawe naye vilevile ni marehemu.
jamani humu ukumbini inabidi tuseparate the man from the boys.NAULIZA je kuna member yoyote humu kacheza disco sansui lililokuwa seaview.
 
Wakuu naomba kutoa ombi kidogo, kwa wananchi wote ni kwamba so far tunakosa kuwa na picha za historia ya Vyama vya upinzani Tanzania kwenye hii thread, kwa hiyo tunawaomba kwa yeyote mwenye anything kuhusiana na historia ya upinzani nchini, tumwagieni wakuu ili tuchambue,

Natanguliza Shukrani.
 

Sawa Sawa Mkulu PM,

1. Tulikuwa na shida lakini masikini jeuri, ni kweli nilisahau hawa Kurugenzi Jazz ya Arusha, ambao nusu yake walimeguka na kuondoka na Simba Wa Nyika, kuhamia Nairobi, Lazaro Bonzo aliyekuwa the right hand man wa Mbaraka Mwinshehe naye baadaye alihamia Nairobi na kuanzisha bendi ya Orc. Lombe Lombe,

2. Kwenye michezo ya Mashirika ya Umma ilikuwa balaa maana huko ndio ulikuwa unawakuta wachezaji wote wakubwa wakicheza kwenye viwanja vya bure, yaani bila kulipa kwenye michuano ya awali, umeisahau Tumbaku ya Morogoro ikiwa na meneja wao aliyewahi kuwa RC wa Morogoro Mzee Lyanda, ambaye alitishia kuwa atamuweka ndani kiongozi yoyote wa Yanga au Simba atakayejaribu kunyemelea wachezaji wa Tumbaku, wakati akiwa RC Mwalimu akam-demote na kumpa u-meneja wa Pamba hapo hapo Morogoro ili aongoze vizuri mpira.

- Halafu kulikuwa na mashindano ya Sekondari Umiseta, duh ile ilikuwa baabu kubwa, maana ni kutoka kwenye hii michezo tuliweza kupata wachezaji kama Nico Njohole, Rahim Lumelezi, Jella Mtagwa, George Kulagwa, Patric Rugaimukamu na wengineo.

Ahsante mkuu.
 

...WHAAAAAT???

Anyway!, ..."Ukubwa jaa", 🙂

...tunaendelea na mapicha, siku hizi ukivaa kama kina Makochela au Braza masouuuuud masoud, utaonekana "mluga luga!"......


View attachment 2387
 
Mzee Fd ES,
Umesahau akina Ibrahim Kiswabi, Ahmed Amasha, Ibrahim Marekano, Daudi Salum aka Kaburu, Mwalusako, Abdalah Mtemi, Said George n.k.,toka timu ya Kamiseta Tabora, hawa ilikuwa chachu kubwa saana fainali ya Umiseta Iringa, nafikiri ilikuwa 76, Tabora ilipokutana na Dar ambayo ilikuwa na safu uliyoitaja hapo. Wakati huo Tabora ilikuwa ilikuwa inavifaa kwelikwli
 

Mzee FMES,

Najua una rekodi kubwa sana ya mambo ya wakati huo, ila nakuomba tena upitie kumbukumbu zako vizuri na kwa makini. Ukweli ni kuwa mtindo alioanza nao Marehemu Maneti pale Vijana Jazz ulikuwa ni Koka Koka. Wimbo wa Kamata Sukuma ulitolewa kipindi kimoja na Niliruka Ukuta, na ulipigwa pia katika mtindo wa Koka Koka, ila kutokana na umaarufu ulioambatana na wimbo ule wa Kamata Sukuma, Maneti akapromote wimbo wa "Kamata Sukuma" kuwa mtindo uliorithi Koka Koka mwaka 1976 hivi, na ulidumu muda mfupi sana kabla hajaanzisha Heka Heka. Kumbukumbu yangu kuhusu wimbo wa "Niliruka Ukuta" ambamo sauti ya Marehemu Maneti ilikuwa haitofautiani na ile ya Marahemu Mbaraka inakuja vizuri sana. Vile vile chini ya mtindo wa Koka Koka, Maneti alipiga wimbo wa "Zuhura Ninaondoka" ambao binafsi nilikuwa nauhusisha sana na mpenzi wangu wa wakati huo Marehemu Zuhura (RIP). Nilikuwa nina T-Shirt moja ya Sunflag iliyokuwa na picha ya kichwa cha tembo kifuani; mgongoni nikaandika pale maneno matatu kwa style ya aina yake: maneno hayo yalikuwa ni Masika, Sokomoko na Koka Koka, ambayo ilikuwa mitindo ya muziki niliyokuwa naizimia sana wakati ule. Marafiki zangu wa wakati huo wa ujingani wakisoma post hii watakumbuka sana ninayosema. Wakati Maneti anatoa wimbo wa "Niliruka Ukuta," Mbaraka naye alitoa wimbo wa "Mshenga" ambapo Marijani naye alikuwa ametoa wimbo uliokuwa unasema "Wapangaji mnawaacha watoto wenu wanavunjavunja milango na madirisha ndani ya nyumba yangu, hivyo ni afadhali muondoke kwani mnaleta sokomoko ndani ya nyumba yangu": jina halisi la wimbo huu silikumbuki tena. Nyimbo hizi zilikuwa kiboko sana wakati huo ndiyo maana kwangu mimi muziki ukawa ni Masika, Koka Koka na Sokomoko.


Kuna watu wengine wanaweza pia kuthibitisha hili. Hebu soma hapa:

 

Mukulu,

Shabaan Dede alihamia Sikinde akitokea Juwata Msondo ngoma ambapo hadithi ni kuwa alinyang'anywa unifomu wakiwa wanapiga mziki.

Alipohamia Sikinde, kibao chake cha kwanza kilikuwa Talaka Rejea akisimulia kisa cha kukimbia msondo. Mwishoni mwa wimbo, Bichuka anaimba majina ya wana sikinde waliotoka Msondo na kuunda sikinde, Abel, Mulenga,Mwanyiro, Gurumo, Bitchuka, Mwarami na wengine.

Msondo chini ya Mabela, Mnenge Ramadhani, Lusungu wakajibu Talaka Rejea na ule wimbo wa "umekubali kuuza nyumba na kununua kiwanja-Radhi ya Wazazi imekupata" kuhusu Dede kuuza kiwanja na kuamia kwa wakwe zake.

Stori moja niliyowahisikia ni ya Gurumo akiwa Sikinde, walikuwa DDC Magomeni, katikati ya wimbo, washabiki wa Msondo walikuwa wameingia wakamtupia "Molotov" la mavi yakiwa ndani ya pakti ya maziwa!

Ushindani kati ya Msondo na Sikinde ulikuwa ni mkubwa sawa na ule wa Kamanyola na Masantula ngoma ya mpwita!
 
Hii aliisema Mtikila wakati anajitahidi kujitafutia "soko" la kisiasa. Sidhani kama ina ukweli wowote.Wazanaki hawana dalili yoyote kuhusiana na makabila yaliyoko Burundi.

WildCard,

Kuna Empire kubwa sana East and Central Africa, inaitwa Bahima kama sikukosea ambayo ni shina ya makabila kadhaa yaliyoko Rwanda, Congo, Burundi, Tanzania, Uganda mpaka Kenya.

Katika ugomvi wa sasa kati ya Museveni na Kagame, chimbuko lake ni hilo la wao wawili kutoka shina moja na ndio maana Museveni anautaka sana ukuu wa EAC!

Sasa kabila la Nyerere Zanaki, inasemekana ni Bahima Empire.
 

Bahima na Bahinda ni koo zinazozunguka maeneo yote ya Uganda, Rwanda, Burundi, Ukanda wa Ziwa wa Victoria, Tabora na Kigoma kwa Tanzania na sehemu kubwa ya nchi ya Congo.
 

Naam, Gerald alikuwa hajui kusoma. Ukienda kumuomba akuweke wimbo fulani na unamtajia yitle ya wimbo huo anakwambia huo hatuna, lakini dakika chache unausikia 🙂. Inasemekana alikuwa anaweka nyota za debe nzito katika kila album, lakini alikuwa anajua kupanga debe moja baada ya nyingine unaweza kujikuta uko kwenye stage saa nzima unacheza debe tu. Mbowe ilikuwa kiboko. DJ KaliiKalii (RIP) alikuwa ni dj mzuri sana maana yeye alikuwa anayaweza mayai pia hivyo siku akiamua kurap na kuweka debe nzito ilikuwa ni balaa tupu. Kulikuwa na squad pale Mbowe ya kukata na shoka na kulikuwa hakuna disco zuri kama Mbowe na ukienda sehemu nyingine tofauti ilikuwa ni kubwa sana kama usiku na mchana.
 

Jamaa wengi hawa tulikuwa nao pale Tabora wakati nikiwa mwanafunzi wa TS. Skwadi kubwa la wanakandanda hao walikuwa wanafunzi wa Kazima Sekondari. Hiyo ni kabla ya Mbunge Mheshimiwa Charles Kajege Muguta hajaingia pale; na kwa bahati mbaya Mbunge Muguta hakuvuma sana kama walomtangulia ingawa alikuwa potential sana kwenye kabumbu, na nadhani imechangia sana kumfikisha bungeni. Kaburu (Daud Salum wa Kilosa) aliondoka TS akiwa Form 5.
 
Msimsahau na marehemu Jabari la Muziki. Nyimbo zake nyingi zilikonga nyoyo za Watanzania wengi sana kama huu hapa.

Wazazi wazazi nachoka na maneno yenu ya kila siku nyie.
Naona bure mnasumbuka mnayoyataka sintowatimizia
mnanilazimisha kuolewa, na mimi ningali mdogo
Ni miaka 12 tu mume nitamuweza wapi

Samahani samahani, samahani Baba na mama
sintoweza kuolewa na miaka 12 sasa
Mnanipa mume mapema mapema, masomo je?
fikiria Baba, dunia ya leo kukosa kisomo ni taabu

~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*

Oh! Georgina, siku uliyoondoka, uliniacha nalia na machozi
Umeenda kuishi kmbali nami, Georgina wa mama
Sipati usingizi nikikumbuka tulivyoishi mimi nawe Georgina aaa
Oh Georgina

Umeondoka Georgina, umeniachia masikitiko
Georgina Georgina Oooooo
Lini utarudi, uniondoe wasi wasi
Georgina wa mama

LOL! Zamani kulikuwa na muziki safi sana Tanzania hauna matusi, hauna maneno machafu machafu kama hizi nyimbo siku hizi za akina bongo flava na upupu gani sijui.
 

Nilishakusanya sana pesa nikiwa dogo 1974-76 pale Seaview Hotel!

Msimsahau DJ Mzee wa Mji Eddy Saly!
 
Ngoja niwarudishe kwenye mpira wa miaka ya sabini tena, kwani wakati huo tulikuwa na kandanada la hali ya juu sana haijapata kutokea. Inawezakana baadhi ya picha zimeshawekwa hapa ila nadhani hakuna tatizo kama nitazirudia, kwani wahenga walitufundisha kuwa jambao jema linastahili kurudiwa tena na tena.

Simba

African Sports


Coastal


Cosmo



Sijaelewa jina hili la Cosmo lilikuwa lina maana gani


Mseto ya Morogoro





Pan African



Yanga Wakitokea Ziarani




Golikipa Semainda akifanya vitu vyake


Picha zote zimetoka Idara ya Maelezo.
 

Attachments

  • simba.jpg
    28.1 KB · Views: 547
  • cosmo.jpg
    46.2 KB · Views: 538
  • mseto.jpg
    24.1 KB · Views: 532
  • pan.jpg
    26.7 KB · Views: 588
  • yanga.jpg
    43.7 KB · Views: 564
  • semainda.jpg
    43.7 KB · Views: 517

Nyimbo karibu zote hizi ninazo; nilinunua kanda zake pale RTD mwaka 2002 nikazi-digitize na kuzifanyia audio editing sana. Ila muda wa kuzisikiliza huwa unakuwa ni wa mkwara sana hasa kulingana na wingi wa nyimbo zenyewe kwa vile nilichukua collection yote ya kuanzia miaka ya sitini. Nyingi huwa nazikumbuka kwa kolasi tu.
 

Mchongoma

Wakati wa Masantula, OSS ilikuwa chini ya uongozi wa Kingi Kiki aliyekuwa akitamba na wale akina dada wa kichaga, nadhani mmoja alikuwa akiitwa Frida ingawa sina uhakika. King Kiki aliwatoa jasho sana OMACO (Orchestra Marquiz Company) ya mahasidi wake akina Chinyama Chiyaza hadi wakaamua kumrudisha kundini tena. Wakati huo Ndala Keshaba alikuwa bado ana hanja hanja mtaani tu. Baada ya Huggo Kissima kushindwa kumkeep King Kiki ndipo akamleta Freddie Ndala Keshaba ambaye aliingia na kombora lake la nyuzi dazaniu na kuibua mitindo mbalimbali mmojawapo ukiwa ule wa Chunusi ambao alikuwa akiwajibu Marquiz (ambako alikokuwa King Kiki wakati huo) kuwa kama wao ni Ogelea Piga Mbizi basi yeye ni chunusi na wasithubutu kuchezea majini tena. Nyimbo zake zilikuwa heavy sana kuliko za hao Marquiz. Hebu chukua nafasi usikilize wimbo kama Marashi ya Pemba au Kesi ya Kanga ndipo ujue kuwa Freddie(RIP) kweli alikuwa Supreme
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…