Tukumbushane ni tukio gani alilokufanyia Mwalimu Shule ya msingi likaleta mabadiliko hasi au chanya katika Elimu Yako

Tukumbushane ni tukio gani alilokufanyia Mwalimu Shule ya msingi likaleta mabadiliko hasi au chanya katika Elimu Yako

matunduizi

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2018
Posts
7,968
Reaction score
19,368
Mwalimu mama mmoja anamacho makubwa aliitwa Iganas.

Alikuwa Mwalimu wa hesabu darasa la sita.
Alikuwa anafundisha kisha anauliza kuna mtu hajaelewa kinafiki na kwa hofu wote tunasema hapana.

Anatoa swali kupima uelewa, kila anayekosa anararuliwa fimbo sio chini ya Tatu za mgongo.

Nilikuwa nakula bakora kila iitwapo Leo. Nilichokifanya ili kuokoa uhai na ubora wa mgongo wangu nilimtafuta mkali wa darasa kwa kumuhadaa akawa ananipitishia majibu kijasusi bila Mwalimu kujua.

Hapo ndipo nilipata likizo ya viboko. Nilikuwa sijawahi kupata zaidi ya 40% hesabu. Raha ya kutopigwa fimbo ilinifanya nikomae hadi namaliza STD 7 pale shuleni matokeo Yangu ya mwisho ilikuwa ni 98% hata Mkali nikamvuka.

Wakuu woga wa fimbo ulinitoa. Na sijawahi kusoma level yoyote bila hesabu kuwepo maana ninaikupali na ninaipenda maana tumetoka nayo mbali.
 
Nikiwa darasa la tano nilikuwa na mwalimu wa kuitwa Mponji,ehhh bwana eeeh!Hiyo topic ilikuwa inaitwa vigao na vigawe Mara vipeo na vipeuo,jamani alikuwa anaingia na fimbo ndefu inanesanesa ni ule mti unaotumika kutengeneza viti vya kukunja, nilikuwa nikimuona tu tumbo lote linanikata,sikuwahi kuelewa zile hesabu hata siku moja kila uchao nilikuwa nmapaja jamevilia damu, hapo ndio ilikuwa mwisho wa safari yangu ya kimahesabu!nimekuwa na allergy na Hilo somo mpaka chuo,alifanya nipate tabu Sana na Statistics for!Mungu mlaze mahali pema peponi mwalimu.
 
Nikiwa darasa la tano nilikuwa na mwalimu wa kuitwa Mponji,ehhh bwana eeeh!Hiyo topic ilikuwa inaitwa vigao na vigawe Mara vipeo na vipeuo,jamani alikuwa anaingia na fimbo ndefu inanesanesa ni ule mti unaotumika kutengeneza viti vya kukunja,nilikuwa nikimuona tu tumbo lote linanikata,sikuwahi kuelewa zile hesabu hata siku moja kila uchao nilikuwa nmapaja jamevilia damu,hapo ndio ilikuwa mwisho wa safari yangu ya kimahesabu!nimekuwa na allergy na Hilo somo mpaka chuo,alifanya nipate tabu Sana na Statistics for!Mungu mlaze mahali pema peponi mwalimu.
Aisee Mimi darasa LA tano ilikuwa kugawanya manamba mengi. Kilisababisha nimchukie kabisa mama Mdogo ambaye alikuwa Mwalimu wa cheti ( waliofutwa juzi).

Kila baadae ndio niligundua alikuwa sahihi
 
Aisee Mimi darasa LA tano ilikuwa kugawanya manamba mengi. Kilisababisha nimchukie kabisa mama Mdogo ambaye alikuwa Mwalimu wa cheti ( waliofutwa juzi).

Kila baadae ndio niligundua alikuwa sahihi
Yaani la tano ni kimbembe😂!na pale ndio ulikuwa msingi,kweli msingi imara hujenga nyumba Bora Mimi nimepata tabu Sana kwenye hili somo.
 
Hii lilimtokea mwenzetu pia ni ndugu kwetu,
alikuwa na tabia ya utoro na uvivu wa kutokuandika
mwisho wa siku mwalimu wa Hesabu akasema kila mtu ashike daftari lake Tukae kwenye mstari atusahishie
Basi bwana jamaa hakuwa na daftari la hesabu akakimbia kununua hela alikuwa nayo akanunua na Bablishi akaja akitafuna

Zamu yake ikafika akaenda mbele ya mwalimu ,mwalimu kucheki daftari jipya, lazamani hamna na hilo jipya limeandikwa madudu kwani alikuwa mtoto,Mwalimu alimzaba bonge la kofi kwa mahati mbaya Mate yakamrukia ,Mwalimu mwenyewe alikuwa mashauzi amejichubua bonge bonge pafyumu kwa sana kalikiti nywele ,akamtazama kwa hasira akamwambia unakula Bablishi unanitemea mate ,akaita wanafunzi akawaaagiza mzigo wa mijeleji kwani fimbo aliyo kuwa anatumia ilishamwishia jamaa.

Jamaa kucheki usawa akaona hapa siyo salama akakimbilia darasani Kisha akaruka kupitia dirishani mbio ,hakuonekana tena ikabaki stori kuwa jamaa alienda machimboni Mirerani hiyo ilikuwa darasa la Nne tukiwa la tano tunakaribia kuingia la sita yule jamaaa karudi kitaani na Pikipiki aina ya Baja ashakuwa kifaru alipiga milioni 70 .

Kila Mvulana Darasani alijilaumu kwa kupoteza muda na fimbo nyingi mwenzetu anakula bata tena kwa Muda mfupi.Malimu naye akawa anajificha akisikia mngurumo wa Pikipiki kwani Pikipiki zilikuwa adimu kwa wakati ule .acha kabisa hii mambo ngoja niishie hapa
 
Nilisoma makole primari Dodoma aisee mwalim Mpilimi sitamsahau alikua anafundisha hesabu aisee alikua anachapa sana daaah
 
Kuna ticha alikuwa anaitwa Sanga kwa wakati ule alikuwa ananihimiza kuhusu shule nilikuwa naona ananikwaruza masikioni tu. Mbaka baada ya Mimi kufukuzwa shule na mshua akasitisha huduma za masomo kwa miaka 2 mfululizo kutokana na mimi na vibaraka wangu kuiba cement ambazo shule ilinunua kwa ajili ya ujenzi wa makaro.
 
Mi nakumbuka enzi hizo darasa la sita shule ya msingi chipukizi iliyopo igunga Tabora,kuna mwalimu alikuwa anaitwa ng'omba nseu wa somo la maarifa ya jamii,alikuwa anatutoa nje tunakaa juani tunakaa mbali mbali kila mtu anapewa karatasi yenye maswali mbalimbali ukipata chini ya marks 50 utakula bakora mpaka utajuta kwanini umeenda shule kusoma.
 
nilikua muoga wa fimbo kwahiyo kufaulu hakukua tabu
mwalimu aliniambia katika maswali 50 ya mitihani mitano ya kila ijumaa nisipate chini ya 40/50 inamaana nikose maswali 10 tu
- Katika mtihani wake wa hisabati swali la 1 -25 nisikose hata 1 nikikosa fimbo 3
nikipata 40/50 konzi 1
- Nikiandika jibu halafu nikakata nikaandika jibu lingine kwa mbele fimbo 3 (majibu yote ya mtihani yawe clean)
- Katika maswali 50 hakuna kuacha Gap jaza yote hata upupu jaza ila sio mtihani uende na Gaps
- Ukipata swali ya Hisabati gumu halafu ushindwe kusolve mbele ubaoni pale fimbo 3

Ilinifanya nifaulu shule ya vipaji maalumu[emoji2] ambayo yeye mwalimu alinitabiria
mpaka kesho kutwa sina muandiko mbaya , nazingatia uandishi mno maana nahisi kama zile fimbo 3 bado zipo
 
nilikua muoga wa fimbo kwahiyo kufaulu hakukua tabu
mwalimu aliniambia katika maswali 50 ya mitihani mitano ya kila ijumaa nisipate chini ya 40/50 inamaana nikose maswali 10 tu
- Katika mtihani wake wa hisabati swali la 1 -25 nisikose hata 1 nikikosa fimbo 3
nikipata 40/50 konzi 1
- Nikiandika jibu halafu nikakata nikaandika jibu lingine kwa mbele fimbo 3 (majibu yote ya mtihani yawe clean)
- Katika maswali 50 hakuna kuacha Gap jaza yote hata upupu jaza ila sio mtihani uende na Gaps
- Ukipata swali ya Hisabati gumu halafu ushindwe kusolve mbele ubaoni pale fimbo 3

Ilinifanya nifaulu shule ya vipaji maalumu[emoji2] ambayo yeye mwalimu alinitabiria
mpaka kesho kutwa sina muandiko mbaya , nazingatia uandishi mno maana nahisi kama zile fimbo 3 bado zipo
Mwalimu huko vzr mno. Ningempata Mimi angeniua Maana kwa kufuta nilikuwa bingwa.
Kusahausahau ilinichukua Muda kubalance bila catalyst ilikuwa sikubali kupitwa na msichana.

Hapo lazima uingie maalum hakuna namna
 
Mwalimu huko vzr mno. Ningempata Mimi angeniua Maana kwa kufuta nilikuwa bingwa.
Kusahausahau ilinichukua Muda kubalance bila catalyst ilikuwa sikubali kupitwa na msichana.

Hapo lazima uingie maalum hakuna namna
yes
na akatenga madarasa la wenye wastani wa 35 mpaka 50 chini ya hapo wana darasa lako linaitwa Scrapers [emoji23]
Basi mtu atasoma atafanya afanyalo atoke kwenye scrapers
 
Mi nakumbuka enzi hizo darasa la sita shule ya msingi chipukizi iliyopo igunga Tabora,kuna mwalimu alikuwa anaitwa ng'omba nseu wa somo la maarifa ya jamii,alikuwa anatutoa nje tunakaa juani tunakaa mbali mbali kila mtu anapewa karatasi yenye maswali mbalimbali ukipata chini ya marks 50 utakula bakora mpaka utajuta kwanini umeenda shule kusoma.
Safi sana. Hana tofauti na Mwalimu tofiki darasa LA tano jiografia. Alikuwa Mkali wa story. Yaani ukihadhithiwa Kilimo cha Mihundi marekani au Mchele Burma Mkuu kama vile uko Texas. Mnakuwa Kama mnasafiri hivi .

Hicho kipindi kikifika hadi wale sugu wasiopenda Shule utawaona class. Kila baada ya hapo akileta mambo ya maswali kipindi kinachofuata wavivu wana kula Kona.

Ila angrongeza na hiyo mbinu Kila mtu angekuwa Anapata A.


Yaani nilishangaa eti walimu na wanafunzi Shule moja ya english medium hawajui TAZAMA ni nini.

Enzi za Mwalimu tofiki hata Ramani ya dunia nilikuwa naweza kuchora. Mini mikuu karibu yote duniani nilikuwa naflow tu. Ila siku hizi nishasahau
 
Kuna ticha alikuwa anaitwa Sanga kwa wakati ule alikuwa ananihimiza kuhusu shule nilikuwa naona ananikwaruza masikioni tu. Mbaka baada ya Mimi kufukuzwa shule na mshua akasitisha huduma za masomo kwa miaka 2 mfululizo kutokana na mimi na vibaraka wangu kuiba cement ambazo shule ilinunua kwa ajili ya ujenzi wa makaro.
Kuna jamaa alikuwa kama wewe. Aliishia darasa LA NNE. Wakati tuko darasa LA saba yeye alikuwa anatuuzia karanga . alikuwa na story nyingi bingwa wa kuchekesha yaani yule angekuwa sehemu yeye exposure angeshafika Hollywood.


Kuangalia movie sio bora kuliko yeye aangalie alafu akuhathie.


Mkuu Tz kunavipaji aisee. Elimu ya darasani sio kila kitu
 
Nilisoma makole primari Dodoma aisee mwalim Mpilimi sitamsahau alikua anafundisha hesabu aisee alikua anachapa sana daaah
Kwa nini walimu wa hesabu huwa wako vizuri sana suala LA stiki ?
 
Mosi:- Nilikuwa mzembe sana Shule ya Msingi lakini Mamaangu alikuwa ananiambia " una akili sana Mwanangu" ila nilikuwa sizingatii kwa sababu Shule msingi unasoma tu huelewi kwa nini unaenda Shule pia Ufaulu ulikuwa mdogo anaweza kufaulu mmoja, wawili au wikijitahidi sana wanne hadi Watano na kwa kweli hili swali liliniwangisha kichwa sana "kwa nini naenda Shule? , nasoma ili iweje? kama Wazazi wanapenda Shule si waje wasome wao mimi nipumzike Nyumbani, Wadogo pamoja na wakubwa zangu wengine wanabaki Nyumbani huku naenda Shule alafu Nasoma nahisi njaa haya mteso hivi mantiki yake nini?" na kweli nilikuwa nafurahia sana wakati wa Likizo maana hatusomi 😂

Tukiwa Darasa la 4 wakati tunafunga Likizo kubwa Mwalimu mmoja anaitwa David Mkangara alizungumza maneno mengi sana ya muhimu pengine ni kwa vile alisoma matokeo ya Madarasa manne ( Darasa la 3, 4, 5 na lake darasa la 7) . Alisema " Ndugu Wazazi hii Shule yetu imekuwa na ufaulu mdogo sana natamani tuwe na Ufaulu mkubwa ili nasi Walimu tujivunie hiyo ndio fahari ya yetu, inahuzunisha sana nafundisha alafu Wanafunzi wanafeli inaonekana tupo hapa kupiga soga za Umbea sio kufundisha. Wazazi nawaasa sana Mtusaidie hawa Watoto wanapokuwa likizo muwasaidie angalau wasome Twisheni au kuwakukumbusha kusoma, natamani siku moja tutoe Mainjinia (Wahandisi) hapa, Mahakimu watoke hapa, Wanasheria, tupate walimu hapa inasikitisha Shule nzima anazungumza Kiingereza Mwanafunzi mmoja peke akamtaja ( alikuwa wa Darasa la 7 ........" ikafika zamu ya Darasa la 4 ambapo nami nilikuwa humo akasoma matokeo akabikisha 3 bora nami nilingia kwa mara kwanza na mwisho akasema " kwa Mfano huyu Mtoto ninaemsoma hapa ana akili sana tatizo ana mzaha, michezo mingi , vurugu nyingi
nyie Wazazi mkazanie sana huyu Mtoto pengine atabadilika amepata English 80 yaani huyu ndio Mwanaume wa Shule nzima kwa English hata Darasa la 6 na 7 waje awafundishe anaweza" kisha akanitaja nikanyanyuka nikawasalimia nikachukua Zawadi zangu nikarudi nikaketi lakini moyoni niiuwa nafuraha sana nimemizidi hadi yule anaezungumza Kiingereza Shule nzima 🙌😂

Tangu siku hiyo maswali yangu yalipata majibu na nilibadilika kwa kiasi kikubwa hasa neno " ana Mzaha na michezo mingi" lilijirudia sana Kichwani mwangu
Ahsante sana Mwl. David Mkangara nimefanikiwa kusoma kwa sababu uliishi ndoto yangu.

Pili:- Darasa la 5&6 kuna Walimu waalinzisha kipindi cha Maswali muda wa kwenda kula ( Saa 6 Mchana) ili upate ruhusa ya kwena lazima ujibu kwa usahihi
Tatu :- Imla imetusaidia sana kujifunza Kiingereza tangu darasa 3 hadi tumaliza Darasa la 7 ilikuwa ni jadi yetu hata sisi wenyewe wanafunzi tunaulizana na kusahihishiana kwa kufuata kile kilichoandikwa kwenye Ki/Vitabu.
 
Back
Top Bottom