Tukumbushane ni tukio gani alilokufanyia Mwalimu Shule ya msingi likaleta mabadiliko hasi au chanya katika Elimu Yako

Darasa la 7 hesabu zilikuwa zinanipa shida Shule ya Msingi Wilolesi, mtihani wa kwanza wa ujirani-mwema nikapata 21/50 kama sikosei. Mwalimu Mkuu wetu, Mwl. Mapunda akaja na wazo zuri kwa wanafunzi kuhusu somo la hesbu kuwa unapoingia kwenye mtihani hakikisha swali la 1 mpaka la 33 ambazo ni hesabu nyepesi nyepesi unapata yote, yaani fanya kwa usahihi swali la 1 mpaka 33, kuanzia swali la 34 ni maumbo na mafumbo, hapo donoa donoa ukipata maswali 7 kati ya 17 yaliyobaki unakuwa umepata maksi 40/50. Aisee, niliitumia kanuni hiyo na mpaka namaliza sikuwahi kupata chini ya 43/50. Na mpaka leo nikikutana na somo la hesabu huwa naendelea kutumia kanuni hiyo, puuza maswali magumu komaa kwa uhakika na mepesi yenye maksi nyingi, magumu waachie wataalamu, donoa donoa tu.
 
yes
na akatenga madarasa la wenye wastani wa 35 mpaka 50 chini ya hapo wana darasa lako linaitwa Scrapers [emoji23]
Basi mtu atasoma atafanya afanyalo atoke kwenye scrapers
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]

Eti scrapers.
 
Nilifungwa chini ya mwembe toka asubuhi hadi jioni nikichapwa viboko kwa awamu kwa siku nzima nikiwa darasa la 5....sababu tu sikupiga salute tukiwa tunaimba wimbo wa taifa kwenye mkusanyiko asubuhi

Toka siku hiyo mambo ya shule yalinikaa kushoto sana niliendelea kusoma tu kuwaridhisha wazazi[emoji23][emoji23]
 
Walimu wangu alikuwa wema Sana...Sijawai palangana na mwalimu yangu yoyote katika level zote za Elimu...

Naikumbuka Shule yangu ya primary Dar ul Muslimeen International Primary School.

Wazazi walijitoa Sana kwa Elimu yangu ya primary

Namkumbuka mwalimu wangu Madam Ufwinki wa Hesabu Msalato girls secondary school.. Hakika Alinifundisha vyema kabisa..nikaipenda Sana Hesabu.

Nakuombea Heri Madam Ufwinki..ulifanya kazi yako kwa kujituma Sana.
 
mwalimu ngovi popote ulipo shikamoo,stiki zako za makalio,mapaja zilinifanya niwe na disclipne kubwa kuanzia darasa La sita adi elimu ya juu,,mpaka sasa sipendi kufanya makosa ya kuepukika maishani,nimekuwa smart kwasababu ya stiki zako za kuadilisha,nlipokuwa nachelewa namba shuleni na kufika saa mbili au tatu asubuhi ulinichapa kwelikweli kama hunijui vile,ulikuwa unatisha haswa shule nzima ilikuogopa,nkifeli hesabu,sayansi,kisw ww unanichapa tu khaaa ila nlikuja kupata faida baada ya kuingia form one toka apo nikabadilika adi kupewa nishani za nidhamu adi Leo mtaani wananikubali sana kama mfano wa kuigwa asante mwalimu ngovi na mwenzako ticha rugeye
 
hoja ni mwalimu ama ni sisi kujua u mkali wa hesabu???
 
hoja ni mwalimu ama ni sisi kujua u mkali wa hesabu???
Hoja ni Mwalimu kusababisha kupenda au kuchukia au kukomalia Shule somo au jambo.

Hayo yalikuwa matokeo yabmwalimu mkuu.


Kuhusu ukali wa hesabu nilikuwa Mkali hapo tu nilikutana na wajomba advance ambao hata sikuwa nanusa anga zao japo nilikuwa najikongoja
 
Tuliosoma shule ya msingi Ligula Mtwara nadhani hatutamsahau Mwl Mayele.
Sijui kama yuko hai au lah!
Mziki wake tunaujua.

Wale wa Mtwara gilrs,nadhani Mwl Ngwada au Ngwadakulima pia hatutamsahau.
Sikupendi tangu nasoma na mpaka sasa kwa bakora zako.
 
Nimesoma Shule ya msingi ya jeshi yaani ni mpelampela kila kitu kijeshi. Fimbo, mazoezi ni vya kufikia.
Awali ilikuwa na walimu wa kawaida wanajeshi walikuwa wawili lakini kuna Intake ilikuja pale jeshini maticha wanajeshi wakaongezeka. Ni shule ya msingi lakini maticha wanajeshi walikuwa 18, tulizoea kuibiana mbona wizi ulikoma. Kichapo kilitembea, utongoze demu afu demu akasema basi mtatajana shule nzima ni kichapo. Paredi wakisema mguuuuu pande! Kuanzia la kwanza hadi la 7 ni kishindo kimoja hakuna kuangusha maembe.

Mbali na kichapo walikuwa peace sana, mnaweza kuwa mpo darasani wakatununulia vitumbua, bajia, maandazi darasa zima mgao unapita au mgao wa karanga mnawekewa kwenye desk sheria unakula karanga mojamoja, sasa bugia uone shoo.

Shule ilitujenga tukawa wakakamavu japo bakora ni kama Mswaki wa asubuhi
 
Ulikuwa na busara. Wengine hulaumu tu fimbo za mwalimu, lakini hawajawahi kufikiria kuwa ziliwabeba wakafika walipofika.

Unamheshimu mwalimu wako hadi leo japo unaishi maisha yako.
 
Hadi sasa asilimia kubwa humu wanakiri kwamba fimbo za walimu ndio zilisaidia kuwanyoosha sasa najiuliza inakuwaje sasa tunawakataza walimu kwa Zama hizi wasitumie Tena fimbo inamaana hatuwapendi watoto wetu au tunataka kizazi Cha aina gani hapo baadae?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…