Tukumbushane ukoloni uliowahi fanyiwa na wazee wako

nakumbuka bro alikua na tabia ya kutoroka usiku na kwenda disko kumbe wazee walimshtukia siku moja wakamlia timing dingi kashika slasher na fimbo afu maza kashika tochi wamebana getini ile mida ya kurudi anavoingia tu kipigo alichokutana nacho wacha kabisa alienda kulala chini ya mti afu kulikua na mvua vibaya
 
daah huyo kiboko[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji342]
 
Yaani acha kabisa, sasa si ushaambiwa hela zote ni zake na ukitaka uombe!
Baada ya hapo ilibidi aanzishe self reliance program, kila mmoja na bustani yake ya mboga na kuku. Yaani yule mama nikimkumbukaga najikuta nacheka tu na kumshukuru.


Haha, ni wa kumshukuru kwa kweli.😀
 
Too bad sina relationship positive sana na mzee wangu ila huyu mzee yeye anakawaida moja tu anapenda kulalamika balaa.
Unakuta labda mnaangalia luninga ghafla chaneli imekata inaonyesha chenga utamsikia "Amigo hiyo TV umeifanya nini mbona imeanza kuonyesha chenga"
Basi inabidi utoke nje uzungushe Antenna mpaka uzipate chaneli ndio lawama zinaisha.
Unakuta ng'ombe analia unaitwa kwa mkwara "Amigo huyo ng'ombe umemfanya nini tena mbona analia"
Pia anapenda Kujifanya yeye ndio anajua kila kitu, ukimpa ushauri hata kama wa kitaalamu lazima uambulie maneno ya shombo... Hapa sita sahau siku moja Ford Escort yake iliaribika akawa anaitengeneza sasa ikafika sehemu akawa amekwama inabidi nimpe mawazo mbadala cha kushangaza nikaambulia majibu yake ya siku zote "tulia huko kwani mimi na wewe nani wa kwanza kuiona spana" lakini alivyo jaribu baada ya kuhangaika sana wazo langu likakubali.
Dah!!! It's too bad things fell apart between us. But I ain't mad at him, I love him dearly.
 
pole sana
 
Hamna kunywa chai bila kuoga
Sa kumi na mbili geti limefungwa...
Alileta ukoloni zaidi pale alipoanza kukusanya simu zetu sa mbili usiku na kuzizima mpaka asubuhi anapoenda kazini.
Wewe bado young sana yani kipindi cha ukoloni wa mzee wako ulikuea unamiliki simu!!!!
 
Mimi nilizuiwa kwenda shule na mzee kisa nimefua nguo vibaya!!
 
[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] du unachapwa kabla ya kosa ,sasa siku ukifanya kosa viboko vitapungua?
Kuna siku mdogo wangu alishindwa kuvumilia huo ukoloni wa mzee alichukua kamera akaipasua et anatafuta hao watu walio pigwa picha kwenye ile kamera ili akawaogeshe aliambulia kuona mkanda tu.sasa mzee alivyorudi home kipigo chake kilikua ni heavy mtu alitundikwa kwenye paa huku kaning'inizwa kama anae pimwa uzito nadhani siku hiyo hata malaika walipatwa na unyonge.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…