Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hakika. Mwaka huo 1994 ndio nimeamza kuangalia World Cup iliyofanyika Marekani. Ndio mwaka dingi amenunua TV home. Halafu ligi kama Barclays (EPL), Bundesliga na Serie A ilikuwa tunaangalia bure tu. Hakuna malipo yoyote, hapa kuwa na ving'amuzi. Mchawi antenna tu ya ndani na nje.Wana jamvi leo nimeona japo turevew miaka hii ya nyuma vipindi vya television enzi zile 1994 kuibukia miaka ya 2000. Binafsi nakumbuka mbali sana hasa vipindi vya television ITV mfano Egoli place of Gold, 21 jump Street, Time trax, movie ya V, Rino Renz, vichekesho Kama Fresh Prince of bell air, family matters, Living Single ya Queen Latifa, Tausi ya mjuba, Vitimbi(masakuu, Ojwang' Othrong'ong'o) Vioja Mahakamani, Mambo hayo ya kina Waridi, Sumbi, bocha na Aisha. Pia kulikuwa na Tamthiliya kama The young and the restless, Sun seat beach, na Acapulco bay.
Aidha nakumbuka tulikuwa tunaangalia UEFA kupitia CFI(Canal France International). Matangazo nakumbuka kama Revola, komoa, lotion ya Jambo, hebu vingine mnisaidie CTN na DTV. Je kipindi kile watangazaji unawakumbuka? Wa ITV, CTN, na DTV. Mimi kwa itv namkumbuka Suzan Mongi nilimpenda sana sana. Karibuni tuflash back jamani.
Makala nzuri sana zile. Umenikumbusha mbali. Kila Jumapili usiku. Muandaaji wa kipindi amefariki ktk ajali ktk harakati za kutafuta habari, alikuwa anaitwa Mohammed Amin. Ndio maana kipindi hakikuonekana tena.Africa journal nilikua nakipenda
Sunday Shomari na Monica MfumiaHuwa nakumbuka kale ka mdundo ka lile tangazo la fanta ambao walikua ndio wadhamini wa kipindi na pia namkumbuka Sunday Shomary na Suzan Mungi walikua wanapendeza sana
Family mattersView attachment 402149hivi mnamkumbuka jina huyu jamaa..? ...vichekesho vyake vilikua itv miaka hio sijui vilikua vinaitwaje
Kipindi hiko anaitwa Suzana Lukindo. Alikuwa anatangaza taarifa ya habari yeye na Fauziat Abood. Kabla ya kuja akina Julius Nyaisanga kutangazaSusan Mungi alikua KISU sana those years, sasa hvi kawa bonge, shepu imekua ya kiutu uzima sana; ulaya sio kuzuri kiviiile.
Dar es Salaam Television (DTV) enzi za akina Godfrey Mngodo (dingi flani hivi). DTV ndio ilianza baadae wakaanzisha Channel tenHahahah kumbee ilikuwa channel Ten zamani DTV sio?
Mwishoni mwa tangazo anaonekana muuza madafu au sioMimi nakumbuka world cup94 Italy ITV walirusha matangazo ya mpira kiufasaa na kulikuwa na tangazo la salama condoms nlikuw nalipenda sana..
Na Lile tangazo la bia ya TUSKER. Ukiona tangazo la TUSKER, REVOLA na SALAMA CONDOM ujue uchambuzi na mechi unakaribia kuanzia. Enzi hizo (world cup 1994) wachambuzi ni Charles Hillary na Mickdad MahmoudMimi nakumbuka world cup94 Italy ITV walirusha matangazo ya mpira kiufasaa na kulikuwa na tangazo la salama condoms nlikuw nalipenda sana..
Hako apo mkuu