Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Fuatilia yanayojiri kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 12, Kikao cha 5, leo Septemba 4, 2023.
Ratiba:
Serikali imesema ipo miongozo mbalimbali inayoongoza suala la kujitolea kwa watu wa kada mbalimbali ikiwemo walimu, lakini hakuna utaratibu maalum unaoongoza suala hili. Serikali imeanza mchakato wa kuandaa sheria itakayotoa mwelekeo wa suala hili na pindi ikiwa tayari italetwa Bungeni ili wabunge waweze kutoa maoni.
Aidha, Ridhiwani amebainisha kuwa Serikali kwa sasa inahifadhi majina ya watu wote wanaoshiriki michakato ya ajira kwenye kanzi data zake na inaishi kwa mwaka 1. Pia, Spika wa Bunge, Tulia Ackson ameishauri Serikali itafute utaratibu wa mpito wa kuwatazama watu wanaojitolea kwenye kada Mbalimbali ili wapewe kipaumbele kwenye ajira.
Ratiba:
- Dua
- Hati za kuwasilisha Bungeni
- Maswali
Serikali imesema ipo miongozo mbalimbali inayoongoza suala la kujitolea kwa watu wa kada mbalimbali ikiwemo walimu, lakini hakuna utaratibu maalum unaoongoza suala hili. Serikali imeanza mchakato wa kuandaa sheria itakayotoa mwelekeo wa suala hili na pindi ikiwa tayari italetwa Bungeni ili wabunge waweze kutoa maoni.
Haya yamefafanuliwa na Ridhiwani Kikwete, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais, menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakati akijibu swali la Mbunge wa Kiteto, Edward Ole Lekaita aliyetaka kufahamu nia ya Serikali katika kuwezesha walimu wanaojitolea kupata upendeleo kwenye ajira za Serikali pindi zinapotangazwa.Aidha, Ridhiwani amebainisha kuwa Serikali kwa sasa inahifadhi majina ya watu wote wanaoshiriki michakato ya ajira kwenye kanzi data zake na inaishi kwa mwaka 1. Pia, Spika wa Bunge, Tulia Ackson ameishauri Serikali itafute utaratibu wa mpito wa kuwatazama watu wanaojitolea kwenye kada Mbalimbali ili wapewe kipaumbele kwenye ajira.