Tulia Ackson: Wanaotaka Kugombea Ubunge Jimbo la Mbeya Mjini Wapime Kina Cha Maji

basi na atulie kama anajiamini
 
Eti utafananisha na huyu anayelingushia miwani na suti mitandaoni. Waliokuwa wabunge wa chadema wanachosahau ni kuwa ccm ikiwa moja hakuna anayetoboa.

Wengi ukiangalia ushindi wao ulitokana na ccm kugawanyika kwenye kura za maoni. Miaka ile wengi walipita kwa rushwa. Watu wakachukia kwa watu muhimu kukatwa.

Wakapigia kura upinzani. Ndio siri ya ushindi upinzani. Sasa wao upinzani wanahisi walipita kwa sababu ya wafuasi wao ama wanapendwa sana.

Ndio maana Sugu anaongea kwa kutamba akidhani alipigiwa kura za haki kumbe ni kura za hasira kutoka ccm wenyewe.

Ye aombee tu ccm wagawanyike, ushindi wake utakuwa saa tatu asubuhi. Ila ccm ikiwa moja atandelea tu kuonyesha miwani na suti huku akizidi kuzeeka kwenye bustani za desderia hotel
 
Mimi naishi mbeya huku tunamuimba sugu
 
Mbeya ipi hii yenye mashimo kila mtaa na lami kilomita za kuhesabika anataka ubunge aweke lami

NJia panda mapele mpaka usaga tigwa
Igodima mpaka machinjion.
Njia panda karobe mpaka maji machafu
Njia panda mbembela mpak halengo kutokea ikuti
Ghana mpaka nzoo
Njia panda juhudi mpaka mapele mwisho

Na nyingine nyinga ambazo anazifaham na sio kutuwekea matamsha ya ngoma za asili.
YAAAN MJI HAUNA MIUNDOMBINU MWENDA ZAKE ALITWAMBIA TUMPE MBUNGE ATATENGEZA LAMI LAKIN WAPI HAMNA KITU.
 
Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson amesema ahofii kukabiliana na aliyewahi kuwa Mbunge Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi ‘Sugu,’ endapo watakutana katika kinya’ng’iro cha kugombea jimbo hilo katika uchaguzi mkuu ujao 2025 utakaokuwa huru na haki.

Dk Tulia ametoa msimamo huo leo Mei 4, 2023 wakati akijibu swali katika mahojiano maalumu na runinga moja nchini na kufanyika katika makazi rasmi ya Spika Jijini Dodoma.

Pamoja na mambo mengine, Spika aliuzwa ikiwa hatishiki kukabiliana na Sugu’ katika uchaguzi unaoitwa huru na haki, hasa ikizingatiwa kuwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020, wapinzani wengi waliamini kuna nguvu ya ziada ya dola ilitumika kuwabeba walioshinda.

“Sihofii kupambana naye, niko vizuri sina wasiwasi na hilo naomba Mungu aniweke, nimefanya kazi kubwa, nyie nendeni Mbeya Mjini mtaamini,’ amejinasibu Dk Tulia.

Na akaongeza kusema: “Hata yeye anajua (Sugu), hao wanaojadili mtandaoni nadhani hawajafika Mbeya wala hawapajui wala kuwasikia Mbeya, sasa nyie (waandishi) mnakaribishwa halafu mtawanyike na mkaulize hapa Mbeya Mjini mbunge ni nani, mtapata majibu.”

Katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 uliolalamikiwa na vyama vya upinzani, Dk Tulia alishinda kwa kura 75,225 dhidi ya Sugu aliyepata kura 37,591 licha ya kuwa aliliongoza jimbo hilo kwa miaka 10 mfululizo kuanzia mwaka 2010/20.
Dk Tulia amejivunia mafanikio yanayotokana na kazi alizozifanya kwa kusema kuwa wakati wa kampeni ahadi zilikuwa nyingi zikiwemo za Mbunge na Ilani ya CCM.

Kati ya ahadi hizo kwa mujibu wa Spika Tulia, ilikuwa ni kujenga barabara ya njia nne kuanzia Igawa hadi Tunduma kwa kilomita 218, ambapo ameomba wameomba awamu ya kwanza ya ujenzi ianzie Mbeya Mjini ili kupunguza changamoto ya foleni.

“Hivi sasa Serikali imeshaingia mkataba na mkandarasi ameshaanza majukumu yake. Jambo jingine ni mradi wa maji Mbeya kuna watu wengi wanaongezeka kwa nyakati tofauti, bado kuna changamoto ya maji baadhi ya maeneo,” amesema.

Kwa mujibu wa Munge huyo, aliwaahidi wapiga kura wake kumaliza changamoto hiyo akisema: “Tuliwaahidi kumaliza changamoto hiyo na kwa sasa mkandarasi yupo eneo la kazi kwa ajili ya kutekeleza mradi mkubwa wa Mto Kiwila utakaoleta maji Mbeya mjini,”amesema Dk Tulia.

Kukamalika kwa ahadi hizi pamoja na mengine mengi, kunamfanya Spika Tulia kama ndiyo vigezo vitakavyo washawishi wana Mbeya kumpigia kura nyingi ili aendelee kuwa Mbuge wa jimbo hilo kwa kipindi kingine cha miaka mitano
 
Hakuna cha maji hapa as long as magufuli sponsor wake hayupo na tuna tume huru ya uchaguzi, hakuna kina cha maji mbele ya Sugu
 
Ameomba jimbo la Mbeya mjini ligawanywe ili amkwepe Sugu.
 
Hao vijana wanaoiimbaimba hiyo Foundation mdiyo wanufaika wakubwa wa hiyo taasisi ma wanajaribu kumuonyesha Tulia kiwa hiyo taasisi ndiyo nguvu yake ili aendelee kuweka mzigo ma wao waendelee kuzipiga.
 
Naunga mkono hoja , Tulia namkubali Sana huyo mother , ni ujinga wa Hali ya juu kukitoa kichwa kama Tulia alaf uingize mvaa mitepesho na mvuta bangi ,
Tunataka watu wenye matokeo sio porojo
 
Kuna km 30 za lami za Tactic zinakuja
 
Nchi ina utoto mwingi sasa, Wananchi wanapaswa kuamka sasa na kuidai nchi yao na mamlaka ya uamuzi ibaki kwao.

Wanasiasa tunawatukuza saana na kuwafanya wafalme ilihali wao ni watumishi wetu na wanapaswa kuwajibika kwetu.

Tumewapa mamlaka wanasiasa na wote kugeuka kuwa machawa wao na kuleta ushabiki kama wa Simba na Yanga.

Wananchi wanapaswa kuchagua kwa kupima na sio ushabiki kama wa simba na yanga.
 
Pesa alipata wapi
 
Tulia hana mvuto wa kisiasa kabisa ni bora arudi kwenye fani yake ya Sheria. Bila Magufuli alikuwa anapigika mapema sana. Mwaka 2015 Sugu ndio alishika rekodi ya kuwa Mbunge aliyepigiwa kura nyingi na Wananchi kuliko Mbunge yeyote nchini. Magufuli aliharibu sana na aliwadhurumu Wananchi haki ya kumchagua kiongozi wanaempenda.
 
Hiyo inaitwa tishia nyau, jimbo la mbeya Mjini ni la Sugu.
 
Tulia ameona maji marefu pale Mbeya Mjini,Ameamua kugawa nguvu mapemaa,Sasa pasipokujua kuwa amejichimbia kaburi ataona Mbilinyi atakapoingia kwa Jimbo lake,Mbeya inakwenda kuwa strong-hood ya Upinzani Tena.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…