Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 4.
Ngumi na makonde yaliendelea pale huku matusi mazito mazito yakichukua nafasi,kiukweli yule Deborah alikuwa na nguvu sana,alikaweka chini kale kabinti akawa anakasukumia ngumi za kike zisizo kuwa na idadi,sasa yule Ema yeye alipoingia ndani hakutoka nje,ilibidi mimi na huyo jamaa aliyeitwa Jackson tuingilie kati ule ugomvi kuachanisha!.
Deborah alikuwa amechukia sana huku akimporomoshea matusi yule mshikaji wake Ema ambaye hakutaka kabisa kutoka nje!.
Mimi " Debo nisikilize,hebu achana na haya mambo ya ugomvi tuondoke,ni usiku sana sasa hivi"
Debo " Hapana umughaka wewe nenda mimi niache"
Kiukweli alikuwa amejaa sumu sana kwa wakati huo!.
Baada ya kuona lile timbwili haliwezi kuisha muda huo,nilimvuta yule jamaa ambaye aliitwa Jackson nikamwambia amchukue huyo dada aliyekuwa akipigwa ampeleke kwao vinginevyo mambo yangekuwa makubwa.
Mimi "Jack hebu sikia,wewe mchukue huyo demu umpeleke kwao ili hawa wabaki wawili wazungumze yataisha"
Jackson "Unajua huyu demu jamaa amekuja nae hapa sijui kamtoa wapi mi ndo mara ya kwanza namuona na wala si mwanafunzi wa skuli"
Mimi "Hebu mwambie Ema namuita"
Nilitaka kusovu ile ishu ili isiendelee kutupigia kelele pale nimchukue binti wa watu Deborah turudi tulipotoka.
Jackson "Jamaa anasema wewe sepa"
Mimi " Anasema nisepe,nisepe wapi?,umemwambia namuita?"
Jackson "Nimemwambia lakini kasema wewe ndiye umemleta huyu demu wake kumfanyia fujo"
Baada ya jamaa kuniambia vile nikaona kumbe yule Ema ni mjinga wa hali ya juu,mimi kikichonipeleka pale ni funguo na wala si mambo ya kijinga kama alivyodhani,sasa hakutaka kabisa kutoka nje kuja kuongea na mimi aliamua kukatalia ndani.
Sasa nikamwambia Jack amchukue yule binti amtoe waende pembeni ya nyumba wajifanye amempeleka ili iwe rahisi kwa Deborah kutoka pale,kweli!,baada ya muda kupita Deborah alipunguza hasira na nikamwambia tuondoke akawa amekubali lakini wakati tunaondoka alikuwa akimtukana sana Ema matusi ya nguoni!.
Tuliondoka sasa kuishika njia ya kuelekea nyumbani huku nikiamini baada ya sisi kuondoka Jack na yule demu wangerudi maana nilimwambia ajidai anamsindikiza ili kwa debora iwe rahisi kuondoka!.
Deborah "Huyu mjinga atanitambua mimi ni nani,we ngoja uje uone!"
Mimi "Huyo ni mshikaji wako debo msamehe tu,ameteleza"
Deborah "Wewe umekuja juzi tu,huyu mjinga huijui akili yake,mara kibao tu nishamfumania,kuna siku nimemfuma akiwa na rafiki yangu"
Basi ikabidi nifunge bakuli langu ili niendelee kumsikiliza Debo akifunguka kwa hasira.
Deborah "Ema ni mshenzi sana,wewe hujamjua vizuri!,yaani safari hii labda ahame shule lakini vinginevyo atanijua mimi ni nani!"
Basi pamoja na kumtaka amsamehe Ema lakini ilionekana kama natwanga maji kwenye kinu!,baada ya mwendo mrefu nilimfikisha kwao na mimi ikabidi nielekee nyumbani usiku huo.Kiukweli lilikuwa giza totoro na sikuwa na tochi na nilikuwa peku!.
Nilipofika nyumbani,nilichota maji kwenye pipa nikaingia bafuni kuoga,baada ya kuoga niliingia jikoni kuangalia jamaa kama alikuwa amepika lakini nikakuta chakula kimeisha,inavyoonekana alikuwa amepika chakula kinachomtosha yeye mwenyewe akala akamaliza,sasa sikutaka kumtupia lawama maana siku zote mtembezi hula miguu yake!.Ilibidi kwa usiku ule nilale na njaa.
Asubuhi kulipo pambazuka,niliwahi kuamka mida ya saa 12 nikasema niende kule kwenye ile miembe miwili nikatafute kile kitochi kabla watu hawajaanza kupita ile njia wasije kuokota kile kitaa halafu nisiwe na majibu ya kumpa Ba'mdogo!.
Niliondoka hiyo asubuhi kwa kukimbia mdogo mdogo mpaka lile eneo la tukio,nilipofika pale cha kwanza kabla ya yote nilitazama kama bado ile maiti ipo au la!,kitu cha ajabu ule mwili haukuwepo lile eneo!,nilibaki najiuliza ni nani aliuweka pale hiyo usiku lakini nikakosa majibu,mpaka wakati huo nilikuwa siamini kabisa ishu za uchawi!,sema nilikuwaga naogopa kutokana na kusimuliwa kuhusu lile eneo.
Basi nikaanza kutafuta ile tochi bila mafanikio,nilicho ambulia kupata ni zile ndala zangu tu!.Niliwaza ningemwambia nini mzee atakaporudi maana ni lazima angeiulizia ile tochi!.
Baada ya kuitafuta kwa muda na kuikosa ilibidi niondoke kurejea nyumbani,nilipofika nyumbani cha kwanza ilikuwa ni kuingia jikoni na kukoroga uji maana nilikuwa nina njaa ya kufa mtu!.Mpaka wakati huo yule jamaa alikuwa bado hajarudi nyumbani.
Nilipomaliza kunywa uji nikakusanya nguo zangu na kuelekea lamboni kwa ajili ya kufua!.
Nilimaliza kufua mida ya saa 4 asubuhi,sasa wakati naondoka zangu kurudi nyumbani nikamuona demu mmoja alikuwa anafua nguo upande wa wanawake,kiukweli alikuwa na mtungi wa maana ila sura ilikuwa ya baba yake(mbovu).Sikuweza kumfuata maana kule kulikuwa na akina mama wengine wakifua hivyo nikaogopa kwenda,nikasema kama nikimuona siku nyingine ingebidi niimbe nae ili awe poozeo langu hapo kijijini!.
Basi nilipofika nyumbani nikamkuta mshikaji keshafika,sasa ajabu ni kwamba nilipo mpa hai jamaa akanikaushia.
Mimi "Mbona nakupa hai unauchuna?,nini shida?"
Ema "Achana na mimi wewe jamaa,kwani lazima niitikie?"
Kiukweli yale majibu yaliniskitisha sana na nikajiuliza ni kipi ambacho nilimkosea,kama ni jana usiku mimi nilienda kwa ajili ya kufuata ufunguo,na nilikuwa najitahidi sana kumtetea kwa demu wake lakini jamaa alidhani mimi ndiye chanzo cha yote!.
Basi na mimi sikutaka kujikomba kwake ilibidi nikaushe,nilipanga kumsimulia mkasa niliokutana nao usiku lakini kwasababu hakutaka maongezi na mimi ilibidi nikaushe!.
Ilipofika mida ya jioni mzee alirejea kutoka mjini kama kawaida!.
Usiku huo jamaa alianza kutafuta kile kitaa kwa ajili ya matumizi lakini hakutaka kuniuliza maana alikataa kuongea na mimi,sasa na mimi nikawa namchora tu!,yaani alisahau kabisa kama jana yake tu alikuwa amenipa wakati naenda kutazama mpira!.
Sasa nadhani uzalendo ulimshinda akaniuliza.
Ema " Hivi ile tochi iko wapi mbona siioni?"
Mimi "Umetafuta kila sehemu umeikosa?"
Ema "Haionekani"
Mimi " Sijui sasa itakuwa wapi"
Namshukuru Mungu jamaa hakukumbuka kabisa kama jana yake tu alikuwa amenipa halafu yeye akabaki na ile ya Headmaster.
Sasa kwakuwa jamaa alikuwa amezira,hakutaka kabisa stori na mimi na ulipofika muda wa kulala alichukua godoro lilikuwa limechomekwa juu ya mbao za dari akatandika chini akalala,mimi nikalala kitandani kama kawaida!.
Ile shule ilikuwa na madarasa manne pamoja na ofisi ya mkuu wa shule na ofisi ya walimu wengine,yaani kuanzia form 1 hadi form 4 kulikuwa na darasa moja moja,shule nzima ilikuwa na walimu wanne pekee ukiongeza na Headmaster.
Walimu wawili walikuwa wameajiriwa na serikali na walimu wengine wawili walikuwa wanalipwa na kijiji,sasa walimu wote hao wao walikuwa wanakaa kule senta,hapo shuleni tulikuwa tunakaa sisi maana kulikuwa na nyumba moja tu ya Headmaster.
Sasa nakumbuka baada ya kupita wiki kadhaa ndani ya mwezi huo wa 3 mwaka 2004,siku hiyo mimi baada ya kumaliza kula nikaenda zangu kulala,jamaa yeye akabaki sebuleni akiwa anasoma,sasa ilipofika mida ya saa 5 naye akawa amekuja kulala,kama kawaida yake hakutaka kabisa kulala na mimi pale kitandani akawa anatandika chini analala.
Sasa usiku mkubwa nikashitushwa na kelele zikiwa zinaita "Mamaaaaa.......Mamaaaaaaa........Mamaaaaaaaa".
Hizo kelele zikawa zinaita kule madarasani,sasa nikaamka kutazama chini kwenye godoro jamaa sikumuona nikajua uenda atakuwa sebuleni anasoma.
Haukupita muda ba'mdogo nae akawa ameamka na kutoka nje kuja kutuita.
Ba'mdogo "Mnazisikia hizo kelele kama mimi navyosikia?"
Mimi "Ndiyo baba na mimi nimeamka kwasababu ya hizo kelele"
Ba'mdogo "Hebu mwambie Ema anipe hilo panga"
Mimi "Ema hayupo"
Ba'mdogo " Hayupo?,ameenda wapi?"
Mimi "Nimeamka sijamkuta baba"
Ba'mdogo "Ina maana jana hakulala hapa"
Mimi"Alilala baba,sema niliposhituka sijamkuta"
Sasa wakati naendelea kumjibu headmaster zile kelele zikaanza tena
"Mamamaaa.....Mamamaaaaa.....mamamaaaaaa"
Sasa safari hii tulisikia sauti ilikuwa ya Ema na ilisika kile madarasani!,hatukujua ametoka vipi nje maana milango ilikuwa imefungwa na makomeo!