Nisikuchoshe na usinichoshe,tusichoshane
Miaka ya fulani baada ya kumaliza shule ya sekondari,niliamua kwenda kumsalimia Ba'mdogo aliyekuwa mkuu wa shule fulani ya sekondari hapo kwenye hicho kijijini.
Wana kijiji walikuwa wakimpa heshima kubwa Ba'mdogo kwasababu wanafunzi wote waliosoma kwenye ile shule walifaulu kuendelea na elimu ya Sekondari ya upili(Advance),japo shule ile ilikuwa ya kata na kwa mwaka ule nilienda mimi ilikuwa imefaulisha kwa awamu ya kwanza,yaani toka hiyo shule ianzishwe wanafunzi waliokuwa wamefika kidato cha ilikuwa tayari ni mara moja,hivyo nilipofika mimi wale nilowakuta ndo walikuwa wa awamu ya pili.
Sasa kwa mwaka ule wa kwanza wanafunzi wa kidato cha nne walimaliza 12 na wote walifaulu kuendelea Advance tena walienda kwenye shule za vipaji maalumu ikiwemo Ilboru.Sasa wanakijiji kiukweli walimpenda sana Dingi mdogo kwa kujitolea kuwaleta waalimu wa ziada ambao kile kijiji kilikuwa kinawalipa.
Nilipofika nilikuta pale kwa Ba'mdogo kila siku iendayo kwa Mungu ilikuwa inakuja Galoni ya maziwa fresh lita 5, kile kijiji kilikuwa na wafugaji wengi sana wa mifugo ya kila aina! Yaani kumuona mwanakijiji anamiliki ng'ombe elfu 10 ilikuwa kitu cha kawaida,sasa mbali na maziwa, kila Jumapili alikuwa analetewa kuku jogoo mmoja na mwanakijiji.
Ba'mdogo aliwahi kuniambia waliwahi kukaa kikao na wana kijiji wakakubali kila kaya kuwa wanakamua maziwa kulingana na zamu walizokuwa wamewekeana kwa ajili ya mwalimu mkuu ikiwemo kitoweo hicho cha kuku.
Nilipofika mara ya kwanza kwa sababu ya uroho na ulafi, nilikuwa nakunywa yale maziwa kwa wingi kana kwamba kesho hayatokuja mengine,yaani kila niliposikia kiu ya maji mimi nilitwanga maziwa, baadae sasa baada ya kuzoea ilifika sehemu tukawa tunayaangalia na tunaishia kuyamwaga tu maana hakukuwa na wakumpa.
Pale kwa Ba'mdogo baada ya mimi kufika,ni kama nilifanya wapumue maana kazi za hapa na pale nilikuwa nikizifanya mimi, ilikuwa ikifika ijumaa dingi mdogo alikuwa akiondoka kuelekea mjini kwa familia yake na ikifika jumapili jioni alikuwa akilejea.
Sasa kwa wakati huo dingi mdogo alikuwa akiishi na bwana mdogo mmoja alikuwa wa rafiki yake ambaye baada ya kufeli shule mahali fulani alimpatia namba na jina akawa amerudia pale kidato cha pili,hivyo nilipofika mimi tukawa watu watatu.
Japo kulikuwa ni kijijini lakini kulikuwa na maisha fulani ya amani sana,kulikuwa na Lambo kubwa ambalo wanakijiji walikuwa wakijipatia maji ya mahitaji yao hapo. Kwa upande wa umeme ulikuwa bado haujafika na wana kijiji walitumia Solar na Majenereta.
Ilipokuwa ikifika wikiendi nilikuwa ninashuka senta kwa ajili ya kuangalia mpira,wakati huo nilikuwa shabiki wa kutupwa wa Arsenal, ingawaje hivi leo sina mahaba kama hapo zamani kwasababu timu haieleweki nini inafanya. Yaani ilikuwa ni bora nilale na njaa kuliko kwenda kuitazama timu yangu pendwa ya Arsenal.
Kwenye ule ukumbi jamaa alikuwa anatumia jenereta na malipo ilikuwa Tsh 100 kwa wakati ule, sasa lile jenereta lilikuwa likiwashwa wakati wa mechi inapoanza tu ili kuokoa mafuta, yale mambo ya kuangalia uchambuzi wa kina Thomas Mlambo na Robert Marawa yalikuwa hayapo.
Sasa nilikuwaga nikimaliza shughuli zangu hapo nyumbani ikifika saa nane mchana,huyoooo naondoka zangu na kurudi mpaka gemu nihakikishe zimeisha ndo narudi nyumbani. Yule jamaa aliyekuwa hapo nyumbani hakuwa mpenzi wa mpira ila alikuwa mpenzi wa papuchi, yaani alikuwa anatembeza stiki si kwa wanafunzi wenzie tu, hadi wanakijiji.
Kutoka hapo nyumbani hadi ufike senta ilikuwa kilomita 3, kwenda na kurudi inakubidi utembee kilomita sita. Kiukweli kile kijiji hakikuwa na ujambazi wala vibaka, shida ya pale ilikuwa Uchawi!
Aiseeee sijawahi kuona asikwambie mtu.
Inaendelea...
- SEHEMU YA PILI (2)