Tulichomfanya yule mchawi hatakuja kusahau kamwe

Tulichomfanya yule mchawi hatakuja kusahau kamwe

Leta jero .....now tupo nae huku telegram [emoji23][emoji23]
Ni kweli yupo Telegram?
Mbona anatusaliti wadau wake humu?
Kuna jamaa Jana alisema ufanisi wake kazini umepungua kwa sababu ya hii story Sasa akiona kuwa hii story watu wa Telegram washaimaliza atajusikia vibaya sana hahaaaaaaa
 
Sema mwanangu umughaka ulikuwa mvumilivu sana. Yaani nachukia sana mtu aniambie nifanye kitu bila kuniambia ni nini.

Sema bamdogo ameyakanyaga monica ataanza na mamduchu wetu.
 
Sio kwa ubaya najua na nyie mmeona Speed ya Episode ya 1-10 ilikua nzuri mtu anaweka tu.

Ila sijui ni katabia ka watu humu jukwaani mtu anaanza vizuri once akishakua na traffic ndio anaanza kunata na dharula zinaanza kumuandama. Mara mbuzi wangu kala mazao ya watu, mara mtoto kameza shoka ili mradi tu kunata.
 
Sio kwa ubaya najua na nyie mmeona Speed ya Episode ya 1-10 ilikua nzuri mtu anaweka tu.

Ila sijui ni katabia ka watu humu jukwaani mtu anaanza vizuri once akishakua na traffic ndio anaanza kunata na dharula zinaanza kumuandama. Mara mbuzi wangu kala mazao ya watu, mara mtoto kameza shoka ili mradi tu kunata.
Najuta kuusoma huu uzi😭😭 imebaki mateso
 
Sio kwa ubaya najua na nyie mmeona Speed ya Episode ya 1-10 ilikua nzuri mtu anaweka tu.

Ila sijui ni katabia ka watu humu jukwaani mtu anaanza vizuri once akishakua na traffic ndio anaanza kunata na dharula zinaanza kumuandama. Mara mbuzi wangu kala mazao ya watu, mara mtoto kameza shoka ili mradi tu kunata.
🤣🤣 mbuzi kameza shoka
 
Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 13.


Niliamka taratibu nikajifanya kumshitua jamaa ili nione kama alikuwa akisikia,nilitaka kama angenisikia basi nimwambie naelekea chooni!,sasa kwakuwa alikuwa amelala usingizi wa pono,niliamka nikafungua mlango taratibu kisha nikairudishia!.Nilifungua mlango wa nje taratibu nikatoka nikakuta yule binti Monica akiwa nje ananisubiri!.


Monica "Yaani muda huu mlikuwa mmelala?"

Mimi "Kwani saa ngapi sasa?"

Monica "Bado mapema sana"

Sasa muda huo ninazungumza naye ilikuwa yapata mida ya saa 5 usiku,sikuwa na saa lakini kwa makadirio sisi tuliingia kulala mida ya saa 3 usiku na baada ya yeye kuja ilikuwa imepita muda kidogo!.
Sasa kwakuwa nilikuwa tayari nishakuwa na hamu na papuchi,sikutaka kabisa kuwaza umbali tutakao tembea kwenda kwao,cha msingi ni mimi kufika na kumcharaza stiki za kutosha na kurudi mapema nyumbani.Kwakuwa mpaka muda huo hapo kijijini sikuwa kabisa na demu mwingine wa kuzugia ilibidi niwe mpole tu kwa yule binti ili angalau niwe napooza njaa ya mashine!.

Basi tulianza kutembea kwa haraka huku nikiwa nimemshika kiuno kana kwamba atanitoroka!.

Monica "Mimi nakupenda sana wewe umughaka,yaani sasa hivi najikuta tu nakupenda"

Mimi "Lakini Moni mimi na wewe tunaiba tu,Ema akijua najua tutakosana"

Monica "Wewe achana nae huyo,mbona yeye anatembea na Deborah"

Monica "Huyo mjinga nitamkomesha aliniambia atanioa kumbe alitaka kupata anachokitaka kwangu halafu aniletee dharau,hanijui vizuri binti Makoye".

Aliendelea kusema "Nilikwambia leo nyumbani kuna ngoma za mwana lemi,ndo maana nimekuja kukuchukua"

Mimi "Ngoma za mwana lemi ndiyo ngoma gani?"

Monica "Wewe twende tu utaona"

Monica "Tukifika nyumbani utafanya kila nitakachokuambia lakini,sawa?"

Mimi "Sawa"

Sasa mwanaume nikadhani ile kuniambia nitafanya kila atakachosema ilikuwa ni kumbadili kila style wakati wa mizaguamuano,moyoni nilifurahi sana na nikawa nina shauku ya kufika nyumbani kwao haraka ili nikaikung'ute papuchi mpaka ichakae!.

Mimi "Mama yako yupo?"

Monica "Yupo ila atakuwa bize kwenye ngoma".

Basi tulitembea kwa dakika kadhaa tu tukawa tumekaribia nyumbani kwao,nilipata mshangao sana kwakuwa haikuwa kawaida kwasababu nyumbani kwao ilikuwa mbali sana!,sasa nikawa najiuliza au kwasababu ni usiku na hakuna kashikashi njiani ndo maana tumefika mapema?,niliwaza pia siku ile nilivyokutana na Monica pale kwenye viwanja vya mnada na namna tulivyokwenda kwao haikuchukua muda mrefu,nilidhani uenda kwasababu ilikuwa usiku hivyo kujikuta unatembea kwa haraka kwasababu hakuna jua wala nini!.

Sikuwa kabisa na mawazo uenda yule binti anaweza kufanya namna yeyote kwasababu hakuwahi kunionyesha jambo lolote baya nala kutisha mpaka nimtilie shaka,isipokuwa ni ile siku moja tu ambayo nilimuona pale lamboni akichuma yale majani ya kutengeneza majamvi ndipo kama nilishangaa namna alivyotokea mbele yangu ghafla!.Basi nikajipa moyo kwasababu alikuwa ananipenda hata kama angekuwa ni mbaya asingenifanyia ubaya mimi.
Kabla ya kwenda kuingia ndani,aliniambia nimsubiri kwanza anarudi.Aliondoka akaenda akazunguka nyuma ya nyumba yao ambako kulikuwa na shamba la mihogo akaingia ndani!.Nilimsubiri pale kwa takribani dakika 5 hivi akawa amekuja na kimfuko cha rambo kilichokuwa kimefungwa ambacho sikufahamu ndani kulikuwa na nini!.

Monica "Chuchumaa chini"

Basi nikachuchuma chini,akakifungua kila kimfuko kisha akatoa vijifuko vingi vingi vilivyokuwa vimefungwa kwa kukazwa sana!.Sikumuuliza chochote nikawa nabaki kumuangalia anataka kufanya jambo gani.

Sasa kwakuwa lilikuwa giza totoro,sikuweza kuona mle ndani ya tule tujifuko tudogo tudogo kulikuwa na kitu gani.

Monica "Kama nilivyokwambia leo hapa nyumbani kuna ngoma,nataka nikupake hii dawa ili wakati wa ngoma usije kuonekana na wacheza ngoma wanaweza kukufanya kitu kibaya na mimi nitaadhibiwa"

Basi akilini mwangu nikasema uenda alitaka kabla ya mizagamuano tukacheze ngoma ya kisukuma iliyoitwa "Mwana lemi" kama alivyokuwa ameniambia hapo awali.

Basi alianza kunipaka ile dawa usoni,miguuni na mikononi na kuna nyingine akawa amenipa ili niirambe.Baada ya lile zoezi akaniambia tuondoke twende ndani!.Safari hii wakati tunaelekea kwenye kile kinyumba cha nyasi alichokuwa akilala Monica tulizunguka kwa nyuma ambako ilibidi kukanyaga matuta ya mihogo na kuingia ndani,ile siku ya kwanza kulala hapo nakumbuka tulipitia moja kwa moja mbele ya nyumba,ila safari hii imekuwa tofauti!.

Nilipofika ndani Monica aliniambia nikae kwa kutulia na kila atakachukuwa akiniambia basi nifanye.Alinisogelea karibu akanivua nguo zote nikabaki mtupu,alipomaliza alianza na yeye kuvua nguo zote,kwakuwa mle ndani kulikuwa na giza totoro hakuna aliyemuona mwenzie kiufasaha,sasa sikujua kama yeye alikuwa akiniona ama la!,alianza kunipaka dawa ambayo sikuitambua mwili mzima na alipomaliza alinipatia mkononi na mimi akasema nimpake,sasa wakati nampaka kufika kiunoni nikakuta amevaa shanga!,nilishangaa sana siku hiyo kumuona ana shanga kiunoni kwasababu siku ile ya kwanza hakuwa na shanga kabisa!.
Basi nikaendelea kumpaka ile dawa kuzunguka mwili mzima,wakati huo abdala kichwa wazi alikuwa amesimama akionyesha kuwa na kiu ya maji ya mdimu!.

Baada ya kumaliza lile zoezi,Monica akawa amenitaka nikae kwenye godoro.

Monica "Umughaka mimi nakupenda sana na nia yangu ni kukusaidia"

Mimi "Kunisaidia na nini Moni?"

Monica "Wewe unadhani uko salama?,hivi huwa hujiulizi kwanini wewe hayakukuti?"

Mimi "Ma nini ambayo hayanikuti"

Monica "Yaani wewe nae umezidi utahira,pamoja na kukueleza tu hujiongezi!"

Aliendelea "Subiri utajionea ila naomba usije kupiga kelele,sawa?"

Mimi "Sawa"

Basi wakati tukiwa mle ndani tukiongea,ghafla nikaona miale ya moto ikitokea nje,ilionekana kuna moto ulikuwa umewashwa,Sasa Monica akanifanyia ishara ya kwamba nifunge domo langu na nisishituke!.Baada ya muda nikaanza kusikia ngoma zinapigwa kwa nguvu huku sauti za kina mama na wanaume wakiwa wanaimba kwa kisukuma.

Zile ngoma zikaanza kukolea huku nikisikia vishindo vya watu kama wakiruka na kucheza!.Sasa baada muda kupita kidogo,Monica akanifanyia ishara ya kwamba nisimame nimsogelee alipokuwa,niliposogea ndipo akaniambia nichungulie kwenye upenyo wa ule mlango wa bati!.Sasa kile kinyumba kilivyokuwa kimejengwa kilikuwa cha mviringo kama simtank(nadhani waliokulia vijijini watakuwa wanazifahamu nyumba hizo),sasa kutokana na kile kinyumba kilivyokuwa kimejengwa,mlango wa kile kinyumba hata kama ungefungwaje,kwa juu kulikuwa na uwazi mkubwa uliowezesha kuchungulia nje na kuona kwa uzuri!.

Basi nikachungulia nje nikaona moto mkubwa mno ukiwa umewashwa pale mbele ya nyumba yao Monica,pia nikawaona watu wake kwa waume wakiwa uchi kama walivyozaliwa(uchi wa mnyama)wakicheza kwa kuzunguka mduara,mpiga ngoma alikuwa mwanaume ambaye yeye alikuwa pembeni kabisa,sasa wakati wakiwa wanazunguka ule mduara huku wakiimba ngoma,nikamuona mama yake Monica naye akiwa mmoja wao,nilipoendelea kutazama vizuri nikamuona na yule mzee ambaye nimewahi kukutana naye jioni wakati natoka Senta akanisalimia kisha akaniambia nimsalimie headmaster,nilipomuuliza jina akaniambia anaitwa Makono.

Pia ni huyu huyu mzee wakati wa kikao pale shuleni baada ya lile sakata la Ema na Maza kukutwa wamelala darasani ndiye aliyekuwa akichangia na akisema mambo ya ushirikina hayakuwepo hapo Kjijini.

Nikabaki nimekodoa macho na nikawa kimya kabisa,sasa baada ya zile ngoma kupigwa kwa sana na wao kuuzunguka ule moto,ghafla kuna mzee akapiga kelele kwa kisukuma akisema "Bhebheeeeeeee",kisha mpiga ngoma akaacha kupiga ile ngoma na watu wote wakasimama.
Heheeee..hatari tupu.

#MaendeleoHayanaChama
 
Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 14.




Kila mcheza ngoma alisimama ghafla na kumtizama yule mzee ambaye ilionekana kabisa alikuwa kiongozi wao.Baada ya hapo alinyoosha mkono juu akiwa ameshika usinga(mkia wa mnyama)ambao sikuweza kufahamu ulikuwa wa mnyama pori au mnyama wa kufugwa!.

Alipoteremsha mkono chini niliona watu wote wameweka mikono mbele kuonyesha unyenyekevu huku vichwa vikitazama chini.Sasa yule mzee alianza kuongea kwa sauti kubwa mno!.

Mzee alisema "Ng'wana Charles"

Aliendelea "Ng'wana ndekeja"

Baada ya kusema hivyo nikaona ananyoosha usinga kuwapa ishara hao aliowaita wasogee mbele,sasa nikaona wazee wawili wamesogea mbele huku wakiwa wameinamisha nyuso chini na mikono imewekwa mbele kuashiria unyenyekevu wa hali ya juu!.

Mzee akasema "Ng'wenagi umnho ng'wenuyo aha"

Basi wale wazee waliondoka na kuingia kwenye ile nyumba ya mama yake Monica,hawakuchukua muda wakawa wametoka ndani huku wakiwa wamembeba mtu ambaye sikumuona kwa haraka,sasa baada ya kumfikisha yule mtu na kumbwaga pale kando ya ule moto ndipo nikamuona vizuri nikawa nimemtambua!,alikuwa ni mzee ambaye alijinasibu ni mganga aliyekuja pale nyumbani kuweka zindiko na kutupiga chale za kutosha!.

Basi yule mzee ambaye ilionekana ndiye mkubwa pale akawa toa amri tena ya kuanza kupiga ngoma na kucheza!,sasa wakati wanacheza kwa kuzunguka ule moto,akajitokeza mama mmoja ambaye alikuwa amejifunga shanga kiunoni na kiremba cheusi kichwani huku mkononi akiwa ameshika kisu!,sasa akamsogelea yule mzee ambaye alikuwa akishanga shangaa kama tahira pale chini,yule mama akafika akamkamata kichwa akaanza kumyoa nywele!.

Wakati mambo yote hayo yanaendelea,mimi na Monica tupo tunachungulia kwenye ule upenyo wa mlango na Monica alinizuia kabisa kutopiga kelele!.

Sasa baada ya lile tukio la kumnyoa yule mzee nywele kukamilika,yule mama alichukua zile nywele akaziweka kwenye kitu kama sahani halafu akamkabidhi yule ambaye alionekana ni kiongozi,sasa wakati anamkabidhi kama kawaida uso uliinama chini kuashiria unyenyekevu!.Baada ya hapo yule mama akaanza kumvua yule mzee nguo zake zote!,alipomaliza aliinama chini kwenye akachukua vitu ambavyo sikuvifahamu akaanza kumpaka yule mzee!.Baada ya kumaliza lile tukio la kumpaka yule mzee vitu visisvyo julikana,akaondoka kinyume nyume kurudi kwenye mstari kuuungana na wenzie kuendelea kucheza ngoma.

Sasa haukupita muda yule mzee tena akatoa ishara ile ngoma ikasitishwa!,baada ya hapo ilikuwa kitendo cha kufumba na kufumbua wakawa wametoweka pale kwenye lile eneo na ghafla kukawa na giza kuu!,nilitaka kufahamu kiliendelea nini na hivyo ikabidi nimuulize Monica.

Mimi "Mbona hawaonekani?"

Monica "Unataka nikupeleke walipoelekea?"

Mimi "Hapana"

Monica "Nakupenda wewe sana ndiyo maana nimekuleta ujionee mwenyewe"

Monica "Mimi nitakulinda wala usiogope"

Aliendelea kusema "Wameelekea kwenye sherehe za kula nyama"

Monica "Ile miembe miwili mikubwa ya kwenye ile njia ambayo tumekutana si unaikumbuka?"

Mimi "Ndiyo"

Monica "Ndo wako hapo"

Mimi "Sasa hapa wameondokaje?"

Monica "wewe bado mdogo ukikuwa utaacha kuuliza uliza maswali"

Sasa nilikuwa nashangaa binti anayeniambia mimi mdogo nabaki kumshangaa kwasababu ulikuwa ukiniangalia mimi na yeye utajua kabisa yeye ndiye mdogo!.

Monica "Halafu wewe una mizimu mikali sana ndiyo maana nataka uwe mume wangu"

Mimi "Mizimu mikali?,mizimu mikali kivipi?"

Monica "Umekuwa ukiwasumbua sana wanapokuwa wakila nyama zao"

Nikashituka sana nikabaki nashangaa mle ndani ambako mpaka muda huo kulikuwa na giza totoro!.

Monica "Unakumbuka siku unapita pale kwenye miembe usiku uliona nini?"

Mimi "Nakumbuka kuna siku nilikuwa natoka senta kuangalia mpira nikaona moto unawaka kwenye ile miembe"

Monica "Achana na mambo ya moto,wewe hukuwahi kuona mtu pale?"

Aisee,sasa nikawa najiuliza huyu binti matukio yote hayo yeye alionaje?,kiukweli nilianza kuingia uoga ila akawa ananisihi ya kwamba nisiogope na yeye yupo kwa ajili ya kunisaidia!.

Monica "Yule mtu uliyemuona siku ile aliliwa nyama,sasa wewe umekuwa ukiwasumbua kupita ile njia kwasababu hakuna mtu anayepita ile njia usiku kama ule".

Aliendelea kusema "Kwa ujasiri ulionao waliona wakujaribu kuona kama unawaona na ndiyo maana walikutega na kukutisha na ulivyotishika na kukimbia wakaona kumbe huna lolote"

Mimi "Sasa nawatesaje?"

Monica "Pale kwenu ni wewe ndiye ambaye huwezekaniki na sijui kwanini,wewe unanyota nzuri mno"

Mimi "Yule mganga amefanya kosa gani"

Monica "Yule ni mjeuri,anaenda kuliwa nyama".


Akaendelea kusema "Kuna siku mama yangu alienda kusenya kuni na mlikutana njiani ukamsaidia zile kuni,hivyo mama yangu akakupenda sana"

Mimi "Mbona sikumbuki siku ambayo nimebeba kuni za mama yako?"

Monica "Wewe bado mtoto mdogo nimekwambia acha maswali utaelewa tu".


Kiukweli nilikuwa ninawaza na kujiuliza sana lakini nakosa majibu!,ndipo sasa nikajua uenda matukio mengi pale nyumbani yalikuwa yanasababishwa na hilo kosi hatari lilikuwa likicheza ngoma,sikutaka kumwambia mama yake ni mchawi ingawa nilimshuhudia kwa macho yangu,nilidhani uenda ningemwambia kuhusu mama yake angenibadirikia mle ndani na nikaipata freshi,sikutaka kabisa kutengeneza matatizo!.

Baada ya maongezi ya muda mrefu mizagamuano ikachukua nafasi!,sasa nikawa nimemwambia Monica inapaswa baada ya mizagamuano ikifika saa 10 usiku anisindikize kurudi nyumbani ili asije akajua mtu yeyote kwamba nilitoka usiku.

Monica "Nalekotogwa natokoreka"

Mimi "Ndiyo nini?"

Monica "Wewe naye,utajifunza lini kisukuma!"

Monica "Nakwambia nakupenda na sitokuacha"

Basi sikutaka kumjibu na mimi akili yangu haikuwa kwake kabisa,kilichokuwa kinanipeleka kwake ni kumpatia maji ya uzima wa milele abdala kichwa wazi ili asihangaike na kiu.
Basi baada ya kasi ya mizagamuano ni kama Monica alipitiwa na usingizi,mimi sikuweza kabisa kupata usingizi kwasababu ya kile nilichokuwa nimetoka kukishuhudia pale!.

Sasa baada ya muda kupita nikiwa natafakari huku usingizi ukianza kunipitia,ghafla nikasikia kishindo kikubwa nyuma ya ile nyumba tulimolala!,sasa nikajaribu kupeleka mkono ili nimpapase Monica ashituke ili na yeye asikie lakini hakukuwa na mtu kwenye godoro!.

Nilikurupuka nikaanza kupiga kelele za uoga kama mwehu!
Lekaji gete.

#MaendeleoHayanaChama
 
Back
Top Bottom