Tulichomfanya yule mchawi hatakuja kusahau kamwe

Tulichomfanya yule mchawi hatakuja kusahau kamwe

Back to the story,
Hata Mimi sija mwelewa pale anasema baba yake angempiga na asingesomeshwa shule na angekua mchunga ng'ombe endapo baba yake angejua amelala kwa Monica....

Huyu anasoma saa ngapi wkt anauza miwa?
Eps 01
UMUGHAKA ni mhitimu wa shule ya upili (sekondari), baada ya kuhitimu vidato vyake aliamua kwenda kumsalimu baba yake mdogo ambaye ni mkuu wa shule moja iliyopo usukumani.

Mpaka kufikia Eps 18 UMUGHAKA bado inaonekana ni mtu ambaye aidha anasubiri matokeo ama anasubiri kuendelea na masomo kwahyo hofu yake ilikuwa ni kwamba endapo baba yake mzazi ( ambaye ni kaka wa mkuu wa shule) ikitokea akapata taarifa hizo zingefanya asimsomeshe( yaani asimpe mahitaji ya shule muda wa kurudi shule utakapofika) badala yake akachunge ng'ombe.

Natumaini nitakua nimempunguzia mtunzi muda wa kutype, ili kuwaelewesha
 
Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 18.



Kiukweli nilikuwa nimechukia sana namna nilivyodharirishwa pale shuleni mbele ya wanafunzi!,sikutaka kuonekana mkorofi na mkaidi,nilifanya kila nilichoambiwa ili mambo mengine yapite!,niliona angalau Ba'mdogo aniadhibu kuliko taarifa za kulala nje ningemfikia baba yangu hakika angeniua kwa kipigo na shule angeweza kuacha kunisomesha nikawa mchunga ng'ombe!.Japo nilifanya kosa la kulala nje bila taarifa lakini nilidhani ile adhabu ya kudharirishwa haikufaa hata kidogo na ilijaa uonevu mkubwa!.

Basi nilianza kutembea kutoka hapo Senta kuelekea nyumbani huku kile kichwa cha cherehani nikiwa nimejitwisha kichwani,kiukweli nilichukia sana lakini niliamua kujikaza mtoto wa kiumwe,niliamini hayo ni mambo ya kawaida tu na yangepita!.Kile kichwa cha cherehani hakikuwa chepesi kama nilivyodhani na ilipelekea nikawa nafika sehemu najitua kichwani nashikiria kwa mikono miwili lakini bado haikusaidia,kwahiyo nilichokifanya ilikuwa nakiweka begani angalau nikawa naona kuna unafuu!

Nilifika nyumbani nikiwa nimechoka sana na kwakweli kuanzia siku hiyo,mimi na Ema tulikuwa kama Paka na Panya,sikutaka kabisa jamaa aniambie chochote wala kunisogelea kwasababu nilimuona ni mnafiki!,mara kibao tu yeye nilikuwa nikimtunzia siri zake lakini jamaa yeye za kwangu hakutaka kabisa kuziweka moyoni.Kitendo cha kumwambia Ba'mdogo nilikuwa natembea na binti Monica tena mbele ya wanafunzi kilifanya nikamchukia sana jamaa!,na nilichoamua ni kwamba kama mbwai na iwe mbwai!.

Haikupita muda Maza mdogo naye akawa ametoka senta,kama kawaida yeye alikuwa akitoka senta alikuwa anaingia kuoga na kusubiri kula,wa kupika sana sana nilikuwaga mimi maana Ema nae alikuwa anajifanya kusoma kila alipokuwa akitoka shule,sasa nilikuwaga najiongeza tu kuingia jikoni kupika ili kuepuka matusi ya Ba'mdogo.
Siku hiyo nilikuwa nimechoka sana na nilikuwa nanuka jasho kwasababu ya zile kazi kuanzia asubuhi hadi ile usiku lakini sikuweza kuyasogelea maji kwasababu niliambiwa na Monica na akanionya nisiguse maji!.

Siku hiyo nililala kwa uchovu sana,namshukuru Mungu palipo pambazuka niliamka nikajiandaa kuondoka zangu senta,sasa nilichofanya nikupiga mswaki tu na kubadili nguo,sikutaka kabisa hata kunawa uso,nilipomaliza niliingia ndani kuwasalimia Headmaster na mkewe!.

Maza mdogo "Wewe unaenda halafu hicho kichwa cha cherehani nani atakipeleka?"

Nikawa kimya kwa muda huku nikiwa natafakari nini cha kujibu!.

Headmaster "Kwani kichwa cha cherehani sikuhizi unakileta nyumbani?"

Maza mdogo "Juzi sinilikwambia wanasema yule mama Mayala aliwahi kuibiwa kichwa cha cherehani pale kibandani kwake,unadhani chanzo cha Mama Mayala kuacha kushona ni nini?"

Headmaster "Sasa kwanini usiwe unamuomba mama Rebecca unakiacha pale nyumbani kwake kuliko kupata kazi ya kukileta huku!".

Maza mdogo "Ngoja nitajaribu kuongea nae!".

Headmaster "Wewe nenda uwahi kwenye shughuli zako bhana!"

Maza mdogo "Sasa nani atanisaidia kukipeleka senta"

Headmaster "Utakamata hapo mwananfunzi akusaidie"

Sasa mimi sikutaka kabisa kuonekana uenda nilichukia kukibeba kile kichwa,niliamua kujikaza na kumwambia ningekifata baada ya kupeleka miwa senta.

Mimi "Haina shida mama ngoja nikachukue miwa nipeleke senta halafu narudi kukichukua".

Maza mdogo "Sawa,uwahi sasa"

Sasa nilidhani uenda Headmaster alivyokuwa amemshauri ya kwamba angekamata pale shuleni mwanafunzi amsaidie kubeba kile kichwa na kukipeleka Senta angekubaliana nae lakini haikuwa hivyo,kitendo cha kuniambia niwahi kurudi kukibeba ilionyesha kabisa alifurahishwa na mimi kwenda senta na kurudi kukibeba!.Basi sikuwa na hiyana mtoto wa kiume nikaondoka zangu kuelekea kwenye mashamba ya mzee Masumbuko kwa ajili kufata miwa kama kawaida,ingawaje miwa iliyokuwepo haikuisha ila niliona ni heri nikakusanya ikawa mingi ili inipunguzie safari ya kila siku kuamka asubuhi na mapema kisa kuwahi miwa!.

Nilipofikisha ile miwa pale senta niliibwaga chini nikaondoka zangu kurejea nyumbani kwa kukimbia ili kuwahi kurudi!,sasa kuna sehemu nilifika nikamuona dogo mmoja akiwa kwa mbele kabeba kile kichwa cha cherehani huku Maza mdogo akiwa nyuma yake,nilipowafikia nilimwambia dogo anipe kile kichwa nimsaidie na yeye arudi shule!.

Nilijifanya kuchangamka na kutabasamu kiunafiki lakini kiuweli nilikuwa nimechukia sana,nikawa najiuliza kama alikuwa anajua angempatia mwanafunzi amsaidie kubeba kwanini alitaka nirudi tena?,kama kawaida yangu sikutaka maneno na mtu nikaamua kufunga bakuli langu ili mwanaharamu apite.Wakati huo kiukweli nilikuwa nimeanza kupoteza nuru ya muonekano wangu kwasababu ya kushinda kule senta wakati mwingine sili kabisa mchana na chakula nilikuwa nakutana nacho usiku tu!,mara nyingi nikiwa pale senta nilikuwa nashindia sana miwa!.

Tulifanikiwa kufika senta na nikakipeleka kile kichwa kwenye kibanda alichokuwa akishonea na mimi kwenda mpaka kwa yule mama ambaye nilikuwa nikilaza ile miwa,niliichukua nikaenda kuinganisha na ile niliyokuwa nimekuja nayo na kuanza kuuza!.Namshukuru Mungu siku hiyo niliuza sana ile miwa,japo haikuisha lakini mpaka kufika mida ya saa 10 alasiri ikawa imepungua kwa kiasi kikubwa!
Sasa nikiwa naendelea kuuza miwa yangu pale,kwa mbali nikamuona yule binti Mwise akiwa na binti mmoja wakiwa wamevaa sketi za shule na tisheti za kawaida wakiwa wanakuja hapo senta, sikufahamu kilichokuwa kimewaleta uenda walifata mahitaji kama watu wengine!.

Yule binti kiukweli ndiye alikuwa binti wa kwanza kwa hapo kijijini kuumiza na kuutesa moyo wangu,nilikuwa nampenda na kumtamani sana kutokana na shepu yake nzuri!,ila baada ya kuanza kutembea na Monica kiukweli upendo na matamanio yangu kwake yakaanza kupungua kwa kasi ya ajabu!.Walipofika karibu waliingia kwenye duka moja wakanunua kilichowaleta kisha wakatoka wakawa wanaelekea kwenye vibanda na maduka ya mbele ambako huko pia ndiko mama mdogo anakofanyia shughuli zake,sasa baada ya kugeuka na kutazama uelekeo niliokuwepo mimi,nikampiga mkono kwa ishara ya kwamba aje!.

Mwise "Narudi!"

Kwakuwa aliniambia anarudi nikasema ngoja nisubiri.Safari hii sikutaka kabisa kuwa na kimuhe muhe kwasababu sikuweza kujificha na ile biashara yangu na yeye alifahamu kabisa nilikuwa muuza miwa!,niliamini kama ni kumpata basi ningempata tu na kama ni kumkosa basi ningemkosa vilevile!.

Haukupita muda wakawa wanarudi na huyo mwenzie,sasa alipofika pale kwenye eneo langu la biashara akaanza kama kuonyesha nyodo na dharau.

Mwise "Nionjeshe muwa rafiki yangu!"

Mimi "Kwahiyo mimi leo nimekuwa rafiki yako?"

Mwise "Jamani!,kwani kuna ubaya wewe kuwa rafiki yangu?"

Basi nikamkatia pingili mbili za muwa yeye pamoja na mwenzie!,basi wakawa wanazungumza na huyo rafiki yake maneno ya kisukuma huku wakicheka kwa kicheko cha kichini chini!,kiukweli walikuwa wanikiteta kwa kisukuma na ishu kubwa walikuwa wakizungumzia zile stiki nilizokuwa nimelambwa na Headmaster mbele ya wanafunzi!,wao walidhani siwaelewi lakini hata kama sikuelewa kisukuma vizuri mtu alikuwa akiteta inafahamika kabisa!.

Walipomaliza kukwangua kwangua miwa kwa kisu akawa ameniambia wanaondoka kuwahi kurudi nyumbani,nikawa nimemuomba anivumilie angalau kwa dakika mbili nizungumze nae!,sasa yule mwenzake akawa amemwambia atamkuta mbele!.

Mwise "Sasa na wewe unaniacha nyanoko"

Mwenzie "Utanikuta mbele bhana"

Mwise "Mmh!,niambie mi nina haraka"

Mwise "Kwahiyo Mwise Ombi langu vipi lakini?"

Mwise "Ombi gani tena jamani"

Mimi "Kwani mara ya mwisho mimi na wewe tuliongea nini?".

Mwise "Siulianimbia unanipenda,nashukuru kwa kunipenda"

Mimi "Usinifanyie hivyo Mwise"

Mwise "Wewe si unaye mwanamke wako"

Mimi "Mwanamke gani tena jamani!?"

Mwise "Wewe ema kaniambia habari zako nyingi tu!,kumbe ulikuwa tu unataka unilale uniache"

Mimi "Daaah!,hebu achana na mambo ya Ema Mwise,Ema anashida kubwa na wewe yule unamfahamu akili yake".

Mwise "Mimi nachelewa bhana,kesho!"

Basi yule binti alianza kukimbia kumfuata mwenzie aliyekuwa akimsubiria.Niliamini kabisa kwa kilichotekea pale shule ukichanganya na uongo wa Ema,haikuwa rahisi mimi kumpata tena yule binti.Niliamua kujipa moyo ya kwamba mademu mabaya siku zote ndiyo yanayoringa lakini kuna muda bado nilikuwa nikifikiria kiuno cha yule binti na kuwaza kinavyo chakatwa na wanaume wengine,kiukweli nilikuwa naumia sana!.

Sikuwa na namna ilibidi niwe tu mpole ili maisha yasonge!.

Baada ya kukamilisha siku ya uuzaji wa miwa niliamua kurudi nyumbani na namshukuru Mungu safari hii sikurudi na kichwa cha cherehani kwasababu maza mdogo alipata pa kukiweka hapo senta.

Sasa nilifika nyumbani mida ya saa 1 usiku,nilielekea lamboni ile usiku kuchota maji ili nije nioge kwasababu nilikuwa sijaoga tangu jana yake!,sasa nilipotoka bafuni kuoga,nikawa nimeingia ndani kwa ajili ya kupaka mafuta!,sasa wakati napaka mafuta nikasikia kuna mtu ananipiga piga mgongoni kwa mkono akiashiria nigeuke!,sasa ile nimegeuka nikawa nimekutana na Monica uso kwa uso!.

Kiukweli nilishituka sana ila akanifanyia ishara ya kidole mdomoni akinitaka nisipige kelele wala kuongea!.

Mimi "Monica kuna nini mbona huko humu"

Monica "Vaa nguo tuondoke"

Mimi "Tuondoke twende wapi tena!?"

Monica "wewe vaa twende"

Mimi "Tunarudi lakini?,maana mwenzio jana jana nimepigwa kwasababu yako"

Monica "Hatuendi mbali tutakuwa nje hapo"

Basi baada ya kuvaa nguo,Monica akawa amenishika mkono na ghafla tukawa nje ya nyumba kwa pembeni kidogo.

Monica "Tusogee pale kwenye lile jiwe!"

Baada ya kufika pale kwenye lile jiwe akanitaka tukae pale na kuna watu tuwasubiri walikuwa wanakuja!.
Katika EPS zote, hii niliiisubiri kwa hamu na kwa muda mrefu sana, na nimeisoma kwa muda mfupi sana.

Ama kweli, KUSUBIRI KUNYONGWA, NI MATESO KULIKO HATA KUNYONGWA KWENYEWE!
 
Kabla hujaandika uwe unasoma ukaelewa. Inaonekana hukuwa na akili au uelewa ndo maana unabisha na kutoa mifano ambayo haiendani. Jifunze to be calm. read,understand and then answer accordingly. You , teenagers nowdays dont take time to think before doing anything. Look before you leap.

Look before you leap. Na bado tunakosea ku look za uso tuu [emoji3][emoji3]
 
Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 18.



Kiukweli nilikuwa nimechukia sana namna nilivyodharirishwa pale shuleni mbele ya wanafunzi!,sikutaka kuonekana mkorofi na mkaidi,nilifanya kila nilichoambiwa ili mambo mengine yapite!,niliona angalau Ba'mdogo aniadhibu kuliko taarifa za kulala nje ningemfikia baba yangu hakika angeniua kwa kipigo na shule angeweza kuacha kunisomesha nikawa mchunga ng'ombe!.Japo nilifanya kosa la kulala nje bila taarifa lakini nilidhani ile adhabu ya kudharirishwa haikufaa hata kidogo na ilijaa uonevu mkubwa!.

Basi nilianza kutembea kutoka hapo Senta kuelekea nyumbani huku kile kichwa cha cherehani nikiwa nimejitwisha kichwani,kiukweli nilichukia sana lakini niliamua kujikaza mtoto wa kiumwe,niliamini hayo ni mambo ya kawaida tu na yangepita!.Kile kichwa cha cherehani hakikuwa chepesi kama nilivyodhani na ilipelekea nikawa nafika sehemu najitua kichwani nashikiria kwa mikono miwili lakini bado haikusaidia,kwahiyo nilichokifanya ilikuwa nakiweka begani angalau nikawa naona kuna unafuu!

Nilifika nyumbani nikiwa nimechoka sana na kwakweli kuanzia siku hiyo,mimi na Ema tulikuwa kama Paka na Panya,sikutaka kabisa jamaa aniambie chochote wala kunisogelea kwasababu nilimuona ni mnafiki!,mara kibao tu yeye nilikuwa nikimtunzia siri zake lakini jamaa yeye za kwangu hakutaka kabisa kuziweka moyoni.Kitendo cha kumwambia Ba'mdogo nilikuwa natembea na binti Monica tena mbele ya wanafunzi kilifanya nikamchukia sana jamaa!,na nilichoamua ni kwamba kama mbwai na iwe mbwai!.

Haikupita muda Maza mdogo naye akawa ametoka senta,kama kawaida yeye alikuwa akitoka senta alikuwa anaingia kuoga na kusubiri kula,wa kupika sana sana nilikuwaga mimi maana Ema nae alikuwa anajifanya kusoma kila alipokuwa akitoka shule,sasa nilikuwaga najiongeza tu kuingia jikoni kupika ili kuepuka matusi ya Ba'mdogo.
Siku hiyo nilikuwa nimechoka sana na nilikuwa nanuka jasho kwasababu ya zile kazi kuanzia asubuhi hadi ile usiku lakini sikuweza kuyasogelea maji kwasababu niliambiwa na Monica na akanionya nisiguse maji!.

Siku hiyo nililala kwa uchovu sana,namshukuru Mungu palipo pambazuka niliamka nikajiandaa kuondoka zangu senta,sasa nilichofanya nikupiga mswaki tu na kubadili nguo,sikutaka kabisa hata kunawa uso,nilipomaliza niliingia ndani kuwasalimia Headmaster na mkewe!.

Maza mdogo "Wewe unaenda halafu hicho kichwa cha cherehani nani atakipeleka?"

Nikawa kimya kwa muda huku nikiwa natafakari nini cha kujibu!.

Headmaster "Kwani kichwa cha cherehani sikuhizi unakileta nyumbani?"

Maza mdogo "Juzi sinilikwambia wanasema yule mama Mayala aliwahi kuibiwa kichwa cha cherehani pale kibandani kwake,unadhani chanzo cha Mama Mayala kuacha kushona ni nini?"

Headmaster "Sasa kwanini usiwe unamuomba mama Rebecca unakiacha pale nyumbani kwake kuliko kupata kazi ya kukileta huku!".

Maza mdogo "Ngoja nitajaribu kuongea nae!".

Headmaster "Wewe nenda uwahi kwenye shughuli zako bhana!"

Maza mdogo "Sasa nani atanisaidia kukipeleka senta"

Headmaster "Utakamata hapo mwananfunzi akusaidie"

Sasa mimi sikutaka kabisa kuonekana uenda nilichukia kukibeba kile kichwa,niliamua kujikaza na kumwambia ningekifata baada ya kupeleka miwa senta.

Mimi "Haina shida mama ngoja nikachukue miwa nipeleke senta halafu narudi kukichukua".

Maza mdogo "Sawa,uwahi sasa"

Sasa nilidhani uenda Headmaster alivyokuwa amemshauri ya kwamba angekamata pale shuleni mwanafunzi amsaidie kubeba kile kichwa na kukipeleka Senta angekubaliana nae lakini haikuwa hivyo,kitendo cha kuniambia niwahi kurudi kukibeba ilionyesha kabisa alifurahishwa na mimi kwenda senta na kurudi kukibeba!.Basi sikuwa na hiyana mtoto wa kiume nikaondoka zangu kuelekea kwenye mashamba ya mzee Masumbuko kwa ajili kufata miwa kama kawaida,ingawaje miwa iliyokuwepo haikuisha ila niliona ni heri nikakusanya ikawa mingi ili inipunguzie safari ya kila siku kuamka asubuhi na mapema kisa kuwahi miwa!.

Nilipofikisha ile miwa pale senta niliibwaga chini nikaondoka zangu kurejea nyumbani kwa kukimbia ili kuwahi kurudi!,sasa kuna sehemu nilifika nikamuona dogo mmoja akiwa kwa mbele kabeba kile kichwa cha cherehani huku Maza mdogo akiwa nyuma yake,nilipowafikia nilimwambia dogo anipe kile kichwa nimsaidie na yeye arudi shule!.

Nilijifanya kuchangamka na kutabasamu kiunafiki lakini kiuweli nilikuwa nimechukia sana,nikawa najiuliza kama alikuwa anajua angempatia mwanafunzi amsaidie kubeba kwanini alitaka nirudi tena?,kama kawaida yangu sikutaka maneno na mtu nikaamua kufunga bakuli langu ili mwanaharamu apite.Wakati huo kiukweli nilikuwa nimeanza kupoteza nuru ya muonekano wangu kwasababu ya kushinda kule senta wakati mwingine sili kabisa mchana na chakula nilikuwa nakutana nacho usiku tu!,mara nyingi nikiwa pale senta nilikuwa nashindia sana miwa!.

Tulifanikiwa kufika senta na nikakipeleka kile kichwa kwenye kibanda alichokuwa akishonea na mimi kwenda mpaka kwa yule mama ambaye nilikuwa nikilaza ile miwa,niliichukua nikaenda kuinganisha na ile niliyokuwa nimekuja nayo na kuanza kuuza!.Namshukuru Mungu siku hiyo niliuza sana ile miwa,japo haikuisha lakini mpaka kufika mida ya saa 10 alasiri ikawa imepungua kwa kiasi kikubwa!
Sasa nikiwa naendelea kuuza miwa yangu pale,kwa mbali nikamuona yule binti Mwise akiwa na binti mmoja wakiwa wamevaa sketi za shule na tisheti za kawaida wakiwa wanakuja hapo senta, sikufahamu kilichokuwa kimewaleta uenda walifata mahitaji kama watu wengine!.

Yule binti kiukweli ndiye alikuwa binti wa kwanza kwa hapo kijijini kuumiza na kuutesa moyo wangu,nilikuwa nampenda na kumtamani sana kutokana na shepu yake nzuri!,ila baada ya kuanza kutembea na Monica kiukweli upendo na matamanio yangu kwake yakaanza kupungua kwa kasi ya ajabu!.Walipofika karibu waliingia kwenye duka moja wakanunua kilichowaleta kisha wakatoka wakawa wanaelekea kwenye vibanda na maduka ya mbele ambako huko pia ndiko mama mdogo anakofanyia shughuli zake,sasa baada ya kugeuka na kutazama uelekeo niliokuwepo mimi,nikampiga mkono kwa ishara ya kwamba aje!.

Mwise "Narudi!"

Kwakuwa aliniambia anarudi nikasema ngoja nisubiri.Safari hii sikutaka kabisa kuwa na kimuhe muhe kwasababu sikuweza kujificha na ile biashara yangu na yeye alifahamu kabisa nilikuwa muuza miwa!,niliamini kama ni kumpata basi ningempata tu na kama ni kumkosa basi ningemkosa vilevile!.

Haukupita muda wakawa wanarudi na huyo mwenzie,sasa alipofika pale kwenye eneo langu la biashara akaanza kama kuonyesha nyodo na dharau.

Mwise "Nionjeshe muwa rafiki yangu!"

Mimi "Kwahiyo mimi leo nimekuwa rafiki yako?"

Mwise "Jamani!,kwani kuna ubaya wewe kuwa rafiki yangu?"

Basi nikamkatia pingili mbili za muwa yeye pamoja na mwenzie!,basi wakawa wanazungumza na huyo rafiki yake maneno ya kisukuma huku wakicheka kwa kicheko cha kichini chini!,kiukweli walikuwa wanikiteta kwa kisukuma na ishu kubwa walikuwa wakizungumzia zile stiki nilizokuwa nimelambwa na Headmaster mbele ya wanafunzi!,wao walidhani siwaelewi lakini hata kama sikuelewa kisukuma vizuri mtu alikuwa akiteta inafahamika kabisa!.

Walipomaliza kukwangua kwangua miwa kwa kisu akawa ameniambia wanaondoka kuwahi kurudi nyumbani,nikawa nimemuomba anivumilie angalau kwa dakika mbili nizungumze nae!,sasa yule mwenzake akawa amemwambia atamkuta mbele!.

Mwise "Sasa na wewe unaniacha nyanoko"

Mwenzie "Utanikuta mbele bhana"

Mwise "Mmh!,niambie mi nina haraka"

Mwise "Kwahiyo Mwise Ombi langu vipi lakini?"

Mwise "Ombi gani tena jamani"

Mimi "Kwani mara ya mwisho mimi na wewe tuliongea nini?".

Mwise "Siulianimbia unanipenda,nashukuru kwa kunipenda"

Mimi "Usinifanyie hivyo Mwise"

Mwise "Wewe si unaye mwanamke wako"

Mimi "Mwanamke gani tena jamani!?"

Mwise "Wewe ema kaniambia habari zako nyingi tu!,kumbe ulikuwa tu unataka unilale uniache"

Mimi "Daaah!,hebu achana na mambo ya Ema Mwise,Ema anashida kubwa na wewe yule unamfahamu akili yake".

Mwise "Mimi nachelewa bhana,kesho!"

Basi yule binti alianza kukimbia kumfuata mwenzie aliyekuwa akimsubiria.Niliamini kabisa kwa kilichotekea pale shule ukichanganya na uongo wa Ema,haikuwa rahisi mimi kumpata tena yule binti.Niliamua kujipa moyo ya kwamba mademu mabaya siku zote ndiyo yanayoringa lakini kuna muda bado nilikuwa nikifikiria kiuno cha yule binti na kuwaza kinavyo chakatwa na wanaume wengine,kiukweli nilikuwa naumia sana!.

Sikuwa na namna ilibidi niwe tu mpole ili maisha yasonge!.

Baada ya kukamilisha siku ya uuzaji wa miwa niliamua kurudi nyumbani na namshukuru Mungu safari hii sikurudi na kichwa cha cherehani kwasababu maza mdogo alipata pa kukiweka hapo senta.

Sasa nilifika nyumbani mida ya saa 1 usiku,nilielekea lamboni ile usiku kuchota maji ili nije nioge kwasababu nilikuwa sijaoga tangu jana yake!,sasa nilipotoka bafuni kuoga,nikawa nimeingia ndani kwa ajili ya kupaka mafuta!,sasa wakati napaka mafuta nikasikia kuna mtu ananipiga piga mgongoni kwa mkono akiashiria nigeuke!,sasa ile nimegeuka nikawa nimekutana na Monica uso kwa uso!.

Kiukweli nilishituka sana ila akanifanyia ishara ya kidole mdomoni akinitaka nisipige kelele wala kuongea!.

Mimi "Monica kuna nini mbona huko humu"

Monica "Vaa nguo tuondoke"

Mimi "Tuondoke twende wapi tena!?"

Monica "wewe vaa twende"

Mimi "Tunarudi lakini?,maana mwenzio jana jana nimepigwa kwasababu yako"

Monica "Hatuendi mbali tutakuwa nje hapo"

Basi baada ya kuvaa nguo,Monica akawa amenishika mkono na ghafla tukawa nje ya nyumba kwa pembeni kidogo.

Monica "Tusogee pale kwenye lile jiwe!"

Baada ya kufika pale kwenye lile jiwe akanitaka tukae pale na kuna watu tuwasubiri walikuwa wanakuja!.
Tunaomba kiti cha UMUGHAKA kisikaliwe na mtu mwengine yoyote kwa kuwa ikifika muda wa kutuletea madude ya Monica plas Mwise basi mambo yote yaende vizuri,sio unafika muda wake UMUGHAKA mara kiti hamna tukazidi kupoteza muda.
 
Basi mzazi wako hakuwa na akili. Yaani umwage mboga nyumbani (mfano) aje akichape assembly? Hakuwa na akili inawezekana aliathiriwa na Bhangi au Pombe. It doesnt make sense. Lakini mbaya zaidi kama wewe si Mwanafunzi ukosee nyumbani akuite assembly akuchape. Hivi ninyi mnaelewa hoja yangu au mnatajipendekeza tu mkidhani jamaa atasusa kuandika hizi stories? Tumieni akili bwana msiwe wavivu

We ni mtoto wa juzi endelea kubishaana but mtu ambaye sio mwanafunzi kupigwa pared na mwl ni kitu cha kawaida sana vijijin
 
Kabla hujaandika uwe unasoma ukaelewa. Inaonekana hukuwa na akili au uelewa ndo maana unabisha na kutoa mifano ambayo haiendani. Jifunze to be calm. read,understand and then answer accordingly. You , teenagers nowdays dont take time to think before doing anything. Look before you leap.
Upo sahihi.Hapo mtunzi ameweka kitu kisicho na uhalisia.Jamaa sio mwanafunzi halafu ni mkubwa kuliko wanafunzi,at least angekuwa mdogo labda.Tena headmaster anamshtakia kwa wanafunzi kuwa hajalala nyumbani eti!

Halafu eti assemble!!Dah!
Hapo kidogo haina uhalisia ila sio kesi,tunaenjoy...
 
Hayajawahi kukukuta mzee tulia hivyohivyo
Hapo pa kupigwa viboko assembly na wewe si mwanafunzi utunzi wako haujaenda sawa. HAIWEZEKANI. unapotunga jaribu kuwa makini sana ili usitoke sana mbali ya Uhalisia. Haijawahi tokea kosa la nyumbani mtu akaadhibiwe Shuleni tena si mwanafunzi. Hapo uwe makini.
 
Ni kweli. Ndo shida kubwa humu ndani. Mtu yeyote akijua kusoma na kuandika anakuwa member.
Kaka we bado mdogo vingine acha vipite tu shule za enzi hizo ukiwa haupo alikuwa anachapika yeyote tu tena mbele ya wanafunzi awe ni mwanafunzi au asiwe mwanafunzi kwa hiyo wewe ni wa juzi kwa hiyo vilivyo juu ya uwepo wako viache tu.

Mfano mleta uzi kwenye simulizi zake nimezifuatilia kwa karibu mfano vitu anavyotaja unagundua kabisa hii stori kama ni chumvi iko kwa mbali sana
 
Mkuu unajifanya mjuaji kwa vyote ilihali hujui. Mimi ni mtoto wa Mwalimu mkuu,nimetandikwa mara kibao tu kwa makosa ya Nyumbani nikiwa Shule! Au makosa ya Shule nachapiwa Nyumbani. Nadhani kama tungekuwa tunatumia uhalisia wa majina Yetu,kuna Watu ninaofahamiana nao wangethibitisha. Siku zote usijifungie Katika kuamini,ulimwengu Huu ni mpana na una mambo mengi,yale unayoyaona Kwako hayawezekani si kwa wote!! Tukiamua tulete shuhuda zetu mbalimbali Katika Jamii Zetu nadhani utaona watu wanatunga!!
Huyo ni dogo hajui chochote achana nae mkuu, amekuta walimu wakuu wa siku hizi wanavaa mlegezo sasa utamwambia nn
 
Huyo ni dogo hajui chochote achana nae mkuu, amekuta walimu wakuu wa siku hizi wanavaa mlegezo sasa utamwambia nn

Atuulize sie watoto wa waalimu wakuu wa Kijijini enzi hizo.

Kwanza Mzee akikuta umejihusisha na ugomvi wa aina yeyote ile, haulizi umeonewa au nani anamakosa, lazima uchezee fimbo zisizo na idadi. Hata kama tayari umeshapewa adhabu na mwalimu mwingine. Na siku hiyo ukifika nyumbani, una kamisheni ya adhabu Kwa kosa lilelile la shule ambalo tayari umeshatumikia adhabu. Hapo anakuadhibu kama Baba Mzazi mbele ya wadogo zako iwe fundisho kwao.

Kuna siku tunalima shambani, akatokeza mjusi, dogo anaenifuatia akajipendekeza kuinama wakati nimeinua Jembe kumkata mjusi, si likatua kichwani kwake! Damu zinamwagika USO mzima, tukaenda nyumbani mbio, Ile amefika tu, akadakwa na fimbo za rasharasha mwili mzima...hapo nikasema kama wanaufanyia hivi mti mbichi, mkavu itakuwaje? Piga picha huyo anatembezewa kipigo ni mtu aliyekatwa Jembe, Sasa mwenye kumkata itakuwaje?
 
Back
Top Bottom