Tulichomfanya yule mchawi hatakuja kusahau kamwe

Tulichomfanya yule mchawi hatakuja kusahau kamwe

Nimeoa hapo muriba ghokegena kwetu Ni hapo hapo keisangora senta. Halafu wewe badala ya kupiga kazi unashinda kwenye social networks utadhani ndio utalisha wanao. Tunakumbushana tu usije ukanimaindi Mana ubongo unachukia ukweli Mana unauma na ubongo haupendi ukweli hata siku moja .


Mana kazi ya ubongo Ni kukutoa kwenye maumivu na kukutafutia Raha Basi yaani hauna kazi nyingine kabisa.
Siwezi kuchukia, kuna mchungaji mmoja napenda kufatilia speech zake anaitwa Mch.Mitomingi(Marehemu kwa sasa) ansema UKIMPATA Kazi napiga sana, nikiwa free napitia pitia social networks kuona kilichomo mura weito na kupumzisha akili.
 
Atuulize sie watoto wa waalimu wakuu wa Kijijini enzi hizo.

Kwanza Mzee akikuta umejihusisha na ugomvi wa aina yeyote ile, haulizi umeonewa au nani anamakosa, lazima uchezee fimbo zisizo na idadi. Hata kama tayari umeshapewa adhabu na mwalimu mwingine. Na siku hiyo ukifika nyumbani, una kamisheni ya adhabu Kwa kosa lilelile la shule ambalo tayari umeshatumikia adhabu. Hapo anakuadhibu kama Baba Mzazi mbele ya wadogo zako iwe fundisho kwao.

Kuna siku tunalima shambani, akatokeza mjusi, dogo anaenifuatia akajipendekeza kuinama wakati nimeinua Jembe kumkata mjusi, si likatua kichwani kwake! Damu zinamwagika USO mzima, tukaenda nyumbani mbio, Ile amefika tu, akadakwa na fimbo za rasharasha mwili mzima...hapo nikasema kama wanaufanyia hivi mti mbichi, mkavu itakuwaje? Piga picha huyo anatembezewa kipigo ni mtu aliyekatwa Jembe, Sasa mwenye kumkata itakuwaje?
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]daaaah
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]daaaah

Najua tu Kuna watu watasema nimezidisha sukari au nipunguze tangawizi. Narudia Tena, hakuna chai hapo. Mbaya zaidi Mzee ilikua hata ukijikwaa mbele yake, utaogelea fimbo tu anakwambia hautembei Kwa umakini.

Kuhusu ugomvi sheria yake ni Moja tu, akisikia au ukikutwa umejihusisha na ugomvi wa aina yeyote, iwe Kwa Mkubwa au mdongo, ni kipigo Cha uzani wa Mandonga mtu kazi, yaani haulizi umechokoza au umechokozwa, umekosea au umekosewa, ni full dozi.
 
Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 19.





Basi wakati tukiwa tumekaa pale kwenye lile jiwe,ghafla wakawa wametokea wale kina mama wawili ambao juzi yake tu nilitoka kwao kupigwa chale!.Walifika pale kwa ghafla sana na wakanitaka nisimame!.Baada ya kusimama,mama mmoja wapo akaniambia nivue nguo ili nipakwe dawa,sikutaka kabisa kupoteza muda nikaanza kuvua nguo na wakaanza kunipaka dawa kwa haraka sana!.Walipomaliza wakawa wamekaa kimya kwa muda kidogo.

Mimi "Kwani kuna nini?"

Monica "Shiiiiiiiiiiii,nyamaza"

Monica alinifanyia ishara ya kidole mdomoni kwamba ninyamaze na aliniambia kwa sauti ndogo sana.Sasa baada ya muda kidogo kupita mama mmoja akamwambia Monica kwa kisukuma aniambie kila kitu!.

Monica "Mpenzi wangu umughaka,unaniamini?"

Mimi "Ndiyo,nakuamini"

Monica "Sasa hawa mama zangu wadogo siunawakumbuka?"

Mimi "Ndiyo,Hawa si ndiyo wale wa juzi?"

Monica "kumbe una kumbukumbu,sasa ni hivi!,mama yangu kawatuma kuja kukusaidia maana kuna kikao kilikuwa kinaendelea kwa yule mzee mshenzi(Makono)na washirika wenzie ya kwamba leo unapaswa ufe!"

Mimi "Kwanini nife Monica!?".

Kiukweli nikaanza kupaniki na amani ikaanza kunitoweka!.

Monica "Yule mzee nilikueleza alipewa adhabu ya kutoa kafara kwasababu alivunja mashariti ya kumtuma yule mwanaye pale nyumbani kwetu akifahamu kabisa mama yangu ni mmoja wapo,sasa hasira zake amehamishia kwangu na kwako,hivyo ndiyo maana nilikwambia nitakulinda usiku na mchana mpenzi wangu!"

Mimi "Kwahiyo tutakaa hapa mpaka asubuhi hawezi kutuona?"

Monica "Hapa tunamsubiri mama afike kwanza atupe maelekezo"

Mimi "Sawa"

Tulikaa pale kwenye yale mawe mimi na Monica wakati huo wale kina mama wakiwa wamesimama!.Haukupita muda ghafla mama yake Monica akawa amefika pale tulipokuwepo.Monica alisimama akamuinamia mama yake kwa heshima na unyenyekevu ikiwemo pia wale kina mama.

Mama Monica "Mwanangu hujambo?"

Mimi "Sijambo mama,shikamoo"

Mama Monica "Marhaba mkwe wangu"

Mama Monica "Sasa hebu shika hii"

Alinipatia kitu kama kibuyu kidogo sana ambacho sikuelewa ndani kulikuwa na kitu gani!.

Mama Monica "Nenda ndani utakiweka pembeni ya mlango chumbani unapolala,sawa?"

Mimi "Sawa mama"

Mama Monica "Ukishaweka hurudi hapa,fanya haraka".

Niliondoka kuelekea ndani ambako nilipofika sikumkuta mtu nje!,basi niliingia ndani nikakiweka kile kibuyu kisha nikatoka nje!,sasa nadhani baada ya kuurudishia ule mlango Headmaster alisikia.

Headmaster "Wewe leo huli?"

Mimi "Nakuja kula baba"

Maza mdogo "Njoo uchukue hili bakuli ukaongeze mboga umughaka"

Basi niliamua kwenda sebuleni na nikawakuta wakiwa wanakula!.Nilichukua lile bakuli nikaingia jikoni kupakua mboga kisha nikarudi sebuleni kula haraka ili niondoke niende kwa mama yake Monica aliyekuwa ameniambia niwahi kurudi!.

Maza mdogo "Uliondoka saa ngapi leo!,nimewahi kufunga ili tuongozane sikukuona"

Mimi "Mimi niliwahi mama baada ya kuona giza limeanza"

Headmaster "Kwani ulikuwa wapi?,mbona mwenzio anasema hukuwepo?"

Mimi "Nilikuwa hapo nje baba"

Headmaster "Mbona tumekuita na hukuitika?"

Mimi sikutaka kujibu kitu nikaamua kukaa kimya ili kuepeusha mambo mengi!.

Headmaster "Biashara inakwendaje?"

Mimi "Leo angalau kidogo nimeuza uza"

Kiukweli wakati huo nilikuwa naona kama wananichelewesha kuondoka kwenda nje,baada ya kupiga matonge kadhaa ya ugali nikaamka nikasema nimeshiba!.

Headmaster "Leo ulikula wapi bhana"

Mimi "Sijala sehemu baba nahisi kushiba".

Headmaster "Hivi mchana huwa unakula wapi?"

Mimi "Huwa nashindia miwa tu pale kijiweni".

Headmaster "Aya bhana"

Niliamka nikanawa kisha nikatoka nje kujifanya kama najikoholesha pale kisha nikafungua mlango na kutoka nje ya nyumba.Nilitembea kwa haraka kuelekea nilipokuwa nimewaacha kina Monica,nilipofika nilimkuta Monica akiwa peke yake,wale kina mama pamoja na mama yake Monica sikuwaona.

Monica "Ila wewe nae kuna muda unakera sana"

Mimi "Sasa nakera nini Moni!".

Monica "Mama alikwambia uende uwahi kurudi wewe umefika ukaamua kukaa!"

Mimi "Haikuwa rahisi Moni kama unavyodhani"

Monica "Hebu tuachane na hayo,shika hii hapa ulambe na hii uweke mfukoni."

Monica alinipatia kitu kama unga ulokuwa mweusi kama mkaa nikalamba kisha akanipatia kitu kilichokuwa kimefungwa kwa kitambaa kidogo cheusi akanitaka niweke mfukoni.

Mimi "Mama anarudi?"

Monica "Arudi huku kufanya nini?,wao ndiyo wameondoka hivyo!".

Monica "Naomba unisikilize kwa makini umughaka"

Aliendelea "Utakachokiona leo usipige kelele na ikawe siri yako,mimi nipo na wewe na nikizidiwa nitamuita mama atatusaidia"

Mimi "Sawa"

Monica "Twende"

Basi tuliondoka kuelekea ndani ya nyumba yetu nikiwa nimeongozana na Monica,sasa nilipofungua geti kuingia ndani ghafla sikumuona,nikabaki kushangaa tu na kujiuliza atakuwa ameleekea wapi kusiko julikana,sasa kwakuwa nilifahamu alikuwa na uwezo mkubwa niliamini ametoka mara moja na angerudi!.Nilipoingia hapo uwani nilimkuta Ema anafua soksi zake za shule na kufuta futa viatu vyake!,kwakuwa sikuwa na stori nae nikaingia zangu ndani!.

Nilipoingia tu chumbani Ghafla nikamuona Monica akiwa amesimama kwenye ile kona ambayo niliweka kile kibuyu!,alinifanyia ishara ya kunyamaza!.Sasa jamaa alipomaliza shughuli zake aliingia ndani akaanza kusoma,mimi niliamua kujilaza kitandani wakati huo namuona Monica huku Ema yeye akiwa haoni kitu chochote!.Sasa baada ya kupiga buku kwa dakika kama ishirini niliona anarudisha madaftari kwenye mfuko kisha akazima ile taa akapanda kitandani kuja kulala!.

Baada ya jamaa kulala,Monica alinisogelea kitandani akanishika mkono akanisogeza kwenye ile pembe aliyokuwepo yeye akanitaka nikae kimya!.

Tulisimama kwa muda mrefu kidogo ndipo nikasikia kuna vishindo hapo uani kama miguu ya watu!,na kwa vishindo vile yaelekea walikuwa watu zaidi ya wawili.Monica akaniambia nitulie tuli kwani hakuna ambaye angetufanya chochote.Kiukweli nilikuwa nina jiamini kupita maelezo kwa wakati huo!.

Haukupita muda nikaona mlango unasukumwa,waliingia watu wanaume wawili waliokuwa uchi ambao sikuwa nikiwafahamu,basi Monica akanitaka nitulie kabisa!,wale jamaa wakaenda mpaka pale kitandani wakawa kama wanashangaa!,basi mmoja akatoka nje,haukupita muda akawa ameingia na mzee mmoja ambae nilimfahamu alikuwa yule mzee makono!.

Yule mzee alisogea mpaka pale kitandani kisha nikaona anaangalia kwa kushangaa na yeye pia!.

Jamaa "Ndiye huyu?"

Makono " Siye huyu"

Makono "Mchukueni huyu tuondoke"

Basi nikaona wale jamaa wanamuamsha Ema akaamka,Ema aliamka akiwa kama mlevi aliyepoteza kumbukumbu kabisa!.Walimtoa nje Ema na ndipo Monica akaniambia tutoke nje na nihakikishe kile kibuyu kidogo alichonipatia mama yake nakibeba!,basi tulipotoka nje tukakutana na grupu la watu wengine kama watano akiwemo Headmaster ambao walikuwa kama wamewelewa pombe na hawakuelewa kitu chochote!.

Wale jamaa wawili mmoja alikaa mbele na mwingine nyuma huku wa mbele akitoa ishara kwamba waondoke,sasa yule wa nyuma alikuwa akiwapiga wale watu akiwemo Headmaster na walisimama wakatoka nje!.Sikumuona tena mzee makono hapo nje kwa wakati huo na sikufahamu alikuwa amekwenda wapi!.

Monica "Twende"

Mimi "Tunaenda wapi?"

Monica "wewe twende"

Basi tukaanza kuwafatilia wale watu wakiwa wanapelekwa kusiko julikana!.
Woyoooooooooooooooo!

Wabheja sana Umughaka!!!
.Mkuje mkujee kitu tayariiiii
 
Atuulize sie watoto wa waalimu wakuu wa Kijijini enzi hizo.

Kwanza Mzee akikuta umejihusisha na ugomvi wa aina yeyote ile, haulizi umeonewa au nani anamakosa, lazima uchezee fimbo zisizo na idadi. Hata kama tayari umeshapewa adhabu na mwalimu mwingine. Na siku hiyo ukifika nyumbani, una kamisheni ya adhabu Kwa kosa lilelile la shule ambalo tayari umeshatumikia adhabu. Hapo anakuadhibu kama Baba Mzazi mbele ya wadogo zako iwe fundisho kwao.

Kuna siku tunalima shambani, akatokeza mjusi, dogo anaenifuatia akajipendekeza kuinama wakati nimeinua Jembe kumkata mjusi, si likatua kichwani kwake! Damu zinamwagika USO mzima, tukaenda nyumbani mbio, Ile amefika tu, akadakwa na fimbo za rasharasha mwili mzima...hapo nikasema kama wanaufanyia hivi mti mbichi, mkavu itakuwaje? Piga picha huyo anatembezewa kipigo ni mtu aliyekatwa Jembe, Sasa mwenye kumkata itakuwaje?
Haha mti mkavu utakua ulipitia shuruba za hatari
 
Duh ongea na Moni awasaidie headmaster na familia yake aiseee watajikuta wamelazwa kusikojulikana[emoji16][emoji16][emoji3577]!
Poor Ema!
 
Samahani Kama nitakua naingilia andiko lako Ila ningeomba Hapo mbele uongeze neno " mbobevu" ili isomeke "MPUMBAVU MBOBEVU" nafikiri itasaidia wasomaji wajue wanamuelewesha mtu wa namna gani
kabisa kuna mwalimu alioa shangaz yetu tena ni miaka ya 2000 tu hapo but alikuwa na uwezo wa kukuchapa mnacheza mpira ana ishu yake ukachelewa kuitikia na wala sio ishu

Miasha yamebadilika sana
 
Najua tu Kuna watu watasema nimezidisha sukari au nipunguze tangawizi. Narudia Tena, hakuna chai hapo. Mbaya zaidi Mzee ilikua hata ukijikwaa mbele yake, utaogelea fimbo tu anakwambia hautembei Kwa umakini.

Kuhusu ugomvi sheria yake ni Moja tu, akisikia au ukikutwa umejihusisha na ugomvi wa aina yeyote, iwe Kwa Mkubwa au mdongo, ni kipigo Cha uzani wa Mandonga mtu kazi, yaani haulizi umechokoza au umechokozwa, umekosea au umekosewa, ni full dozi.
Mlimpeleka mirembe au??
 
kabisa kuna mwalimu alioa shangaz yetu tena ni miaka ya 2000 tu hapo but alikuwa na uwezo wa kukuchapa mnacheza mpira ana ishu yake ukachelewa kuitikia na wala sio ishu

Miasha yamebadilika sana
tena nilikuwa na ndugu yangu msumbufu anafuatwa home na stik anakula mbele ya ndugu zetu na ole upate na adhabu utasikia na hii ya shangazi yako
 
Back
Top Bottom