Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Acha tabia za kikeWewe jamaa unaringa Hatari Aisee...
Yaani kastory kakuisha siku moja ila visingizio kama vyote mwamba.
Mara oon sijui hiki mara kile.
Tushawazoea wasimuliaji wote wa Jf wanamalingo kuanzia ile story ya mpwayungu hata yako wewe pia kwanza unatunga.
Ahsante
Ndio yeye kabisaMonica UmughakaView attachment 2386631
Naona sasa tunakaribia kujua mlichomfanya Mzee makono aka LamekiTulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 24.
Baada ya Maza mdogo kurudi,ulikuwa ukiwaangalia yeye na Headmaster ilionekana kuhuzunika sana na sikuelewa sababu ilikuwa ni nini!,nimewazoea mara zote tukiwa pale sebuleni eidha tukila chakula au tukiwa tumekaa,mara zote mazungumzo yenye utani na ucheshi mwingi huwa yakishika kasi,safari hii imekuwa tofauti kabisa!.
Headmaster "Ulisema ulikuwa na jambo la kutuambia,ni jambo gani hilo bhana"
Mimi " Ni jambo la kawaida tu Baba"
Mimi "Baba mimi nina rafiki yangu wa kike anaitwa Monica,na niseme tu ukweli baba ile siku uliyoniadhibu ni kweli nili lala kwao".
Mimi "Sasa nimeamua Kuwaita ili niwashirikishe jambo"
Mimi " Yule binti kiukweli kwao ni wataalamu wakusaidia watu na wameshawasaidia watu wengi,sasa huwa nikienda kwao kumsalimia ananielezaga mambo mengi kuhusu hii nyumba tunayoishi".
Sasa niliamua mambo mengine kukoleza chumvi ili mradi tu waniamini na wakubali hatua za haraka zifanyike!.
Mimi " Jana nilipotoka senta nilikutana nae njiani akawa amesema nimsindikize hadi kwao,sasa nilipofika kwao mama yake akaanza kuniambia kuna mtu amewahi kuja hapa nyumbani kufanya zindiko,sasa lile zindiko lilifeli kwasababu yule mtu aliuawa kichawi"
Sasa baada ya kusema hiyo sentensi,nikaona Headmaster na mkewe wanaangaliana kwa mshangao!.
Mimi "Yule mama aliniambia adui wa hii nyumba ni mzee makono!".
Headmaster "Hivi huyo mzee makono ndiye nani?"
Mimi "Kama unakumbuka baba nimewahi kukwambia nilikutana nae akaniambia anakusalimia na akajitambulisha kwamba anaitwa makono"
Headmaster "Sawa nakumbuka lakini najaribu kuvuta picha ni mzee gani huyo"
Mimi "Unakumbuka ile siku Ema amening'inizwa darasani?"
Headmaster "Mmh!"
Mimi "Sasa siulikuja na wazee wawili kama unakumbuka,yeye ni yule mwemamba mrefu"
Headmaster "aaaaaaah!,hivi kumbe ndiyo anajiita makono!"
Maza mdogo "Ni nani?"
Headmaster "Si yule mzee lameki"
Headmaster "Sawa,sasa hapa ndipo naanza kupata picha!"
Aliendelea "Basi hilo jina litakuwa la kisukuma au la kwao huko,kama ni yule mzee jina lake ni Lameki"
Aliendelea "Na alikuwa rafiki yangu sana lakini siku za karibuni naona ananikwepa sana".
Headmaster "Sisi bhana tumekuelewa na labda kwa niaba ya mama yako mdogo nikuombe radhi kwasababu kuna mahali tulienda na tukaambiwa mambo mengi sana,hata suala wewe kumchungulia mama yako akiwa anaoga haikuwa kweli,tumeambiwa ni mtu mmoja ambaye anazo nguvu za kutosha tu,na kwa maelezo yako sasa angalau nduyo napata mwanga".
Aliendelea "Kumbe matukio yote yanayofanyika hapa ndani kuna watu ndiyo wanatufanyia hiyo michezo na tumeambiwa anayeongoza genge ni mwanaume mwenye nguvu haswa,sasa namna ya kukabiliana nae ndiyo changamoto,ingawaje kuna dawa tumepewa ndo tunataka kuzijaribu tuone!"
Alisema "Je mama yake huyo binti anapatikana wapi?"
Mimi "Wao wanaishi kule masairo"
Headmaster "Aisee mnazurura,hadi Masairo ushafika!"
Aliendelea "Huyo mama yukoje?"
Basi baada ya kumuelezea namna mama yake Monica alivyo,mzee alishangaa sana!.
Headmaster "Siyo mke wa mzee Kulola kweli?,maana kwa unavyoniambia ni kama yeye"
Aliendelea "Yaani yule mchawi ndiyo unasema anasaidia watu?,wale inasemekana walifukuzwa huko vijijini kwasababu ya uchawi!"
Baada ya kuniambia hivyo nikaona kabisa bila kujitetea nitaharibu mambo!.
Mimi "Hata mimi mara ya kwanza baba nilikuwa nasikia watu wanasema hivyo,lakini nilivyombananisha yule binti alikataa na hata pia nikaongea na mama yake akaniambia walikuwa wanasingiziwa tu,hakukuwa na ushahidi dhidi yao"
Headmaster "Mimi na yule mama hatupatani na yeye analijua hilo,kuna kipindi nilimtukana sana"
Mimi "Lakini baba asingekuwa mtu mwema asingeniambia haya yote"
Maza mdogo "Ila kweli,kama ni mchawi unadhani angesema hivyo?"
Mimi "Kuna dawa alinipatia jana akawa amesema tuitumie na kama ukikubali mimi nitamuita aje atusaidie ili kumnasa mtu anayetusumbua"
Headmaster "Hiyo dawa iko wapi?"
Basi niliondoka kwenda ndani kuchukua ile dawa na kuileta!.
Headmaster "Ndiyo hii?"
Mimi "Ndiyo baba"
Maza mdogo "Matumizi yake yakoje?"
Mimi "Hii tunaogea watu wote mama"
Maza mdogo "Baada ya hapo"
Mimi "Nitaenda kumuita mama yake Monica aje atuelekeze cha kufanya"
Headmaster "Shida tukitumia dawa zote hatutajua ni nani ametusaidia"
Aliendelea "Sawa,ngoja tumuone huyo mama,kama amekwambia yote hayo inawezekana akawa mkweli "
Kwakuwa nilifahamu ikifika usiku mama yake Monica angekuja kama alivyokuwa ameniahidi,sikuwa na presha na niliwaambia ningemfata kumbe mimi nilikuwa ninaujua ukweli.
Headmaster "Hivi huyo mjinga bado hajarudi tu"
Mimi "Bado sijamuona"
Headmaster "Ngoja licheze na dunia,sikuhizi badala ya kusoma limeanza kuhangaika na wanawake!"
Aliendelea "Mabinti wa hii shule niwa kuhangaika nao?,ngoja acheze na hiki kijiji kama hatujamuacha hapa".
Baada ya maelekezo ya namna ya kutumia ile dawa,namshukuru Mungu walikubali na walioga!,sasa kitu kilichokuwa kinasubiriwa ni mama yake Monica kuja,niliwaambia ikifika jioni nitaenda kumuita,lengo langu lilikuwa ni kusubiri mpaka atakapokuja mwenyewe maana nilichoka kutembea mpaka Masairo ambako kulikuwa mbali!.
Headmaster alihuzunika sana kusikia ya kwamba aliyekuwa akitufanyia uhuni pale nyumbani alikuwa huyo mzee aliyejiita makono ilihali jina lake ni Lameki.Nakumbuka Headmaster alisema akipatikana huyo basi angejuta kuzaliwa!.
Ilipofika mida ya saa 11 jioni,niliwaaga nikasema naelekea kwao Monica kumchukua mama yake!,sasa kwa muda ule niliona nitembee kwa kukimbia ili niwahi kufika maana palikuwa mbali!.Baada ya safari ya muda mrefu kidogo nilifanikiwa kufika kwao Monica.
Nilimkuta bibi yake Monica akiwa amelala kwenye jamvi kwa nje!,nilipiga hodi yule bibi akaitikia kisukuma,sasa kasheshe ilikuwa ni kuongea nae kumuuliza Monica na mama yake wako wapi kwasababu sikuwakuta!,nilipojaribu kumuuliza kwa kiswahili,yeye alinijibu kwa kisukuma,niliamua kusimama kando ya nyumba ili kuvuta muda angalau nikiamini wangekuja maana walikuwa wamemuacha bibi peke yake.
Baada ya muda kwenda ikiwa inakaribia saa 1 usiku,nilimuona Monica akiwa anakuja akiwa amebeba gunia kichwani na jembe mkononi!,alipofika nilienda kumtua ule mzigo ndipo nikakuta alikuwa amebeba mihogo mibichi.
Mimi "Mlienda shambani?"
Monica "Eeeh!,umekuja muda mrefu?"
Mimi "Nimekuja muda ndiyo"
Mimi "Mama yuko wapi?"
Monica "Anakuja,nimuacha hapo nyuma"
Mimi "Sasa hii mihogo mtamenya saa ngapi?"
Monica "Hii itamenywa kesho,nani wakumenya sasa hivi nimechoka"
Mimi "Sawa,kesho nikipata nafasi nitakuja kuwasaidia kumenya".
Ile mihogo ilikuwa ni ile michungu(rumala) iliyokuwa inavundikwa ikishamenywa kwa ajili ya kutengenezea unga wa muhogo(Udaga).
Basi haukupita muda mama yake Monica naye akawa amekuja na yeye akiwa na mzigo wa mihogo kichwani.
Mimi "Mama shikamoo"
Mama Monica "Marhaba mwanangu"
Aliendelea "Umefika zamani?"
Mimi "Ndiyo mama,nimefika muda tu"
Mama Monica "Tusamehe mwanangu,tulienda kuchimba mihogo tumtengenezee bibi yako unga wa kuondoka nao"
Mimi "Sawa mama haina shida"
Mimi "Sidhani kama nitakaa sana,maana nimetumwa ba Ba'mdogo "
Mama Monica "Mwalimu anasemaje?"
Mimi "Mama niliwaeleza jambo uliloniambia na wamekubali"
Mama Monica "Kweli?"
Mimi "Kweli mama"
Mama Monica "Basi wewe nenda ukawaambie nakuja,ngoja nijiandae nikawachukue wenzangu tunakuja"
Sikutaka kupoteza muda nilitoka nduki kurudi nyumbani kwasababu ilikuwa tayari ni usiku!.Nilifika nyumbani mida ya saa 2 usiku nikamueleza headmaster na mkewe na wao wakawa wanawasubiri!.
Kila mtu hapo nyumbani alikuwa amekwisha kuoga ile dawa na hata Ema ambaye nae pia wakati naondoka sikkumuacha ila alipo rudi alipewa maelekezo namna ya kuoga ile dawa!.
Sasa wakati usiku tukiwa tunakula,nilisikia mlango wa nje unagongwa,Ema alienda kufungua ule mlango na alikuja kuniita akisema naitwa!.Basi nilinyanyuka kuelekea nye ndipo nikamuona mama yake Monica akiwa na wale wanawake wawili,safari hii walikuja wakiwa wamevaa nguo za kawaida na wametanda Khanga!.
Mimi "Karibu mama"
Mama Monica "Haya tushafika,hao wapo?"
Mimi "Wapo mama,ingieni ndani?"
Basi waliingia mpaka uani wakawa wamesimama,mimi niliingia ndani kumwambia headmaster.
Mimi "Amekuja baba"
Headmaster "wewe msukuma njoo tule bhana"
Mama Monica "Nyie endeleeni sisi tumekula"
Headmaster "Toa viti hapo nje"
Basi nikatoa viti vya idadi ya wale kina mama nikapeleka!.
Tulivyomaliza kula,headmaster alitoka nje na mkewe ili kumsikiliza mama yake Monica!.
Headmaster "Mmh!,we msukuma lete maneno"
Mama Monica "Mimi nipo mkurya"
Mazungumzo ya kutaniana kati ya headmaster na mama yake Monica yalipokwisha maliza,sasa usiriasi ulichukua nafasi!.
Headmaster "Huyu kijana wangu amenifikishia yote uliyomwambia,na sisi tumeyapokea kwa mikono miwili"
Aliendelea "Hebu nisaidie maana nimeshahangaika sana na sijui nitakulipa nini nikifanikiwa"
Aliendelea "Hayo yaliyopita tuachane nayo,mimi na wewe tuanzie hapa sasa!"
Mama Monica "Tusipoteze muda,nileteeni karai na maji"
Nilichua karai nikasogezea mama yake Monica.
Alisimama akafungua mfuko uliyokuwa na makorokoro mengi yasiyoeleweka,alichukua unga akawa amemwaga ndani ya yale maji kwenye karai,baada ya hapo alizungumza kisukuma na mmoja ya wale kina mama ndipo mmoja wapo akawa amebeba lile karai na kutoka nje,haukupita muda akawa amerudi yale maji ndani ya karai yakiwa yameisha!.
Mama Monica "Leo wabaya wako wapo kwenye kikao mwalimu,hivyo wakiishatoka tu lazima waje hapa,wakifika hapa ndipo wataipata freshi"
Aliendelea "Sasa nawapatia hii kitu kila mmoja ahakikishe analala nayo kwa kuishikiria na usije ukaiachia"
Alitukabidhi watu wote kitu kikiwa kimeshonwa na kitamba kigumu mno,mimi sikupata shaka kuelewa kwamba ile ilikuwa ni irizi!.
Mama Monica "Hizi hapa mtapakaa kila mtu usoni kabla ya kulala"
Aliendelea "Mwalimu shika hii"
Headmaster alipewa kibuyu kidogo kama kile ambacho nilipewa mimi siku ile.
Mama Monica "Hiki kibuyu hakikisha unakiweka nyuma ya kona ya mlango"
Headmaster "Sawa"
Mama Monica "Mwanangu shika hii"
Na mimi pia alinikabidhi kile kibuyu kidogo na akanitaka nikiweke nyuma ya mlango kwenye kona.
Mimi na ndugu zangu hawa tutakuwa mazingira ya karibu,hivyo msiwaze!.
Headmaster "Kwahiyo hapa ushamaliza?"
Mama Monica "Kila kitu tayari"
Aliendelea "Msije mkapiga kelele kwa mtakachokiona,mkipiga kelele tu ,mtakuwa mmeharibu kila kitu!"
Mama Monica "Kama kuna mtu anajua hatokuwa mvumilivu aseme kabisa"
Baada ya hilo swali na wote kumuhakikishia tutakuwa wavumilivu ndipo aliendelea akasema.
Mama Monica "Mwalimu utakachokishuhudia wewe simama na chukua kibuyu nilichokupatia na ukifungue kikae wazi"
Aliendelea "Ukishakifungua tu,huyo mbaya wako atajuta kuitembelea hii nyumba"
Baada ya muda mama yake Monica na wale kina mama waliaga kuondoka,Headmaster na mkewe walitoka kuwasindikiza.
😂😂😂 Hapana Mkuu, nasoma huku SMG nimeikumbatia kama demUkinogewa wahuni watapita na SMG mkuu😂
Uishi na mchawi hachelewi kukutoa sadakaKwa ninavyoona hii story ikawa mwanzo wa story nyingine ya maisha baada ya kuwakomesha wachawi. Yaani maisha ya Umughaka na Monica hadi Umughaka kumaliza shule na kuanza kujitegemea ilihali Monica alikuwa mjamzito.
Je Monica alizaa?
Walioana?
Wanaishi pamoja au waliachana?
Mm nadhni umughaka ndio amemuoa Monica na anaishi na sas HV tusibiri tuone Wenda jama akaja na nmna walivyo ishi na Monica toka 2004 had 2022 siyo mchezoKwa ninavyoona hii story ikawa mwanzo wa story nyingine ya maisha baada ya kuwakomesha wachawi. Yaani maisha ya Umughaka na Monica hadi Umughaka kumaliza shule na kuanza kujitegemea ilihali Monica alikuwa mjamzito.
Je Monica alizaa?
Walioana?
Wanaishi pamoja au waliachana?
Kusubiria sasaaaaa! Sijui ni kesho……..sijuini leo hii hii jioniiii!UMUGHAKA nafikiri episode inayofata ndo inaenda kubeba kichwa cha uzi cha mlichomfanyia huyo Mzee makono ama Mzee lameki hata kaa aje asahau. Staring mama Monica na Monica [emoji23]
Watu mna nongwa.. [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]Oyaa malizia chapu asi apo kila mtu apite ivi na mambo ake asee
Atutaki kuelewa sisi tunataka shoo iisheWatu mna nongwa.. [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]