Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Baada ya mama mdogo kurudi Toka Senta ,nikawakalisha na Baba mdogo ,nikawaambia kuhusu dawa niliyopewa na mama Monica,pia nikawaambia dawa hii sharti lake mama mdogo natakiwa nimpake Mimi,akijipaka mwewewe haitafanya Kazi,Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 23.
Baada ya mazungumzo ya muda mrefu pale nje,mama yake Monica alituaga akawa ameingia ndani kwa ajili ya kulala,basi na sisi hatukutaka kupoteza muda kabisa tukawa tumeingia ndani ya kwa ajili ya kulala.Ilipofika asubuhi niliamaka mapema nikawa nimemwambia Monica inapaswa nielekee nyumbani!,siku hiyo nakumbuka ilikuwa jumamosi.
Monica "Subiri basi mama aamke kwanza"
Basi Monica alinipatia maji nikanawa uso kisha nikarudi ndani kusubiri hadi mama yake aamke maana alikuwa ameniambia usiku ya kwamba angenipatia kitu ambacho ningeenda nacho nyumbani ili kitusaidie!.
Ilipofika mida ya saa 1 asubuhi mama yake Monica alikuwa ameshaamka na alikuja kugonga mle ndani nilimo lala ili atusalimie,wakati huo nilikuwepo mimi peke yangu na Monica alikuwa yupo jikoni akiandaa uji kwa ajili ya mlo wa asubuhi!.
Mama Monica "Hujambo baba"
Mimi "Sijambo mama,shikamoo!"
Mama Monica "Marhaba,baba yangu"
Aliendelea "Mbona mapema yote hii,unawahi wapi?"
Mimi "Nilitaka kuwahi nyumbani mama nikaendelee na shughuli zangu,siunajua tena ninapaswa kuelekea senta"
Mama Monica "Ni kweli baba"
Aliendelea "Basi njoo umsalimie bibi yako"
Basi nilitoka mle chumbani nikaelekea mpaka nje ya mlango wa ile nyumba aliyokuwa amelala bibi yake Monica!.Kwakuwa kisukuma changu kilikuwa cha salamu tu na kuombea maji ilibidi mama yake Monica niwe naongea halafu na yeye anamtafusiria bibi maana alikuwa hakijui kiswahili hata tone!.
Baada ya salamu na mazungumzo mafupi,mama yake Monica akawa amenitolea kiti nje akanitaka nikae nisubiri uje uive ninywe wakati ambao yeye ananiandalia mitishamba na dawa aliyokuwa ameniambia angenipatia.Kiukweli niseme tu ukweli,mama yake Monica alitokea kunipenda sana na kuna muda nilikuwa nikifika pale kwa Monica najihisi niko kwenye dunia nyingine,mara kwanza nilikuwa naogopaga sana,lakini baada ya kuhakikishiwa usalama wangu,kwakweli sikuwa naogopa tena!.Yule mama alikuwa yuko radhi afanye jambo lolote ili mimi na mwanaye tusalimike!.
Basi haukupita muda Monica akawa ameivisha uji na maboga akatenga kwenye jamvi!,nilishuka kutoka kwenye kiti na kukaa kwenye jamvi kwa ajili ya kupata brekifasti!,kama ambavyo nilisema hapo awali,ile familia haikuwa na hela ila ilikuwa na uchawi wa kutosha!,kunywa uji usiyokuwa na sukari halikuwa jambo la mjadala na kiukweli japo sikuwahi kunywa uji wa sukari hapo kwa Monica lakini uji ulikuwaga mtamu sana kwasababu walikuwa wakiweka maziwa!,hivyo kuufanya kuwa mtamu sana!.Nilipomaliza kupata ile brekifasti,mama yake Monica aliniita ndani ya nyumba kubwa kule alikokuwa amelala bibi yake Monica.
Mama Monica "Mwanangu nisikilize kwa makini!"
Aliendelea "Najua wewe na mwanangu mtakwenda kuniletea mjukuu hivi karibuni,hivyo wewe ni mtu muhimu sana kwasasa katika familia hii"
Mama Monica "Najua Mwalimu Wambura ni Mkurya wa Musoma huko na ndiyo maana ni mjeuri,ila wewe nimekupenda kwakuwa unanisikiliza sana mwanangu,nakuomba usije ukachukua roho ya mwalimu Wambura!"
Aliendelea "Naamini hautanitesea mwanangu pekee Monica"
Mama Monica "Baba yake alikufa angali bado mdogo,hivyo nimemlea kwa matatizo makubwa mno!"
Aliendelea "Tulihamia huku baada ya kufukuzwa huko Ilungu-Magu,na hii yote ni kwasababu ya baba yake Monica"
Mama Monica "Haya yote unayoyaona tumerithishwa na huyu bibi yako unayemuona ningali binti mdogo"
Aliendelea "Kwakuwa baba yake Monica alitaka kuniulia mwanangu wa pekee kwenye michezo yao,ndipo huyu bibi yako tukasaidiana kummaliza kabla hajafanya jambo baya".
Aliendelea kusema "Baada ya mambo kuharibika ndipo tukahamia hapa,kutoka huko Ilungu".
Aliendelea kusema "Hivyo nikuombe mwanangu,hata nikifa leo,nakuomba umtunze mwenzio kwa gharama kubwa maana aliniambia anakupenda sana".
Aliendelea kusema "Mwanangu hajasoma,lakini ni mwerevu na anajua mambo mengi,hivyo na wewe nakuomba umpende!.
Kiukweli siku hiyo mama yake Monica aliamua kunipasulia ukweli kuhusu mwananye na familia yake kwa ujumla, ndipo nikaona kabisa nilikuwa nimethaminiwa kwa kiasi kikubwa na ile familia.
Mimi "Mimi nampenda sana Monica mama na sitaki kumpoteza na yote uliyoongea nimekusikia!".
Mama Monica "Sawa nisubiri nakuja".
Mama yake Monica aliingia chumbani akawa anazungumza na bibi yake Monica kisukuma.Sasa wakati nikiwa nasubiri mama atoke chumbani,ndipo Monica naye akawa ameingia ndani!.Haukupita muda mama yake Monica alitoka ndani akiwa amebeba furushi la mfuko wa rambo la blue!.
Alianza kuufungua ule mfuko kisha kutoa vitu ambavyo sikuvielewa.
Mama Monica "Kamata hii"
Aliendelea "Hiyo niliyokupa ukifika pale nyumbani kwenu,nenda kule nyuma lilipo dirisha la chumba cha Mwalimu na uhakikishe unachimbia chini usawa wa dirisha!".
Mimi "Sawa mama"
Aliendelea "Kamata na hii"
Alisema " Hii naomba umwambie mwalimu aogee yeye na mkewe,halafu wakimaliza kuoga wajipake hii hapa".
Aliendelea kusema "Wewe na mwenzio pia mfanye hivyo hivyo,baadae nitakuja mimi mwenyewe na nitakupatia maelekezo namna ya kufanya"
Mama Monica "Nataka kumsaidia mwalimu ili aepukane na hii fedheha ya yule mpumbavu na wenzie"
Aliendelea "Mwalimu amewahi kunitusi na tulikuwa hatusalimiani,ila inapaswa akushukuru sana wewe".
Mimi "Mwalimu hatakataa nikimwambia?"
Mama Monica "Wewe mwambie,akikataa shauri yake"
Aliendelea "Kama anataka kuondoa fedheha na kumuahibisha mbaya wake mwambie atumie,akikataa usimlazimishe muache".
Mimi "Nashukuru sana mama"
Mama Monica "Andaeni sherehe kesho mtafurahi na itakuwa fedheha hapa kijijini"
Basi baada ya mama yake Monica kunikabidhi zile dawa nikawa nimeaga na kuondoka kurudi nyumbani.Muda huo ilikuwa yapata saa 3 asubuhi.
Baada ya kutembea kwa muda namshukuru Mungu nikawa nimefika nyumbani salama,nilipofika mida hiyo bado sikumkuta mtu yeyote pale nyumbani!.Basi niliingia stoo nikachukua jembe nikazunguka kule nyuma ya nyumba ambako kulikuwa na dirisha la chumba alichokuwa analala Ba'mdogo.Nilichimba haraka haraka na kufukia ile dawa kama ambavyo mama yake Monica alikuwa amenielekeza.
Nilipomaliza nilirudisha jembe stoo kama kawaida,nilichukua dumu la maji nikaelekea lamboni kuchota maji ili nije nikaoge ile dawa ambayo alinipatia maelekezo na kututaka wote tuoge kama tunataka kuwa salama ikiwemo Headmaster na mkewe!.Basi baada ya kumaliza kuoga nilianza zoezi la kuosha vyombo na kumwaga ule ugali nikiyokuwa nimeupika jana na ukakosa walaji!.
Baada ya ile kazi iliyochukua muda wangu mwingi,niliingia ndani kulala!.Nilishituka nikiwa naamshwa na Ema mida ya Saa 7 mchana,wakati huu jamaa alikuwa akijechekelesha chekelesha na nikajua kutakuwa na kitu lazima kwasababu haikuwa kawaida yake,mara nyingi alikuwaga akiharibu mahali basi alikuwa akinichangamkia sana kwakuwa mimi nilikuwa mtetezi wake!.
Mimi "Vipi".
Ema "Mwanangu si Headmaster amenifuma nampiga Deborah mate"
Mimi "Amekufuma wapi"
Ema "Situlikuwa tumesimama pale karibu na ule muale".
Mimi "Sasa amewaona vipi"
Ema "Yaani mwanangu na mimi sifahamu,nimeshituka namuona huyu hapa"
Mimi "Amekwambia nini"
Ema "Ametuchora tu,hajaniambia chochote"
Nilijua tu atakuwa ameharibu mahali na ndiyo maana akajifanya kuja kwangu na kuanza kujichekesha!,kimoyo moyo nilimuhurumia maana nilijua fika stiki atakazokutana nazo si za kitoto!.
Sasa ilipofika mida ya saa 9 alasiri nilitoka zangu ndani na kwenda kumsalimia Headmaster ambaye alikuwa amesharudi,lakini haikuwa kawaida yake nilivyomuona,kiukweli alio alionekana kama mtu aliyekata tamaa na kuchoka kwingi,sasa sikufahamu huko alipokuwa ameenda kilikuwa kimemkuta nini!.
Headmaster "Hivi mwalimu Dani huwa unafahamu anapokaa"
Mimi "Hapana,sijawahi kufika kwake"
Headmaster "Hebu mwambie huyo mjinga aje nimuagize"
Basi nilitoka kwenda kumuita Ema.
Headmaster "Wewe mwalimu Dani siunapafahamu anapokaa?"
Ema "Eeenh,napajua"
Headmaster "Nenda ukimkuta umwambie akupatie mzigo wangu,na uwahi kurudi".
Basi baada ya Ema kuondoka,nilimwambia baba nilikuwa nina mazungumzo nae yeye pamoja na mama.
Headmaster "Kwani huwezi kuniambia mimi mpaka awepo mama yako mdogo?"
Mimi "Ni vizuri akiwepo na mama baba"
Headmaster "Sawa,nilimuacha kwa mama Salome,ngoja tumsubiri arudi".
Nilitaka awepo Maza mdogo maana nilifahamu ningemwambia Headmaster angeweza kukataa,ila Maza mdogo akiwepo isingekuwa rahisi yeye kukataa!.
Monica Umughaka
Monica ni mweupe kidogo ila umbo wamefananaMonica UmughakaView attachment 2386631
Hahaaa....mooosarheka!Tamoha amasenti tata[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Sent from my SM-T555 using JamiiForums mobile app
Pisi ya ukweli na hapo ipo naturalMonica UmughakaView attachment 2386631
So ajabu uwezi kusoma kitabu Cha story ila ya umughaka anaangaika kumlaumu Mbna vitambu viko vingi Sana vya story ,.Wewe jamaa unaringa Hatari Aisee...
Yaani kastory kakuisha siku moja ila visingizio kama vyote mwamba.
Mara oon sijui hiki mara kile.
Tushawazoea wasimuliaji wote wa Jf wanamalingo kuanzia ile story ya mpwayungu hata yako wewe pia kwanza unatunga.
Ahsante
Yaani sahih San mm mwenyewe namshanga namuona jamaa analalamika as if kwamba Hana kitu kingine Cha kuperuzi sas namtaka UMUGHAKA piga Kaz zako Hadi utulie ndio uandike usiache Kaz zako uje uwafurahiishe watu hat kipande kilichobaki ukileta week ijayo nayo ni sawaa tuSi bure, kuna kitu umefanya kitandani. Kama sio umeumwaga basi utakuwa umekata gogo kabisa.
Pengine labda jana haukushiba umeamka ni hasira yako ya kulazwa njaa.
Mtu mwenye kuelewa majukumu na uwajibikaji hawezi asubuhi hii kuamka analilia story. Ukikosa unapita kushoto unaendelea na mengine.
Tatizo unageuza story kuwa kisubirishio cha chai na mkate.
Acha kuwafananisha mtot wa watu na wachawiMonica UmughakaView attachment 2386631
Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe - 3
Baada ya kuambiwa yale maneno na yule jamaa kiukweli ilibidi niwe na tahadhari ingawa mpaka wakati huo sikutaka kabisa kuamini mambo ya kishirikina.
Sasa nakumbuka Jumamosi moja kama kawaida niliamka na shughuli za hapo nyumbani zilichukua nafasi ikiwemo kwenda lamboni kuchota maji na kuleta hapo nyumbani.
Headmaster ambaye alikuwa ba'mdogo wangu yeye ijumaa tu alikuwa ameshaondoka kuelekea mjini kuiona familia yake, kama nilivyowaambia ya kwamba, kila ilipofika Ijumaa ya kila wiki alikuwa akiondoka na kurejea jumapili jioni kwa ajili ya mambo ya shule!
Sasa siku hiyo kulikuwa kuna mechi kati ya Arsenal na Blackburn ambayo ilikuwa inachezwa saa 12 jioni, lakini pia kulikuwa na mechi nyingine!,kama kawaida ilipofika saa 11 jioni nilimwambia jamaa tuondoke tukacheki gemu akagoma akadai ataenda kusoma baadae kwao na demu wake! Basi nikachukua zangu tochi au taa ya sola kwa ajili ya kumulika njiani pindi nitakaporudi maana ingekuwa usiku.
Kipindi kile kulikuwa na vile vitaa vya sola ambavyo ulikuwa unaviweka juani vinapata chaji halafu usiku vinamulika kama taa ya umeme, vilikuwa na mwanga sana!,sasa hapo nyumbani vilikuwepo 2,moja alikuwa anaitumia Headmaster chumbani kwake na nyingine alikuwa anaitumia jamaa kule kwenye chumba alichokuwa akilala.
Ile nyumba ilikuwa na chumba na sebule pamoja na stoo,lakini kwa nje pia kulikuwa na chumba kimoja ambacho pembeni yake kulikuwa na jiko ambalo humo humo ilikuwa stoo. Kulikuwa na milango miwili mikubwa, mmoja ulikuwa wa mbele ambao mara zote ulikuwa ukifungwa lakini pia kulikuwa na mlango wa nje ambao ulikuwa umeshikamanishwa na ukuta wa fensi,huu mlango ndiyo ulitumika mara zote kutoka na kuingia!
Sasa wakati naondoka nilimwambia jamaa anipe kile kitaa chake niende nacho halafu yeye angetumia kile cha Headmaster.
Niliondoka zangu kuelekea kucheki boli kama kawaida,ijapokuwa jamaa alinionya kuhusu ile njia sikutaka kabisa kuacha kwasababu ilikuwa fupi kuliko ile aliyokuwa amenielekeza ya kupitia lamboni ambayo ilikuwa ya mzunguko!.Wakati huo mvua ilikuwa imemaliza kunyesha kama siku mbili zilizopita,hivyo bado ardhi ilikuwa na unyevunyevu wa kutosha!
Nilifanikiwa kufika lakini nilikuta tayari mechi imekwisha kuanza. Sasa baada ya kutazama mechi ya Arsenal ambayo tulishinda 2-0,nilitazama na mechi nyingine. Mpaka namaliza kutazama mechi ilikuwa yapata saa 3 usiku,nikaamua sasa ni wakati wa kurudi nyumbani.
Kabla sijaondoka niliwaza nipite njia ipi kati ya zile mbili,lakini nilifikiria ile njia ya lamboni ilivyo ya mzunguko ingenichukua muda mrefu kufika,nikaona nirudi na ileile niliyoizoea,nikajifariji kwa kuwa nilikuwa na taa ya sola hivyo kisingeharibika kitu!
Basi bana nikaanza mdogo mdogo kupiga kwato huku nikimulika mulika kwa madaha njia nzima,nina tochi tena!,utaniambia nini!.Sasa kadri nilivyokuwa nikisogea ndivyo utulivu na ukimya ulivyo tawala,kama kawaida nikawa nimeikaribia ile miembe miwili ambayo kila nikifika hapo moyo wangu unashituka sana,sasa safari hii sikuona moto wala nini, nikasonga kuikaribia ile miembe,sasa nilipofika katikati ya ile miembe mikubwa nikahisi kuna mtu nyuma yangu na nikageuka ghafla lakini sikuona mtu, nikahisi yalikuwa mawenge tu ya kitete,kiukweli nilikuwa nasisimkwa na nywele sana kila nikifika hilo eneo!.
Sasa ili kujiamini na kutoa uoga,niliamua kunyanyua kile kitaa na kuanza kumulika juu ya ile miembe angalau nione kuna nini ili nipite kwa amanj, nilipomulika sikuona chochote, sasa ile nashusha tochi chini ghafla nikajikuta nimejikwaa kwenye kitu ambacho sikukiona hapo awali, kiukweli nilianguka pale chini na ile taa ikawa imeanguka kwa mbele na kuzimika, ndala moja pia ikawa imechomoka mguuni nikawa nimebakiwa na moja, sasa nikawa najiuliza nini kile ambacho kimefanya nimejikwaa mpaka nimeanguka, niliamka kwenda kuchukua kile kitochi nikawa nakiwasha nimulike kutafuta ndala yangu ili nivae niondoke lakini kinagoma kuwaka,sasa ikabidi nianze kukipiga piga nikadhani uenda kilipata hitilafu!
Nimekipiga piga sana hatimaye kikawa kinawaka na kuzima, kinakaa muda kinawaka halafu kinazima, nikaendelea kukipiga tena sasa kikawaka kama ilivyokuwa mwanzo, ikabidi nianze kumulika kuitafuta ndala yangu itakuwa imehangukia wapi!,sasa ile namulika kwa nyuma nikaona mtu amelala akiwa uchi wa mnyama!,daaah nikashituka sana na nikataka kukimbia lakini nikajikaza na kuanza kuita kwa nguvu "wewe ni nani?" Niliita sana lakini mtu yule alikuwa hasemi wala hatikisiki,nikagundua uenda ndiye aliyefanya nikadondoka ingawa wakati najikwaa nilihisi kitu kama jiwe na maeneo yale hakukuwa na mawe!.
Sasa akili yangu ikadhani uenda yule mtu alikuwa mlevi ambaye alikuwa amekunywa pombe zikamzidi akawa amelala pale chini,nilisahau kutafuta ile ndala akili yangu ikaamia kwa yule jamaa,nilimsogelea na kuanza kumtikisa kwa mguu huku nikisema " wewe....wewe....wewe" lakini hakuamka,nilipomulika vizuri nikagundua ile ilikuwa maiti na hakuwa mlevi kama nilivyodhani.
Hakuna siku ambayo sitakuja kuisahau kama ile siku na ndipo nikaamini kuna wachawi!,sikumbuki nilifikaje nyumbani mpaka wakati huo maana nilipopata kumbukumbu nilijikuta nipo kwenye mlango wa nyumbani nikiwa ninahema balaa! Kibaya zaidi pale nyumbani nilikuta jamaa hayupo na mlango wa kuingia ndani ukiwa umefungwa kwa nje na kofuli,niliamua kukaa chini kwanza ili kutuliza presha nikawa najiuliza kile nilichokiona kilikuwa kweli au uenda nilikuwa naota? Baada ya kutulia kwa dakika kadhaa, kujiangalia chini nilikuwa peku na kile kitochi nacho sina mkononi!.
Sasa nikawa nimekaa pale nje kwa uoga mwingi,kwakuwa jamaa aliniambia angeenda kwao demu wake kusoma nikaondoka kuelekea kwao yule demu wake ili nikachukue funguo nirudi kulala,wakati naenda nilipitia njia ya lamboni lakini sikutaka kabisa kutembea ilibidi nikimbie maana ilikuwa usiku wa saa 4 kuitafuta saa 5, kiukweli nilikuwa nikifika kwenye vichaka nilikuwa napita kwa spidi kali mno kama ngiri!
Nilipofika kwa na yule demu wake jamaa nikaona mbwa wanaanza kubweka kwa sana!,sasa ile boma yao ilikuwa imezungukwa na miti na katikati kulikuwa na zizi kubwa la ng'ombe,nyumba aliyokuwa akilala yule binti na mdogo wake ilikuwa kwa pembeni ambako ilinibidi kufanya kazi ya kuzunguka ili kuwakwepa wale mbwa!
Nilipofika kwa nyuma nilichungulia kwenye upenyo wa kidirisha nikaona kuna mwanga,basi angalau moyo wangu ukatulia nikajua walikuwa wakijisomea.Nilianza kugonga nikimuita jamaa ili asikie aje anipe funguo za nyumba,sasa wakati nagonga na kumuita jamaa yule demu wake aliuliza "we nani?"
Mimi " Mimi Umughaka"
Demu " oooh,ngoja nije"
Basi yule demu akafungua nyumba akaniambia "Zunguka huku mbele".
Kwakuwa alikuwa ametoka nje,sikuwa tena na mashaka kuhusu wale mbwa.
Mimi " Mambo Debo"
Deborah "Poa umughaka"
Deborah "vipi mbona usiku?"
Mimi " Mwambie ema aniletee funguo"
Deborah "Kwani hayupo nyumbani?,na wewe kwani ulikuwa wapi?"
Mimi " Mimi natoka senta kuangalia mpira,wakati naondoka aliniambia angekuja huku kwa ajili ya kujisomea"
Baada ya yale maelezo yule demu akaniambia wala huyo jamaa aliyeitwa emmanuel hakwenda kwake,sasa akaniambia huenda alienda kwa rafiki yake mmoja alikuwa akiitwa maganga.
Mimi "Duuu sijui nitafanyaje na mlango amefunga"
Deborah " Kwani kwao maganga hupafahamu?"
Mimi " mimi napajua hapa kwenu tu Debo,kwao marafiki zake sipajui!"
Debo "Nisubiri nivae nije nikupeleke".
Mimi "Kama ni mbali tusiende ni bora nikarudi ili nisije kupishana nae njiani"
Debo " Yule mimi naijua akili yake,unadhani anarudi muda huu,utakaa nje mpaka uchoke,wewe subiri nije nikupeleke"
Basi baada ya Deborah baada ya kujiandaa alitoka ndani na taa ya chemri tukandoka kuelekea kwa huyo Maganga ambaye ni rafiki yake na jamaa ambapo Deborah aliyekuwa demu wa jamaa alidhani uenda angekuwa hapo!
Tulipofika hapo kwao Maganga tulianza kumgongea,cha ajabu jamaa akatoka akionyesha kabisa alikuwa amelala!.
Maganga " Mambo vipi"
Deborah " Poa,Ema yuko wapi?"
Maganga "Alipita hapa mida fulani akaniambia anaenda kupiga buku kwao Jackson"
Deborah "Jackson yupi?"
Maganga "Jackson Mashida"
Maganga "Kwani kuna nini?"
Deborah "Aah ameondoka na funguo za nyumba,sasa ndugu yake alikuwa anazihitaji!"
Maganga " Nendeni kwao Jack mtamkuta"
Basi tuliondoka tena nikifuatana na binti Jasiri Deborah,ingawa ilikuwa saa 5 ya usiku lakini Deborah hakuonyesha kabisa kujali hilo,nadhani kwakuwa wao walikuwa wamezaliwa vijijini na kukulia huko haikuwa taabu kwao!.
Haikupita muda tukawa tumefika kwa huyo dogo tuliyeelekezwa kwao.
Tulipofika Deborah aligonga mlango na hatimaye mlango ulifunguliwa!.
Jamaa "Oooh Debo mambo"
Debo "Poa,vipi"
Debo " Ema yuko wapi?"
Jamaa akaanza kuita "Oyaa ema,njoo unaitwa huku"
Sasa kile kinyumba kilikuwa na chumba na sebule halafu juu kimeezekwa kwa nyasi,mimi wakati huo nilikuwa nimesimama kwa mbali kidogo,Deborah yeye alikuwa pale mlangoni.
Jamaa haikuchukua muda akawa ametoka nje.
Aliponiona akaanza kusema " Aaah kaka,nilijisahau nikaondoka na funguo,ila ningewahi kurudi"
Sasa anasema angewahi kurudi wakati muda huo ni saa 5 ya usiku!,nilimtazama kwa jazba lakini ilibidi nikaushe,sikutaka kunyesha kuchukizwa!
Sasa kumbe wakati ameenda kuchukua funguo ndani si ikasikika sauti ya binti,nadhani kuna kitu alikuwa akimuiliza na jamaa akimjibu.
Kumbe wakati huyo Jackson yeye akipiga buku hapo sebuleni,ema yeye alikuwa akivinjari na kibinti fulani kule chumbani!.
Aliponiletea funguo ndipo Deborah akaanza kumuuliza " Ema huyo ni nani?"
Jamaa akawa anajifanya kama hajasikia "Unasema?"
Baada ya kukabidhiwa funguo nilikuwa namsubiria Debo tuondoke lakini binti wa watu akaanza kuwaka,akaiweka ile taa chini akasukuma mlango akazama mpaka ndani!,baada ya muda akatoka amemkwida binti fulani ambaye alikuwa yupo na chupi tu!,ngumi na makonde ya kike yakaanza kurindima hapo na matusi juu!.
Sehemu ya Nne