Tulichomfanya yule mchawi hatakuja kusahau kamwe

Tulichomfanya yule mchawi hatakuja kusahau kamwe

Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 15.




Kila mcheza ngoma alisimama ghafla na kumtizama yule mzee ambaye ilionekana kabisa alikuwa kiongozi wao.Baada ya hapo alinyoosha mkono juu akiwa ameshika usinga(mkia wa mnyama)ambao sikuweza kufahamu ulikuwa wa mnyama pori au mnyama wa kufugwa!.

Alipoteremsha mkono chini niliona watu wote wameweka mikono mbele kuonyesha unyenyekevu huku vichwa vikitazama chini.Sasa yule mzee alianza kuongea kwa sauti kubwa mno!.

Mzee alisema "Ng'wana Charles"

Aliendelea "Ng'wana ndekeja"

Baada ya kusema hivyo nikaona ananyoosha usinga kuwapa ishara hao aliowaita wasogee mbele,sasa nikaona wazee wawili wamesogea mbele huku wakiwa wameinamisha nyuso chini na mikono imewekwa mbele kuashiria unyenyekevu wa hali ya juu!.

Mzee akasema "Ng'wenagi umnho ng'wenuyo aha"

Basi wale wazee waliondoka na kuingia kwenye ile nyumba ya mama yake Monica,hawakuchukua muda wakawa wametoka ndani huku wakiwa wamembeba mtu ambaye sikumuona kwa haraka,sasa baada ya kumfikisha yule mtu na kumbwaga pale kando ya ule moto ndipo nikamuona vizuri nikawa nimemtambua!,alikuwa ni mzee ambaye alijinasibu ni mganga aliyekuja pale nyumbani kuweka zindiko na kutupiga chale za kutosha!.

Basi yule mzee ambaye ilionekana ndiye mkubwa pale akawa toa amri tena ya kuanza kupiga ngoma na kucheza!,sasa wakati wanacheza kwa kuzunguka ule moto,akajitokeza mama mmoja ambaye alikuwa amejifunga shanga kiunoni na kiremba cheusi kichwani huku mkononi akiwa ameshika kisu!,sasa akamsogelea yule mzee ambaye alikuwa akishanga shangaa kama tahira pale chini,yule mama akafika akamkamata kichwa akaanza kumyoa nywele!.

Wakati mambo yote hayo yanaendelea,mimi na Monica tupo tunachungulia kwenye ule upenyo wa mlango na Monica alinizuia kabisa kutopiga kelele!.

Sasa baada ya lile tukio la kumnyoa yule mzee nywele kukamilika,yule mama alichukua zile nywele akaziweka kwenye kitu kama sahani halafu akamkabidhi yule ambaye alionekana ni kiongozi,sasa wakati anamkabidhi kama kawaida uso uliinama chini kuashiria unyenyekevu!.Baada ya hapo yule mama akaanza kumvua yule mzee nguo zake zote!,alipomaliza aliinama chini kwenye akachukua vitu ambavyo sikuvifahamu akaanza kumpaka yule mzee!.Baada ya kumaliza lile tukio la kumpaka yule mzee vitu visisvyo julikana,akaondoka kinyume nyume kurudi kwenye mstari kuuungana na wenzie kuendelea kucheza ngoma.

Sasa haukupita muda yule mzee tena akatoa ishara ile ngoma ikasitishwa!,baada ya hapo ilikuwa kitendo cha kufumba na kufumbua wakawa wametoweka pale kwenye lile eneo na ghafla kukawa na giza kuu!,nilitaka kufahamu kiliendelea nini na hivyo ikabidi nimuulize Monica.

Mimi "Mbona hawaonekani?"

Monica "Unataka nikupeleke walipoelekea?"

Mimi "Hapana"

Monica "Nakupenda wewe sana ndiyo maana nimekuleta ujionee mwenyewe"

Monica "Mimi nitakulinda wala usiogope"

Aliendelea kusema "Wameelekea kwenye sherehe za kula nyama"

Monica "Ile miembe miwili mikubwa ya kwenye ile njia ambayo tumekutana si unaikumbuka?"

Mimi "Ndiyo"

Monica "Ndo wako hapo"

Mimi "Sasa hapa wameondokaje?"

Monica "wewe bado mdogo ukikuwa utaacha kuuliza uliza maswali"

Sasa nilikuwa nashangaa binti anayeniambia mimi mdogo nabaki kumshangaa kwasababu ulikuwa ukiniangalia mimi na yeye utajua kabisa yeye ndiye mdogo!.

Monica "Halafu wewe una mizimu mikali sana ndiyo maana nataka uwe mume wangu"

Mimi "Mizimu mikali?,mizimu mikali kivipi?"

Monica "Umekuwa ukiwasumbua sana wanapokuwa wakila nyama zao"

Nikashituka sana nikabaki nashangaa mle ndani ambako mpaka muda huo kulikuwa na giza totoro!.

Monica "Unakumbuka siku unapita pale kwenye miembe usiku uliona nini?"

Mimi "Nakumbuka kuna siku nilikuwa natoka senta kuangalia mpira nikaona moto unawaka kwenye ile miembe"

Monica "Achana na mambo ya moto,wewe hukuwahi kuona mtu pale?"

Aisee,sasa nikawa najiuliza huyu binti matukio yote hayo yeye alionaje?,kiukweli nilianza kuingia uoga ila akawa ananisihi ya kwamba nisiogope na yeye yupo kwa ajili ya kunisaidia!.

Monica "Yule mtu uliyemuona siku ile aliliwa nyama,sasa wewe umekuwa ukiwasumbua kupita ile njia kwasababu hakuna mtu anayepita ile njia usiku kama ule".

Aliendelea kusema "Kwa ujasiri ulionao waliona wakujaribu kuona kama unawaona na ndiyo maana walikutega na kukutisha na ulivyotishika na kukimbia wakaona kumbe huna lolote"

Mimi "Sasa nawatesaje?"

Monica "Pale kwenu ni wewe ndiye ambaye huwezekaniki na sijui kwanini,wewe unanyota nzuri mno"

Mimi "Yule mganga amefanya kosa gani"

Monica "Yule ni mjeuri,anaenda kuliwa nyama".


Akaendelea kusema "Kuna siku mama yangu alienda kusenya kuni na mlikutana njiani ukamsaidia zile kuni,hivyo mama yangu akakupenda sana"

Mimi "Mbona sikumbuki siku ambayo nimebeba kuni za mama yako?"

Monica "Wewe bado mtoto mdogo nimekwambia acha maswali utaelewa tu".


Kiukweli nilikuwa ninawaza na kujiuliza sana lakini nakosa majibu!,ndipo sasa nikajua uenda matukio mengi pale nyumbani yalikuwa yanasababishwa na hilo kosi hatari lilikuwa likicheza ngoma,sikutaka kumwambia mama yake ni mchawi ingawa nilimshuhudia kwa macho yangu,nilidhani uenda ningemwambia kuhusu mama yake angenibadirikia mle ndani na nikaipata freshi,sikutaka kabisa kutengeneza matatizo!.

Baada ya maongezi ya muda mrefu mizagamuano ikachukua nafasi!,sasa nikawa nimemwambia Monica inapaswa baada ya mizagamuano ikifika saa 10 usiku anisindikize kurudi nyumbani ili asije akajua mtu yeyote kwamba nilitoka usiku.

Monica "Nalekotogwa natokoreka"

Mimi "Ndiyo nini?"

Monica "Wewe naye,utajifunza lini kisukuma!"

Monica "Nakwambia nakupenda na sitokuacha"

Basi sikutaka kumjibu na mimi akili yangu haikuwa kwake kabisa,kilichokuwa kinanipeleka kwake ni kumpatia maji ya uzima wa milele abdala kichwa wazi ili asihangaike na kiu.
Basi baada ya kasi ya mizagamuano ni kama Monica alipitiwa na usingizi,mimi sikuweza kabisa kupata usingizi kwasababu ya kile nilichokuwa nimetoka kukishuhudia pale!.

Sasa baada ya muda kupita nikiwa natafakari huku usingizi ukianza kunipitia,ghafla nikasikia kishindo kikubwa nyuma ya ile nyumba tulimolala!,sasa nikajaribu kupeleka mkono ili nimpapase Monica ashituke ili na yeye asikie lakini hakukuwa na mtu kwenye godoro!.

Nilikurupuka nikaanza kupiga kelele za uoga kama mwehu!
Ila Mkuu UMUGHAKA Story yako ni nzuri sana Naomba niambie Nikitaka kuchangia Bando hapo natumaje??
 
KUFANIKIWA NA KUFELI KWA MWANDISHI

KUFANIKIWA
1. Mwandishi kafanikiwa kutupa visa vilivyopangika katika muundo mzuri wa moja kwa moja vilivyojaa SUSPENSE ya kufuatilia episode moja baada ya nyingine

2. Uumbaji mzuri wa wahusika umeipamba vilivyo hadithi hii ukichagizwa na mandhari sadifu.


KUFELI KWA MWANDISHI

1. Mwandishi bado katuacha njiani na maswali mengi yaliyopaswa kuhitimishwa kulingana na jina la hadithi mathalani

.a..Inaonekana mzee Makono tu ndiye aliyedhurika katika kisa hiki je wachawi wengine katika kijiji waliishia vipi?

b. Mkasa wa mapenzi ulivyokuwa ukihadithiwa baina ya Umughaka na Monica pamoja na maagano ya kutomuacha kama ahadi ya kumnasua na kurogwa uliishia vipi?
 
Aisee hii shule isije ikawa ni Idete pale wilaya ya Uyui maana niliwahi kutana na visanga pale Ilalwansimba
 
Shukrani sana UMUGHAKA yaani umetuburudisha na kutuelimisha sana. Sasa na mimi naenda kununua kibuyu Kariakoo sokoni kisha nikilala nakiacha wazi ili wachawi wakija wanase na wawe wqnazunguka tu chumbani.

Weka namba ya Tigopesa/M-Pesa/Airtel money nk Basi tukutumie shukrani maana umetuburudisha bure kiroho safi kabisa.....

Atakayependa atakuwekea Muamala kidogo 🙏🙏🙏
 
KUFANIKIWA NA KUFELI KWA MWANDISHI

KUFANIKIWA
1. Mwandishi kafanikiwa kutupa visa vilivyopangika katika muundo mzuri wa moja kwa moja vilivyojaa SUSPENSE ya kufuatilia episode moja baada ya nyingine

2. Uumbaji mzuri wa wahusika umeipamba vilivyo hadithi hii ukichagizwa na mandhari sadifu.


KUFELI KWA MWANDISHI

1. Mwandishi bado katuacha njiani na maswali mengi yaliyopaswa kuhitimishwa kulingana na jina la hadithi mathalani

.a..Inaonekana mzee Makono tu ndiye aliyedhurika katika kisa hiki je wachawi wengine katika kijiji waliishia vipi?

b. Mkasa wa mapenzi ulivyokuwa ukihadithiwa baina ya Umughaka na Monica pamoja na maagano ya kutomuacha kama ahadi ya kumnasua na kurogwa uliishia vipi?
Mkuu Impimpi Mbona nimeeleza vizuri kuhusu wale wachawi wengine!,baada ya wale waliokuwa wameingia ndani kushituka na kuondoka aliyeshughulikiwa ni mzee makono,ndiyo maana hata mama yake Monica alisema watapata habari huko waliko,yaani watasimuliana!,sasa unadhani kwa tukio lile lililokuwa gumzo pale kijijini kuna mchawi alirudi?,nilisema kuanzia hapo Headmaster na nyumba yake viliogopwa na mpaka anahama hakuwahi kuona tena viroja!.

Kuhusu mimi na Monica,nimeeleza vizuri ya kwamba niliondoka hapo kijijini kwenda shule advance na Monica nikamuacha kwao,sikufahamu maisha yake yaliendelea vipi kwa wakati huo huko kwao kwasababu sikuwa hata na simu,ila nikasema kuna mwaka nilikutana na mtu mmoja tuliyekuwa tukifahamiana pale kijijini na akaniambia Monica sikuhizi anaishi Mwanza ila sijajua ni sehemu gani maana hata aliyeniambia aliishia tu kusema anaishi Mwanza,maisha ya mimi na Monica yalikuwa niyale ya ujana lakini baada ya hapo hatujawahi kuonana!
 
KUFANIKIWA NA KUFELI KWA MWANDISHI

KUFANIKIWA
1. Mwandishi kafanikiwa kutupa visa vilivyopangika katika muundo mzuri wa moja kwa moja vilivyojaa SUSPENSE ya kufuatilia episode moja baada ya nyingine

2. Uumbaji mzuri wa wahusika umeipamba vilivyo hadithi hii ukichagizwa na mandhari sadifu.


KUFELI KWA MWANDISHI

1. Mwandishi bado katuacha njiani na maswali mengi yaliyopaswa kuhitimishwa kulingana na jina la hadithi mathalani

.a..Inaonekana mzee Makono tu ndiye aliyedhurika katika kisa hiki je wachawi wengine katika kijiji waliishia vipi?

b. Mkasa wa mapenzi ulivyokuwa ukihadithiwa baina ya Umughaka na Monica pamoja na maagano ya kutomuacha kama ahadi ya kumnasua na kurogwa uliishia vipi?

KUFAULU NA KUFELI KWAKO KWENYE KUMCHAMBUA NDUGU MWANDISHI

KUFAULU
Ume elezea vizuri jinsi matukio,visa vilivyo patikana katika muundo mzuri wa moja kwa moja vilivyo jaa mashaka{suspense} ya kufatilia kipindi{episode} moja baada ya nyengine.

KUFELI KWAKO MTOA MAONI.
Ume haribu kiswahili adhimu/murua katika kujibu kwako,ilifaa utumie misamiati fasaha ya kiswahili pale ulipo weka msamiati wa kwanza ilifaa uweke MASHAKA{SUSPENSE} na KIPINDI{EPISODE.}
 
Kuna matukio fulani ya kichawi yalimtokea mdogo wangu wa damu 5 years back mpaka waleo hao walozi wanamsumbua sumbua sana na kumfatilia dogo! Wakati nasoma hii Story nilikua nilifuatilia hakua kwa step moja baada ya nyingine... na kuna vitu vingine UMUGHAKA umesimulia nikihusianisha na matukio yanayompata dogo umepita muleemuleeeee! Kiukweli Nawish sana kujua hizo dawa ili nimsaidie dogooo japo yeye mpaka waleo hatujui tuwafanyeje kuwaaibisha kisawasawa hao Wachawi wanaomsumbua!
Nenda eagt city centre Kwa pastor Katunzi mpeleke huyo dogo pale Kwa maombi utqkuja simulia hapa Yule pastor katunzi namba wani in Tz nenda tu kanisani Kwa maombi bure kbsa Trust me nimempeleka mtu pale nimeonabkwa macho sasa HV anatoa shuhuda tu
 
Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 25.





Baada ya Headmaster kutoka kuwasindikiza wageni,tuliamua kukaa kikao cha kifamilia na kuzungumza mambo kadhaa yaliyotuweka sawa.Sasa kila mtu alielekea chumbani kulala,baba mdogo na mkewe waliingia chumbani kwao,mimi na Ema pia tuliingia chumbani kwetu kulala.

Siku hiyo mle chumbani hakuna aliyepata usingizi kabisa,kabla ya kulala nakumbuka tulipakaa usoni dawa aliyokuwa ametupatia mama yake Monica,pia tukashikiria na zile hirizi mkononi kama alivyokuwa ameagiza tufanye!.Kadri muda ulivyokuwa ukisonga tuliona kimya,mimi nilianza kupitiwa na usingizi maana nilikuwa nimechoka sana!,kumbe wakati mimi napitiwa na usingizi,Ema yeye alikuwa macho kabisa na jamaa alikuwa na shauku ya kuona ni kitu gani kingetokea!.

Sasa ilipofika mida ya saa 8 usiku,nilishitushwa na Ema akiniamsha!.


Ema "Umesikia hicho kishindo?".

Mimi "Hapana,kishindo cha kitu gani?"

Ema "Kutakuwa na kitu nadhani!"

Ema alikuwa akiniambia kwa sauti ndogo kabisa na yenye uoga ndani yake!.

Mimi "Nyamaza"

Niliamka kitandani nikaenda kuwasha taa,nilifahamu kabisa kile kishindo Ema alichosikia hakikuwa cha kawaida na uenda wale jamaa wakawa wamekuja kama kawaida yao,kiukweli mimi kwa upande wangu sikuwa kabisa na hofu kwasababu kwa siku chache nilikuwa nimeshazoea yale mazingira ya kuwaona wachwawi laivu!.Nilimwambia na kumbusha Ema ya kwamba chochote atakachokiona asipige kelele wala kushituka!.

Haukupita muda,mara ghafla wakaonekana watu watatu wakiwa wamesimama mle chumbani huki wakiwa uchi kama walivyozaliwa,watu wale safari hii walikuja wawili wanaume na mmoja akiwa mwanamke!.Niliwaangalia kwa kuibia kama vile sielewi chochote!,Ema alikuwa akitetemeka sana na nilimpatia ishara ya kwamba atulie kabisa!.Basi nadhani yule mwanamke alihisi jambo maana niliona anamsogelea Ema akawa kama anamtisha aone kama amemuona,sasa alipoendelea kumtisha Ema nikaona anaweza kupiga kelele,nikaanza kumpigisha Ema stori ili kupotezea ile hali!.

Mimi "Mwanangu wewe piga kimya kabisa wala usimfanye chochote yule demu"

Ema "Yule demu mwanangu anazingua kinoma"

Mimi "Halafu Headmaster alisema ukamuamshe aandae yale masomo"

Ema "Halafu kweli umenikumbusha,ngoja nikamuamshe!"

Sasa wakati tunaongea yule mwanamke alirudi kwa wenzie na wakaendelea kushangaa shangaa,tulichokifanya na Ema pale kwa ule muda mfupi ni hakika walidhani hatuwaoni kumbe lengo lilikuwa ni kumuondolea Ema uoga na kuwapoteza maboya!.
Ema aliamka akatoka kwenda kumgongea Headmaster chumbani kwake ili aje ajionee!,sasa wakati Ema ameondoka,nilianza kujipigisha mruzi wa uongo na kweli ili kuikabili ile hali kwasababu ilikuwa inatisha si kitoto!..

Headmaster "Umughaka tacho omahe"

Baba alipotoka nje aliniita kwa kilugha nikawa nimetoka nje,sasa alianza kutueleza ya kwamba tusishituke na tuendelee kuwa watulivu,alitwambia Ema achukue madaftari tuelekee wote sebuleni ili iwe rahisi kuwakabili,mimi nilimwambia wao wakae sebuleni na mimi nirudi chumbani kukaa karibu na kibuyu kwa kazi maalumu!.
Basi wale watu wakawa wamepotea ghafla mle chumbani!,nilitoka nje kwenda kumwambia Headmaster.

Headmaster "Ngoja tusubiri,yawezekana wakawa wameshituka"

Mimi "Lazima warudi"

Headmaster "Halafu mbona yule mzee hayupo?"

Mimi "Uenda leo kawaagiza hawa"

Wakati tukiwa tunaendelea kuongea pale,Maza mdogo akamwambia Headmaster kwa kikurya kwamba,wale watu wako kule chumbani kwake na anawaona,Headmaster akamwambia atulie na asipige kelele!.Sasa tukiwa tunaendelea kuongea pale sebuleni huku Headmaster akijifanya kumpigisha Ema pindi,tukasikia kishindo kikubwa tena pale uani!.

Haukupita muda akawa ametokea yule mzee makono akiwa na usinga mkononi huku akiwa uchi kama wenzie!,akaja mpaka pale sebuleni huku tukiendelea kumpimia tu!,aliendelea kuangaza huku na huko na hatimaye akawa ameingia mle chumbani kwa Headmaster.Basi baada ya kuingia chumba cha Headmaster,Headmaster aliinuka kwa ghadhabu huku akisema "Lero n'uramanye uwe tombanyoko" (Leo utanitambua).

Sasa Headmaster alipoingia chumbani alijifanya kuongea na mkewe huku wakiwatazama,sasa nadhani mzee makono aliwaambia wale watu waende wakawalete watu wa kwenda kulima ili wakifika watuunganishe na sisi tuondoke!,wale watu watatu walitoweka wakamuacha mzee makono mle chumbani akitaka kufanya mambo yake ili amchukue Headmaster kama kawaida aje atuunganishe na sisi tuelekee kwenye kilimo cha usiku kisichokuwa na tija!.

Wale watu walipotoweka tu na mzee makono kubaki mwenyewe,Headmaster alichukua kile kibuyu alichopewa na mama yake Monica akakifungua,alipokifungua tu!,yule mzee akaanza kucheza kwa kuzunguka mle chumbani kama mwendawazimu!.Headmaster alituita tukaingia kumtazama,yaani kuna muda nilianza kumuonea huruma maana alikuwa kama amepagawa kwa kushikwa ugoni.

Kadiri muda ulivyokuwa ukienda,wale watu waliotumwa na mzee makono hawakurudi kabisa na nadhani watakuwa walishituka mapema!.Ile hali ilifanya maza mdogo kutoka kule chumbani akabaki mzee makono akizunguka chumba kizima kama mwendawazimu.Usiku huko hakuna mtu aliyepata usingizi kabisa,tumekuja kushangaa imefika saa 11 alfajiri bila kujua!.
Sasa ilipofika saa 12 asubuhi,Mama yake Monica alikuja akiwa na wale kina mama,alihuzunika sana kwanini tuliamua kuwaachia wale watu watatu wakaondoka!.


Mama Monica "Mwalimu nilikwambia,nadhani sasa unaniamini"

Headmaster "Sikuzote Msukuma nakuamini,si leo tu!".

Mama Monica "Kwanini mmewaachia wale washenzi?"

Headmaster "Wameondoka wenyewe"

Mama Monica "Nilikwambia wakifika tu,ungefungua kibuyu"

Headmaster "Nilipoingia chumbani kufungua kibuyu wakawa wameondoka akabaki mzee lameki"


Mama Monica "watasimuliana,hakuna kilichoharibika"

Aliendelea "Haya sema,unataka tumfanye nini huyu mzee"

Headmaster "Nadhani kama kuna uwezo muondolee uwezo wake asije akaponyoka halafu mengine utaniachia mimi"

Mama Monica "Huyu ameshakwisha,hapa hawezi kukuponyoka kamwe"

Aliendelea "Mimi namshughurikia halafu nakuachia wewe utajua cha kumfanya".


Basi mama yake Monica alimsogelea yule mzee akachukua ule usinga kisha akamvua shanga alizokuwa amejivika kuanzia begani kuteremkia kiunoni!,baada ya hapo kuna dawa alimpatia Headmaster akamwambia kukishapambazuka vizuri atampaka ile dawa na kisha atamuondoa mle ndani!.Mama yake Monica na wale kina mama waliondoka wakawa wamemuacha mzee makono humo ndani akizinguka kama mwehu!.

Kulipopambazuka,Headmaster alielekea kwa mwenyekiti wa kijiji na kutaka yowe ipigwe karibia kijiji kizima ili wananzengo wahalifiwe ya kwamba kulikuwa kuna tukio kubwa la kushangaza!,Basi yowe ilipigwa na watu wakawa wanakuja pale nyumbani huku wengine mikoni wakiwa wameshika mapanga na mafimbo!.Haukupita muda mrefu watu wakawa wamejazana pale nyumbani huku wengine wakichungulia dirishani wakishangaa lile tukio!.

Ilipofika mida ya saa 3 Asubuhi baada ya watu kujazana pale nyumbani,Headmaster alifanya kama alivyoambiwa afanye na mama yake Monica,baada ya kupakwa dawa yule mzee alikurupuka akawa anashangaa sana!,alikuwa akizunguka kitafuta usinga wake lakini hakuuona,ndipo Headmaster aliamrishwa na wananzengo ya kwamba amtoe yule mzee nje ya nyumba ili akapambane na viboko vilivyokosa huruma!.

Yule mwenyekiti aliamuru yule mzee avishwe nguo hadi kwenye ofisi ya serikali ya kijiji lakini wananzengo wakagoma,walisema inapaswa atembezwe kijiji kizima huku akila mboko na inapaswa siku hiyo hiyo ahame kijiji!.

Basi nakumbuka Headmaster alimuagiza Ema akalete viboko ili aanze nae mle ndani kwasababu alikuwa akimtafuta sana,viboko vilipoletwa kiukweli yule mzee alichezea kiasi kwamba sikutaka hata kuangalia,viboko vilipozidi aliamua kutoka ndani spidi akikimbilia nje,kufika nje wananzengo wakamdaka nako wakaanza kumsulubisha!.
Alitembezwa kijiji kizima huku akiwa uchi kama alivyozaliwa,kiukweli lilikuwa ni tukio la aibu mno!,sasa walipomfikisha kwake wananzengo hawakutaka mjadala,walimwambia avae nguo kisha atoke,alipotoka waliwasha moto nyumba yake na kila kitu kiliteketea kwa moto!.

Baada ya pale alirudishwa serikali ya kijiji na kutakiwa apotee kwenye kile kijiji ndani ya masaa 2!,hakutakiwa kubaki pale na wananzengo walimwambia watamuua endapo angebaki kwa siku hiyo!.

Lile tukio lilivuta hisia kubwa sana pale kijijini na kiukweli lilimpatia Headmaster ujiko na heshima sana ingawaje mimi ndiye niliyepambana sana mpaka kufikia ile hali.Headmaster aliogopeka sana tangu siku ile lile tukio litokee na hakukuwahi tena kuwa na mambo ya ajabu pale nyumbani.

Headmaster kwa baadae alihama ile shule na kuhamia huko Biharamulo ambako amejenga na anaishi hadi leo,mimi niliondoka na kurudi nyumbani kisha kuelekea shuleni Advance!.

Ema yupo hapo Shinyanga anauza duka la vipuri vya magari,amejenga na anaishi hapo hapo shinyanga.

Monica kuna wakati niliambiwa yupo Mwanza ila sijajua ni Mwanza sehemu gani!,kuna mtu nilikutana nae wa pale kijijini akawa ameniambia hivyo,kwasababu baada ya mimi kuondoka pale kijijini sikurudi tena hivyo tukawa tumepotezana na mpenzi wangu huyo!.

Mimi kwasasa nipo Dar es salaam napambana na maisha ya kukimbizana!,nina kiboda boda changu japo kimekwisha lakini tunapambana na maisha!.Kijiwe changu huwa ni hapo Bunju ndugu zangu!.



MWISHO.
Bravo
 
Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 11




Safari mpya ya maisha ilianza rasmi pale nyumbani baada ya Maza mdogo kuja,kabla hajaja kutoka mjini tuliishi kwa kujiachia kama vile tupo mamtoni na tulikula na kunywa tutakavyo,lakini sasa yale maisha ya mwanzo yakatoweka,kula nyama ya kuku tena ilikuwa muujiza uliohitaji Mungu mwenyewe kuingilia kati!,kuku wale wa wikiendi walikuwa wakisafirishwa kupelekwa mjini na sisi hapo nyumbani kula Kayabo wa chukuchuku bila viungo,ilifikia sehemu ukila mboga iliyoungwa kwa mafuta na nyanya unamshukuru Mungu kwa muujiza wa kipekee!.
Kuku alipopikwa mimi na Ema vyetu ilikuwa ni miguu,shingo na kichwa na tunyama twa kuzugia kama tuwili hivi,nyama nyingine yote iliyobaki ilimuhusu Maza mdogo na mumewe!.

Tabia ile japo haikuwa nzuri lakini mumewe hakuwahi kuikemea,yeye alitulia tuli kana kwamba mkewe alichokuwa akitenda kilikuwa sawa.Sasa tulidhani siku si nyingi angeondoka lakini kumbe tulikuwa tunajidanganya!.Hatukufahamu kumbe kilichomleta hapo kijijini ilikuwa ni kuweka kambi kwa ajili ya biashara ya ushonaji wa nguo!.Pale senta kwa wakati ule hakukuwa na fundi cherehani,sasa nadhani mumewe alimwambia aichangamkie ile fursa iliyokuwa na hela za kutosha kwa kipindi kile hapo kijijini!.

Basi baada ya yule mzee Masumbuko kukataa ile miwa pamoja na mapapai alinikabidhi,nilimuomba anichumie majani ya mgomba ili nifungie ile miwa nipate urahisi kuibeba,yale mapapai aliniwekea kwenye kigunia cha chumvi chumvi(salfeti).Sasa nikanyanyua mzigo wa miwa nikajitwisha kisha nikamwambia yale mapapai aniwekee juu ya mzigo wa miwa ili nitandike kwato kuitafuta senta.

Ule mzigo haukuwa wa kitoto hata kidogo,lakini sikuwa na wakumdekea!,niliogopa endapo nikiutua ili nipumzike ni nani tena angenitwisha?,hivyo nilikomaa nao hivyo hivyo.Ingawaje Senta palikuwa mbali sikutaka kabisa kupumzika njiani,kuna muda nilikuwa nahisi shingo inauma lakini nilijikaza kisabauni kama mtoto wa kiume niliyetokea jamii ya Kikurya!.

Baada ya safari ndefu hatimaye nikafika senta.Sasa nilitafuta sehemu ambayo ni nzuri na yenye kivuli ili niweke ile miwa na mapapai nianze kuuza.Basi nilisogea kwenye mti mmoja ambao hakuwa mkubwa sana kisha nikaisimamisha ile miwa kwenye ule mti na yale mapapai nikayotoa kwenye ile salfeti nikayapanga yakawa tayari kwa kuuzwa!.

Nilipata taabu sana kuuza zile bidhaa kwasababu aliyesema nikauze hakuniambia niuzeje au alitaka faida ya kiasi gani!,nilichokuwa nakumbuka ni yeye kuununua ule mzigo kwa bei ya shilingi elfu 3.
Sasa ilibidi mimi mwenyewe nijiongeze kwenye namna ya uuzaji ili utoe hela ya watu na faida ipatikane.Nilianza kuuza ule mzigo hiyo mida ya saa 4 asubuhi lakini hakukuwa na wateja waliojitokeza kununua.Ilipofika mida ya saa 5 asubuhi,alikuja jamaa mmoja akiwa amefunga mzigo kwenye baiskeli na kuweka kambi lile eneo nililokuwepo.

Jamaa "Aisee mambo vipi?"

Mimi "Mambo poa"

Jamaa "Mbona umenivamia kwenye eneo langu?"

Mimi "Eneo lipi?"

Jamaa "Hapo ulipoweka mapapai ni eneo langu ambalo huwa naweka biashara yangu"

Mimi "Sikujua kaka,ngoja niondoe"

Jamaa "Hapana usiondoe,wewe sogeza kidogo kule kushoto ili na mimi nikipate kivuli"

Basi nikaamua kuyasogeza mapapai kushoto ya ule mti ambao nilikuwa nimesimamisha miwa.Yule jamaa alikuwa mstaarabu sana,japo kweli nilikuwa nimevamia eneo lake lakini hakutaka kunifukuza pale,alichoniambia ni kwamba nisogeze ili kila mmoja afaidi kivuli cha ule mti!.
Jamaa alifungua ule mzigo kwenye baiskeli kisha akatandika kavelo(turubai) ndipo akaanza kutoa kwenye boksi viatu aina ya kata mbuga(sendeu).Sasa kumbe jamaa ile ndiyo ilikuwa biashara yake pale siku zote ya uuzaji wa kata mbuga!.

Kiukweli baada ya jamaa kufika sikujiona tena mnyonge kwakuwa nilikuwa na mtu wa kupiga nays stori.

Muda ulipozidi kusonga na wateja wa miwa nao walianza kuja,sasa ishu ikawa ni kisu cha kukatia pingiri za miwa ningekitoa wapi!.Kuna kiduka kimoja ambacho kwa nyuma kulikuwa kuna nyumba,nikajongea mpaka pale nikaomba waniazime panga au kisu kwa ajili ya kukatia miwa halafu ningewarudishia!,yule aliyekuwa akiuza kwenye kile kiduka alikuwa mama mmoja ambaye alimuagiza mwanaye aniletee panga ila akasema nikimaliza nirudishe.

Kiukweli miwa niliuza sana ila mapapi hakuna aliyenunua hata moja.Sasa ilipofika mida ya saa 8 mchana nilikuwa nahisi njaa kishenzi na sikujua ningekula nini kwa wakati huo!,sikuwa na namna zaidi ya kukata pingiri tatu za muwa na kuanza kutafuna ili kupoza njaa!.Ilipofika mida ya saa 10 alasiri nilihesabu hela niliyokuwa nayo mfukoni ilikuwa jumla elfu 2600/=,Hiyo ilikuwa ya miwa pekee,papai hakuna lililonunuliwa mpaka muda huo.

Sasa nikiwa naendelea kuuza zile bidhaa pale,kwa mbali nikamuona Ba'mdogo akiwa anakuja pale senta,sasa kwakua alinicheki akiwa mbali hakupata taabu kunitafuta,hata hivyo ile senta haikuwa kubwa kiasi hicho mpaka nishindwe kuonekana.Alipofika niliona kama ananihurumia lakini hakutaka kuonyesha ile hali alijifanya kuvunga.

Ba'mdogo "biashara inaenda?"

Mimi "Ndiyo baba inaenda ila mapapai hayajanunuliwa"

Ba'mdogo "Ningejua ukaja na miwa tu,watu wa huku si walaji wa mapapai,wanapenda miwa"

Sikutaka kumjibu nikawa nimekaa kimya namtazama.

Ba'mdogo "mpaka sasa umeuza shilingi ngapi?"

Mimi "Nimeuza elfu mbili na mia sita baba".

Ba'mdogo "Sawa nipe hiyo hela"

Basi nikatoa ile hela mfukoni nikampatia akawa ameondoka kuelekea kwenye maduka yaliyokuwa upande wangu wa kulia.Hakukaa sana kule akawa amerejea nilipokuwepo.

Ba'mdogo "Yule mama anamuona?"

Akawa anionyesha kwa kidole uelekeo alipokuwa mwanamke mmoja aliyekuwa amekaa kwenye matofali ya kuchoma.

Mimi "Ndiyo baba namuona"

Ba'mdogo "Ikifika jioni hayo mapapai hujauza,nenda umpelekee yule mama,nimemwambia tayari"

Mimi "sawa"

Baada ya maelekezo yale yeye akawa ameondoka na mimi kubaki pale.

Ilipofika mida ya saa 12 jioni,kweli nilimpelekea yule mama yale mamapai baada ya kudoda kutwa nzima pale chini!.

Miwa nayo ikawa imebaki miwili,sasa nikaona nimuombe yule mama aliyeniazima kisu ile miwa niilaze pale kwake ningekuja kuifuata asubuhi,yule mama hakuwa na tatizo alikubali!.

Sasa nikaanza kuwaza wakati wa kurudi nyumbani nipite njia ipi,je nipite ile ya mzunguko wa lamboni au nipite ileile fupi iliyokuwa katikati ya ile miembe mikubwa!.Wakati huo mfukoni nilikuwa nina shilingi 700.Basi nikaone ni heri nipite ile fupi ili niwahi kufika nyumbani.
Nilimuaga yule jamaa tuliyekuwa tukiuza wote hapo nikamwambia tungeonana kesho yake,jamaa nae akawa ameniambia naye angeondoka muda si mrefu.

Nikaanza kupiga kwato mdogo mdogo kurudi nyumbani.Wakati natembea kiukweli nilikuwa nina mawazo mengi sana,ukizingatia nilikuwa sijala chochote zaidi ya kutafuna vipande kadhaa vya muwa!.Niliona kabisa mambo endapo yangenishinda ningerudi nyumbani!.Wakati huo giza nalo lilikuwa halichezi mbali maana ilikuwa mida ya saa 1 usiku.

Sasa wakati natembea huwaga nina kawaida ya kuangalia chini kama kondoo,huwa naangalia mbele,kushoto na kulia kwa muda mfupi sana lakini muda mwingi huwa natazama chini!,sijajua ni kwanini uenda ndivyo nilivyozaliwa na kurithi kwa mzee wangu!.
Sasa wakati nakwenda sikumuona mtu nyuma yangu wala mbele yangu akiwa anakuja,nilishitukia tu ghafla naitwa jina langu na mzee ambaye nilikuwa napata taabu kumkumbuka.

Mzee "Hujambo Umughaka"

Nikashituka sana!,nikabaki nashangaa ametokea wapi yule mzee mtu mzima!,nikadhani uenda muda ambao nilikuwa natembea huku nikitazama chini sikumuona.

Mimi "Sijambo,shikamoo"

Mzee "Marhaba,vipi mwalimu yupo?"

Mimi "Eenh yupo"

Mzee "sawa utamsalimia"

Mimi "Sawa,nimwambie nani vile!"

Mzee "we mwambie Makono anamsalimia"

Mimi "Sawa"

Yule mzee nilianza kuvuta taswira nimewahi kumuona wapi lakini nikawa sikumbuki vizuri!.Alikuwa mtu mzima mwenye miaka kama 50 -60 hivi!.

Sasa wakati natembea zangu nikawa nageuka nyuma ila cha ajabu yule mzee sikumuona!,nikabaki nashangaa kwasababu lile eneo pembe zoni hakukuwa na njia ya mchepuko,pia kulikuwa na katani za kutosha ambazo kama ungejifanya kuchepuka basi zingekuchoma na ile miba yake mpaka uchanganyikiwe na kile kibarabara kilikuwa kimenyooka moja kwa moja.Tulikuwa tumetoka kuzungumza kwa sekunde kadhaa tu lakini cha ajabu kugeuka nyuma sikumuona tena!,Kuhusu jina langu sikuwaza sana nikawa nasema huenda Ba'mdogo aliwahi kumwambia mimi ni kijana wake na jina langu ni umughaka.

Basi namshukuru Mungu siku hiyo niletembea kwa amani kabisa hakukuwa na viroja wala vituko nilivyokutana navyo pale kwenye miembe.Nilifika nyumbani mida ya saa 2 usiku.Sasa wakati usiku tukiwa tunakula Ba'mdogo akawa ameniambia hela niliyokuwa nayo nihakikishe asubuhi naelekea kwa mzee masumbuko kufata miwa mingine ili nikauze kwa kuwa hiyo ndiyo iliyokuwa kazi yangu.

Tulipokuwa tukiendelea kula nikamwambia Ba'mdogo alikuwa anasalimiwa na yule mzee niliyekutana naye muda si mrefu.

Ba'mdogo "Makono?,makono ndiyo nani?"

Mimi "mimi sijui baba,yeye ameniambia nikwambie hivyo utamfahamu"

Ba'mdogo "Uenda atakuwa mzee mwalukala huyo,yule ndiye huwa anamajina mengi ya utani"

Basi mimi sikutaka makuu,nilipomaliza kula nilielekea zangu kulala kwakuwa nilikuwa nimechoka,Ema yeye alipoingia ndani akaanza kupiga buku kama kawaida.
Sasa picha ya yule mzee ikaanza kunijia vizuri na nikakumbuka ni yule mzee ambaye alikuja na mwenyekiti pale nyumbani siku ile ambayo Ema alikuwa ametoka kukung'utwa viboko darasani na watu wasiofahamika.Yule mwenyekiti wakati anakuja na headmaster pale nyumbani kumohoji Ema alikuwa na huyo mzee,ndipo nikawa nimemkumbuka vizuri.

Basi asubuhi mida ya saa 1,niliwahi kuamka lakini sikumuona Ema,nikasema uenda aliwahi mapema kwenda shuleni wakati mimi nikiwa nimelala.Nilipomaliza kupiga mswaki wakati navaa viatu ili niende nikamsalimie Maza mdogo na mumewe ili niondoke zangu,mara nikaanza kusikia sauti za wanafunzi huko shuleni wakipiga kelele kwa nguvu.
Emma kayavagaa tena[emoji23]
 
Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 25.





Baada ya Headmaster kutoka kuwasindikiza wageni,tuliamua kukaa kikao cha kifamilia na kuzungumza mambo kadhaa yaliyotuweka sawa.Sasa kila mtu alielekea chumbani kulala,baba mdogo na mkewe waliingia chumbani kwao,mimi na Ema pia tuliingia chumbani kwetu kulala.

Siku hiyo mle chumbani hakuna aliyepata usingizi kabisa,kabla ya kulala nakumbuka tulipakaa usoni dawa aliyokuwa ametupatia mama yake Monica,pia tukashikiria na zile hirizi mkononi kama alivyokuwa ameagiza tufanye!.Kadri muda ulivyokuwa ukisonga tuliona kimya,mimi nilianza kupitiwa na usingizi maana nilikuwa nimechoka sana!,kumbe wakati mimi napitiwa na usingizi,Ema yeye alikuwa macho kabisa na jamaa alikuwa na shauku ya kuona ni kitu gani kingetokea!.

Sasa ilipofika mida ya saa 8 usiku,nilishitushwa na Ema akiniamsha!.


Ema "Umesikia hicho kishindo?".

Mimi "Hapana,kishindo cha kitu gani?"

Ema "Kutakuwa na kitu nadhani!"

Ema alikuwa akiniambia kwa sauti ndogo kabisa na yenye uoga ndani yake!.

Mimi "Nyamaza"

Niliamka kitandani nikaenda kuwasha taa,nilifahamu kabisa kile kishindo Ema alichosikia hakikuwa cha kawaida na uenda wale jamaa wakawa wamekuja kama kawaida yao,kiukweli mimi kwa upande wangu sikuwa kabisa na hofu kwasababu kwa siku chache nilikuwa nimeshazoea yale mazingira ya kuwaona wachwawi laivu!.Nilimwambia na kumbusha Ema ya kwamba chochote atakachokiona asipige kelele wala kushituka!.

Haukupita muda,mara ghafla wakaonekana watu watatu wakiwa wamesimama mle chumbani huki wakiwa uchi kama walivyozaliwa,watu wale safari hii walikuja wawili wanaume na mmoja akiwa mwanamke!.Niliwaangalia kwa kuibia kama vile sielewi chochote!,Ema alikuwa akitetemeka sana na nilimpatia ishara ya kwamba atulie kabisa!.Basi nadhani yule mwanamke alihisi jambo maana niliona anamsogelea Ema akawa kama anamtisha aone kama amemuona,sasa alipoendelea kumtisha Ema nikaona anaweza kupiga kelele,nikaanza kumpigisha Ema stori ili kupotezea ile hali!.

Mimi "Mwanangu wewe piga kimya kabisa wala usimfanye chochote yule demu"

Ema "Yule demu mwanangu anazingua kinoma"

Mimi "Halafu Headmaster alisema ukamuamshe aandae yale masomo"

Ema "Halafu kweli umenikumbusha,ngoja nikamuamshe!"

Sasa wakati tunaongea yule mwanamke alirudi kwa wenzie na wakaendelea kushangaa shangaa,tulichokifanya na Ema pale kwa ule muda mfupi ni hakika walidhani hatuwaoni kumbe lengo lilikuwa ni kumuondolea Ema uoga na kuwapoteza maboya!.
Ema aliamka akatoka kwenda kumgongea Headmaster chumbani kwake ili aje ajionee!,sasa wakati Ema ameondoka,nilianza kujipigisha mruzi wa uongo na kweli ili kuikabili ile hali kwasababu ilikuwa inatisha si kitoto!..

Headmaster "Umughaka tacho omahe"

Baba alipotoka nje aliniita kwa kilugha nikawa nimetoka nje,sasa alianza kutueleza ya kwamba tusishituke na tuendelee kuwa watulivu,alitwambia Ema achukue madaftari tuelekee wote sebuleni ili iwe rahisi kuwakabili,mimi nilimwambia wao wakae sebuleni na mimi nirudi chumbani kukaa karibu na kibuyu kwa kazi maalumu!.
Basi wale watu wakawa wamepotea ghafla mle chumbani!,nilitoka nje kwenda kumwambia Headmaster.

Headmaster "Ngoja tusubiri,yawezekana wakawa wameshituka"

Mimi "Lazima warudi"

Headmaster "Halafu mbona yule mzee hayupo?"

Mimi "Uenda leo kawaagiza hawa"

Wakati tukiwa tunaendelea kuongea pale,Maza mdogo akamwambia Headmaster kwa kikurya kwamba,wale watu wako kule chumbani kwake na anawaona,Headmaster akamwambia atulie na asipige kelele!.Sasa tukiwa tunaendelea kuongea pale sebuleni huku Headmaster akijifanya kumpigisha Ema pindi,tukasikia kishindo kikubwa tena pale uani!.

Haukupita muda akawa ametokea yule mzee makono akiwa na usinga mkononi huku akiwa uchi kama wenzie!,akaja mpaka pale sebuleni huku tukiendelea kumpimia tu!,aliendelea kuangaza huku na huko na hatimaye akawa ameingia mle chumbani kwa Headmaster.Basi baada ya kuingia chumba cha Headmaster,Headmaster aliinuka kwa ghadhabu huku akisema "Lero n'uramanye uwe tombanyoko" (Leo utanitambua).

Sasa Headmaster alipoingia chumbani alijifanya kuongea na mkewe huku wakiwatazama,sasa nadhani mzee makono aliwaambia wale watu waende wakawalete watu wa kwenda kulima ili wakifika watuunganishe na sisi tuondoke!,wale watu watatu walitoweka wakamuacha mzee makono mle chumbani akitaka kufanya mambo yake ili amchukue Headmaster kama kawaida aje atuunganishe na sisi tuelekee kwenye kilimo cha usiku kisichokuwa na tija!.

Wale watu walipotoweka tu na mzee makono kubaki mwenyewe,Headmaster alichukua kile kibuyu alichopewa na mama yake Monica akakifungua,alipokifungua tu!,yule mzee akaanza kucheza kwa kuzunguka mle chumbani kama mwendawazimu!.Headmaster alituita tukaingia kumtazama,yaani kuna muda nilianza kumuonea huruma maana alikuwa kama amepagawa kwa kushikwa ugoni.

Kadiri muda ulivyokuwa ukienda,wale watu waliotumwa na mzee makono hawakurudi kabisa na nadhani watakuwa walishituka mapema!.Ile hali ilifanya maza mdogo kutoka kule chumbani akabaki mzee makono akizunguka chumba kizima kama mwendawazimu.Usiku huko hakuna mtu aliyepata usingizi kabisa,tumekuja kushangaa imefika saa 11 alfajiri bila kujua!.
Sasa ilipofika saa 12 asubuhi,Mama yake Monica alikuja akiwa na wale kina mama,alihuzunika sana kwanini tuliamua kuwaachia wale watu watatu wakaondoka!.


Mama Monica "Mwalimu nilikwambia,nadhani sasa unaniamini"

Headmaster "Sikuzote Msukuma nakuamini,si leo tu!".

Mama Monica "Kwanini mmewaachia wale washenzi?"

Headmaster "Wameondoka wenyewe"

Mama Monica "Nilikwambia wakifika tu,ungefungua kibuyu"

Headmaster "Nilipoingia chumbani kufungua kibuyu wakawa wameondoka akabaki mzee lameki"


Mama Monica "watasimuliana,hakuna kilichoharibika"

Aliendelea "Haya sema,unataka tumfanye nini huyu mzee"

Headmaster "Nadhani kama kuna uwezo muondolee uwezo wake asije akaponyoka halafu mengine utaniachia mimi"

Mama Monica "Huyu ameshakwisha,hapa hawezi kukuponyoka kamwe"

Aliendelea "Mimi namshughurikia halafu nakuachia wewe utajua cha kumfanya".


Basi mama yake Monica alimsogelea yule mzee akachukua ule usinga kisha akamvua shanga alizokuwa amejivika kuanzia begani kuteremkia kiunoni!,baada ya hapo kuna dawa alimpatia Headmaster akamwambia kukishapambazuka vizuri atampaka ile dawa na kisha atamuondoa mle ndani!.Mama yake Monica na wale kina mama waliondoka wakawa wamemuacha mzee makono humo ndani akizinguka kama mwehu!.

Kulipopambazuka,Headmaster alielekea kwa mwenyekiti wa kijiji na kutaka yowe ipigwe karibia kijiji kizima ili wananzengo wahalifiwe ya kwamba kulikuwa kuna tukio kubwa la kushangaza!,Basi yowe ilipigwa na watu wakawa wanakuja pale nyumbani huku wengine mikoni wakiwa wameshika mapanga na mafimbo!.Haukupita muda mrefu watu wakawa wamejazana pale nyumbani huku wengine wakichungulia dirishani wakishangaa lile tukio!.

Ilipofika mida ya saa 3 Asubuhi baada ya watu kujazana pale nyumbani,Headmaster alifanya kama alivyoambiwa afanye na mama yake Monica,baada ya kupakwa dawa yule mzee alikurupuka akawa anashangaa sana!,alikuwa akizunguka kitafuta usinga wake lakini hakuuona,ndipo Headmaster aliamrishwa na wananzengo ya kwamba amtoe yule mzee nje ya nyumba ili akapambane na viboko vilivyokosa huruma!.

Yule mwenyekiti aliamuru yule mzee avishwe nguo hadi kwenye ofisi ya serikali ya kijiji lakini wananzengo wakagoma,walisema inapaswa atembezwe kijiji kizima huku akila mboko na inapaswa siku hiyo hiyo ahame kijiji!.

Basi nakumbuka Headmaster alimuagiza Ema akalete viboko ili aanze nae mle ndani kwasababu alikuwa akimtafuta sana,viboko vilipoletwa kiukweli yule mzee alichezea kiasi kwamba sikutaka hata kuangalia,viboko vilipozidi aliamua kutoka ndani spidi akikimbilia nje,kufika nje wananzengo wakamdaka nako wakaanza kumsulubisha!.
Alitembezwa kijiji kizima huku akiwa uchi kama alivyozaliwa,kiukweli lilikuwa ni tukio la aibu mno!,sasa walipomfikisha kwake wananzengo hawakutaka mjadala,walimwambia avae nguo kisha atoke,alipotoka waliwasha moto nyumba yake na kila kitu kiliteketea kwa moto!.

Baada ya pale alirudishwa serikali ya kijiji na kutakiwa apotee kwenye kile kijiji ndani ya masaa 2!,hakutakiwa kubaki pale na wananzengo walimwambia watamuua endapo angebaki kwa siku hiyo!.

Lile tukio lilivuta hisia kubwa sana pale kijijini na kiukweli lilimpatia Headmaster ujiko na heshima sana ingawaje mimi ndiye niliyepambana sana mpaka kufikia ile hali.Headmaster aliogopeka sana tangu siku ile lile tukio litokee na hakukuwahi tena kuwa na mambo ya ajabu pale nyumbani.

Headmaster kwa baadae alihama ile shule na kuhamia huko Biharamulo ambako amejenga na anaishi hadi leo,mimi niliondoka na kurudi nyumbani kisha kuelekea shuleni Advance!.

Ema yupo hapo Shinyanga anauza duka la vipuri vya magari,amejenga na anaishi hapo hapo shinyanga.

Monica kuna wakati niliambiwa yupo Mwanza ila sijajua ni Mwanza sehemu gani!,kuna mtu nilikutana nae wa pale kijijini akawa ameniambia hivyo,kwasababu baada ya mimi kuondoka pale kijijini sikurudi tena hivyo tukawa tumepotezana na mpenzi wangu huyo!.

Mimi kwasasa nipo Dar es salaam napambana na maisha ya kukimbizana!,nina kiboda boda changu japo kimekwisha lakini tunapambana na maisha!.Kijiwe changu huwa ni hapo Bunju ndugu zangu!.



MWISHO.
Asante sana Umughaka, bila shaka kupitia uzi huu utaongeza ndugu jamaa na marafiki, barikiwa kwa kuchangamsha jukwaa
 
Hadithi imesimuliwa imeisha bila mbamba safi sana. Kuna wengine wanasusa au wanaanza kujbizana na wale wavamizi wa uzi tuseme wachafuzi.
 
Back
Top Bottom