Tulikamatwa kinyume na sheria kwa sababu za kisiasa na tukaachiwa kisiasa

Hawa ndiyo wazalendo wanaopigania Maliasili ambazo watafaidi watoto wetu na wajukuu wetu.Wekeni utaratibu tuwachangie chochote ili kuwapa hamasa ya kuishughulikia hii serikali OVU inayouza maliasili zetu kwa kuahidiwa zawadi za kijinga ambazo ni punguani na kichaa pekee anayeweza kukubali.Aluta continua
 
Historia imeandikwa kwa wino wa dhahabu.
Hawa ndio wazalendo.
Mungu anaonekana waziwazi kupitia kwa hawa watu.
 
Niliwahi sema na leo narudia:

Wengi tulizaliwa ili kuishi katika huu ulimwengu, ila kuna wachache walizaliwa kwa malengo maalumu ili wengine tuweze kuishi/ku-survive kulingana na mapenzi ya alietuweka hapa duniani.

You are one those few selected individuals.

Congratulations!!
 
Hizi aya 2 ni nimezipenda sana:

"Msimamo wetu ni kwamba tumewajulisha polisi kwamba hawana hiyo mamlaka ya kutuzuia sisi kusafiri kwa mujibu wa sheria na katiba ya nchi. Kwamba tutasafiri na wakitusumbua tumewaambia wadhamini wetu waandike barua za kujitoa halafu waturudishe mahabusu na kisha watupeleke mahakamani. Lakini pia bado niko kwenye mashauriano na mawakili wangu nataka kuwafungulia kesi baadhi ya maafisa wa polisi kwa majina yao badala ya vyeo vyao maana askari unapofanya vitu kinyume na sheria hiyo ni utashi wake binafsi na anapaswa kuwajibika mwenyewe."

"Msimamo wetu ni kwamba maandamano ya nchi nzima yako palepale. Kitu pekee kitakachositisha maandamano haya ni serikali kusitisha mkataba huu mbovu wa bandari kati ya nchi yetu na DP World ya Dubai. Kwenye hili sisi tuko tayari kunyongwa, kwanza kunyongwa kwa ajili ya kupigania rasilimali za nchi hii ni fursa tunayoitaka hata kesho. Hatumuogopi yoyote isipokuwa Mungu muumbaji wa mbinguni."
 
Hawa ndio wanaume hapa Tz.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ