Tulimchukia Hayati Magufuli bila sababu za msingi, sasa tumetambua kuwa alikuwa sahihi, yanayofanyika sasa ni aibu

Hapana, Magufuli tulimchukia Sana kwa sababu za msingi na sababu kubwa za kumchukia Magufuli ni kuendesha nchi kama kampuni ya mama yake, kuunda vikosi vya kiharamia kuumiza watu, kusigina katiba na haki za BinAdamu!

Ushenzi unaofanyika sasa hivi hauwezi kuwa sababu ya kumsafisha Magufuli hata kidogo!
Kila awamu ibebe kiroba Cha dhambi zake! [emoji3525]
 
Pokea maua yako Mkuu.
 
Sijawahi kuwa Mtumishi wa Serikali,
Niko Sekta binafsi ambako nalipwa vizuri,
Naendesha shughuli zangu binafsi za kibiashara zinazoniingizia kipato cha kunitosha na familia yangu na hivyo sitegemei mwisho wa mwezi Hazina wameweka nini.
 
Sijawahi kuwa Mtumishi wa Serikali,
Niko Sekta binafsi ambako nalipwa vizuri,
Naendesha shughuli zangu binafsi za kibiashara zinazoniingizia kipato cha kunitosha na familia yangu na hivyo sitegemei mwisho wa mwezi Hazina wameweka nini.
Basi utakuwa mkwepa kodi au mdhulumaji au mshabiki mfata mkumbo wa wachumia tumbo
 
Maiti zinazidiana kunuka....

Haikatazwi kuwa na the Best of Both Worlds
 
Je ni kwa nini enzi za Magufuri kupitia chama chako cha Mapinduzi ukabila na ukanda vilizaliwa?Je kwa nini leo katika utawala wa Mama Samiah kupitia chama chako cha Mapinduzi udini umezaliwa?Inapendeza mtu kufikiri fikra sahihi za ubongo wake mwenyewe na siyo Sera za Zidumu Fikra sahihi za Mwenyekiti wa CCM.Ambapo leo tunalalamika kutokana na sera hiyo mbovu.Isingekuwa hiyo sera mbovu chama chako kingetenda kwa werevu na maarifa ya hali ya juu.Sasa hizo fikira sahihi za kipumbavu zinaligawanya Taifa.
Na hakuna mahali popote mimi nimehamasisha kugawanywa Taifa hili isipokuwa Muungano feki unaozinufaisha familia chache za ccm Tanganyika na familia nyingi za Zanzibar kwa kisingizio cha usalama.Ona leo kila familia ya Mzanzibar ina mtumishi wa umma au kiongozi kwa kupitia muungano huu lakini Tanzania bara kuna familia hawatahi pata mtumishi au kiongozi wa S
 
Hawatawahi pata mtumishi au kiongozi wa Serikali mpaka mwisho wa dunia kwa sababu tu hawana Refarii na wataendelea kuimba ccm mbele kwa mbele huku wakitarajia muda wa kampeni wapewe kofia,T shirt na Kanga pamoja na pombe ya kienyeji.Ewe mwanadamu punguza upumbavu.
 
Heko ndugu yangu Mtanzania ila Ukabila mnaupenda sana,Mimi nikuambie hata siku moja siwezi kuwa mfuasi wa Waarabu kwa sababu wao katika maisha yao wanaamini Mwafrika ni kafiri.
 
Bora aliyejenga Uwanja wa Ndege Chato kwa sababu Chato ni Tanzania kuliko aliyeuza nchi Falme za Kiarabu.
 
Kila mmoja ana mazuri yake na mapungufu yake.
Habari ya kutopanda daraja kwa watumishi ilikuwa kero, ukabila na upendeleo kwa wasukuma kwenye ajira ilikuwa tatizo pia.
Kupotea kwa watu na watu wasiojulikana ilikuwa tatizo pia.
Ukandamizaji wa vyama vya upinzani lilikuwa tatizo pia na uongozi wa ubabe wa kina sabaya, makonda na hapi ilikuwa ni shida
Aidha kurudisha nidhamu kwa watumishi, kuondoa watumishi hewa, ujenzi wa bwawa la kufua umeme na mengine yalikuwa mema kwa nchi. Tutoe maoni yetu na tuikosoe serikali yetu Ila lazima tukubali kutofautiana kimitazamo.
Unayemuona mzuri wewe, pengine Mimi nisione hivyo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…