Tulio na wake zaidi ya mmoja, tukutane tubadilishane uzoefu

Tulio na wake zaidi ya mmoja, tukutane tubadilishane uzoefu

DALA

JF-Expert Member
Joined
Aug 24, 2009
Posts
2,256
Reaction score
4,647
Natumai siku imeenda vizuri!

Moja kwa moja kwenye mada, katika jamii yetu ya Kiafrika kuwa na wake zaidi ya mmoja (ndoa ya mtaala) ni jambo la kawaida toka enzi. Changamoto iliyojitokeza ni ujio wa dini ambayo kwa kiasi kikubwa ilitumika kutuweka chini na tamaduni zetu hivyo wengi wetu walipojiunga na dini ya mkoloni husuani ukristu, waliona ni dhambi.

Kwa wengine sisi ambao baadae tulitambua upuuzi uliokuwepo nyuma ya pazia, badala ya kujificha eti una mke mmoja anayetambulika huku nje ya ndoa kuna vimada lukuki, tumeamua kujitokeza hadharani kuitetea huu utamaduni.

Mimi binafsi nina wake wawili, wanafahamina na hapa nipo mbioni kuongeza watatu na wanne ifikapo mwakani.

Ninapokutana na mwanamke, mimi nakuwa muwazi kabisa toka mwanzo hivyo anajua anaingia kwenye uhusiano wa aina gani.

Kuna changamoto nyingi tu kama mahusiano mengine ila mafanikio ya ndoa ya aina hii, mwanaume lazima uwe unajitambua, uwe na msimamo, usiwe mbaguzi, kulinda heshima ya wake zako, usiongee madhaifu ya mke A na mke B.

Hebu wengine tuoeane maujuzi.

Uzi tayari.
 
Thread 'Mwaka wa kwanza wanaripoti UDsm na Ardhi lini?' Mwaka wa kwanza wanaripoti UDsm na Ardhi lini?

Hebu piga shule kwanza dogo.

Kuuliza mwaka wa kwanza wanaripot lini maana yake ni dogo.

Hujui kuna watu wanaenda chuo wakiwa watu wazima ama wazee

Na kuna watu wanafanya biashara zinazotegemea uwepo wa wanafunzi.

Lazima wapeleleze kujua wanafunz wanafungua lini

Hoja ya hapa ni mke mmoja. Je babu yako alikuwa na mke mmoia?
 
Kuuliza mwaka wa kwanza wanaripot lini maana yake ni dogo.

Hujui kuna watu wanaenda chuo wakiwa watu wazima ama wazee

Na kuna watu wanafanya biashara zinazotegemea uwepo wa wanafunzi.

Lazima wapeleleze kujua wanafunz wanafungua lini

Hoja ya hapa ni mke mmoja. Je babu yako alikuwa na mke mmoia?
Swali lako limekaa kimtego mtego.

Vyovyote nitakavyojibu utanisulubu tu Mr Freshman.

Mr Freshman punguza hasiraaaaaa.
 
Mimi nilikua naipinga mitala ila imenikuta na hii imetokana na mtu ambae nilikua namtarajia kuoa kushindikana ikabidi nioe mke wa kutafutiwa na ndugu baadae nikaona utofauti kwa mke wa kwanza ikabidi nitafute mwingine ila wako mbalimbali huyu wa kwanza naishi nae ila huyu wa pili yupo Jijini ana shughuli zake
 
Mimi nilikua naipinga mitala ila imenikuta na hii imetokana na mtu ambae nilikua namtarajia kuoa kushindikana ikabidi nioe mke wa kutafutiwa na ndugu baadae nikaona utofauti kwa mke wa kwanza ikabidi nitafute mwingine ila wako mbalimbali huyu wa kwanza naishi nae ila huyu wa pili yupo Jijini ana shughuli zake

Wanawake wana wivu mbaya sana hivyo hata kuwatambulishia mke mwenza inabidi ujipange.

Cha muhimu huyo unayemchukua kama wa pili au watatu anafahamu kinachoendelea ili akupe muda wa kuweka mambo sawa.

Baada ya muda yule wa kwanza atajua tu.
 
Back
Top Bottom