Tulioangalia Kombe la Dunia mwaka 1986 nyumbani kwa Sheikh Yahya Magomeni tukutane hapa

Tulioangalia Kombe la Dunia mwaka 1986 nyumbani kwa Sheikh Yahya Magomeni tukutane hapa

mdukuzi

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2014
Posts
20,925
Reaction score
51,688
Huu uzi kuna watu watapita kama hawaoni maana wengi mwaka huo walikuwa viunoni mwa wazazi wao, wengine mlikuwa Sitimbi huko hamjui hata video ni mdudu gani.

Mwaka 1986 kulikuwa na fainali za Kombe la Dunia nchini Mexico, Germany Magharibi anapigwa 3-2 na Argentina, Argentina anachukua ubingwa. Bonge moja la mechi haijawahi tokea ila imefunikwa na mechi ya jana achana na Messi kuna mtu akiitwa Zicco unamkumbuka.

Kuna timu ya Uruguay walikuwa wanasifika kwa kucheza rafu mbaya hadi huku mtaani timu ikicheza rafu ikawa inaitwa Uruguay.

Kipindi hicho Dar nzima tunaenda Magomeni Mikumi kwa sheikh Yahya ndio alikuwa na hiyo video big screen mithili ya ukubwa wa kioo cha fuso.

Hii screen iliwekwa nje ya nyumba yake sehemu ya wazi watu tulijazana kama tuko Uwanja wa Taifa
pembeni amepaki range rover milango sita.

Huyu ndiyo alikuwa Don Dar nzima, Bakhresa kipindi hicho hajaanza hata kuuza mikate anauza icecream tu.

Mwaka huo Tabata nzima bar ziko mbili tu,Camp bar na Hai bar
 
Mimi niliangalia Kombe la Dunia Mwaka 1990 pale Mikoroshini Maganga nyumbani kwa Mzee Omari Omari,Baba mzazi wa yule mwimbaji Marehemu wa Mchiriku na Singeli Omary Omary.
Mwaka 1990 luninga zilishaanza kuwa nyingi, halafu anaibuka mjinga mmoja anasema Mzee Ruksa hakufanya kitu.

Mwaka 1986 hata mwaka ulikuwa haujatimia tangu Mwinyi aingie madarakani ndio maana hali ilikuwa hivyo.

Tumetoka mbali
 
Sisi wengine tuliangalia majumbani mwetu fainali ya 1978 kupitia TVZ (Television Zanzibar) ambapo Argentina ilikuwa ni mwenyeji na ndio iliyoibuka bingwa. Huku washabiki wao waki chant " AARGENTINAAA AARGENTINAAA AARGENTINAAA"
Baada ya Kum bamiza Uholanzi 3-1
Hata mitaani watoto wakishinda kwenye chandimu ndio ilikuwa chant yao hiyo.
 
Sisi wengine tuliangalia majumbani mwetu fainali ya 1978 kupitia TVZ (Television Zanzibar) ambapo Argentina ilikuwa ni mwenyeji na ndio iliyoibuka bingwa. Huku washabiki wao waki chant " AARGENTINAAA AARGENTINAAA AARGENTINAAA"
Baada ya Kum bamiza Uholanzi 3-1
Hata mitaani watoto wakishinda kwenye chandimu ndio ilikuwa chant yao hiyo.
Makwega7 kumbe ulikuwa wa kishua kitambo
 
Back
Top Bottom