Tulioishi Dodoma miaka ya 90's mpaka miaka ya 2000 tukutane hapa tujikumbushe

Tulioishi Dodoma miaka ya 90's mpaka miaka ya 2000 tukutane hapa tujikumbushe

Kitambo sana Dodoma. Toka Makole Primary nakatisha kiwanja cha Ndege kati navuka naenda twisheni kwa Mwal. Kikanya hapo K/Ndege shule ya msingi. Area C walikuwa wanakaa watoto wa matajiri, enzi hizo Area D ndo inaanza chipukia. Dah nimekumbuka mengi sana Dodoma. Matajiri walikuwa wakina Mzee Chove wa mabasi ya Urafiki. Bunge enzi hizo lipo mjini huku karibu na Hospitali ya General. Kwa leo ngoja niishie hapo.
 
Kitambo sana Dodoma. Toka Makole Primary nakatisha kiwanja cha Ndege kati navuka naenda twisheni kwa Mwal. Kikanya hapo K/Ndege shule ya msingi. Area C walikuwa wanakaa watoto wa matajiri, enzi hizo Area D ndo inaanza chipukia. Dah nimekumbuka mengi sana Dodoma. Matajiri walikuwa wakina Mzee Chove wa mabasi ya Urafiki. Bunge enzi hizo lipo mjini huku karibu na Hospitali ya General. Kwa leo ngoja niishie hapo.
kikanya na paper zake za 50 kwa mtihani kila weeken kama hakutajirika basi tena
 
Daaah dodoma ile ya shule ya Mazengo, Club NK, Ushuani area C tulikua tunaenda kutembea for no reason, Matajiri walikuwa wananunua viwanja area d Chan'gombe ilikuwa ya watukutu, kisasa ilikuwa vichaka tu, hakuna ilazo makuru ndio mapori kabisa hatugusi
 
Daaah dodoma ile ya shule ya Mazengo, Club NK, Ushuani area C tulikua tunaenda kutembea for no reason, Matajiri walikuwa wananunua viwanja area d Chan'gombe ilikuwa ya watukutu, kisasa ilikuwa vichaka tu, hakuna ilazo makuru ndio mapori kabisa hatugusi
Kamji kalikuwa kadogo mno.. mji unaishia maili mbili, kikuyu, kizota, makole

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Enzi hizo Dodoma washua wote wanaishi uzunguni
Watoto wa kishua wanasoma stockley
Kina sie tunasoma amani, na mlimwa ambazo ndio zilikuwa shule bora mjini
Club ilikuwa ni NK pamoja na shilla disco mitaa ya iringa road
Picnic tunajichanga tunaenda pnde za mkalama kule ma miyuji kwenye ile swimming juu ya jiwe ama weekend swimming pool ya kule mirembe mixture na kucheza basketball
Zunny ice cream ilikuwa chimbo hatari sana watoto wa mjini lazima tukutane hapo
Enzi hizo nyerere square ndio lilikuwa soko kuu la Dodoma kabla halijavunjwa baada ya kujengwa la majengo
Mnadani ilikuwa veyula
Watoto wa mailimbi,chang'ombe tuliwaogopa hasa
Na sisi wa Bahi na wa Mpwapwa tu comment wapi? Au ndio kusema sisi hatukukaa Dodoma?
 
DODOMA YA VUMBIIIIII TU PUMBAFU.
Acha hizo,huwezi kulinganisha Dodoma ya miaka hiyo na sasa,ambapo barabara nyingi zina lami na maeneo mengi ni makazi ya watu,sasa vumbi linatoka wapi,sikatai msimu wa baridi kuna vumbi kama ilivyo Morogoro na mikoa mingine kwa sababu ya upepo.Ushauri ninaotoa kwa authorities,mvua zinakuja wahamasishe upandaji wa miti mkoa mzima hasa mijini kwani msimu wa mvua ni karibu miezi 5 hivyo unatosha sana kuotesha miti...
 
Daah Dodoma yangu, enzi hizo wagogo walibeba mzegamzega kupeleka mkaa na nyanya mjini.

Kingcross, urafiki, mshikamano na zafanana zinapita Iringa road kuelekea huko Bihawana hadi Iringa.
 
Mnzega daaaah unakuta anavyotembea linanesa nesa linatoa kasauti Fulani hivii[emoji28][emoji28]
Mtu anatembea kwa kutroti kidogo, ukichoka bega hili unahamishia bega jingine.

Namkumbuka mzee Chakula Bora alituletea sana maji kipindi cha ukame na shida ya maji.
 
Back
Top Bottom