Nyamwage
JF-Expert Member
- Oct 16, 2020
- 712
- 1,748
Nilipojua kua sijui yangu ilikua katika biashara ya nafaka
Ilikua mwaka 2011 baada ya kufanya vibarua vya hapa na pale nikawa nimesave pesa kiasi cha tsh 750,000 nilikua na shauku sana ya kujiingiza katika biashara yoyote ya halali ili niachane na vibarua vya kutokua na uhakika wa kukipata kila siku
Sasa katika tafuta tafuta ushauri nikakutana na jamaa mmoja zamani alikua anafanya biashara ya nafaka lakini aliacha kwa kufilisika aliwekewa dawa za usingizi kwenye pombe na wahuni wakatoroka na pesa zake zote
basi jamaa hakuwa mchoyo akanipa muongozo wote wa jinsigani gani alikua anafata mahindi huko porini akanipa na mawasiliano ya rafiki yake mmoja ni mkazi wa hicho kijiji pale ambapo jamaa alipokua anafikia analala hapo kwa huyo jamaa
jamaa anafamilia mke na watoto wengi kiasi huyu mshikaji akaniambia kua kule wanahitaji mboga tu sababu ugali wanao basi nikaenda soko kuu pale mwanza nikanunua dagaa visado viwili nyanya na vitunguu
nikanunua na mifuko ile ya debe 6 na kamba na sindano ya kushonea magunia akaniambia pia nitafute debe la plastic na kisado nivichemshie maji ya moto alafu vikiisha pata moto nijaze mchanga huku naushindilia ili hilo debe na kisado vitanuke ili niweze kupata mahindi mengi kutoka kwa wanakijiji
alafu inahitajika niwe na chenji noti ndogo ndogo ili iwe rahisi maana kule nako chenji ni tabu nikaenda bank kuu pale mwanza karibu na keep left nikawaambia shida yangu wakachukua pesa zangu 750,000 wakaziweka katika mashine ya kuhakiki noti kama ni bandia
zote zilikua safi basi wakanipa chenji za vibunda vipyaaa vya 2,000 na 1,000 na 500 bila vikwazo vyovyote basi asubuhi nikaenda stendi ya mabasi nyegezi nikapanda vi HIACE vya kwenda MISUNGWI MISASI
nikashuka misasi kuna baiskeli za kwenda huko porini kijijini panaitwa NKUNGUHUMULU nauli ya baiskeli ni 500
ni kipande kirefu aisee wasukuma wanapiga pedeli baiskeli inapanda mlima kama inatelemka unapigwa na upepo tu kama umepanda bodaboda
nilifika pale kijijini jamaa mwenyeji akanipokea nikamuelezea basi akawajulisha wanakijiji kuwa kwake kuna mnunuzi wa mahindi basi wana kijiji wakaanza kuniletea mahindi mwenye kisado mwenye debe moja mwenye gunia sawa ilinichukua kama siku 3 kukamilisha gunia 21
nikawa nimebakiwa na akiba ya 80,000 nikasema hapa inatosha sasa nirudi maana mjini nimeeacha mahindi gunia wanauziwa 38,000 mpaka 40,000 kwa bei ya jumla na mimi nimemenunua kila gunia 27,000 mpaka 28,000 nikawa napiga hesabu za kwenda kukunja 200,000 kama faida
sasa kipengele kilikua usafiri kumbe kule porini fuso haiji kama hauna gunia 100 maana wale wenye fuso wanabeba kila gunia moja kwa bei ya 1,000 basi nilisota huko porini maji ya kunywa yenyewe wanachota kwenye bwawa ambalo wanako kunywa maji ng'ombe na punda wanyeji wenyewe wanayatwanga hawaoni tatizo mimi ndio siwezi yaani maji ukiyaangalia hunywi mpaka uangalie juu ndio unywe
nimekaa kama siku sita nika mpigia tena jamaa alie nielekeza, kaka vipi natokaje huku jamaa akawapigia wadau wenzake wa zamani kama wapo vijiji jirani ili anionganishe nao ili fuso lije lituchukue wadau wanasema bado mzigo wao hawaja maliza wako mjini bado
dah nimeka jamaa kampigia mdau mwingine na yeye akawa ana gunia 25 na yeye kakwama porini
basi kuna fuso moja inaitwa MAMBO YA CHINGA ilikua imeleta wamachinga vijijini sasa wanatafuta mzigo wa chap wapeleke mjini ili jioni wawarudie machinga wao hio ndio ikawa ponapona yangu ya kutoka porini
tukapakia mzigo tukafika sehemu kuna watu wa ushuru tukalipa ushuru kila gunia moja 1,000 jumla gunia moja likawa limesimamia 30,000 tumeenda mpaka sehemu moja inaitwa bugarika kuna masine ya kuuza mahindi nikapiga mzigo wangu pale kwa kua jamaa mwenyeji alikua ana kijiwe pale basi mzigo nikawa naulaza bure
tatizo likawa hapa katikati kipindi nilipokua polini kumbe kuna watu wenye mitaji mikubwa wamemwaga mahindi pale mwanza kila mtu ana mahindi basi na bei ikaanza ku drop ikashuka mpaka 34,000 kwa kila gunia da nikazidi kuvurugwa nikasemaa niki kaa sana hapa mahindi yanaweza yakashuka zaidi nikapata hasara basi mimi nikashusha bei maradufu nikayauza 32,000 mengine nikawakopesha wanao uza lejaleja lakini walinilipa kila walipo maliza mzigo
dah nikaja piga mahesabu faida niliyo pata ni 40,000 na hela yenyewe ya faida nimeshaila kuangalia mkononi mtaji wangu umebaki kiasi gani najikuta nina 690,000 kati ya 750,000 kwahio nikawa nimepoteza muda na pesa yangu kama 60,000 imepungua wanaosema biashara ni mtaji hawakukosea kipindi hicho ningekua nina mtaji kama 3,500,000 hata kama kwa kila gunia ningekua napata faida ya 2,000 bado ningekua na faida nzuri tu
BIASHARA NI MTAJI
Sent from my SM-A127F using JamiiForums mobile app
Ilikua mwaka 2011 baada ya kufanya vibarua vya hapa na pale nikawa nimesave pesa kiasi cha tsh 750,000 nilikua na shauku sana ya kujiingiza katika biashara yoyote ya halali ili niachane na vibarua vya kutokua na uhakika wa kukipata kila siku
Sasa katika tafuta tafuta ushauri nikakutana na jamaa mmoja zamani alikua anafanya biashara ya nafaka lakini aliacha kwa kufilisika aliwekewa dawa za usingizi kwenye pombe na wahuni wakatoroka na pesa zake zote
basi jamaa hakuwa mchoyo akanipa muongozo wote wa jinsigani gani alikua anafata mahindi huko porini akanipa na mawasiliano ya rafiki yake mmoja ni mkazi wa hicho kijiji pale ambapo jamaa alipokua anafikia analala hapo kwa huyo jamaa
jamaa anafamilia mke na watoto wengi kiasi huyu mshikaji akaniambia kua kule wanahitaji mboga tu sababu ugali wanao basi nikaenda soko kuu pale mwanza nikanunua dagaa visado viwili nyanya na vitunguu
nikanunua na mifuko ile ya debe 6 na kamba na sindano ya kushonea magunia akaniambia pia nitafute debe la plastic na kisado nivichemshie maji ya moto alafu vikiisha pata moto nijaze mchanga huku naushindilia ili hilo debe na kisado vitanuke ili niweze kupata mahindi mengi kutoka kwa wanakijiji
alafu inahitajika niwe na chenji noti ndogo ndogo ili iwe rahisi maana kule nako chenji ni tabu nikaenda bank kuu pale mwanza karibu na keep left nikawaambia shida yangu wakachukua pesa zangu 750,000 wakaziweka katika mashine ya kuhakiki noti kama ni bandia
zote zilikua safi basi wakanipa chenji za vibunda vipyaaa vya 2,000 na 1,000 na 500 bila vikwazo vyovyote basi asubuhi nikaenda stendi ya mabasi nyegezi nikapanda vi HIACE vya kwenda MISUNGWI MISASI
nikashuka misasi kuna baiskeli za kwenda huko porini kijijini panaitwa NKUNGUHUMULU nauli ya baiskeli ni 500
ni kipande kirefu aisee wasukuma wanapiga pedeli baiskeli inapanda mlima kama inatelemka unapigwa na upepo tu kama umepanda bodaboda
nilifika pale kijijini jamaa mwenyeji akanipokea nikamuelezea basi akawajulisha wanakijiji kuwa kwake kuna mnunuzi wa mahindi basi wana kijiji wakaanza kuniletea mahindi mwenye kisado mwenye debe moja mwenye gunia sawa ilinichukua kama siku 3 kukamilisha gunia 21
nikawa nimebakiwa na akiba ya 80,000 nikasema hapa inatosha sasa nirudi maana mjini nimeeacha mahindi gunia wanauziwa 38,000 mpaka 40,000 kwa bei ya jumla na mimi nimemenunua kila gunia 27,000 mpaka 28,000 nikawa napiga hesabu za kwenda kukunja 200,000 kama faida
sasa kipengele kilikua usafiri kumbe kule porini fuso haiji kama hauna gunia 100 maana wale wenye fuso wanabeba kila gunia moja kwa bei ya 1,000 basi nilisota huko porini maji ya kunywa yenyewe wanachota kwenye bwawa ambalo wanako kunywa maji ng'ombe na punda wanyeji wenyewe wanayatwanga hawaoni tatizo mimi ndio siwezi yaani maji ukiyaangalia hunywi mpaka uangalie juu ndio unywe
nimekaa kama siku sita nika mpigia tena jamaa alie nielekeza, kaka vipi natokaje huku jamaa akawapigia wadau wenzake wa zamani kama wapo vijiji jirani ili anionganishe nao ili fuso lije lituchukue wadau wanasema bado mzigo wao hawaja maliza wako mjini bado
dah nimeka jamaa kampigia mdau mwingine na yeye akawa ana gunia 25 na yeye kakwama porini
basi kuna fuso moja inaitwa MAMBO YA CHINGA ilikua imeleta wamachinga vijijini sasa wanatafuta mzigo wa chap wapeleke mjini ili jioni wawarudie machinga wao hio ndio ikawa ponapona yangu ya kutoka porini
tukapakia mzigo tukafika sehemu kuna watu wa ushuru tukalipa ushuru kila gunia moja 1,000 jumla gunia moja likawa limesimamia 30,000 tumeenda mpaka sehemu moja inaitwa bugarika kuna masine ya kuuza mahindi nikapiga mzigo wangu pale kwa kua jamaa mwenyeji alikua ana kijiwe pale basi mzigo nikawa naulaza bure
tatizo likawa hapa katikati kipindi nilipokua polini kumbe kuna watu wenye mitaji mikubwa wamemwaga mahindi pale mwanza kila mtu ana mahindi basi na bei ikaanza ku drop ikashuka mpaka 34,000 kwa kila gunia da nikazidi kuvurugwa nikasemaa niki kaa sana hapa mahindi yanaweza yakashuka zaidi nikapata hasara basi mimi nikashusha bei maradufu nikayauza 32,000 mengine nikawakopesha wanao uza lejaleja lakini walinilipa kila walipo maliza mzigo
dah nikaja piga mahesabu faida niliyo pata ni 40,000 na hela yenyewe ya faida nimeshaila kuangalia mkononi mtaji wangu umebaki kiasi gani najikuta nina 690,000 kati ya 750,000 kwahio nikawa nimepoteza muda na pesa yangu kama 60,000 imepungua wanaosema biashara ni mtaji hawakukosea kipindi hicho ningekua nina mtaji kama 3,500,000 hata kama kwa kila gunia ningekua napata faida ya 2,000 bado ningekua na faida nzuri tu
BIASHARA NI MTAJI
Sent from my SM-A127F using JamiiForums mobile app