Tuliokurupukia kuanzisha biashara baadaye tukajua hatujui tukutane hapa

Tuliokurupukia kuanzisha biashara baadaye tukajua hatujui tukutane hapa

Biashara na ujasirimali kiujumla ni safari ya mafunzo na mafanikio. Mafunzo ni sehemu ambazo unashindwa, unakosea, unapata hasara. Inabidi kufanya tathmini hili linapotokea ili mara zijazo uwe na somo litalokusaidia mbeleni hata kama ni vitu kama uvumilivu na bidii.

Nishawahi fanya biashara zaidi ya 20 hadi sasa na ni biashara 5 tu zilipata faida na mbili tu zilizoniingizia zaidi ya milioni 100. Kila moja ilikuwa na funzo katika hatua moja au nyingine. Naamini nisingefika hapa bila kupitia biashara ambazo zilifeli.
Dah Mkuu nipe mkopo hata wa laki 5 aisee, demand naiona but mtaji mdogo
 
Biashara yoyote ni rahisi kwa mtu anayeifanya. Ukisikia biashara fulani ni nzuri inanipa faida jua mtu yule katumia muda na yuko na Wateja hadi kufika hapo.

Ukiingia kichwa lazima mbavu ziwake moto, niliwai jaribu biashara moja yaani ikafika kipindi bora niuze kwa bei yoyote wateja huoni kudadek
 
Nilienda ilala kununua mitumba nije niuze mkoa dakika ya mwisho hizi nguo nazivaa mwenyewe za kike nilimpa demu wang
Nacheka kama mazuri pole mkuu, ila sababu ni wateja hamna ama hukufanya jitihada zaidi za kuwatafuta au pia ulizitamani uzivae mwenyewe 😛
 
Nacheka kama mazuri pole mkuu, ila sababu ni wateja hamna ama hukufanya jitihada zaidi za kuwatafuta au pia ulizitamani uzivae mwenyewe [emoji14]
Sema ht hivyo changamoto zinafahamika.kwanza nilinunua mzigo wa laki nne Tena za kupoint mwenyewe sio balo...majeje,makoti,ma t shirt na vigauni vya kike...ishu ya kwanza NI kuzinguana kwenye frem na aliyenipangisha nilitaka anifanyie marekebisho akashindwa.pili NI pointer Wangu niliyetaka aniuzie alianza kuingiza tamaa tukazinguana urafiki Hadi leo ukawa umepungua..niliamua kuanza kuzungusha mwenyewe nikitoka job saa tisa naweka kwenye bag ila ndo wateja sijapata nikaishia kuuza nguo zisizozidi 10 kwenye nguo zaidi ya 200...nikaona isiwe case demu Wangu mpya nikampa Kama nguo 20 Mimi navaa zozote Hadi Sasa Niko nazo sema TU Niko busy nataka nikitulia nitafute wauza mitumba niwauzie Bei ya chini... biashara sio mchezo.now ninawaza nimfungulie demu Wangu genge la matunda yaani mtaji wa kawaida around laki ili hata ukipotea nisiumie sana
 
Baada ya kuingia kibaruani na kusave miaka 3 niliona watu wenye bus barabaran wanafaidi sana 😃😃😃
Nikawa na ham ya hiyo biz nikanunua bus used kwa mtu daah hakuna rangi niliacha kuona
 
Nilipojua kua sijui yangu ilikua katika biashara ya nafaka

Ilikua mwaka 2011 baada ya kufanya vibarua vya hapa na pale nikawa nimesave pesa kiasi cha tsh 750,000 nilikua na shauku sana ya kujiingiza katika biashara yoyote ya halali ili niachane na vibarua vya kutokua na uhakika wa kukipata kila siku

Sasa katika tafuta tafuta ushauri nikakutana na jamaa mmoja zamani alikua anafanya biashara ya nafaka lakini aliacha kwa kufilisika aliwekewa dawa za usingizi kwenye pombe na wahuni wakatoroka na pesa zake zote

basi jamaa hakuwa mchoyo akanipa muongozo wote wa jinsigani gani alikua anafata mahindi huko porini akanipa na mawasiliano ya rafiki yake mmoja ni mkazi wa hicho kijiji pale ambapo jamaa alipokua anafikia analala hapo kwa huyo jamaa

jamaa anafamilia mke na watoto wengi kiasi huyu mshikaji akaniambia kua kule wanahitaji mboga tu sababu ugali wanao basi nikaenda soko kuu pale mwanza nikanunua dagaa visado viwili nyanya na vitunguu

nikanunua na mifuko ile ya debe 6 na kamba na sindano ya kushonea magunia akaniambia pia nitafute debe la plastic na kisado nivichemshie maji ya moto alafu vikiisha pata moto nijaze mchanga huku naushindilia ili hilo debe na kisado vitanuke ili niweze kupata mahindi mengi kutoka kwa wanakijiji

alafu inahitajika niwe na chenji noti ndogo ndogo ili iwe rahisi maana kule nako chenji ni tabu nikaenda bank kuu pale mwanza karibu na keep left nikawaambia shida yangu wakachukua pesa zangu 750,000 wakaziweka katika mashine ya kuhakiki noti kama ni bandia

zote zilikua safi basi wakanipa chenji za vibunda vipyaaa vya 2,000 na 1,000 na 500 bila vikwazo vyovyote basi asubuhi nikaenda stendi ya mabasi nyegezi nikapanda vi HIACE vya kwenda MISUNGWI MISASI
nikashuka misasi kuna baiskeli za kwenda huko porini kijijini panaitwa NKUNGUHUMULU nauli ya baiskeli ni 500
ni kipande kirefu aisee wasukuma wanapiga pedeli baiskeli inapanda mlima kama inatelemka unapigwa na upepo tu kama umepanda bodaboda

nilifika pale kijijini jamaa mwenyeji akanipokea nikamuelezea basi akawajulisha wanakijiji kuwa kwake kuna mnunuzi wa mahindi basi wana kijiji wakaanza kuniletea mahindi mwenye kisado mwenye debe moja mwenye gunia sawa ilinichukua kama siku 3 kukamilisha gunia 21

nikawa nimebakiwa na akiba ya 80,000 nikasema hapa inatosha sasa nirudi maana mjini nimeeacha mahindi gunia wanauziwa 38,000 mpaka 40,000 kwa bei ya jumla na mimi nimemenunua kila gunia 27,000 mpaka 28,000 nikawa napiga hesabu za kwenda kukunja 200,000 kama faida

sasa kipengele kilikua usafiri kumbe kule porini fuso haiji kama hauna gunia 100 maana wale wenye fuso wanabeba kila gunia moja kwa bei ya 1,000 basi nilisota huko porini maji ya kunywa yenyewe wanachota kwenye bwawa ambalo wanako kunywa maji ng'ombe na punda wanyeji wenyewe wanayatwanga hawaoni tatizo mimi ndio siwezi yaani maji ukiyaangalia hunywi mpaka uangalie juu ndio unywe

nimekaa kama siku sita nika mpigia tena jamaa alie nielekeza, kaka vipi natokaje huku jamaa akawapigia wadau wenzake wa zamani kama wapo vijiji jirani ili anionganishe nao ili fuso lije lituchukue wadau wanasema bado mzigo wao hawaja maliza wako mjini bado

dah nimeka jamaa kampigia mdau mwingine na yeye akawa ana gunia 25 na yeye kakwama porini
basi kuna fuso moja inaitwa MAMBO YA CHINGA ilikua imeleta wamachinga vijijini sasa wanatafuta mzigo wa chap wapeleke mjini ili jioni wawarudie machinga wao hio ndio ikawa ponapona yangu ya kutoka porini

tukapakia mzigo tukafika sehemu kuna watu wa ushuru tukalipa ushuru kila gunia moja 1,000 jumla gunia moja likawa limesimamia 30,000 tumeenda mpaka sehemu moja inaitwa bugarika kuna masine ya kuuza mahindi nikapiga mzigo wangu pale kwa kua jamaa mwenyeji alikua ana kijiwe pale basi mzigo nikawa naulaza bure

tatizo likawa hapa katikati kipindi nilipokua polini kumbe kuna watu wenye mitaji mikubwa wamemwaga mahindi pale mwanza kila mtu ana mahindi basi na bei ikaanza ku drop ikashuka mpaka 34,000 kwa kila gunia da nikazidi kuvurugwa nikasemaa niki kaa sana hapa mahindi yanaweza yakashuka zaidi nikapata hasara basi mimi nikashusha bei maradufu nikayauza 32,000 mengine nikawakopesha wanao uza lejaleja lakini walinilipa kila walipo maliza mzigo

dah nikaja piga mahesabu faida niliyo pata ni 40,000 na hela yenyewe ya faida nimeshaila kuangalia mkononi mtaji wangu umebaki kiasi gani najikuta nina 690,000 kati ya 750,000 kwahio nikawa nimepoteza muda na pesa yangu kama 60,000 imepungua wanaosema biashara ni mtaji hawakukosea kipindi hicho ningekua nina mtaji kama 3,500,000 hata kama kwa kila gunia ningekua napata faida ya 2,000 bado ningekua na faida nzuri tu

BIASHARA NI MTAJI

Sent from my SM-A127F using JamiiForums mobile app
Umenikumbusha kipindi Corona inaingia wakawa wanasema watu wengi watakufa
Mwanaume nikaingia bank kukopa kama 7m hivi ili nipanue mradi wangu wa majeneza nikiamini ndo mwaka wangu wa kutoboa lakini cha ajabu mambo yakaenda tofauti mpaka ikafikia nakosa hata hela ya marejesho!
Kuna jamaangu ana gereji yake Dar akanishauri nichukue mzigo wa majeneza kiasi nikaweke branch Dar maana hapa Dom biashara iligoma kabisa ikabidi huyo rafiki yangu anitafutie eneo zuri Dar nikapeleka mzigo wa majeneza kama pc 250 hivi lakini huko ndo hali iligoma sana kiasi kwamba lile eneo nilipokuwa misiba mingi ni waislamu hawatumii majeneza yaani ilikuwa mpaka namaliza week nimeuza jeneza moja wakati mwingine namaliza week bila kuuza ikabidi nifunge maana hata hela ya kulipia eneo nilishindwa kulipa ikabidi nirudi Dom kuendelea na kijiwe changu cha huko.
Yaani kifupi nililazimika kuuza kagari kangu( kama ka Mr Bean) ili nipunguze deni la mkopo sintosahau mpaka nazeeka
 
Umenikumbusha kipindi Corona inaingia wakawa wanasema watu wengi watakufa
Mwanaume nikaingia bank kukopa kama 7m hivi ili nipanue mradi wangu wa majeneza nikiamini ndo mwaka wangu wa kutoboa lakini cha ajabu mambo yakaenda tofauti mpaka ikafikia nakosa hata hela ya marejesho!
Kuna jamaangu ana gereji yake Dar akanishauri nichukue mzigo wa majeneza kiasi nikaweke branch Dar maana hapa Dom biashara iligoma kabisa ikabidi huyo rafiki yangu anitafutie eneo zuri Dar nikapeleka mzigo wa majeneza kama pc 250 hivi lakini huko ndo hali iligoma sana kiasi kwamba lile eneo nilipokuwa misiba mingi ni waislamu hawatumii majeneza yaani ilikuwa mpaka namaliza week nimeuza jeneza moja wakati mwingine namaliza week bila kuuza ikabidi nifunge maana hata hela ya kulipia eneo nilishindwa kulipa ikabidi nirudi Dom kuendelea na kijiwe changu cha huko.
Yaani kifupi nililazimika kuuza kagari kangu( kama ka Mr Bean) ili nipunguze deni la mkopo sintosahau mpaka nazeeka
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] Mkuu nimecheka Sana kudadeki
 
Umenikumbusha jamaa yangu mmoja baada ya kutoka ulaya na dollar zake kadhaa, akasema anataka akalime ni akang’ang’ania kulima vitunguu.

Kwa ufupi ile hasara aliyoipata hataki hata kusikia neno KILIMO,

  • Moja, shambani hakuvuna kama alivyotarajia
  • Pili, vile vitunguu alivyovuna alitegea eti soko lipande kumbe vitunguu vinakawaida ya kuoza

Milioni zake kadhaa ziliteketea kule na alijutavni bora angefuga ng’ombe wa maziwa kama mimi tu.
 
Umenikumbusha kipindi Corona inaingia wakawa wanasema watu wengi watakufa
Mwanaume nikaingia bank kukopa kama 7m hivi ili nipanue mradi wangu wa majeneza nikiamini ndo mwaka wangu wa kutoboa lakini cha ajabu mambo yakaenda tofauti mpaka ikafikia nakosa hata hela ya marejesho!
Kuna jamaangu ana gereji yake Dar akanishauri nichukue mzigo wa majeneza kiasi nikaweke branch Dar maana hapa Dom biashara iligoma kabisa ikabidi huyo rafiki yangu anitafutie eneo zuri Dar nikapeleka mzigo wa majeneza kama pc 250 hivi lakini huko ndo hali iligoma sana kiasi kwamba lile eneo nilipokuwa misiba mingi ni waislamu hawatumii majeneza yaani ilikuwa mpaka namaliza week nimeuza jeneza moja wakati mwingine namaliza week bila kuuza ikabidi nifunge maana hata hela ya kulipia eneo nilishindwa kulipa ikabidi nirudi Dom kuendelea na kijiwe changu cha huko.
Yaani kifupi nililazimika kuuza kagari kangu( kama ka Mr Bean) ili nipunguze deni la mkopo sintosahau mpaka nazeeka
Dah dah nmecheka kama mazuri Dah kwahyo mkuu ulitaka watu wafe wengi [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Dah Mkuu nipe mkopo hata wa laki 5 aisee, demand naiona but mtaji mdogo
Tafuta unachoweza kufanya kwa mtaji ulionao au ingiza pesa kwa njia nyingine usave ufike kiwango unachotaka. Kiwango hiki cha pesa kinapatikana kirahisi kwa njia hizo mbili si lazima kukopa.

Pia njiani hapo utajifunza kitu kitachokusaidia katika safari yako mbeleni.
 
Tafuta unachoweza kufanya kwa mtaji ulionao au ingiza pesa kwa njia nyingine usave ufike kiwango unachotaka. Kiwango hiki cha pesa kinapatikana kirahisi kwa njia hizo mbili si lazima kukopa.

Pia njiani hapo utajifunza kitu kitachokusaidia katika safari yako mbeleni.
Yeah Mkuu, polepole nasonga.
 
Back
Top Bottom