Tuliokuwa tunashabikia Uvamizi wa Urusi, Ukraine. Tuendelee kuchochea Kuni? Yajayo yanasikitisha

Tuliokuwa tunashabikia Uvamizi wa Urusi, Ukraine. Tuendelee kuchochea Kuni? Yajayo yanasikitisha

Mtu Asiyejulikana

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2017
Posts
2,254
Reaction score
5,161
Watanzania wengi kwa ukosefu wa Elimu bora na Ufahamu jumuifu walijikuta wanashabikia sana Vita ya Urusi na Ukraine. Wengi sana wakichukua pande kama wanavyoshabikia Simba na Yanga.

Na wengi walikuwa hawaelewi kwa nini NATO au USA haiingizi miguu yake. Kwa akili ile ile ya kishabiki wakimsifu either putin au rais wa ukraine.

Na wakaenda mbali kusema NATO wanaiogopa Urusi au pengine Urussi inaiogopa NATO. maneno mengi na ubishani vijiweni na kwenye mitandao usio na tija.

Leo mnaona Watawala wanatumia Vita hivi kuwaumiza wananchi zaidi. Kodi zinachomekewa humo ndani kwa ndani ukiuliza utaambiwa ni Vita ya Urusi Ukraine.

Athari za Vita hivyo zipo, lakini kuna wahuni ambao wameamua kwa makusudi to swim with the current. Tutegemee ufisaidi mkubwa sana kipindi hiki hasa kwa nchi zetu za kiafrika nyingi. Zila chache kuna marais wanapambana kupunguza makali ya maumivu kwa wananchi wao.

Na kwa zile ambazo zina bahati mbaya Marais wanatumia nafasi hiyo kuwa nyonya damu wananchi wao. Sasa kila kitu kimepanda. Hadi pipi zimepanda bei. Vita vya Urusi Ukraine.

Je, tuendelee kushabikia kama tunavyozishabikia Manchester na Liverpool au sasa tuanze kuangalia tuna viongozi wa namna gani?
 
Jikusanye watu wote,jambeni mishuzi kama yote hii inaweza kutusaidia kutengeneza gas yetu asilia kwa ajili ya kutumia majumbani na kwny Viwanda vyetu na kupunguza gharama za Maisha.
FO8ZDkZXEAwed6v.jpg
 
Watanzania wengi kwa ukosefu wa Elimu bora na Ufahamu jumuifu walijikuta wanashabikia sana Vita ya Urusi na Ukraine. Wengi sana wakichukua pande kama wanavyoshabikia Simba na Yanga.

Na wengi walikuwa hawaelewi kwa nini NATO au USA haiingizi miguu yake. Kwa akili ile ile ya kishabiki wakimsifu either putin au rais wa ukraine.

Na wakaenda mbali kusema NATO wanaiogopa Urussi au pengine Urussi inaiogopa NATO. maneno mengi na ubishani vijiweni na kwenye mitandao usio na tija.

Leo mnaona ... Watawala wanatumia Vita hivi kuwaumiza wananchi zaidi. Kodi zinachomekewa humo ndani kwa ndani ukiuliza utaambiwa ni Vita ya Urusi Ukraine.

Athari za Vita hivyo zipo...lakini kuna wahuni ambao wameamua kwa makusudi to swim with the current. Tutegemee ufisaidi mkubwa sana kipindi hiki hasa kwa nchi zetu za kiafrika nyingi. Zila chache kuna marais wanapambana kupunguza makali ya maumivu kwa wananchi wao.

Na kwa zile ambazo zina bahati mbaya Marais wanatumia nafasi hiyo kuwa nyonya damu wananchi wao. Sasa kila kitu kimepanda. Hadi pipi zimepanda bei. Vita vya Urusi Ukraine.

Je tuendelee kushabikia kama tunavyozishabikia Manchester na Liverpool au sasa tuanze kuangalia tuna viongozi wa namna gani?

Nasimama na Putin. Mpaka sasa ushindi ni wake. Achana na propaganda za media za Magharibi.
 
Jikusanye watu wote,jambeni mishuzi kama yote hii inaweza kutusaidia kutengeneza gas yetu asilia kwa ajili ya kutumia majumbani na kwny Viwanda vyetu na kupunguza gharama za Maisha.View attachment 2181283
Hii teknolojia sio lazima ulazimishwe ila kwenye level ya household itengeneze
Utakuja kunishukuru mi naitumia home yaan gharama ya mkaa, gas na umeme wakupikia ni zero
 
Kwamba Watanzania tusingeshabikia hii vita Russia asingetia maguu Ukraine?
... the point is; badala ya kuona hadaa za watawala kutumia hiyo vita kama kisingizio cha kuchomekea mikodi kuumiza wananchi; badala ya kuwabana watawala kupunguza ukali wa maisha ulioletwa na hii vita; tumebaki na ushabiki wa kijinga huku watawala wakitumia mwanya huo kuumiza wananchi.
 
Putin endelea kukinukisha, hadi mwezi wa 12 kila Mtanzania atakuwa amerudiwa na ufahamu wake. Hasa waliopenda kujiita wanyonge enzi za simba wa yuda
 
Ishu ya maisha kupanda siyo sababu ya Russia kumgonga Ukraine,bali ni undezi wa waoga EU na NATO yao ya kukimbilia kumuwekea vikwazo jianti wa uzalisha duniani.
Hapa wasababishi wa ugumu huu ni walioweka vikwazo badala ya kuingia frontline kwenye vita.
 
Back
Top Bottom