Tuliokuwepo enzi za utawala wa Ali H Mwinyi tukutane hapa!


Awamu yake ndiyo iliwafanya Wahindi na Waarabu waanze kuwa na ' Jeuri ' kubwa na ' Nyodo ' ndani ya nchi hii huku Dawa za Kulevya ndiyo zikianza kushika kasi nchini ambapo ' Wakubwa ' wake kadhaa waliokuwa katika Serikali yake walikuwa wakijihusisha nazo. Naomba niishie hapa tafadhali.
 
Utawala wa mwanzo ndo ulituletea umasikini kutokana na Sera za kimasikini za kijamaa,maana vitu muhimu vilionekana ni anasa,Sera za kijamaa zilizalisha walevi na wazinzi ikiwemo ndoa nyingi za mitaala maana ukiwa na hela ya ziada ukuruhusiwa kumiliki mali,hivo lzm uzitumie kwenye ulevi au kuhonga malaya. Ndio maana nyingi nyingi za kariakoo zilikuwa za wakinamama wengi walihongwa na makuli wa Bandari au watumishi wengi.
 
Na Kingunge ndio alikuwa Mkandarasi wa Azimio la Arusha
Tunawaaadhimisha sana Waasisi wa Umaskini na Ujinga wetu
 
ni kweli japo nilikua shule niliyaona hayo yalikua mazuri Mitumba wazazi wakaanza kutununulia tulifurahi mno
 
Enzi hizo ndo sukari iliingia sumu.

Watanzania nia wezangu sukari imeingia sumu. Kauli ya Mzee wetu Ally Hassan Mwinyi

Hahahaha misemo tata ya Mzee Mwinyi

Nzi kafia Dondani

Wa Morogoro kazaneni kwenye Mihogo Kama Wahaya wanavyokazana kwenye Migomba!
 
Nafikiri awamu hii Ilikuwa Ruksa kufanya kila unachojisikia kufanya.

Mzee aliruhusu watu wawe huru, Ilikuwa furaha kwa wengi maana mzee Mwalimu aliwabana sana watu Toka nchi inapata uhuru.


Ingawa uhuru huu wa manyani ulikuwa na Madhara kadhaa kwa taifa!
 
Umeongea kweli
 
In any capitalist country hayo mambo lazima yawepo refer China licha ya sheria kali lkn madawa yanaingia

Sabb kubwa ya madawa kuanza kuingia kipindi chake ni baada ya wananchi kuruhusiwa ku-import bidhaa jamba ambalo awamu ya kwanza individual was prohibited to own any wealth or import things under the umbrella of ujamaa ..

Ili madawa yasiingie nchini basi Magu afunge bandari no more importation tena kwa wafanyabiashara tuwaige marafiki zetu wa zamani North Korea huwezi kukuta heroine ,cocaine kule
 
Kweli maisha yamebadilikq sana
 
Rupia walikuwa wanaishi kama malaika walahi!
Kuna liaharusi la mtoto wake alio mtoto wa Kahama nadhani!
Ilikuwa pata shika!
Mwinyi kawekwa katikati ya bwana na bibi harusi!
Duh!
Sasa hivi ndiyo hao wanaishi kama mashetani, ndoa bye bye!
Mhhh!
Dunia hii!
Mwenye Enzi Mungu tuongoze!
 
Mzee Mwinyi alikuwa mwenye busara, hekima na ustahamilivu mkubwa hasa kwa wale waliyompinga na kumtukana, alikuwa akishaurika na wala hakurupuki, alipokea kijiti cha uraisi wakati nchi ilikuwa ikihitaji mabadiliko makubwa ya kisiasa na kiuchumi kutokana na shinikizo la mataifa makubwa yaliyokuwa yakisaidia nchi maskini.
 
Kumbe walikuja kipindi cha ruksa!? nilikuwa sijui
 
Kumbe walikuja kipindi cha ruksa!? nilikuwa sijui
Yup ndugu yangu hii kero ya kunguru weusi!
Namwomba Mola awaondoe kabisa hawa kunguru kutoka Pakistan walahi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…