Tuliosoma Iringa: The Highlands, Lugalo, Iringa Girls, Mkwawa HS na Mwembetogwa tukutane hapa!

Tuliosoma Iringa: The Highlands, Lugalo, Iringa Girls, Mkwawa HS na Mwembetogwa tukutane hapa!

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Binafsi nilimaliza kidato cha 4 pale The Highlands mwaka 1984 na tukio ninalolikumbuka ni mwalimu wa Chemistry Mr Kibasa kuja kuwa mbunge wa kwanza wa upinzani Iringa mjini mwaka 1995 akitokea Mwembetogwa sec alikohamia baadae akiwa Head Master. Kadhalika namkumbuka Salim Asas ambaye alikuwa kijana mdogo na sasa ni nguzo ya CCM hapo mkoani. Je wewe uliyewahi kusoma Iringa tupe kwa uchache mambo uliyaweka katika kumbukumbu. Wakati wetu alikuwepo mzee Mbigili aka Damu ya chama aliipenda CCM kupita maelezo. Karibu!
 
Umenikumb
Tosa wanakaribishwa lakini huko nyuma Tosamaganga, Pomelini na Ifunda zilihesabika kama shule za " shamba" walikuwa wanakuja mjini kwa mialiko ya Disco kutoka Lugalo na Iringa Zoo!
Umenikumbusha nilisoma Pomerini dah miaka ile kupigika balaa
 
Enzi za evening classes zilizoitwa Taasisi au hukuzikuta mkuu?!
Miaka ya nyuma kabisaaaa kabla ya kipindi unachoskisema Head master alikuwa Elia Staki (RIP)baadae alikuja kuwa mwenyekiti wa C.C.M mkoa wa Iringa
 
Miaka ya nyuma kabisaaaa kabla ya kipindi unachoskisema Head master alikuwa Elia Staki (RIP)baadae alikuja kuwa mwenyekiti wa C.C.M mkoa wa Iringa
Hakika, binti yake alisoma Lugalo anaitwa Rose Sitaki ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Wilaya ya Same Kilimanjaro!
 
Pamoja. Mwaka 1998 tulienda kuiba ulanzi wa jamaa mmoja aliitwa mbegasi nikakamatwa mimi nakupelekwa kwa walimu na walimu walilipa 200 kwa mbegasi ikawa pona yangu na baada ya hapo nilikuwa kwenye uangalizi mkubwa sana ila wenzangu walihama wote
Na pale Ifunda zaidi ya ulanzi hapakuwa na starehe nyingine!
 
Labda ametarget shule zilizopo town tu hahaha. Team Ifunda hapa.

Nakumbuka tukio la wanafunzi wa Ifunda Tech walipolala barabarani kuzuia msafara wa Nyerere. Nyerere aliwasikiliza na baadae akaendelea na safari yake. Viongozi wa wanafunzi wakawekwa ndani pale Iringa mjini na wakawa wanaletwa kula Lugalo Sec nilipokuwa nasoma. Wanaokumbuka mkasa ule jamani wekeni vizuri ili tutunze vizuri kumbukumbu ile maana vijana wa leo hawawezi kudai hata haki yao ya msingi ya kufundishwa na walimu! Tena Chuo Kikuu! Kweli Magu anawatia vijana wetu ujinga wa hali ya juu sana. Taifa liendako siko na kumbukumbu hizi tukiwa hatupo, pengine zitawasaidia kuona walipokosea.
 
Hakika, binti yake alisoma Lugalo anaitwa Rose Sitaki ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Wilaya ya Same Kilimanjaro!
Upo sahihi mkuu, JF hata vibabu tumo. Mate wangu ni mbunge wa sasa wa Igunga ila ni different combination
 
Back
Top Bottom