Tuliotembea umbali mrefu kwa miguu kwa sababu yoyote ile tukutane hapa

Tuliotembea umbali mrefu kwa miguu kwa sababu yoyote ile tukutane hapa

Nyerere alitembea. Wanzie walifika na malengelenge wengine hawakumaliza. Yakwangu ilikuwa kukimbia jeshi miaka ile ya 80 jeshi likikuwa hatari. Imagine huna pesa, hujui unaenda wapi lakini unatoroka ili mradi kukimbia mateso ya jeshi. Tuliishia mikononi ya maafande. Jela ya jeshi mwezi we acha tu!!!
hongera yake hayati Baba wa Taifa,
Kutoroka nasikia ilibidi ujipange kwelikweli
 
Mi kutembea toka msasani Hadi posts,go and return sio ishu,ama toka igoma Hadi mz mjini,go and return,sijui ni km ngapi,
Kiufupi Kama mi natembea sana hata Kama Niko full loaded mfukoni
 
Mi kutembea toka msasani Hadi posts,go and return sio ishu,ama toka igoma Hadi mz mjini,go and return,sijui ni km ngapi,
Kiufupi Kama mi natembea sana hata Kama Niko full loaded mfukoni
mkuu igoma cocacola hadi roundabout pale town ni 10Km nadhani. utakuwa vzr, kwenda na kurudi nikiwa primary route za kirumba airport zilikuwa kawaida sana.

joto vipi mkuu, maana posta napo ukifika unajasho, ukikutana na Bashite anaweza kukunasa makofi
 
Ha ha
mkuu igoma cocacola hadi roundabout pale town ni 10Km nadhani. utakuwa vzr, kwenda na kurudi nikiwa primary route za kirumba airport zilikuwa kawaida sana.

joto vipi mkuu, maana posta napo ukifika unajasho, ukikutana na Bashite anaweza kukunasa makofi
haha ha,
kipindi hicho alikuwa Bado la tatu,ila kwa ruti ya igoma centre Hadi kamanga ferry,go and return ni juzi tu
 
Hata sisi babu alikuwa anatutembeza kama 50km au zaidi kwenda kwa ndugu zake huku tumebeba pombe yake. Tulikuwa wadogo ila tulivumimila saana sababu babu alikuwa na stori nyingi njiani. nakumbuka nilikuwa na miaka 9 nilipoanza tembea na babu.
Mie safari yangu na baba mdogo pamoja na bro ilikuwa mbaya ndio maana naikumbuka tena Kuna wakati nakasirika kuwa walinionea,kwanza nilikuwa mdogo halafu umbali mrefu sehemu nyingine tunapita pori na mara zote walikuwa wananiacha nyuma hata sioni mtu mbele,wakifika sehemu wananisubiri,mie nikifika wanaondoka bila kunipa muda wa kupumzika.Badaye nikakata tamaa ya safari sikutaka tena kuwa nao nikakaa chini nikalala.Mtu unatembea huku machozi yanakulengalenga
 
Mkuu unaambiwa nilitoka mazimbu ipo ipo saa kumi na mbili, nikazama tumbaku, then kasanga, nikapita kwenye hayo mashamba kuelekea mzinga, nikaibukia mzumbe hivyo hivyo nikanyoosha mashambani nikaja kuibukia barabara ya mlali, nikanyoosha panda milima shuka mabonde kufika saa tatu usiku Niko mgeta police station. Kurudi hivyo hivyo nilikuja kusikia uchovu wa kufa mtu siku tatu mbele.

Huezi amini nilikuwa napiga mazoezi tu na mpango wangu ulikuwa kuishia mzumbe ila utamu wa mashamba na mifugo niliyokuwa napishana nayo plus vilima na mabonde nikajikuta nishafika huko kote. Nashukuru sikuibukia mikumi ningeliwa na tembo au Simba mazima.
Duuuh, mkuu ulikomaa Sanaa toka Mazimbu, IPO IPO, Modeko,.chamwino, kasanga utoboe Hadi mzumbe,mlali Hadi kufika Mgeta daaah heshima kwako
 
Bulombora hii hii ninayo ijua meme ukapasua mpka kigoma mkuu?
Ubungo kariakoo ni distance fupi hata ukiwa na nauli unatembea tu.Sema ukiwa umekula hela ndo panaonekana parefu balaaaa
Nyerere alitembea toka Butiama mpaka Mwanza. Mimi nilitembea toka Bulombola mpaka Kigoma nikijongo majeshi nikaishia kukamatwa na kuswekwa lupango ya jeshi kwa mwezi. That was during Kagera war hata nyoka karibu atung'ate na mtoro mwenzangu.
 
Pale Unguja mwaka 2005,Niliwahi kutembea kutoka pale Bungeni mpaka Jozani kuleee! Sijui ni km Ngapi?
 
Mie safari yangu na baba mdogo pamoja na bro ilikuwa mbaya ndio maana naikumbuka tena Kuna wakati nakasirika kuwa walinionea,kwanza nilikuwa mdogo halafu umbali mrefu sehemu nyingine tunapita pori na mara zote walikuwa wananiacha nyuma hata sioni mtu mbele,wakifika sehemu wananisubiri,mie nikifika wanaondoka bila kunipa muda wa kupumzika.Badaye nikakata tamaa ya safari sikutaka tena kuwa nao nikakaa chini nikalala.Mtu unatembea huku machozi yanakulengalenga
Wote yalitukuta. Mimi nilitembezwa na baba mdogo wakati nipo period, nilidondoka tena kwenye daraja la miti wakadhani najifanya. I wished to die. Ndo nikapewa kapombe kidogo kuleta nguvu kumbe ndo wameharibu. I will never forget lakini tulikuwa na maisha ya raha. Hakuna wa kusema huyu ni baba mdogo wala nani ikifika safari twende tena huko ni kwenye makoro yaani kwa ndugu wa babu zetu. Sasa hivi hivyo vitu vimekufa na tumeua undugu.
 
Ni siku tofauti.
Ya kwanza nilikwenda kuomba kibarua pale tazara kiwanda cha Panasonic cha betri. Nikakosa kibarua na nauli sina. Ikabidi nirudi kwa mguu kutoka tazara mpaka manzese.

Ya pili nilitoka manzese kwenda kwa ndugu zangu kimara suka.kuwatembelea nilitoka saa 12 asubuh.mpaka saa sita nipo kimara suka. Kurudi wakanipa 5,00.ya nauli.
Sikuwaambia nilienda vipi.

Ya tatu.katika kutafuta vibarua nilikwenda pale ubungo stendi ya shamba. Pale kuna vibarua wengi na mafundi uwa wanakaa wanasubiri magari ya kuwapeleka masaiti.
Kuna tipa likaja watu Waka panda na mimi nikadandia sijui linakwenda wapi . na wale watu.
Nimekaa kwenye gari naona tunapita vituo tu.
Kibo,baruti,Kimara mwisho,stop over ,tumbo temboni. Mara mbezi MWISHO.na bado linaendelea tu.nikasema ohooo.naenda wapi huku?
Nikabidi nimuulize jamaa. Akasema wanaenda kwembe kuna shule inajengwa na kazi za vibarua zimeisha.
Basi nilienda mpaka kwembe.
Shughuli ilikuwa kurudi.acha kabisa.
Ni lite Nilitembea kwa miguu kutoka kwembe mpaka kimara suka kwa wale ndugu zangu. Nikazuga nimekwenda kuwatembelea kumbe nilikuwa sina nauli ya kurudi manzese.
Wakanipa tena 5,00.
Nilivyorudi nililala kama nimekufa
mjingamimi,
mkuu hizi ni kama nyingi sana, Ungekuwa kijijini ungeelewa vizuri.
Wabongo tunapitia mengi mkuu
 
Back
Top Bottom