Tuliowahi kuathirika na washindani wapya katika biashara tukutane hapa, ulipitia wakati gani, ulijiongeza, ulihama au ulifunga biashara?

Tuliowahi kuathirika na washindani wapya katika biashara tukutane hapa, ulipitia wakati gani, ulijiongeza, ulihama au ulifunga biashara?

Inaweza kuwa biashara yako inaenda poa yani kila ukifunga hesabu kimoyo moyo unasema “mambo si ndio haya ! ”

Mara paaaap! Anatokea mshindani mpya aidha
  • anafungua pembeni/karibu yako biashara kama yako, copy paste
  • mwenye bei za chini,
  • bidhaa zake zina ubora zaidi,
  • anafanya free delivery,
  • anauza kwa mkopo
  • Ana connection
Wataeja haoooo!! Taratibu ama instantly unaona mauzo yamepungua sana, wateja wanakauka, siku nzima ni kubadilisha pozi la miguu tu ofisini na kwenda kupiga story hapo nje mpaka jioni.

Hapa ndipo watu huingia tamaa ya kuanza kwenda kwa waganga kutafuta dawa za mvuto wa biashara, kumuangamiza mshindani, n.k. wengi wanaishia kupigwa tu
Ukiona hivo hama location Afu hukohuko unakoenda copy na paste mbinu za aliekuhamisha
 
Jamaa alikuja kwa speed alifungua duka la vyakula kama langu karibu yangu
Aisee ilikua ni vurugu mchele maharage alikua anaagiza kutoka mbeya basi alikua anauza bei ya vunja bei kwenye mchele na Maharage, mfano mchele alikua anauza mpaka 1900 kwa sisi wengine ili upate angalau faida kidogo unatakiwa uuze angalau 2200 nikamfuata nikamueleza ndugu biashara haiendi hivyo alichonijibu ni kwamba yeye anapata faida kwa hiyo hajali, basi mimi nikatoa zile bidhaa za maharage na mchele nikatumia nyumbani na familia ila wife aliona uchungu kwa sababu ndio alikua anakaa dukani
Haikupita muda nikapata kazi ifakara Morogoro, nilikuta mchele huo huo anaouza 1900 unauzwa 800 kwa kilo halafu napata usafiri wa bure mpaka mikumi au iringa mjini kwa gari ya ofisi ,yaani mchele ulikua unafika Tanga kwa Tsh 1100 kwa kilo, niliuza mchele 1500 kwa kilo na mzigo ulikua haukauki store, aliona aibu kunifuata mimi akamfuata wife kuomba yaishe, nilikaza kwa sababu nilijua project yangu kule kilosa ni ya miaka minne, hivyo ndani ya mpaka minne ningemnyoosha vya kutosha ila baadae huruma ikanijia
Noma Sana jamaa alikosa utu
 
Mimi kuna mmiliki wa kinboss spare parts hivi alinifungisha duka la spare za pikpiki mtwara mjini,sisi tulikuwa tunachukua mzigo kwao kule dar tunakuja kuuza huku ila chakushangaza wakafungua branch mtwara mjini mfano kama bulb tunachukua dar kwa 1000 ili tuje kuuza huku 1500 wao wakawa wanauza 1000 kwa rejareja,mfano cam shaft bei ya jumla 10000 wao wanauza kwa rejareja 11000 hii hali iliua sana biashara zetu kwasababu wao wanachukuwa china moja kwa moja
 
Mimi kuna mmiliki wa kinboss spare parts hivi alinifungisha duka la spare za pikpiki mtwara mjini,sisi tulikuwa tunachukua mzigo kwao kule dar tunakuja kuuza huku ila chakushangaza wakafungua branch mtwara mjini mfano kama bulb tunachukua dar kwa 1000 ili tuje kuuza huku 1500 wao wakawa wanauza 1000 kwa rejareja,mfano cam shaft bei ya jumla 10000 wao wanauza kwa rejareja 11000 hii hali iliua sana biashara zetu kwasababu wao wanachukuwa china moja kwa moja
Hii alifanya baada ya kuona mzigo mnaochukua ni mkubwa alafu mnaenda Mara kwa mara,navyoona
 
Nafatilia comments
1687900357487.jpg
 
Nikweli mkuu uko sahihi ndicho kilichotokea kinboss aliona 70% ya wateja walikuwa ni kutoka mtwara akajua huko mtwara kuna hela ndio maana akaja kufungua hilo tawi na akaja kutuua njaa
Kwa hiyo uliishia Wapi ?
 
Kwa hiyo uliishia Wapi ?
biashara ikafa huku nina madeni kibao pango nililimbikiza mpaka ikatimia 1800000 na pia kuna kampuni inaitwa Hairoad nao nikawakopa mali ya milion 12 na kampuni ya SLL nao wananidai milion 4 mpaka leo sijawalipa na laini nimebadilisha sitaki usumbufu mimi na mtwara nimehama
 
biashara ikafa huku nina madeni kibao pango nililimbikiza mpaka ikatimia 1800000 na pia kuna kampuni inaitwa Hairoad nao nikawakopa mali ya milion 12 na kampuni ya SLL nao wananidai milion 4 mpaka leo sijawalipa na laini nimebadilisha sitaki usumbufu mimi na mtwara nimehama
Kwanini usingebeba mzigo uhamie masasi?

Naona pamekaa vizuri ki biashara ungepiga hela kama mwanzo tu
 
Kwanini usingebeba mzigo uhamie masasi?

Naona pamekaa vizuri ki biashara ungepiga hela kama mwanzo tu
Unajua tatizo ni mazoea mkuu na ile hali ya kujipa moyo kuwa labda kesho itakuwa hivi kumbe ndio nadidimia ila nashukuru nimekomaa shambani kwenye ufuta nimepata kiasi fulani na nikichanganya na kiasi fulani nakuwa na kama milion 8 ndio nawaza nifungue goli la viatu vya kike au nifungue goli la urembo na vipodozi masasi
 
biashara ikafa huku nina madeni kibao pango nililimbikiza mpaka ikatimia 1800000 na pia kuna kampuni inaitwa Hairoad nao nikawakopa mali ya milion 12 na kampuni ya SLL nao wananidai milion 4 mpaka leo sijawalipa na laini nimebadilisha sitaki usumbufu mimi na mtwara nimehama
🤣🤣🤣🤣
 
Unajua tatizo ni mazoea mkuu na ile hali ya kujipa moyo kuwa labda kesho itakuwa hivi kumbe ndio nadidimia ila nashukuru nimekomaa shambani kwenye ufuta nimepata kiasi fulani na nikichanganya na kiasi fulani nakuwa na kama milion 8 ndio nawaza nifungue goli la viatu vya kike au nifungue goli la urembo na vipodozi masasi
Hakika mkuu ingia masasi pamechanganya sana kibiashara
 
Unajua tatizo ni mazoea mkuu na ile hali ya kujipa moyo kuwa labda kesho itakuwa hivi kumbe ndio nadidimia ila nashukuru nimekomaa shambani kwenye ufuta nimepata kiasi fulani na nikichanganya na kiasi fulani nakuwa na kama milion 8 ndio nawaza nifungue goli la viatu vya kike au nifungue goli la urembo na vipodozi masasi
kwa ujumla wake hii biashara ya kuuza spare kwa watu wa rejareja unaionaje kiongozi.

kuna kitu kinaitwa Return On Investment vipi kwa biashara hii ya spare za pikipiki inaweza chukua mda gani kurudisha mtaji wako?
 
kwa ujumla wake hii biashara ya kuuza spare kwa watu wa rejareja unaionaje kiongozi.

kuna kitu kinaitwa Return On Investment vipi kwa biashara hii ya spare za pikipiki inaweza chukua mda gani kurudisha mtaji wako?
Kiukweli hii biashara ni kama biashara nyingine huwa inategemea ni mji gani upo mfano hebu nijielezee mwenyewe nilianza na mtaji wa milion 28 mwaka 2010 mwezi na wakati huo maduka pale mtwara yalikuwa yakuhesabika kwa pale sokoni maduka yalikuwa 4 tu mpaķa inafika 2013 niliweza kuushika mtaji wangu mkononi huku biashara bado ipo yakutosha
 
Kiukweli hii biashara ni kama biashara nyingine huwa inategemea ni mji gani upo mfano hebu nijielezee mwenyewe nilianza na mtaji wa milion 28 mwaka 2010 mwezi na wakati huo maduka pale mtwara yalikuwa yakuhesabika kwa pale sokoni maduka yalikuwa 4 tu mpaķa inafika 2013 niliweza kuushika mtaji wangu mkononi huku biashara bado ipo yakutosha
oky shukrani mkuu.
 
Mimi kuna jamaa alikuja akanikuta hapa nnapouziaga majeneza naye akachukua chumba jirani tu nikawa namuuliza anafungua biashara gani akasema duka la rejareja lakini cha ajabu alipomaliza kukarabati tu nikaona anashusha mzigo wa majeneza kama 200 hivi nikasema poa!
Nikamuacha kama week hivi nione kama ana madhara yoyote kwangu maana mie nilishakuwa maarufu hapa Dodoma nafahamika sana pia najuana na madaktari wengi kiasi kwamba wananiunganishia wateja kila siku then nawapa 10%
Kumbe hii jamaa ilishafanya uchunguzi njia zote za mimi kupata wateja akaanza kupita mule mule akatengeneza connection na hao watu wa hospital ya karibu halafu akawa anawapa zaidi hata ya hiyo 10% kwa kila kichwa halafu bado angle ambayo office yake ilikuwepo ni mbele kidogo karibu na barabara yaani mteja akifika tu anaanzia pale kwake!
Nikaona isiwe tabu nikasafiri kodogo kutafuta mtaalamu wa ndumba kijijini kwetu niliporudi huyu jamaa hakuchukua hata week akafunga na kuhama kabisa! Sitakagi ujinga kwenye mambo ya biashara yangu.
 
Mimi kuna jamaa alikuja akanikuta hapa nnapouziaga majeneza naye akachukua chumba jirani tu nikawa namuuliza anafungua biashara gani akasema duka la rejareja lakini cha ajabu alipomaliza kukarabati tu nikaona anashusha mzigo wa majeneza kama 200 hivi nikasema poa!
Nikamuacha kama week hivi nione kama ana madhara yoyote kwangu maana mie nilishakuwa maarufu hapa Dodoma nafahamika sana pia najuana na madaktari wengi kiasi kwamba wananiunganishia wateja kila siku then nawapa 10%
Kumbe hii jamaa ilishafanya uchunguzi njia zote za mimi kupata wateja akaanza kupita mule mule akatengeneza connection na hao watu wa hospital ya karibu halafu akawa anawapa zaidi hata ya hiyo 10% kwa kila kichwa halafu bado angle ambayo office yake ilikuwepo ni mbele kidogo karibu na barabara yaani mteja akifika tu anaanzia pale kwake!
Nikaona isiwe tabu nikasafiri kodogo kutafuta mtaalamu wa ndumba kijijini kwetu niliporudi huyu jamaa hakuchukua hata week akafunga na kuhama kabisa! Sitakagi ujinga kwenye mambo ya biashara yangu.
😂😂😂 sio upo pale chako ni chako kweñye kona ukiwa unashuka kwenda katikati ya jiji
 
Back
Top Bottom