Tuliowahi kudhulumiwa na Mtandao wa Tigo Tanzania tukutane hapa

Tuliowahi kudhulumiwa na Mtandao wa Tigo Tanzania tukutane hapa

Mwaka 2013 nilikuwa natumia line hii 071X008580. Kuna deni nilikuwa nadaiwa kama Tshs.35,000/-, Nikamtumia mdai wangu kiasi hicho mida ya saa tano usiku, Sikupata meseji yeyote ya uthibitisho, kuwa ujumbe wangu umefika kwa mlengwa japokuwa salio langu lilikuwa limekatwa tayari, na nilipojaribu kupiga call centre niliambiwa kuna tatizo la network mafundi wanajaribu kulitatua, nitapata mrejesho baadaya ya masaa 24. Ilinibidi nizisubirie hizo saa, japokuwa mdai wangu alionyesha kama kutoniamini kwa kile nilichomwambia...baada ya masaa hayo kupita sikupokea ujumbe wowote..Nilifuatilia takribani mwezi bila ya majibu yenye uhakika..zaidi ya tatizo letu la kiufundi likitatulia utaona ujumbe huo mfupi. Nizungumzavyo mpaka leo sikupokea ujumbe wowote na hela yangu ilikatwa. ilipita mwaka sikuwa na imani tena na hii kampuni...Mpaka leo siitaki hata kuisikia...Majuzi nilipiga hiyo namba yangu ikapokelewa na bidada mmoja nasikia yupo mbeya.


Sent using Jamii Forums mobile app
Daah hii ilinitokea pia 2017 nlituma hela haikwenda na majibu yao ndo hayo hayo wanakwambia tatzo la mtandao subiri masaa 72, yakiisha ukiwafata tena wanakwambia subiri masaa 24... miezi na miaka ikapita hela yangu ikapotelea hewani.
Huu utapeli sio kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jana nimemtukana mtu wa customer care. Laini yangu ni mpya, nilihamisha salio kutoka mpesa kila nikijaribu kununua kifurushi naambiwa transaction declined. You are not registered with this service, tangu wiki iliyopita.... kile kitoto kikanijibu ' tigo pesa yako iko vizuri, haina tatizo lolote...una tatizo lingine nikusaidie'? Angekuwa jirani nahisi ningemchapa makofi

Sent using Jamii Forums mobile app
Huo mtandao ni shida
 
Nilijiunga kifurushi cha mwezi wakashindwa kuniunganisha nikakaa masaa matano ikashindikana nikajiunga tena wakanipa. Ajabu wakakata hela ya mwanzo na kifurushi hawakuwa wamenipa. Kuwapigia wakanambia wataniwekea kifurushi nikawaambia acheni upuuzi nirudishie hela tigopesa maana ndo natumia kujiunga.

Walisema ndani ya masaa 24, ndani ya lisaa nikapata ujumbe kuwa nimerudishiwa muhamala. Hapa ndo nilichoka, muhamala wa sms lakini kwa tigopesa hakuna hela.
Nikawapigia walichokifanya ni kuniunganisha tena kifurushi, nikasema sawa. Kikiisha hamnioni. Siwezi tumia network ina uswahili mwingi utadhani management wameiokota kilabuni.
 
Nishawai enda pale makumbusho ,hakuna mlinzi aliyeweza zuia nikuwa mkali kupita maelekezo..niliweka vocha ya 5000 ghafla kifurushi kinagoma kuunganisha kutazama salio ni zero, nilianza na yule binti wa huduma kwa wateja toa maneno sana..nikamwambia kesho nakuja nimevaa hivi ukiweza andaa polisi kabisa

Walirudisha ndani ya nusu saa
 
Ona tigo wanavyonitesa.
[08/12/2019, 07:19] Laigwanan: [14/11, 21:08] Laigwanan: Have bought an internet bundle worth 3000 but the same have not been credited into my account. Please do the needful.
[14/11, 21:08] Laigwanan: Payment Successful. Amount: TSh 3,000. New balance is TSh 351,314. TxnID 32493546632.
[08/12/2019, 07:22] Laigwanan: If you don't understand that, then tigo must be employing the wrong people and may be that is6 why it is almost a month the problem still stands.
[08/12/2019, 08:38] Tigo WhatsApp: Laigwanan.Thank you for communicating with us we are still working on your issue kindly wait.

Hi Laigwanan, We apologize for such delay, We are still working on your transaction with ID 324935466992. We will let you know when your issue sorted kindly wait.


Laigwanan,Tafadhali tunaomba rejea maelekezo tuliokupatia hapo awali taarifa zako zipo katika utatuzi.
 
Tigo ya mwaka gani hiyo, mbona sahiz naona wanajitahid kuliko mtandao flan wa mabosi,
Saa zingine huwa kunatokea matatizo ya kiufund tu mfano Voda tangu juzi internet haipo, kukatwa salio ndo usiseme hayo n matatizo ya kimtandao yapo kwote,
Mnamo Jumanne ya Tarehe 11 mwezi huu (Februari 2020) nilinunua kifurushi cha Internet kwa njia ya Tigo Pesa. Ndugu zangu wana JamiiForums yakapita masaa 24 bila ya kupewa kifurushi wala kupewa taarifa yoyote.

Nilichukua hatua ya kuwapigia Huduma kwa Wateja, nikajibiwa kifurushi changu kitawezeshwa baada ya masaa 24. Kwa hakika nilidanganywa.

Nikawa nikiwapigia simu kila baada ya masaa 24 lakini hakuna nilichosaidiwa zaidi ya kuambiwa nisubiri masaa 24 mengine na hadi leo hakuna nilichorudishiwa si fedha wala si kifurushi.

Huu mtandao umekubuhu kwa huduma mbovu lakini cha kushangaza sasa wamehamia hadi kuiba fedha za wateja.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Walivyo wajinga wamewatoa vifurushi vya chuo Wateja wao wote wa zamani tofauti na wenzao mitandao wengine na kuleta saizi yako badala kuboresha kwenda mbele wao wamerudi nyuma wamewapa wenzao fursa kuongeza Wateja ila mjifunze siku nyingine mnaangalia mteja kifurushi anachopenda mnamuacha na mnamuekea kingine yeye ndiye achague ila nyinyi mnalazimisha utake usitake jiunge hivi mnafeli na mtaendelea kufeli mkiendelea na ujinga wenu
 
Mimi 2017-2018 Nilihamisha pesa Laki 4 mara mbili kutoka Voda kwenda TIGO. Muhamara wa kwanza ilikua Successfully. Muhamara wa 2 Tsh laki 2 haukua succeful na Message ilikuja kuwa within 24 hrs pesa itarudishwa.
Nikasubiri baada ya masaa 48 hakuna pesa. Kwenda TiGo shop wakasema haada ya masaa 72 pesa itarudishwa. Na kwenye Kompyuta wanasema walikua wanaiona ipo hewani haijawa delivered. baada ya 5 days kurudi wakasema pesa ilishakua delivered kama kuna shida niende Voda. Kwenda Vodashop nikawaomba Wa-trace mihamara nilioifanya. Wakasema Nilituma pesa kutoka Voda kwenda Tigo ktk siku husika mihamara 2 inapishana kwa almost dakika kadhaa kila m1 Tsh Laki 2. Nikawaomba Voda wani printie transaction history wakakataa. Ila wakasisitiza niende Tigo pesa yangu ipo hapo.
Ukweli kuna wizi mkubwa unaofanywa kwenye Makampuni kwa kugezo cha Network problem.
TCRA tunaomba watafute jinsi ya kuwasaidia wananchi.
 
Mnamo Jumanne ya Tarehe 11 mwezi huu (Februari 2020) nilinunua kifurushi cha Internet kwa njia ya Tigo Pesa. Ndugu zangu wana JamiiForums yakapita masaa 24 bila ya kupewa kifurushi wala kupewa taarifa yoyote.

Nilichukua hatua ya kuwapigia Huduma kwa Wateja, nikajibiwa kifurushi changu kitawezeshwa baada ya masaa 24. Kwa hakika nilidanganywa.

Nikawa nikiwapigia simu kila baada ya masaa 24 lakini hakuna nilichosaidiwa zaidi ya kuambiwa nisubiri masaa 24 mengine na hadi leo hakuna nilichorudishiwa si fedha wala si kifurushi.

Huu mtandao umekubuhu kwa huduma mbovu lakini cha kushangaza sasa wamehamia hadi kuiba fedha za wateja.
Mimi juzi tu hapa nimeacha jero kwenye Salio la kawaida wamekata eti wamechukua kwa ajili ya kifurushi cha SOCIAL kitu sijawahi hata jiunga na sikijui nkawapigia wanalazimisha nlijiunga WAHUNI SANA JAMAA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wiki iliyopita niliweka salio nikawa nataka kujiunga kifurushi cha intaneti cha sh 2000 1gb kipindi hicho ilikuwa, Kila nilipojaribu kujiunga niliambiwa salio halitoshi nikiangalia limo nikaona nijiunge kifurushi cha chini yake sh 1000 ilikuwa mb 300 wakati huo, kujaribu ikakubali. Kuanza kuperuzi youtube hakikumaliza hata dk 3 kikaisha. siyapendi Tigo majizi sana.

Siku hiyo walikuwa wanaiba kwa njia mbili
1. Ku encourage watu kujiunga kifurushi cha siku badala ya wiki ili kuvuna pesa nyingi kwa siku.

2. Kutoa mb pungufu ya kiwango ulichonunua. Mbin hii nimeiona hata kwenye vifurushi vipya vya sasa walivyotoa wanaotumia kuibia watu. Jana nilijiunga kile cha gb 3 sh 2000 sikufanya chochote nikaanza download video kuja kujumlisha saizi ya nyimbo nilizodownload hazikufika gb 3 ziliishia gb 1.4 kama sikosei
Njia nyingine ni kukata fedha ukijiunga kupitia Tigo Pesa na kutotoa kifurushi. Wizi kila kona ukiwapigia wanasema wanashughulikia
 
Mwaka 2013 nilikuwa natumia line hii 071X008580. Kuna deni nilikuwa nadaiwa kama Tshs.35,000/-, Nikamtumia mdai wangu kiasi hicho mida ya saa tano usiku, Sikupata meseji yeyote ya uthibitisho, kuwa ujumbe wangu umefika kwa mlengwa japokuwa salio langu lilikuwa limekatwa tayari, na nilipojaribu kupiga call centre niliambiwa kuna tatizo la network mafundi wanajaribu kulitatua, nitapata mrejesho baadaya ya masaa 24. Ilinibidi nizisubirie hizo saa, japokuwa mdai wangu alionyesha kama kutoniamini kwa kile nilichomwambia...baada ya masaa hayo kupita sikupokea ujumbe wowote..Nilifuatilia takribani mwezi bila ya majibu yenye uhakika..zaidi ya tatizo letu la kiufundi likitatulia utaona ujumbe huo mfupi. Nizungumzavyo mpaka leo sikupokea ujumbe wowote na hela yangu ilikatwa. ilipita mwaka sikuwa na imani tena na hii kampuni...Mpaka leo siitaki hata kuisikia...Majuzi nilipiga hiyo namba yangu ikapokelewa na bidada mmoja nasikia yupo mbeya.


Sent using Jamii Forums mobile app
Ona sasa, huu ni utapeli wa wazi wazi. Tigo Tanzania unatuchosha wateja wenu kwanini mnatufanyia hivi? biashara inaendana na uaminifu sio hiki mnachifanya

Internet yao yenyewe ni speed ya kobe lakini now wanaongeza na wizi juu
 
Jana nimemtukana mtu wa customer care. Laini yangu ni mpya, nilihamisha salio kutoka mpesa kila nikijaribu kununua kifurushi naambiwa transaction declined. You are not registered with this service, tangu wiki iliyopita.... kile kitoto kikanijibu ' tigo pesa yako iko vizuri, haina tatizo lolote...una tatizo lingine nikusaidie'? Angekuwa jirani nahisi ningemchapa makofi

Sent using Jamii Forums mobile app
Nadhani hata watu wanaowaajiri akili na uwezo wao kwenye taaluma na kazi ya Huduma kwa Wateja iko chini sana na yawezekana hata mishahara hawalipi vizuri au wanawatapeli pia maana hata huduma kwa wateja nayo ni ya ovyo
 
Back
Top Bottom