Tuliowahi kudundwa siku ya kufunga shule primary tukutane hapa

Tuliowahi kudundwa siku ya kufunga shule primary tukutane hapa

Yaani[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]nilikuwa nawashangaa walivyo wakubwa nikawa najiuliza hawa walichelewa wapi?...na walikuwa wanavaa uniform kabisaa basi ni balaaa,nadhani walimu walikuwa wakiingia darasa la MEMKWA walikuwa wapole sana.

Halafu ukiwachokoza unaambiwa "wewe huyo MEMKWA shauri yako ee"..
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Kama kichwa cha habari kinavyosema. Enzi zile tunasoma kulikuwa na list ya wakali wa masomo darasani (kumi bora)ambayo ilikuwa official na pia kulikuwa na list ya wababe katika kupigana kuanzia wa kwanza mpk wa mwisho.

Sasa mie nilikuwa mkali sana darasani ila kwenye kupigana nilikuwa kama wa tano wa mwisho hivi so kuna jamaa mmoja alikuwa nae wa mwisho mwisho akataka kupigana na mie ili apande kwenye chat ya ngumi na pambano likapangwa siku ya kufunga shule

Jamaa alikuwa mfupi kuliko mimi so nilikuwa nina uhakika wa ushindi. Siku hiyo shule ilipofungwa pambano likapangwa uwanja wa mpira na darasa zima walikuwepo. Mchezo ulianza vizuri na niliutumia urefu wangu vizuri nikawa ninampa nakozi za kutosha sasa kuna kipindi nikawa naona naelekea kushinda nikawa napigana style ya Mohamed Ali ile ya kuruka ruka kwa mguu mmoja (wahenga mtakuwa mnaikumbuka hii) kumbe yule mpinzania wangu alikuwa ananilia timing.

Jamaa alinitisha kama ananipiga kwa kushota nilipokwepa alinipa konde moja la paji la uso na kulia niliona nyota kama 100 hivi usoni na wakati natafakari jamaa alinirukia kichwa kimoja cha usawa wa mdomoni na nikajing'ata ulimi na kutoka na damu balaa, wakati nikiwa nimevurugwa jamaa alinipiga mtama mmoja mkali nikadondoka kama gunia.

Ilikuwa bahatu yangu maana jamaa alinidhibiti kwa juu lakini wataalam wakaamulia na kusema zipigwe za juu juu ili tupate mshindi

Tuliposimama huku damu zikinivuja mdomoni kama teja anavyotokwa mate nilicheki watu waliotuzunguka nikaona upenyo mmoja nikatoka baruti kama Juma Ikangaa unaambiwa darasa zima likaanza kunikimbiza huku wakinizomea mpk demu wangu wa utotoni (Pili) nae alikuwepo ktk watu waliokuwa wananizomea na kunikimbiza. Nilitimkia ofisi ya mwalimu mkuu ndipo nilipookokea hapo
We utakuwa ulisoma mkoa wa Kilimanjaro manake kule ndio tulikuwa na mambo hayo kila shule zikifungwa, mikoa mingine sidhani sana.
 
Kuna demu mmoja aliwahi kunidunda njiani siku ya kufunga shule, full kunigalagaza chini hadi walipokuja kuniokoa, alikuwa na mwili mimi nilikuwa kimbaumbau. Kuanzia siku hiyo nilikosa raha yaani full kutaniwa[emoji16], nakumbuka alikuwa anaitwa Augusta kifupi anaitwa 'Ugu', nilikuwa nikizingua kidogo utasikia tutakuitia Ugu, basi nakuwa mpole[emoji13][emoji13], hivi karibuni nimejaribu kumtafuta nimuoe sijafanikiwa kujua alipo wala kupata mawasiliano. Mniombee
 
Kuna mkaka nakumbuka tukiwa standard 5 tumeenda uwanjani kwenye mazoezi akanipigia mpira nilimdunda mpaka akazimia ile wanampandisha kwenye school bus akazinduka ikabidi baba aitwee shuleee nilichezea vitasa sitakaaa nisahau kabisaaaaa
 
Kuna demu mmoja aliwahi kunidunda njiani siku ya kufunga shule, full kunigalagaza chini hadi walipokuja kuniokoa, alikuwa na mwili mimi nilikuwa kimbaumbau. Kuanzia siku hiyo nilikosa raha yaani full kutaniwa[emoji16], nakumbuka alikuwa anaitwa Augusta kifupi anaitwa 'Ugu', nilikuwa nikizingua kidogo utasikia tutakuitia Ugu, basi nakuwa mpole[emoji13][emoji13], hivi karibuni nimejaribu kumtafuta nimuoe sijafanikiwa kujua alipo wala kupata mawasiliano. Mniombee
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] aisee
 
Enzi hizo ukitaka uwe vizuri inabidi akili zichaji na mpira uwe unaujua,hutasumbuliwa maanake unafit groups zote. Kuna wale manunda shule zero ila mpira balaa hawa utaelewana nao kwasababu ya mpira. Kuna wale watoto wa mama john visomo hawajui mpira so utaelewana nao kwenye masomo! Enzi zangu nilikuwa naombwa nibaki kucheza mechi za madarasa.
 
Kwa waliosoma muhimbili primary school nadhani mnaukumbuka Barafu Centre

Hicho ndio kilikuwa kiwanja cha hukumu siku za kufunga shule lazima mtu akapigwe au akapige tu

Utoto hahaha siku za kufunga shule zilipokaribia kuwa makini sana mpirani, darasani au mabishano yoyote ilikuwa ndio tiketi ya kwenda kupigana huko muda wa kwenda nyumbani

Na kosa kubwa pale unapojipandisha ktk chati ya wababe wa kupigana wakati wewe ni kibonde...yalinikuta hayo hahaha
 
Kuna demu mmoja aliwahi kunidunda njiani siku ya kufunga shule, full kunigalagaza chini hadi walipokuja kuniokoa, alikuwa na mwili mimi nilikuwa kimbaumbau. Kuanzia siku hiyo nilikosa raha yaani full kutaniwa[emoji16], nakumbuka alikuwa anaitwa Augusta kifupi anaitwa 'Ugu', nilikuwa nikizingua kidogo utasikia tutakuitia Ugu, basi nakuwa mpole[emoji13][emoji13], hivi karibuni nimejaribu kumtafuta nimuoe sijafanikiwa kujua alipo wala kupata mawasiliano. Mniombee
Hahaa angalia asije akakudunda tena mkuu
 
Nina sura shit balaa mtu alikua akiniangalia anaghairi ugomvi.

Ila roho iliniuma nilizipanga na Mikidadi kisa Salome halafu Salome bado akanichomolea.
 
Back
Top Bottom