Wadau,leo nimeona nielezee kisa hiki kilichonikuta kwenye basi nikitoka mbeya/tukutu kwenda dsm.
picha linaanzia hapo natoka zangu nyumbani,ilikuwa safari yangu ya kwanza kuja dam kujiunga na chuo cha duce baada ya kumaliza masomo yangu ya advance.
kwakua sikua na wa kusafiri nae basi niliamua kusafiri mwenyewe baada ya kupewa maelezo ya kutosha na braza wa kijijini kwetu ambaye yeye alikuwa mwaka wa pili udsm.
basi bwana kama unavojua sisi wanyaki,siku moja kabla ya safari ulikuwa ni mkesha wa kuniaga,nyumbani kulifanyika mkusanyiko kidogo wa ndugu hasa wajomba na mshangazi,kila mmoja akaleta cha kuleta nyama za kuchoma,viazi vitamu na mviringo,maziwa freshi,maziwa mgando,unga wa ugali,mchele,maharagwe na kunde,pilipili n.k vitu vilipikwa mkesha ukakaliwa ukaisha.
usiku ule nilikula sana,nilivimbiwa kwa kifupi,sasa kimbembe kikawa asubuhi,ile saa kumi na mbili naamka mara tumbo likaanza kuvuruga kama utani,nikajua hapa tayari safari yangu imeingia mdudu,sababu najuaga nini kitatokea...basi bwana nikaenda chooni nakuta hola ila tumbo linanguruma as if kuna mtu anakoroga vitu kwa ndani.
muda wa kupanda gari letu kyela express ukafika,nikapanda kiujasiri japo bado tumbo linavuruga,nikiwa na akiba yangu ya viporo vya vyakula vya jana...nikafika uyole nikajiongezea akiba kidogo ya aepo na soda.
kwenda weeeee kufika mbele kuna mbaba huwa anauza kababu na kashata kwenye magari ya mbeya dsm ni maarufu sana,nikagonga kashata zangu na bagia,nikashushia na maziwa mgando,nikanywa soda ya spaleta baridi na epo zangu tatu,kufika makambako nikanywa maziwa yalikuwa kwenye kopo,nikashushia na maji...nikawa taratiiiibu nafikicha karanga narushia mdomoni kwa mbwembwe flani za kisela....
sijui nini kilitokea lakini nikahisi tukiwa maeneo ya misitu ya sao hill...tumbo ghafla lilijaaaa kama limejazwa upepo hivi,nikajua tu hapa leo siyo salama,mimi nikajinyanyua kidooogo ile kisailensa,nikapanua mguu mmoja katika style ambayo hakuna aliegundua..then nikaanza kuiachia ile hewa sasa ili itoke huku nikisikia uafadhali wa hali ya juu tumboni...
basi bwana,tukio lilidumu kwa muda kama wa dakika mbili hivi ile hewa inatoka tu,inatoka tu...baada ya sekunde kama kumi hivi nikaanza kuhisi utulivu wa watu kunizunguka unapungua,kuna mtoto mchanga alikuwa pembeni alipiga chafya moja kali sana,kali sana,basi wakaanza kufungua madirisha na kupeperusha magazeti hivi na vitabu,sasa ikawa ni basi zima wakahisi labda kuna kitu kimeoza.
muda ote huo mnyambala nawachora tu wanavohangaika na vitu vidogo tu hivi....
nasikia ule ushuzi ulikuwa na half life ya dakika 5 (kwa waliosoma radioactivity)
sasa wale waliowahi kufanya tendo hili la kishujaa kwenye halaiki waweke ushuhuda wao hapa ilikuwaje.....