Mangungo II
JF-Expert Member
- Jul 6, 2012
- 18,133
- 26,766
Usiwalaumu watu kwa matatizo Yako.Ulifika fedha kiasi gani ukapoteza, hiyo itanipa msingi wa ushauri.
Unanikumbusha ipo siku nauguliwa na mtu kisha nampigia simu mtu ninaemuamini nikope laki 2 nimtibu mgonjwa ananijibu hana kitu ilihalu nilikuwa na uhakika anayo, nilikaa sehemu nililia sana, nikajisemea hela nilizokuwa nazo mimi wa kukopa mtu leo laki mbili nimtibie mtu ninyimwe.
Anyway yule mgonjwa akafa.
Dah watu wahonga aisee..mi nilihonga afu ishirin naiwaza hadi leoMi sister angu aaah alikua anahongwa hadi mil 50, mil 20, mil kumi......Kuna rfk ake na Ridhiwani Mzungu mmja hiv kam spoil sana sister sir tupo tunatoa mimacho tu.....eeh ukimuona sa hv sister angu yani sio yule R Dangote yani hata ukimwambia ccy twende ukanispoil anakwambia mdg angu sina ubavu huo
Mim kuhongwa pesa kubwa kabisa ni mil 5 nkahongwa mara ya pili tena mil 3 nkaongezea nkafungua biashara siku ya siku nliibiwa kila kitu dukani nlikua chizi fresh
Ulifika fedha kiasi gani ukapoteza, hiyo itanipa msingi wa ushauri.
Unanikumbusha ipo siku nauguliwa na mtu kisha nampigia simu mtu ninaemuamini nikope laki 2 nimtibu mgonjwa ananijibu hana kitu ilihalu nilikuwa na uhakika anayo, nilikaa sehemu nililia sana, nikajisemea hela nilizokuwa nazo mimi wa kukopa mtu leo laki mbili nimtibie mtu ninyimwe.
Anyway yule mgonjwa akafa.
Kufilisika kusikie tu. Binamu yangu alipataga mil. 600. Aliuza nyumba mikocheni , akanunua nyingine Mbezi beach milioni 200, na kuifanyia finishing iliyokuwa imebaki. Milioni 350 ziliisha hivihivi, alifungua duka la spear used za magari likafa etc. Aliishiwa hata hela ya nauli alikosa. Mbaya zaidi watoto na mkewe walimtenga kwa kuugua. Alikufa mwaka jana na stress.
Na wanajua kunusa hela hao. Ulifulia ndio utajua ni kina naniMbongo akipata pesa anachanganyikiwa anakuwa na machawa kibao wnaamfilisi
We acha tu bei uwa inacheza vibaya sana.Nimekuelewa vizuriMwaka 2011 soko kuu mwanza nikiwa ninauza nafaka zikiwemo karanga, njugu, choroko,dengu,ufuta,ulezi,uwele,mtama,maharage na kunde.
Kamtaji kalivyokuwa nikawa naendea karanga tabora tani kadhaa nauza jumla. Nilipata pesa kwa njia hiyo. Basi kufkia December karanga zikawa chache Sokoni hivyo mwenye nazo alipiga pesa balaa.
January 2012 nikaingia poli kusaka karanga mpya ili niwahi bei sokoni. Basi nikapata kama gunia 30 (tani 3). Kufkisha Sokoni ziligombaniwa kama nyama. Nikaona pesa si hii apa. Nikazoa msingi wote around kama 22.8m. ili nikapige mkupuo mmoja nije nitulie.
Kuleta mzigo nafika Sokoni nakutana na fuso 6 zinashusha mzigo. Sasa kila mmoja ashajua ni dil acha bei ishuke. Nilijikuta karanga nimezinunua 2300 natakiwa niziuze 1600. Sasa nilipoharibu nikapiga mzigo stoo kwamba bei ikikaa sawa nitauza duh! Kumbe mzigo si haujakauka vizuri, nilikaa kama wiki nafungua stoo nakuta mzigo wote umevunda... Duh!
We jamaa hiyo 70 kwa week ni 280k kwa mwezi usidhani ni hela ya maana.@King Kong III ebhana kama unaipata kiuhakika hiyo hela ni kubwa na ukiwa na nidhamu ndio kabisa unabadilika kimaisha mdogo mdogo
@kikiboxer unaiona haina maana coz unapata zaidi ya hiyo kuna kipindi hiyo inakuwa kama milion 1We jamaa hiyo 70 kwa week ni 280k kwa mwezi usidhani ni hela ya maana.
Uko wapi now kikaziAsante Sana mkuu,Hadi SASA nakula msoto nakazi nimehamishwa kwenda eneo ambalo sio la kupata pesa naishi Kwa kibangaaiza Tu nakibarua chenyewe nikichungu ,huuu Uzi umenifariji Sana Sana Sana Tu.
Aisee haya maarifa wengi hatuna. Ila tunajifunza humu JF.Mtaji wowote, Ili mradi uwe na shareholder. Unaweza kumpa mtu asilimia 3% baba au mama.
LLC ni body corporate kwa hiyo itashitaki na kushitakiwa, itaweza kukopeshwa na benki.
Itakuwa na akaunti yake, TIN namba yake.
Itakuwa na assets zake na liabilities zake.
Muhimu zaidi itatofautisha kati ya wewe na biashara zako. Huu ndiyo mwanzo wa heshims ya matumizi ya hela.
Ukiwa na hela nyingi kiasi, kopa na uendeshe biashara yako kwa kutumia mkopo wa benki.
Ndiyo matajiri wanachofanya. Kopa benki, kwa kutumia LLC.
Itakusaidia kwenye Kodi. Loans don't get taxed.
Biashara ni imani..fanye utafiti pia kujua nini hasa tatizo.Bora wewe 70 mimi kuna mtu nimemfungulia salon na niko mwenyewe kwanza na check upepo week nzima imeingia tsh 2500 hahahah saloon ina week 2. Na hlo eneo salon ni mimi tu
2011, nilianza biashara ya kuuza milango na anko na muuzaji akawa mdogo wangu.Nikiwa nimemaliza chuo sina hili wala lile, niko kitaa nikijipanga, nikachangiwa na ndugu zangu mtaji wa milion 4 point something huko, niende nikafanye biashara ya mchele toka Moro vijijini kuleta mijini na kusambaza kwa bei ya jumla.
Biashara mwanzo ilienda vizuri, mwisho wateja wangu wa siku zote wakawa wakopaji wangu wakubwa, malipo yakawa ya kuzungushana, nikawa mkali kidogo ila kwa bahati mbaya pesa ikawa ndogo kwenye mzunguko wangu, sinunui tena zile kilo nilizoanza nazo kwa wakati, mambo yakawa tofauti kidogo, nikaenda weee.
Mwisho wa siku nikachanganyiwa mchele kipuuzi kabisa na mtu ambae nilikua namuamini, nikajikuta nipo na mchele wa vitumbua na jamaa yule kakimbia, hapo ndio ukawa mwisho wangu, nilifilisika kama kuku, ndugu zangu hawakunielewa tena, nilipata stress kama tani 7 hivi.
Wakati tena nikapataga milion 3 kwa enzi zile haikua haba aisee, nikawa naishi vizuri tu, hizo elf 10 kwangu zilikua buku, sina cha kujibania kwa kweli, kuja kustuka nimenunua friji na tv tu vya geto tena ka friji kale kadogoo kabisaa, hela yotee imeisha katika njia zisizoeleweka, nilichanganyikiwa tena, sina nidhamu ya fedha.
Mwisho nikarudi zangu kusoma tena chuo ndio nikaja kutoboa kwa njia zingine kabisa kwa kutumia kazi niliyosomea.
Je, wewe unakumbuka vipi? Nini kilikupata?
Mwezi wa tatu mwaka jana nikapewa mil 8 za mirathi. Nikawaza nifanyie nini? Wazo langu la kwanza, ninunue shamba porini, nifuge mbuzi na kondooo. Nikaenda minada ya mbuzi na kondooo, nikakuta hali siyo nzuri. Yaani vitoto vinauzwa kwa bei ya mbuzi na kondoo waliokomaa.Hela za urithi hazina hasara.
Nilizitumbuaaaa.
KATIKA MAISHA HAKUNA KITU KIZURI KAMA KWENDA KU WITHDRAW ATM.
Ule wimbo wa Selina selina, uongo wako selinaDu acheni kunikumbisha, nilikuwa nafanya kazi sehemu flani wafanyakazi wenzangu wakashawish kampuni iwe inatoa mkopo Mara pa ikakubaliwa na wenzangu walichukua mkopo mkubwa na Mimi nikachukua 8ml, do kwanza sijazigusa mwezi mzima najaza mipango kwenye makaratasi, usiku naamka napanga mipango, nikapata wazo nidroo pesa zote nikae nazo Ndani.
Nikadraw, siku moja kama demu wangu kaniambia mbona siku hizi unapiga mahesabu sana na makaratasi mengi mezani, nikamwambia hamna mipango tu, Mara akajua Nina pesa, akaja home sijui alinitime VIP akaiba zote, kuna machinga nilimuambia aniletee pas original asijal gharama, siku kaja nachek bahasha sioni pesa nampigia simu Selina hapatikani, nauliza nkaambiwa ameenda Morogoro, jamaa anasema pasi elfu 40, kaiacha hapo,
Mmh aisee bhasi ilikuwa kama zariiiNakumbuka 2018 wakati bado nilkuwa o-level niliweza kubana pesa kuifikia kiasi cha laki 7 ni kapata wazo la kuwekeza ktk kilimo cha mihogo wilayani mkuranga kata ya hoyoyo kijiji cha hoyoyo. Bahati mbaya mvua ikawa adimu jua kali mbegu yote ikauka nikaweka nyngne pia nayo hvohvo nikakata tamaa kutokana na ckuwa na pesa nyngne na istoshe nilkuwa naingia kidato cha nne ambapo nilitakiwa kuspend much time kweny masomo. Nakumbuka iyo siku nilrudi nyumbani nimechanganyikiwa nililia sana nikaona kama mkosi. Mungu c Athuman nilipokea kiasi cha shilingi million moja na laki tatu kweny bank account yangu. Sikuamini nikaacha week ipite hatimae mwezi hamna mtu aliyenitafuta, nilifatilia bank kama Kuna miss deposits nikaambiwa hamna tatzo nikatoa pesa zote nikanunua kiwanja Alhamdulillah machungu yalifutika