Tuliowahi kupata pesa na kufilisika/kufulia, tujikumbushe hapa

Tuliowahi kupata pesa na kufilisika/kufulia, tujikumbushe hapa

Yap! Niliipata kimazabe sihitaji kuizungumzia sana, ila ilinitoka hivyo hivyo kama mm nivyoipata. Nilipigwa mkuu, zaidi ya b1.9 kuna kazi hiyo pesa ni ndogo sana na unaweza kuwa nayo na bado mfukoni usiwe na kitu, pesa inazunguka, sasa apo kwenye kuzunguka hapo, kuna kifo, dhulma ama utoboe mazima japo chance ya kutoboa mazima ni ndogo mno sababu maadui ni wengi hasa usiowajua..ndani ya saa 1 tu nilibaki kapuku mpaka hivi. Sijutii sana sababu naamini ilippaswa tu kuwa hivyo.
Pole
 
Mwaka 2011 soko kuu mwanza nikiwa ninauza nafaka zikiwemo karanga, njugu, choroko,dengu,ufuta,ulezi,uwele,mtama,maharage na kunde.

Kamtaji kalivyokuwa nikawa naendea karanga tabora tani kadhaa nauza jumla. Nilipata pesa kwa njia hiyo. Basi kufkia December karanga zikawa chache Sokoni hivyo mwenye nazo alipiga pesa balaa.

January 2012 nikaingia poli kusaka karanga mpya ili niwahi bei sokoni. Basi nikapata kama gunia 30 (tani 3). Kufkisha Sokoni ziligombaniwa kama nyama. Nikaona pesa si hii apa. Nikazoa msingi wote around kama 22.8m. ili nikapige mkupuo mmoja nije nitulie.

Kuleta mzigo nafika Sokoni nakutana na fuso 6 zinashusha mzigo. Sasa kila mmoja ashajua ni dil acha bei ishuke. Nilijikuta karanga nimezinunua 2300 natakiwa niziuze 1600. Sasa nilipoharibu nikapiga mzigo stoo kwamba bei ikikaa sawa nitauza duh! Kumbe mzigo si haujakauka vizuri, nilikaa kama wiki nafungua stoo nakuta mzigo wote umevunda... Duh!
Babu pole wew

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
pole sana ndugu ni maumivu makubwa.
Mimi December tarehe 10 nilikuwa na 10M hadi kufikia tarehe 5 mwaka huu nilikuwa sina hata 100,.
Jana kuna mama tulikuwa tunapiga story anamjengo mkali kinoma akawa anasema kuna kipindi alikuwa na pesa nyingi zaidi ya mil 300 Bank akawa anawapa hadi watoto wake kadi wakatoe pesa hata wakizidisha hafatili ila sasa amefulia hata account ya bank hana.
Maisha yana siri nzito.!
 
Hivi kuna uhusiano gani Kati ya kukosa pesa na njaa?..
Maana ukiwa na pesa hata njaa husikii.

Ila uwe huna pesa sasa!!!
[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2]
Kweli kabisa mwanawane....ndio maana mie nashindwa kuelewa mtu tajiri anakuwa na litumbo likubwa🤣🤣🤣
 
Mimi story yangu Ni ndefu zaidi, hila nilikuwa na mtaji wa Kama milioni 120, utawala wa Magu mtaji wote ulikata na kesi juu,

Tulipewa economic case na money laundering, tulikaa keko na segerea miezi mitatu + ,

Yaani biashara za halali lakini zilituweka jela na makesi juu, tuliweka wakili akawa tapeli, tukajapata wakili mwingine alitupambania mwisho wa siku kesi iliisha na miguu juu wote mam'ae,

Sasaivi kidogo ramani zinaanza kusoma baada ya kuingia huyu mama
Ila magu jmn mbna alikuwa kiazi HV Ila nilikuwa namkubali ila kwa ishu zake hz hpn kwa kweli

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Bahati mbaya sana kuna ambao wakisha lost hua hawaji kurudi kwn gemu

Kuna bro wangu mmoja enzi za JK alikamata mradi fulani serikalini aisee jamaa nadhani ndani ya 2 years alichezea kati ya 400 -600m au zaidi. Piga sana pombe na starehe za kila aina.

Amekuja kutemwa hana hata ki starlet wala kiwanja achilia mbali asset nyingine. Mbaya zaidi ile kitu ni kama ilimu affect kisaikolojia ikawa hata akipata kazi nyingine anaona hela ni ndogo anaacha. Mpaka leo jamaa bila bila yupo anakunywa pombe za kienyeji mpira karudisha kwa kipa[emoji20]
Kafariki?
 
Namaliza chuo tu napta kazi. Inalipa mbaya nakodisha apartment. Nikifunga hesabu ya mwezi haina kwere nawatafuta washkaji tunasherehekea. Madem hawakauki kwangu full kujiachia ndani ya self contained. Luxury life. Sina saving. Siku nivofanyiwa auditing nakubaini madudu kazi ikaisha. Nilipagawa nikarudi kwa baba na mama. Nikapatwa na maradhi ya watu wazima mapresha wakati niko kijana mbichii. Washkaji walinitenga. Mpaka leo sijapata kazi ya mana nahangaika kwa wahindi kazi mlima mshahara kichuguu. Nawazaga Sana'a.
updates hali ikoje huko kwa baba na mama?
 
Ukifilisika ndo utajua Nani mchaw wako
Binafs sinaga moyo wa huruma.

Nafunga vioo kabisa. Inabaki salamu TU.

Kila nikiombwa Ela, jibu Ni "Sina hela"
Watajiongeza wenyewe kua jamaa hataki shobo
We' jamaa kwenye hili tunafanana tabia. Lazima ujue kuwa na uso mkavu na usiwe na huruma za kijinga. Hata Yesu hakuwa na huruma za kijinga. Kuoneana haya ndiyo kunafanya tunawakubali tena wale waliotutenga na kutuumiza. Hilo kwangu NO, sina aibu kwenye hilo.

Big Up Bruder!
 
Back
Top Bottom