Tuliowahi kupata pesa na kufilisika/kufulia, tujikumbushe hapa

Tuliowahi kupata pesa na kufilisika/kufulia, tujikumbushe hapa

Mwanzon mwa miaka ya 70s ndio niliingia mjini kutoka kijijini kabisa huko mkoani, Elimu niliyokuwa nayo ni ya darasa ya VII na sikuwa na mtaji au chochote cha maana kinibebe nilipofika town zaidi ya kuwa na misuli imara iliyotokana na jembe la bush na ujasiri niliotoka nao kijijin.
katika harakati za maisha nikapata mtu alienipa idea ya kujiunga na mfunzo ya ufundi na kweli nikaanza mafunzo. Baada ya kumaliza mafunzo nikaingia mtaani kufanya kazi za hapa na pale kwa kujiajiri na baadae nashukuru Mungu kupitia fani yangu ya ufundi milango ilifunguka na hadi kumiliki nyumba ya kwanza nikiwa na miaka sio zaidi ya 30(yaani kijana haswa huku nikiwa na usafiri wangu wa gari pendwa miaka ya 80s).

Niliendelea na shughuli zangu za ufundi kwa kipindi chote na ndio ulikuwa msingi wa kuendesha familia yangu kwa kusomesha watoto shule nzuri, kuhudumia mama(wife) na bata za mjini[emoji482]. Miaka ilisonga nikapata nyumba ya pili na kubadili magari hadi kufikia gari zaidi ya 4 zilizopita mkononi mwangu(kuzimiliki) . Ilipofika mwanzoni mwa miaka ya 2000 nikapata ushawishi wa kujiingiza kwenye shughuli za ukandarasi( contractor), ofcoz niliipenda hii na mwanzo hela niliiona, nikaingia mazima na balah likaja baada ya kupata kazi/tender ya sio chini ya 350Milioni, hapa ikumbukwe sikuwa na mtaji pia Serikali kama mjuavyo kidogo kunakuwaga na ucheleweshwaji wa malipo.

Hivyo sasa ikabidi niingie kwenye mikopo ya mtaani tena kwa hawa jamaa hata wasio kuwa authorized kufanya kazi za ukopeshaji, kiukweli lengo lilikuwa nikope nikimbize site(tender) kisha malipo yakitoka nirudishe deni, ila hawa mabwana ni kama waliniloga maana mikopo ilikuwa na riba kali tena za hovyo ikifika hatua malipo niliyotegemea hayatoshelezi tena kulipa madeni niliyo nayo, hapa nilipoteza nyumba, gari yote kufidia madeni hadi ikafika hatua na kampuni ikafa kabisa nikawa sina kazi yoyote huku nikiwa na madeni yanayozidi milion30 na hayana kichwa wala miguu, niliishi kwa kujicha kama digidigi mtaani, hapa niliona dharau za wazi wazi kwa wale nilidhani ni wema kwangu before. Nashukuru Mungu nilihama eneo husika na kuanza maisha eneo jingine na milango mipya ikafunguka na maisha yanasonga hadi sasa.
Somo nililopata ni usivamie biashara/tenda kubwa ikiwa bado hujajiimarisha mtaji wako kisa tu unaona bajeti ya tenda digits zinakuvutia, lakini pia hii isikufanye uache kuchangamkia fursa mpya kila mara zinapo jitokeza
 
Kweli kabisa yaani ukiwa unadate na mwanamke alafu ata siku moja hajakununulia kitu huyo ujue ni selffish promax.
Kuna mmoja ananipiga vibomu hapa namsikilizia tuu anavyo be jua mdomo oh mzabzab utanioa. Rohonni nasema wee nakulia timing tuu nikukule tigo nisepe zangu. Mwanamke hana huruma kabisa na hela zangu kha
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji1787][emoji1787] huyo demu anayedate na wewe ni chizi tu
 
Mwanzon mwa miaka ya 70s ndio niliingia mjini kutoka kijijini kabisa huko mkoani, Elimu niliyokuwa nayo ni ya darasa ya VII na sikuwa na mtaji au chochote cha maana kinibebe nilipofika town zaidi ya kuwa na misuli imara iliyotokana na jembe la bush na ujasiri niliotoka nao kijijin.
katika harakati za maisha nikapata mtu alienipa idea ya kujiunga na mfunzo ya ufundi na kweli nikaanza mafunzo. Baada ya kumaliza mafunzo nikaingia mtaani kufanya kazi za hapa na pale kwa kujiajiri na baadae nashukuru Mungu kupitia fani yangu ya ufundi milango ilifunguka na hadi kumiliki nyumba ya kwanza nikiwa na miaka sio zaidi ya 30(yaani kijana haswa huku nikiwa na usafiri wangu wa gari pendwa miaka ya 80s).

Niliendelea na shughuli zangu za ufundi kwa kipindi chote na ndio ulikuwa msingi wa kuendesha familia yangu kwa kusomesha watoto shule nzuri, kuhudumia mama(wife) na bata za mjini[emoji482]. Miaka ilisonga nikapata nyumba ya pili na kubadili magari hadi kufikia gari zaidi ya 4 zilizopita mkononi mwangu(kuzimiliki) . Ilipofika mwanzoni mwa miaka ya 2000 nikapata ushawishi wa kujiingiza kwenye shughuli za ukandarasi( contractor), ofcoz niliipenda hii na mwanzo hela niliiona, nikaingia mazima na balah likaja baada ya kupata kazi/tender ya sio chini ya 350Milioni, hapa ikumbukwe sikuwa na mtaji pia Serikali kama mjuavyo kidogo kunakuwaga na ucheleweshwaji wa malipo.

Hivyo sasa ikabidi niingie kwenye mikopo ya mtaani tena kwa hawa jamaa hata wasio kuwa authorized kufanya kazi za ukopeshaji, kiukweli lengo lilikuwa nikope nikimbize site(tender) kisha malipo yakitoka nirudishe deni, ila hawa mabwana ni kama waliniloga maana mikopo ilikuwa na riba kali tena za hovyo ikifika hatua malipo niliyotegemea hayatoshelezi tena kulipa madeni niliyo nayo, hapa nilipoteza nyumba, gari yote kufidia madeni hadi ikafika hatua na kampuni ikafa kabisa nikawa sina kazi yoyote huku nikiwa na madeni yanayozidi milion30 na hayana kichwa wala miguu, niliishi kwa kujicha kama digidigi mtaani, hapa niliona dharau za wazi wazi kwa wale nilidhani ni wema kwangu before. Nashukuru Mungu nilihama eneo husika na kuanza maisha eneo jingine na milango mipya ikafunguka na maisha yanasonga hadi sasa.
Somo nililopata ni usivamie biashara/tenda kubwa ikiwa bado hujajiimarisha mtaji wako kisa tu unaona bajeti ya tenda digits zinakuvutia, lakini pia hii isikufanye uache kuchangamkia fursa mpya kila mara zinapo jitokeza
Madeni vipi uli clear
 
Mwanzon mwa miaka ya 70s ndio niliingia mjini kutoka kijijini kabisa huko mkoani, Elimu niliyokuwa nayo ni ya darasa ya VII na sikuwa na mtaji au chochote cha maana kinibebe nilipofika town zaidi ya kuwa na misuli imara iliyotokana na jembe la bush na ujasiri niliotoka nao kijijin.
katika harakati za maisha nikapata mtu alienipa idea ya kujiunga na mfunzo ya ufundi na kweli nikaanza mafunzo. Baada ya kumaliza mafunzo nikaingia mtaani kufanya kazi za hapa na pale kwa kujiajiri na baadae nashukuru Mungu kupitia fani yangu ya ufundi milango ilifunguka na hadi kumiliki nyumba ya kwanza nikiwa na miaka sio zaidi ya 30(yaani kijana haswa huku nikiwa na usafiri wangu wa gari pendwa miaka ya 80s).

Niliendelea na shughuli zangu za ufundi kwa kipindi chote na ndio ulikuwa msingi wa kuendesha familia yangu kwa kusomesha watoto shule nzuri, kuhudumia mama(wife) na bata za mjini[emoji482]. Miaka ilisonga nikapata nyumba ya pili na kubadili magari hadi kufikia gari zaidi ya 4 zilizopita mkononi mwangu(kuzimiliki) . Ilipofika mwanzoni mwa miaka ya 2000 nikapata ushawishi wa kujiingiza kwenye shughuli za ukandarasi( contractor), ofcoz niliipenda hii na mwanzo hela niliiona, nikaingia mazima na balah likaja baada ya kupata kazi/tender ya sio chini ya 350Milioni, hapa ikumbukwe sikuwa na mtaji pia Serikali kama mjuavyo kidogo kunakuwaga na ucheleweshwaji wa malipo.

Hivyo sasa ikabidi niingie kwenye mikopo ya mtaani tena kwa hawa jamaa hata wasio kuwa authorized kufanya kazi za ukopeshaji, kiukweli lengo lilikuwa nikope nikimbize site(tender) kisha malipo yakitoka nirudishe deni, ila hawa mabwana ni kama waliniloga maana mikopo ilikuwa na riba kali tena za hovyo ikifika hatua malipo niliyotegemea hayatoshelezi tena kulipa madeni niliyo nayo, hapa nilipoteza nyumba, gari yote kufidia madeni hadi ikafika hatua na kampuni ikafa kabisa nikawa sina kazi yoyote huku nikiwa na madeni yanayozidi milion30 na hayana kichwa wala miguu, niliishi kwa kujicha kama digidigi mtaani, hapa niliona dharau za wazi wazi kwa wale nilidhani ni wema kwangu before. Nashukuru Mungu nilihama eneo husika na kuanza maisha eneo jingine na milango mipya ikafunguka na maisha yanasonga hadi sasa.
Somo nililopata ni usivamie biashara/tenda kubwa ikiwa bado hujajiimarisha mtaji wako kisa tu unaona bajeti ya tenda digits zinakuvutia, lakini pia hii isikufanye uache kuchangamkia fursa mpya kila mara zinapo jitokeza
Kwani ni utaratibu gani unatakiwa ili uweze pata tenda za barabara?

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Uzi mzuri sana huu. Vijana wote muusome mara kadhaa. Jambo la kwanza kabisa na muhimu kuliko yote ni NIDHAMU yako wewe binafsi ndani ya moyo wako. Unapopata pesa (ya halali), kwanza kabisa toa zaka au sadaka yoyote ya shukrani kwa Mungu. Ukifanya hivyo, unakuwa umeanza hatua ya kwanza ya kujijengea nidhamu ya nafsi yako.

Hatua ya pili:- Ziache hizo pesa benki kwa muda fulani (miezi kadhaa) UJIFANYE KAMA HUJAZIPATA. Hilo ni JAMBO GUMU (amini usiamini). Ni vigumu sana mtu kupata pesa nyingi kwa ghafla na kuacha kujionyesha. Ukishaweza kuwa na nidhamu ya kuendelea na maisha yako kama zamani wakati ulikuwa huna pesa, utakuwa umeshashinda kwa sehemu kubwa uwezo wa kuha kufilisika kirahisi.

Jambo la tatu ni kujaribu kwa nguvu zote KUZIMA MSUKUMO WA KUTAKA KUTAJIRIKA HARAKA. Nashauri ukipata pesa yoyote, usijaribu kuwekeza zaidi ya theluthi moja ya pesa hizo. Yaani ukipata milioni kumi na mbili, fikiria biashara unayoweza kufanya ambayo mtaji wake hauzidi milioni nne. Ng'ang'ana na hiyo biashara weee...Ukishaona inalipa, ndipo uongeze mtaji wake au uanze ya aina ingine ambayo nayo haizidi milioni nne. Kumbuka:- Kamwe USIANZE CHOCHOTE BILA KUKIFANYIA UPEMBUZI MKUBWA KABISA KWANZA. Unaweza ukalima na ukapata mazao mengi lakini kama huna soko la uhakika tayari umeanguka.

Unaweza kuanza biashara (k.m. duka au saluni n.k.) ambayo kwa kawaida inalipa vizuri lakini ukawa huna watendakazi wazuri au biashara haipo mahali penye wateja wengi wa biashara hiyo. Ni afadhali utafute fremu ya biashara yako uwe unalipa laki sita kwa mwezi mahali ambapo kuna wateja wengi kuliko kutafuta fremu ya laki tatu mahali ambapo wateja ni wa kubahatisha. Ni afadhali "umtoe"mfanyakazi bora uliyemwona mahali umlipe ghali ahudumie wateja wako vizuri kuliko utafute tu "wa kuokoteza" Ndio maana nimesema unatakiwa kufanya "upembuzi" wa kina kabla ya kuanza biashara. Lakini mwisho wa siku, jambo muhimu kuliko yote yanayomfanya mtu asifilisike ni NIDHAMU.

Watu wote duniani ambao waliwahi kupata pesa nyingi lakini zikaisha fasta walifilisiwa na TAMAA ZAO (yaani kukosa nidhamu). Kutaka fahari ndio kumefilisi wengi. Ukiwa baa unanunulia wote ili wakuone "unazo za kumwaga" Fahari ya kumchukua kila demu mzuri anayekatiza mbele yako, kuvaa mavazi ya ghali sana uonekane wewe ni bora zaidi n.k. Mimi binafsi nilishapata nyingi tu zikaisha- Nilikuwa nataka kutajirika haraka nikawekeza zote. Mtaji wote ukakata. Ni kama vile kuna "shetani fulani" anakufanya usishituke haraka- unakuja kutambua wakati zimebakia milioni mbili kwenye milioni hamsini ulizokuwa nazo.

Mimi nilipozinduka ndipo nikajiuliza ni wapi nilikosea. Nilipojua, nikajirekebisha. Sikukata tamaa nilianza tena kuanzia hatua ya kwanza lakini safari hii nikawa mjanja sikufanya tena kosa. Usisahau kamwe !!! Wanawake "wadangaji" wanajua "kunusa" ukiwa na pesa ni ajabu !! Waogope kama ebola !!

Aisee kumbe mm n mdogo sana hii misemo n ya zaman aisee wanawake huwa wananusa
 
Pesa ya mkopo au ya dill usifanyie biashara.We 4m zinakuumiza,mi nishawahikopa 20M zikapotea heri ningefungulia hata zipu,nimejaribu bnezz nyingi nimeambulia hasara kwa miaka 15 ni jumla ya 120M zimepotea sijakata tamaa napambana bado najua iko siku.Huwezi kuwa tajiri bila kufilisika hata uwe smart vipi

Duuh aisee
 
Uzi mzuri sana huu. Vijana wote muusome mara kadhaa. Jambo la kwanza kabisa na muhimu kuliko yote ni NIDHAMU yako wewe binafsi ndani ya moyo wako. Unapopata pesa (ya halali), kwanza kabisa toa zaka au sadaka yoyote ya shukrani kwa Mungu. Ukifanya hivyo, unakuwa umeanza hatua ya kwanza ya kujijengea nidhamu ya nafsi yako.

Hatua ya pili:- Ziache hizo pesa benki kwa muda fulani (miezi kadhaa) UJIFANYE KAMA HUJAZIPATA. Hilo ni JAMBO GUMU (amini usiamini). Ni vigumu sana mtu kupata pesa nyingi kwa ghafla na kuacha kujionyesha. Ukishaweza kuwa na nidhamu ya kuendelea na maisha yako kama zamani wakati ulikuwa huna pesa, utakuwa umeshashinda kwa sehemu kubwa uwezo wa kuha kufilisika kirahisi.

Jambo la tatu ni kujaribu kwa nguvu zote KUZIMA MSUKUMO WA KUTAKA KUTAJIRIKA HARAKA. Nashauri ukipata pesa yoyote, usijaribu kuwekeza zaidi ya theluthi moja ya pesa hizo. Yaani ukipata milioni kumi na mbili, fikiria biashara unayoweza kufanya ambayo mtaji wake hauzidi milioni nne. Ng'ang'ana na hiyo biashara weee...Ukishaona inalipa, ndipo uongeze mtaji wake au uanze ya aina ingine ambayo nayo haizidi milioni nne. Kumbuka:- Kamwe USIANZE CHOCHOTE BILA KUKIFANYIA UPEMBUZI MKUBWA KABISA KWANZA. Unaweza ukalima na ukapata mazao mengi lakini kama huna soko la uhakika tayari umeanguka.

Unaweza kuanza biashara (k.m. duka au saluni n.k.) ambayo kwa kawaida inalipa vizuri lakini ukawa huna watendakazi wazuri au biashara haipo mahali penye wateja wengi wa biashara hiyo. Ni afadhali utafute fremu ya biashara yako uwe unalipa laki sita kwa mwezi mahali ambapo kuna wateja wengi kuliko kutafuta fremu ya laki tatu mahali ambapo wateja ni wa kubahatisha. Ni afadhali "umtoe"mfanyakazi bora uliyemwona mahali umlipe ghali ahudumie wateja wako vizuri kuliko utafute tu "wa kuokoteza" Ndio maana nimesema unatakiwa kufanya "upembuzi" wa kina kabla ya kuanza biashara. Lakini mwisho wa siku, jambo muhimu kuliko yote yanayomfanya mtu asifilisike ni NIDHAMU.

Watu wote duniani ambao waliwahi kupata pesa nyingi lakini zikaisha fasta walifilisiwa na TAMAA ZAO (yaani kukosa nidhamu). Kutaka fahari ndio kumefilisi wengi. Ukiwa baa unanunulia wote ili wakuone "unazo za kumwaga" Fahari ya kumchukua kila demu mzuri anayekatiza mbele yako, kuvaa mavazi ya ghali sana uonekane wewe ni bora zaidi n.k. Mimi binafsi nilishapata nyingi tu zikaisha- Nilikuwa nataka kutajirika haraka nikawekeza zote. Mtaji wote ukakata. Ni kama vile kuna "shetani fulani" anakufanya usishituke haraka- unakuja kutambua wakati zimebakia milioni mbili kwenye milioni hamsini ulizokuwa nazo.

Mimi nilipozinduka ndipo nikajiuliza ni wapi nilikosea. Nilipojua, nikajirekebisha. Sikukata tamaa nilianza tena kuanzia hatua ya kwanza lakini safari hii nikawa mjanja sikufanya tena kosa. Usisahau kamwe !!! Wanawake "wadangaji" wanajua "kunusa" ukiwa na pesa ni ajabu !! Waogope kama ebola !!
[emoji123]
 
Idris Sultan alipata Tsh 500m ambazo ni zaidi ya U$D 200,000. Zilienda wapi? Na kama mtu anaweza kuchezea USD 200,000 watu wanashangaa nini mtu kuchezea USD 1m? Umesema vizuri kabisa starehe hazina mwisho. Ukiwa na USD 1m, demu akikuambia umlipe 50m utaona mbona hela ndogo sana hiyo..?

Mzee watu ambao hawajawah shika pesa wanaona kama watu kukamata pesa nyingi kama izi haiwezekan
 
Kwenye huu uzi ukisoma matukio mengi mengine ni ya kutunga ambao awajakamata hta milioni 1, wengne ni kweli wamezikamata na kuishia kuteseka, yote kwa yote ni bora uanzie msoto alafu Mungu akupe utakua umepata Elimu flani ya maisha, nilianzia mtaji wa laki5 mwaka2006 nilikua nachukua2 marudio ya mkonge (from Tow ) nadunduliza Kwenye viwanda vya magunia, leo hii Historia ni nyingine kbsa inahitaji vitabu na vitabu kuandika NAMSHUKURU MUNGU

Inaonesha hujawah shika pesa mzee ndo maana huwez waamin hawa ila ndo ukweli mambo watu wanashika
Hela
 
Mimi wakati tunakaribia kufunga ndoa tu na mume wangu akafukuzwa kazi ,kazi iliyokuwa ikimlipa vizuri sanaaaa weee nikakaa nikajiuliza niendelee na hii ndoa au lah maana nilikuwa nawaza mimi nafanya kazi kwa wahindi mshahara wangu hauwezi kulipa kodi ya nyumba na sisi tukala nikamuomba Mungu nikasonga mbele na ndoa aisee si mchezo yani ukipokea mshahara ushaisha unaanza upya yani kila ikifika mwisho wa mwezi ndo machungu yanaanza.
Nikapata mimba hapo mume haingizi hata senti tano ila akawa tu ni mtu mzuri hana makwazo kwahiyo tukawa tunaongea lugha moja.Wakati kwa kujifungua ukafika ile nimemaliza mwezi mimi ni HR boss wangu kanipigia simu tukaongee kwenda ananiambia inabidi tufunge ofisi hataweza kuendelea kulipa wafanyakazi hivyo ni bora alipe watu akiwa bado ana pesa aiseee tulikuwa sehemu nilikuwa sielewi nini naongea mana nilikuwa nawaza mtoto nyumbani mwenzangu bado hajapata kazi [emoji1544] nilijikaza nikamjibu boss wangu sawa mana mimi ndo natakiwa kwenda kubreak the news.

Turudi nyuma kidogo mwenzangu kuna pesa aliipataga zamani basi akanisaidia kiasi kikubwa kuanzisha biashara yangu (na hii ndo sababu niendelee mbele na ndoa mana nilishajua ni mtu wa namna gani). So wakati haya yote yakiendelea tuliyokuwa tukiiendesha kwa hasara lakini sababu nilikuwa na kazi nikawa naendesha hvyo hivyo najipiga tafu kupitia kazi yangu ya kuajiriwa basi nilivyoona familia imeongezeka nikaona sitaweza kuihudumia biashara nikataka kuifunga kumbe Mungu ananichelewesha kuifunga kwani anajua nitakosa kazi,kazi ilivyoisha bahati nzuri nilikuwa nimepata maternity yangu karibuni nikachukua kiasi nikatemgeneza ofisi kidogo na tulipofunga ofisi sababu nilikuwa maternity nilipata mishahara kama mitano hvyo plus kiiunua mgongo basi tukakaa na mwenzangu tukaenda buguruni tukanunua kila kitu cha ndani at least kitakachotupeleka kwa miezi mitatu tukiwa tunajitafuta.

Mungu ni mwema hatuna maisha kama ya zamani lakini nimewekeza akili na kila kitu kwenye ile biashara yangu na sababu nipo mwenyewe naifanya mwenyewe na pesa sasa inaendesha maisha + na mume wangu anafanya kazi zake hakosi pesa za chakula.

Tusikate tamaa na kumuomba Mungu mana kila anapokupa jaribu anakupa na mlango wa kutokea mlango ni akili zinazokuongoza kutafuta namna ya kuzitatua na tujitume na kutokata tamaa.
Na zaidi kwenye maisha kukosa ni kawaida kama sio leo ni kesho.

Real meaning ya mwanamke
 
Back
Top Bottom