Tajiri Kichwa
JF-Expert Member
- Apr 2, 2017
- 9,021
- 22,016
nataka kuchukua mkopo wa 20m ninunue gari ...nitaweka hati ya nyumba kama dhamana....hii blanda ndio plan yangu
Fanya hivyo ili uje kua shuhuda juu ya namna gani mikopo ni kichefu chefu
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
nataka kuchukua mkopo wa 20m ninunue gari ...nitaweka hati ya nyumba kama dhamana....hii blanda ndio plan yangu
Niwe baloziFanya hivyo ili uje kua shuhuda juu ya namna gani mikopo ni kichefu chefu
Kwa hiyo unataka kugaiwa pesa za baba ako?Mkuu mimi Mzazi wangu kakopa pesa Banki lakini kwa marejesho ya banki kukata kwenye pensheni yake sasa pensheni yake Azina hawaja muingizia benki miezi 4 imefika sasa Afisa mikopo wa Banki ana tusumbua sisi watoto tumpeleke mzee wetu Azina akahakikiwe, Mimi nimekataa simpeleke kwasababu pesa alivyokopa haja tugaiya kaitumia peke yake, sasa hatujui afisa mikopo wa benki atazipataje pesa zaidi ya Milioni 10
Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
Mkopo sio zawadi hakikaaWanasema mkopo sio zawadi, nimejitoa kwenye mfumo wa kukopa kabisa, nakumbuka nilikuwa na project ndogo ya serikali, nikakopa nikijua payment ingefanya ndani ya wakati ningelipa.. Ohoooo.. ilipigwa delay ya maana sana, nikajikuta nauza gari mbili kwa mpigo na sikuwa nimekaa nazo hata zaidi ya miezi mitatu.. Kuanzia hapo naogopa mikopo kama ukoma na ninashukuru nimetoka kwenye mikopo yenyewe labda mbeleni huko
Huuu upoje mkuuuKuna mkopo unaitwa c.h.u.p.i mkononi.... wake za watu wanatafunwa sana
Na wala sio posa wala hela ya kuolea au kula bata.. Na sio boom😅😅😅Mkopo sio zawadi hakikaa
Hatari kwenye langoNa wala sio posa wala hela ya kuolea au kula bata.. Na sio boom😅😅😅
Ilikuwa mwaka 2011 mwezi wa 7 mara yangu ya kwanza kuchukua mkopo benki, Tsh 3m. Ule mkopo niliufanyia biashara vizuri na nikarejesha bila changamoto kubwa ndani ya miezi 6. Wale maafisa mikopo wakafurahia na kunishauri nichukue mwingine wa Tsh 5m. Nikafikiria na baada ya mwezi nikachukua mkopo mwingine. Ikawa kama bahati wakati nachukua mkopo nikawa nimepata tenda ya kushona uniform za shule flani. Nikaona hili ni dili zuri na kwa bahati wateja wangu wakanilipa pesa za advance zaidi ya 90%. Kilichofuata nikaamua nitafute mafundi wazuri Nairobi wanishonee uniform zote. HAPA NDO BALAA LILIPOANZA. Niliingia choo cha kike. Mkenya niliyempa kazi kumbe ni mshenzi mno... kadhulumu watu wengi sana. Ni kweli ofisi anayo na mafundi anao ila kwa bahati mbaya huwa hatimizi makubaliano. Ujinga mwingine niliofanya ni kumlipa karibu hela zake zote.
Hadi shule zinafunguliwa Januari sikuwa nimepeleka nguo yoyote kwa mteja. Basi presha ikaanza kutoka kwa mteja wangu ambaye pia alikuwa anawashiwa moto na wanafunzi + wazazi. Baada ya kusumbuana na mzabuni wangu nikaona isiwe ishu nichukue hela za kwenye biashara yangu niliyoombea mkopo wa 5m ili kupambana na tatizo ambalo lilikuwa limefikia pabaya. Kwa maana nitafute fundi mwingine nitengenezee kwake huku nikiendelea kupambana na huyu wa mwanzo. Changamoto iliyojitokeza tena ikawa kwa muda ule wauza uniform wengine wana kazi zingine nyingi na bei zao zimeshaenda juu. Gharama za nauli nenda rudi Ars - Nrb nazo zikawa zinanipiga kama ngoma.
Hadi kuja kufanikiwa kupeleka nguo angalau kwa 70% tayari kiuchumi nilishayumba hivyo marejesho yakawa yanasuasua. Ninachokumbuka ule mkopo niliotakiwa niwe nimemaliza kulipa kabla hata ya August nilimaliza December kwa mafaini kibao huku nikiwa nimefilisika. Wale maafisa mikopo walijua kuniwashia moto.
Pamoja na yote hayo nilijipanga upya na baada ya miaka kama mitatu nilirudi tena benki na kuchukua mkopo. Ninamshukuru Mungu kwamba ninakopesheka na ninaendelea kuchukua mkopo. Somo kubwa ni kwamba usichukue mkopo kuanzisha biashara.
Una uhakika kuwa hatarudisha lkn unakubali akope.Dadangu anafosi nimwandikie barua ya mkopo,
Anakopea kiwanja cha urithi,hii ni mali yetu mimi na yeye....hii pesa nina wasiwasi hatarudisha.
Naandika kesho kuepuka lawama ila najua ili deni nitalipa mimi dadeki.
Riba yao ikoje??Kifupi nikopa NMB 10ml nialipa marjesho kama 6 biashara ikaanza kuyumba.aisee nilihangaika huku na huko nyumba isiuzwe bila mafanikio.mwisho niliongea na marafiki zangu wanimlizie deni then mambo yakiwa mazuri niwarejeshee wao badala ya benk,hivyo nilipigwa tough kama 4ml nikaokoa nyumba yangu..sasa deni limehamia kwa washkaji ndo mziki upo hapo.Mungu nisaidie
Hilo Jina tu linatishaKweli hiyo kausha damu yani hakuna nafasi ya kujipanga ata wiki
Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
Hahahaa kuna dada nilijiroga nikamchukulia mkopo ASA, ndio mara yangu ya kwanza rejesho moja tuu akasafiri hajarudi mpaka leo na simu inapatikana ila huwa hapokei namba yoyote.Fanya yote ila usikope ASA
Mwanangu DeepPond hata mimi kuanzia September sielewi kabisa. Rejesho langu 3m napata kichaaPole Sana mkuu,
Imenikumbusha mwezi ulopita
Tangu September mzunguko hausomeki kabisa
ASA ni nini?Hahahaa kuna dada nilijiroga nikamchukulia mkopo ASA, ndio mara yangu ya kwanza rejesho moja tuu akasafiri hajarudi mpaka leo na simu inapatikana ila huwa hapokei namba yoyote.
Nilimchukulia 600,000 mwezi wa 5 juzi kati mwezi wa 10 ndio nimemaliza kulipa sina hamu,rejesho ni 28000 kwa wiki ila ukikumbuka unamlipia mtu roho inachafuka. Afisa mikopo ananiuliza lini unachukua tena mkopo huwa namjibu nitakuja tuu hajui maumivu niliyonayo mpaka akiba niliwaachia.
Sent using Jamii Forums mobile app
Vip unataka uache kaz ukimbie na mkopo? [emoji3]Hivi watumishi wa serikali wakikopa wakiacha kazi kabla mkopo kuisha huwa wanatafutwa?
Na kama hawatafutwi na hulipa hela zao?
Na kama wanatafutwa je huwa wanauza mali zao kufidia madeni?
Hapana nimewaza tu bado sijaajiriwa mimiVip unataka uache kaz ukimbie na mkopo? [emoji3]