trudie
JF-Expert Member
- Jan 15, 2014
- 3,668
- 8,745
Ni kampuni, inakopesha kina mama tuu, wanakopesha kuanzia 600,000 na kuendelea ipo kila mtaa.ASA ni nini?
Sent using Jamii Forums mobile app
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ni kampuni, inakopesha kina mama tuu, wanakopesha kuanzia 600,000 na kuendelea ipo kila mtaa.ASA ni nini?
ya mikopo ya Mhindi, anakopesha kuna mama tu, wanalipa kila alhamisASA ni nini?
Afadhali umejua mapema hivo umejipanga ili hata huko mbeleni wala hutonung'unika kwakuwa ulishaona mbele.Dadangu anafosi nimwandikie barua ya mkopo,
Anakopea kiwanja cha urithi,hii ni mali yetu mimi na yeye....hii pesa nina wasiwasi hatarudisha.
Naandika kesho kuepuka lawama ila najua ili deni nitalipa mimi dadeki.
Rejesho 5.8m kwa mwezi nadhani mi mngenizika kabisa.Mimi mkopo ulichonifanya sitokaa nikope milele mpk naingia kaburin
Nitaridhika na ninachopata
Bora sahiz nasave hela naiona aisee
Mkopo ulikuwa unifirisi kabisa
Ila afsa mkopo ni mbwa hawana huruma
Rejesho mil 5.8 kwa mwez halaf sikuwa mzoefu wa mikopo hata kunishaur nisogeze mbele mkopo ilo marejesho yapungue wakashindwa wakaniacha nakufa na tai shingon mbwa wale sitowasahau kamwe
Ukakopa kabisaa ufanye harusi.Nina mkopo wa 1M point...
Leo natakiwa nianze rejesho ila pesa yote imeishia kwenye harus
Nawazaaaaa
Miujuza itendeke tuu
Afadhali kikoba ndugu na ndio mana ulikopa kwa ujasiriMajukumu yaliingiliana ndugu uzalishaji haukufanyika muda muafaka.
Kwanza ni kikoba so wakiona vipi watakata hisa zangu. Maana nlikopa hisa.
Japo napigana niulipe
YeahAfadhali kikoba ndugu na ndio mana ulikopa kwa ujasiri
Soma ufafanuzi next post baada ya hyoUkakopa kabisaa ufanye harusi.
Kweli kuna watu mna moyo mie nifunge tu hiyo ya mkeka niishi kwa amani kuliko kufurahisha watu ndoa yenyewe nije iona chungu.
Funzo lingine usichukue mkopo kusolve ishu zako binafsi[emoji1787][emoji1787] hi nitakuja kuleta ushuhudaIlikuwa mwaka 2011 mwezi wa 7 mara yangu ya kwanza kuchukua mkopo benki, Tsh 3m. Ule mkopo niliufanyia biashara vizuri na nikarejesha bila changamoto kubwa ndani ya miezi 6. Wale maafisa mikopo wakafurahia na kunishauri nichukue mwingine wa Tsh 5m. Nikafikiria na baada ya mwezi nikachukua mkopo mwingine. Ikawa kama bahati wakati nachukua mkopo nikawa nimepata tenda ya kushona uniform za shule flani. Nikaona hili ni dili zuri na kwa bahati wateja wangu wakanilipa pesa za advance zaidi ya 90%. Kilichofuata nikaamua nitafute mafundi wazuri Nairobi wanishonee uniform zote. HAPA NDO BALAA LILIPOANZA. Niliingia choo cha kike. Mkenya niliyempa kazi kumbe ni mshenzi mno... kadhulumu watu wengi sana. Ni kweli ofisi anayo na mafundi anao ila kwa bahati mbaya huwa hatimizi makubaliano. Ujinga mwingine niliofanya ni kumlipa karibu hela zake zote.
Hadi shule zinafunguliwa Januari sikuwa nimepeleka nguo yoyote kwa mteja. Basi presha ikaanza kutoka kwa mteja wangu ambaye pia alikuwa anawashiwa moto na wanafunzi + wazazi. Baada ya kusumbuana na mzabuni wangu nikaona isiwe ishu nichukue hela za kwenye biashara yangu niliyoombea mkopo wa 5m ili kupambana na tatizo ambalo lilikuwa limefikia pabaya. Kwa maana nitafute fundi mwingine nitengenezee kwake huku nikiendelea kupambana na huyu wa mwanzo. Changamoto iliyojitokeza tena ikawa kwa muda ule wauza uniform wengine wana kazi zingine nyingi na bei zao zimeshaenda juu. Gharama za nauli nenda rudi Ars - Nrb nazo zikawa zinanipiga kama ngoma.
Hadi kuja kufanikiwa kupeleka nguo angalau kwa 70% tayari kiuchumi nilishayumba hivyo marejesho yakawa yanasuasua. Ninachokumbuka ule mkopo niliotakiwa niwe nimemaliza kulipa kabla hata ya August nilimaliza December kwa mafaini kibao huku nikiwa nimefilisika. Wale maafisa mikopo walijua kuniwashia moto.
Pamoja na yote hayo nilijipanga upya na baada ya miaka kama mitatu nilirudi tena benki na kuchukua mkopo. Ninamshukuru Mungu kwamba ninakopesheka na ninaendelea kuchukua mkopo. Somo kubwa ni kwamba usichukue mkopo kuanzisha biashara.
Inachekesha[emoji1787][emoji1787][emoji1787]Aisee hii mikopo iko nzuri na mibaya, nilishawai kuchukuwa M10 za mkopo hapo sikujua namna ya kurejesha maana ilikuwa haraka haraka siku yule jamaa ananipa utaratibu wa kurejesha niliishiwa nguvu, maana nilitakiwa nilipe jumla ya M16 kwa miezi sita, cha kustaajabu hela yote niliijengea, nyumba nikaiuza nikageuka mpangaji kwenye hiyo nyumba, alienunua hiyo nyumba nae akanipa notisi niachie nyumba yake.
Hatareee tupu. [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Kua uyaone[emoji23][emoji23][emoji23]
Niliuza laptop kwa mazingira haya haya[emoji3][emoji3][emoji3] kipindi nipo chuoKuna kikampuni hapo dodoma kinakopesha kwa dhamana ya kiwanja, chombo cha moto, ama nyumba, muhimu uwe mmiriki halali, watafute hao, uwapige hela, ukishindwa kurudisha wanachukua chako kinakuwa chao, unakuwa kama umeuza mali na kupata pesa...THE DEAL DONE, hivyo ndivyo maharamia tulifanya biashara bila kuhangaika na wateja[emoji16][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Inachekesh pia[emoji1787][emoji1787][emoji1787]Pole sana mzee ulijipiga bomu mwenyewe.....Just imagine umenunua kiwanja umeanza ujenzi,nyumba yako inakamilika halafu ghafla unageuka mpangaji kwenye nyumba uliyoisotea kuijenga halafu mwisho wa siku unatimuliwa kwenye nyumba yako.
Daah inachoma kama pasi hii mzee [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Kukopa mtu inatakiwa ukope materials siyo pesa!Hivi unakopa kabisa pesa ili ukajenge?!
😀😀hawa nao ni balaa na hela yao hailali! Wife alikopaga huko ilifika kipindi kila alhamisi siku ya marejesho ni msala,yaani ilikuwa lazima nimuongezee kidogoFanya yote ila usikope ASA
Imarika, jengo la haloteli, opposite na nyerere square barabara ya kutokea NMB kwenda ilipokuwa maisha Club.Mkuu UGM BIN CHAMPION ni Kampuni gani hiyo ya DODOMA na Ofisi zao zipo wapi??naomba direction au contact zao
Me haya mambo namdhamini mama yangu tu...... Nje ya hapo asante kwa kushirikiHili nalo balaa linginee.
Nilimdhamini mfanyakazi mwenzangu kuchukua mkopo kidogo tuu,Mara jamaa akashindwa kurejesha kwa mwezi km ilivyotakiwa
Gafla nikaambiwa inabidi nianze kumlipia ,yaani nikalipa marejesho mwezi mmoja,ikabidi nifanye maarifa boss amkate juu kwa juu Deni likalipwa Ila Mimi nikiwa mhanga,acha tuuu.
Sitakuwa mwepesi kumdhamini mtu tena