Tulishawaonyeni sana hapa JamiiForums kuwa hawa 'QNET' ni 'Matapeli' hamkusikia sasa ngojeni 'Wawanyoosheni' ili mkome

Hebu naomba nisimulieni vizuri wanafanya nini siku hizi hao QNet?

Maana nilishawahi kuwaonya watu toka miaka kumi na tano iliyopita enzi hizo QNet wanauza viglass fulani wanaita biodisc.

Naomba mkanda kamili wa hizo ajira za QNet ndo zikoje?
 
Acha kutetea utapeli. Network marketing ni utapeli hata huko kwenye nchi tajiri. Sema tajiri akitapeliwa maisha yanaendelea. Lakini kuna tahadhari kibao kuhusu MLM na study kibao jinsi gani ni utapeli.

Kikubwa ni kuna kitu wanaita uwazi na ukweli. Marekani watu walilalamika sana ikabidi Fair Competition Commission yao iwalazimishe makampuni ya MLM kuweka wazi taarifa za mapato ya mbuzi wao.

Ikagundulika kwamba mbuzi wanaokula ni 1% tu. 99% wanaliwa.
 
Serikali kwa nini huwa inachelewa sana kuchukua hatua?Yule MR KUKU nae kawapiga hela wananchi kashtakiwa kalipa fine katoka saivi kaanza tena halafu serikali inamuangalia tu
Pesa tamu, huenda wamemwambia kapige tena ulete.
 
Laana itawatafuna tuu...cjui hii dhambi mtaitubu wapi?? Mnatuma watoto wa watu wakauze saa Mil 3?!! Tena mtaani!!..wakija shtuka wamepigwa wanachanganyikiwa mpaka barabara ya vumbi wanavushwa na watoto wa chekechea..!!!![emoji41][emoji41][emoji41]
Hahaha [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Duh, kumbe hata weupe wanatambarizwa [emoji23][emoji23]
 
niliwahi kukalishwa masaa zaidi ya manne na hawa jamaa pale ilala walipoona sijaelewa somo wakanileta ofisi yao nyingine pale nyuma ya bamaga, nikalishwa maneno nikayatapika yote. Lakini nilikuta walimu kibao wanadanganyana eti unanunua mkufu kwa usd 1900 au water filter, niliwadharau sana.

imagine mtu anakushauri eti ununue holiday package ya kwenda Tahiti, Vanuatu, Fiji, Tuvalu na kwingineko ktk bahari ya pacific ilhali hata uwezo wa kwenda ngorongoro au mikumi huna!!
 
Mbn hi hbr Ni wiki mbili imeshatoka sas. iliripotiwa na itv na jackline dilemwa ktk kipindi chake kile Cha usku hata mkuu waa wilay bwna kher James alikuepo ilikuwa Ni kichekesho Sana. Walivyokuwa wnaojiwa wale vijana
 
Hawa matapeli wanafanya utapeli kwa mujibu wa sheria, yaani wanafuta sheria, taratibu na na kanuni zote, hivyo hata kuwafungia haiwezekani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…