Kilio, kilio, ni kilio cha kudai Tume Huru ya Uchaguzi Mkuu, kutoka kwa karibu viongozi wote wa vyama vya upinzani. Maswali kadhaa yanajitokeza:
1) Je, kuna haja ya kuwepo kwa hiyo tume?
2) Je, Tume ya Uchaguzi iliyopo ina mapungufu gani?
3) Hiyo Tume Huru inapaswa kuwa na vigezo gani?
Pamoja na kupata tafsiri sahihi ya Tume Huru ya uchaguzi, ikiwa ni pamoja na vigezo vyake, Serikali itumie busara kuundwa kwa Tume ya Uchaguzi. Kutekeleza hilo kutaziba mianya ya wanasiasa kuweka kwapani mpira wa uchaguzi, siku ya siku.