Serikali yetu si secular, rais haishi kumtaja Mungu kwenye mambo ya serikali. Mpaka bunge linafunguliwa kwa dua...labda hii hatua ya kuweka msisitizo kwamba serikali yetu ni secular.
Serikali yetu si secular, rais haishi kumtaja Mungu kwenye mambo ya serikali. Mpaka bunge linafunguliwa kwa dua.
Hawajakataza hili kwa sababu wanataka kuwa secular.
Hawataki viongozi wa dini wapate cha kusema ikiwa kuna figisu kwenye kuiba kura huko.
Hashimu "Dogo Mwanaharamu" aliimba "hivi vitu viko wazi kama vazi la kahaba..." katika "In the Shadow of a Dark Destiny"...asante sana kwa kuliona hili.
..umelisema kwa usahihi, na ufasaha, kuliko ambavyo ningelisema mimi.
Huku wanasmbiwa Wauombee Uchaguzi kule Hawaruhusiwi kuwa Waangalizi nini Kinaogopwa?Jamani habari ya mjini ndiyo hiyo.
Tangu uchaguzi wa 1995 viongozi wa Dini wamekuwa waangalizi wa uchaguzi mkuu.
Lakini uchaguzi wa mwaka huu Tume imeamua viongozi wa Dini wasishirikishwe.
Nilitegemea kwamba ili malalamiko yasiwepo basi waangalizi walipaswa kuwa wengi.
Waswahili tena msemo wetu, "Penye wengi hapaharibiki neno. "
Na kama sisi ni taifa linalomtegemea MUNGU kwanini tunawatenga viongozi wa DINI ktk jambo kubwa na muhimu kama uchaguzi mkuu?