Tume ya Katiba Iondoke Sasa Isiongezewe Muda ni Kupoteza Kodi za Wananchi Bure!!

Tume ya Katiba Iondoke Sasa Isiongezewe Muda ni Kupoteza Kodi za Wananchi Bure!!

Joined
Apr 27, 2006
Posts
26,584
Reaction score
10,400
warioba_1_bc902.jpg

Tume ya Mabadiliko ya Katiba imeomba kuongezewa muda wa mwezi mmoja kutokana na ugumu wa kazi ya uchambuzi wa maoni yaliyotolewa na wananchi na asasi mbalimbali.
Tume hiyo inayoongozwa na Jaji Joseph Warioba ilitakiwa kufanya kazi kwa miezi 18 kwa mujibu wa Sura ya 83 ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba.
Maana yake ni kuwa Tume hiyo iliyoanza kazi Mei 1, mwaka jana ilitakiwa kukamilisha kazi yake Novemba 1, mwaka huu.
Ikiwa maombi hayo ya Tume yatakubaliwa ina maana watatakiwa kukabidhi ripoti yake Desemba 1, mwaka huu.

- Big nah! hawa tume ya Katiba wamegeuka kuwa opposition Institution ndani ya Serikali, wasiongezewe muda ni muhimu sana wakaondolewa hata leo kwa sababu tayari walishaamua mapema sana matokeo kabla hata ya kukusanya maoni kama walivyotakiwa na Sheria iliyowaunda. Nimeshuhudia kwa macho na masikio yangu nikiwa Moshi kwenye mkutano wa Tume hii na wananchi, Mjumbe wa Tume hii Butiku akiwakaripia wananchi kwamba Serikali tatu haina mjadala tena imeshapita, wananchi walipomjia juu akasema kwamba hana muda wa kusikiliza tena maana hiyo hoja tayari imeshapita, hivi hii tume ni kweli iliundwa kulazimisha wananchi hoja au maoni yao?

- Tume imejitwika madaraka makubwa mno ya kutengeneza maoni ya wananchi badala ya kusikiliza maoni ya wananchi, kama tume ina tatizo na maoni ya wananchi kuwa sio yao basi ingeandika kwenye majumuisho kwamba ina wasi wasi maoni mengi ya wananchi hayakuwa yao yalikuwa ni ya vyama vya siasa kwa sababu vyama vyote vya siasa nchini vinahusika na kuwapiga msasa wananchama wake kuhusu interest za vyama vyao kwenye katiba mpya wala sio siri. I mean kwa wajumbe wa Tume kuwakaripia wananchi wakitoa maoni yao kama nilivyoona Moshi na Singida, ni very clear kwamba Tume ilishapoteza uhalali wake kisheria siku nyingi sana.

- sijawahi kuona Tume ya kukusanya maoni tu, ipo kwenye media kila siku wajumbe wa tume wanaongea na media almost kila wakati WHY? Kazi yao ni kukusanya maoni tu sasa kwenye media wanatafuta nini? Wajumbe wa Tume wameingia mpaka kwenye malumbano na wanasiasa WHY? Kazi yao si ilikuwa kukusanya maoni tu ya wananchi, mbone tume zingine zilizopita hatukuwasikia kwenye media mpaka walipofikia kutoa ripoti tu, hii tume ya Katiba imepata wapi haya mamlaka mazito ya mpaka kukemea wananchi kuhusu maoni yao binafsi kwenye mikutano yake?

- The more wanavyozidi kuwepo ni more wanavyozidi kutuchanganya na kutugawa wananchi kwa sababu wanapenda sana media, nilijua muda hautawatosha maana kila wakati wapo kwenye malumbano na wanasiasa kwenye media sasa muda wa kuchambua maoni watautoa wapi? Nasema hivi Ikulu isiwape muda zaidi maana hii tume ni useless na ni waste, I mean katika kutembelea Dunia nzima as I have done except nchi 10 tu sijawahi kusikia tume inayokusanya maoni ya wananchi inalumbana na na walioituma kabla ya kuwasilisha ripoti yake, kwa kawaida huwa kunakuwa na malumbano baada ya kuwasilisha sio in the process ya kukusanya maoni, ndio ninasema hii ni tume iondolewe now inapotesa muda bure na mapesa ya wananchi, haifai kwa sababu ina wajumbe waliokwisha amua mapema sana maamuzi yao yawe ya wananchi na huku wakijua wazi kwamba ni against the law!

- HII TUME WANATUVURUGA VICHWA BURE WANANCHI IONDOLEWE NOW NA ISIONGEZEWE MUDA KABISA KWA SABABU TAYARI MWANANCHI KAMA MIMI NAJUA MATOKEO YA UCHAMBUZI WAO UTAKUWA NI NINI KUTOKANA NA MANENO YAO MENGI SANA KWENYE MEDIA NA MIKUTANO YAO, SO WAPO COMPROMISE HAWAFAI! NA NASHAURI IN THE FUTURE TUME KAMA HIZI WAPIGWE MARUFUKU KUONGEA NA MEDIA AU KUWEKA MAONI YAO KWA WANANCHI!!

- KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI!!


Le Big Shoow - The King Of All Bongo Network Social Media@ Blogu ya Wananchi.
 
Wewe una bifu na ukoo wa Warioba nadhani huu mtifuano una mizizi ya uhasama unaoanzia kwa Baba yako.
 
RIP My dearest Mwl J.K Nyerere!
Ulimkomesha Mtaka urais J4 Malechela...Ona na hili dude lake kubwa jinga?:crying::A S 39:

- U know what I love me kwa sababu all my topics huwa hamuwezi kujibu hoja kwa hoja, maana mnajua ukijaribu nitawachana zaidi so huwa mnaleta hizi za ujinga ujinga kujaribu kubadilisha topic, ok boss fungua thread ya Mwalimu na Malecela hii inahusu Tume ya katiba, ha! ha! ha!

Le Mutuz
 
Mimi nadhani unapigana na giza!.

Utamaliza risasi zako za kisiasa bure wakati adui siyo Tume ya Jaji Warioba bali yule aliyeiweka hiyo tume ambaye unfortunate, ni Mwenyekiti wako wa chama Taifa. You better start shooting him down (Rais Kikwete) kwa sababu anawachanganya kimawazo na kimtazamo watu kama wewe ambazo siasa zenu niza mlengo wa confrontation politics!.

Kama huwezi kum-shoot down Mwenyekiti wako wa taifa basi spare the bullets ili uzitumie wakati wa kura za maoni ya katiba. Wahamasishe wanachama wako waikatae rasimu ya katiba mpya kwenye kura za maoni badala ya kupiga kelele barabarani bila targeted audience.

You are missing a political opportunity wakati time is money!.
 
Upo mstari wa mbele sana kutaka Tanzania isipate Katiba bora na inawezekana kabisa lengo lako ili muendeleze biashara yenu na huyo jamaa yako kwani tutakuwa na sheria legelege na dhaifu na kufanya kesi kama za akina Masogange kuishia hewani (Mtu anakamatwa na Mzigo wa Billion 6 analipa faini Million 4)
 

Attachments

  • Le mutuz.jpg
    Le mutuz.jpg
    28 KB · Views: 406
Ukweli ni kwamba wewe na wenzako ndani ya ccm kuikubali ama kutoikubali Tume ya Katiba hakumsaidii mtu yeyote anayeujua ukweli wa dhiki, shida na kero zinazotokana na mapungufu yaliyomo kwenye katiba tuliyo nayo sasa. Wananchi wamechoka kuona wanaendelea kuishi maisha yaliyojaa ufukara na yasiyo na mwelelekeo wala dira wakati watu wachache wanafaidika. Kero za wananchi sasa hivi ni kama jua la asubuhi, kila kukicha linachomoza. Kuanzia Lindi na Mtwara, kwenda Kigoma, Arusha na Manyara, Zanzibar ndiyo basi tena, juzi juzi tumesikia mpaka Dodoma wananchi wameandamana dhidi ya fisadi CDA. Kila wanapopita viongozi wa nchi (watawala) wanakutana na mabango na hata wananchi wakizuiwa kuonyesha mabango basi wanakutana na wananchi wanaowaeleza kuhusu shida zao! Kuanzia migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji, wananchi kunyang'anywa ardhi na wawekezaji, kukosa huduma muhimu kama afya, elimu, barabara, maji, umeme n.k. Suala la haki za binadamu zinavunjwa mchana kweupe na wanaozivunja wanalindwa mfano mzuri ni kauli ya Waziri Mkuu kusema 'wapigwe'. Suala la Muungano ambalo limeanza kuzungumziwa miaka mingi sana na walio madarakani wakajifanya wametia pamba masikioni hawasikii la mtu. Haya yote ni mapungufu yaliyomo kwenye katiba hii ya sasa!

Tufanyeje? Lazima tupate katiba mpya ambayo itakuwa dira ya kutuonyesha njia ya kutufikisha huko tuendako. Tuache kuongozana kama vipofu bali tunahitaji msaidizi angalau atakayekuwa macho yetu kwenye safari hii. Ndipo Tume hii iliposimamia. Kwa kuwa sasa inaonekana dhahiri ya kuwa zile kero za wananchi, hata kama si zote, zimeanza kumulikwa, na ukweli wa namna ya kuziondoa unaelekea kutafutwa, lazima kuna watu kama wewe na wenzako ndani ya chama na serikali ambao mnapata kizunguzungu na hofu kuu. Kwamba sasa ile 'mirija' aliyoikata Mwalimu ambayo mliweza kuiunga upya sasa inaelekea kuwa na uwezekano wa kukatwa upya. Huenda sasa katiba mpya ikipatikana basi si 'mirija' tu itakayokatwa, bali hata mizizi yote ya unyonyaji itang'olewa, ili matunda ya Tanzania huru yaweze kufaidiwa na kila mtanzania, na si yule tu ambaye ana baba, mjomba, shemeji, mume ama mke aliye kwenye sehemu yenye nafasi ya kuwanyonya wananchi.

Ukweli unawauma na unawatisha. Siku zenu zinahesabika. Waeleze wenzako ya kwamba tunakuja, na tunaitaka nchi yetu!!!
 
Kweli Wewe Umepitwa Na Wakati! Katiba Ni Ya Wananchi, Lakini Hoja Zako Zina Mlengo Wa Kichama Hebu Ona Aibu Ndugu Yangu. Mtu Mzima Unapo Andika Utumbo Ni Fedheha Kwako! Pia, Unamdharirisha Babayo. Acha Apumzike Kwa Amani!
 
Ni mtanzania aliyekosa uzalendo wa dhati katika taifa letu ndo ataleta mawazo kama hayo! Yaani wewe unataka wanasiasa waishambulie tume kwenye media, wakati huohuo unataka wasijibu kwenye media! Huo ni uharo mtupu!
 
Naona uko obsessed na mambo ya wanawake,vipi jamaa kuwa na vimada kila mahali.Tuna data nyingi,tukimwaga hapa tutapata ban.Au vipi uhusiano wa baba yako na mama yako mzazi?

Lazima utetee ulaji wa familia yenu ,maana serikali hii ya magamba inawalea.

Dada zako wanategemea serikali hii ku-hold vyeo vyao
Baba yako pensheni,ulinzi ,house boy/girl analipiwa na serikali.Kucheck afya yake Ulaya etc kama operation aliyofanyiwa UK kwenye private hospital hata Queen wa UK hawezi kutibiwa pale.

Nimeona picha ya baba yako huko New York na mama yako(anatumia mikorogo awe kama mzungu).Eti anazungumzia amani na utulivu,what a bollocks,amani ya kwenda Ulaya kila siku?

- Ungefungua thread yake hapa ninaongelea tume ya katiba, pole sana una muda mpaka wa kufutailia maisha yangu na familia yangu ina maana huna kazi bro? ha1 ha! ha!

- Le Big Shoow
 
Unamdharau kikwete sana wwewe basi tu na vijana wa ccm walivyo vichwa maji wanakuchekea
 
Mimi nadhani unapigana na giza!.

Utamaliza risasi zako za kisiasa bure wakati adui siyo Tume ya Jaji Warioba bali yule aliyeiweka hiyo tume ambaye unfortunate, ni Mwenyekiti wako wa chama Taifa. You better start shooting him down (Rais Kikwete) kwa sababu anawachanganya kimawazo na kimtazamo watu kama wewe ambazo siasa zenu niza mlengo wa confrontation politics!.

Kama huwezi kum-shoot down Mwenyekiti wako wa taifa basi spare the bullets ili uzitumie wakati wa kura za maoni ya katiba. Wahamasishe wanachama wako waikatae rasimu ya katiba mpya kwenye kura za maoni badala ya kupiga kelele barabarani bila targeted audience.

You are missing a political opportunity wakati time is money!.

- Nah! sina sababu ya kumshoot down aliyeunda tume kwa sababu ametumia katiba, na so far hajakosea ninataka katiba mpya lakini inayofuata Sheria ya kuibadilisha ambayo ipo wazi sana ndio ninasema Wapinzani ombeni kuahirishwa kwa hili zoezi la katiba mpya maana time is not on your side now hata ianguke mvua ya mawe ni CCM yenye Wabunge wengi bungeni ndio itakayokuwa na haki kisheria kuamua katiba iwe vipi,

- NI USHAURI WA BURE TU SUBIRINI MPAKA MUWE NA WABUNGE WENGI BUNGENI SASA HAMNA NAMBA ZA KUTOSHA KUBADILISKA KATIBA AS U WANT!!

LE Mutuz
 
Upo mstari wa mbele sana kutaka Tanzania isipate Katiba bora na inawezekana kabisa lengo lako ili muendeleze biashara yenu na huyo jamaa yako kwani tutakuwa na sheria legelege na dhaifu na kufanya kesi kama za akina Masogange kuishia hewani (Mtu anakamatwa na Mzigo wa Billion 6 analipa faini Million 4)

- Nah nataka katiba bora na ili kupata katiba bora Wapinzani mnahitaji kuomba kuahirishwa kwa mchakato wa sasa mpaka mtakapokuwa na wabunge wa kutosha bungeni so far hamna, ndio political fact on our land, poleni sana huwa mnapenda kurukia rukia sana mambo bila kufanya utafiiti!!

Le Mutuz
 
Ukweli ni kwamba wewe na wenzako ndani ya ccm kuikubali ama kutoikubali Tume ya Katiba hakumsaidii mtu yeyote anayeujua ukweli wa dhiki, shida na kero zinazotokana na mapungufu yaliyomo kwenye katiba tuliyo nayo sasa. Wananchi wamechoka kuona wanaendelea kuishi maisha yaliyojaa ufukara na yasiyo na mwelelekeo wala dira wakati watu wachache wanafaidika. Kero za wananchi sasa hivi ni kama jua la asubuhi, kila kukicha linachomoza. Kuanzia Lindi na Mtwara, kwenda Kigoma, Arusha na Manyara, Zanzibar ndiyo basi tena, juzi juzi tumesikia mpaka Dodoma wananchi wameandamana dhidi ya fisadi CDA. Kila wanapopita viongozi wa nchi (watawala) wanakutana na mabango na hata wananchi wakizuiwa kuonyesha mabango basi wanakutana na wananchi wanaowaeleza kuhusu shida zao! Kuanzia migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji, wananchi kunyang'anywa ardhi na wawekezaji, kukosa huduma muhimu kama afya, elimu, barabara, maji, umeme n.k. Suala la haki za binadamu zinavunjwa mchana kweupe na wanaozivunja wanalindwa mfano mzuri ni kauli ya Waziri Mkuu kusema 'wapigwe'. Suala la Muungano ambalo limeanza kuzungumziwa miaka mingi sana na walio madarakani wakajifanya wametia pamba masikioni hawasikii la mtu. Haya yote ni mapungufu yaliyomo kwenye katiba hii ya sasa!

Tufanyeje? Lazima tupate katiba mpya ambayo itakuwa dira ya kutuonyesha njia ya kutufikisha huko tuendako. Tuache kuongozana kama vipofu bali tunahitaji msaidizi angalau atakayekuwa macho yetu kwenye safari hii. Ndipo Tume hii iliposimamia. Kwa kuwa sasa inaonekana dhahiri ya kuwa zile kero za wananchi, hata kama si zote, zimeanza kumulikwa, na ukweli wa namna ya kuziondoa unaelekea kutafutwa, lazima kuna watu kama wewe na wenzako ndani ya chama na serikali ambao mnapata kizunguzungu na hofu kuu. Kwamba sasa ile 'mirija' aliyoikata Mwalimu ambayo mliweza kuiunga upya sasa inaelekea kuwa na uwezekano wa kukatwa upya. Huenda sasa katiba mpya ikipatikana basi si 'mirija' tu itakayokatwa, bali hata mizizi yote ya unyonyaji itang'olewa, ili matunda ya Tanzania huru yaweze kufaidiwa na kila mtanzania, na si yule tu ambaye ana baba, mjomba, shemeji, mume ama mke aliye kwenye sehemu yenye nafasi ya kuwanyonya wananchi.

Ukweli unawauma na unawatisha. Siku zenu zinahesabika. Waeleze wenzako ya kwamba tunakuja, na tunaitaka nchi yetu!!!

- Kama maneno yako ni ya kweli basi fuateni utaratibu wa Sheria, nendeni muwashawishi wananchi uchaguzi ujao wawape kura kama kweli wanaichukia CCM, ili muwe na namba kubwa bungeni ndio mtaweza kuwabadilishia katiba kama mnavyotaka kwa sasa hamuwezi kwa sababu hamna namba za kutosha bungeni, Sheria ipo wazi Dunia nzima Katiba ni lazima ibadilishiwe bungeni kwa kura za wabunge, sasa hivi kweli unahitaji kuwa na PhD kujua kwamba wabunge 280 against wabunge 46 ni 280 ndio watakaoshinda, hivi kweli unahitaji tume kujua huu ukweli?

Le Mutuz
 
Yaani hizi ni chuki za wewe na Ustazi John baada ya kushindwa kuishi IKULU. Tunajua mnavyomuunganisha mzee huyu Warioba na kushindwa wewe na baba yako kwenda kuishi ikulu. Vipi ule mzigo mliopokea toka Uarabuni ulishaisha?

mudushi
 
Kwa hio wakabidhi wakati hawajakamilisha, bora wamesema ukweli waongezewe muda kuliko kupata blabbla,
 
Back
Top Bottom