Uchaguzi 2020 Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) iachane na njama za kuvuruga uchaguzi, zitaligharimu Taifa

Uchaguzi 2020 Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) iachane na njama za kuvuruga uchaguzi, zitaligharimu Taifa

Sawa
Hawa Jamaa wanaandaa mazingira ya wizi wa wazi wa kura,ukitaka kuhakiki hili watapinga ushauri na kushupaza shingo zao.Refa anawezesha fouls za wazi na goli LA mkono.Hii ni aibu na ndiyo maana tunasema Tume ya Uchaguzi siyo Huru hats kidogo. Inawezekana hizi kanuni zimeandaliwa na Polepole & co.
Sibili kipigo kama cha serkali za mtaa
 
Haya ni maandalizi tu ya kujiongezea muda madarakani baada ya vipindi viwili kupita.hawa jamaa akili itawakaa vizuri June 2024.
Mh rais alisema hata ongeza hata dk moja usitafute pakutokea
 
Hawa NEC wakitaka taifa liwe salama wasithubutu kabisa kufanya kazi na yule mzee kijana wa Lumumba..atawaharibia credibility kabisa. . Maana 2020 watu wameapa kufia kwenye vituo cha kupigia kura...uhuni uhuni sasa basi.
Utafanya nini zaidi ya kukaakwenye keyboard na kushupaza shingo
 
Mengine yote ya taarifa yake Ado Shaibu, Katibu Mkuu wa ACT Mzalendo ni ya porojo tu zao za kisiasa, kutafuta mahali pa kutokea ( kuweka mpira kwapani) kukwepa uchaguzi ambao wana uhakika wa kutoka kapa, isipokuwa hili analokiri na kuthibitisha uchanga wake kisiasa.

Ati Chama cha ACT Wazalendo ambacho mimi nilikiwakilisha kiligomea kusaini na kuomba haki ya kusaini baada ya kuona toleo la mwisho la Maadili ya Uchaguzi lenye maboresho yaliyotokana na maoni ya wadau. Jawabu la NEC kuwa Chama ambacho hakitasaini Maadili ya Uchaguzi siku hiyo hakitashiriki kampeni, lilitulazimisha kusaini sambamba na vyama vingine vilivyosaini siku hiyo.

Yaani anakiri kusaini kwa kulazimishwa kweli! Ado msomi anayejitambua! Katibu Mkuu wa aina hiyo ni FUKUZILIA MBALI.
Waoga sana wanajua jpm anafanya Kazi kubwa wanatafuta pa kutokea
 
Jiwe anapanga kutumia staili ya Nkurunzinza type kwenye uchaguzi ujao ila , mabeberu watatumia Benghazi staili kumpa mambo.
Jpm alisema hata ongeza hata sekunde acheni kuleta hisia
 
Waoga nawaogopa kama ukoma
Chama cha mapinduzi ni waoga, tuliwaambia toka mwanzo kama kweli mtu wao anakubalika mbona figisu nyingi? Yaani wanahangaika acha, sasa wameingia time, tume bila aibu inafanya mambo ya hovyo, hapa ndipo umuhimu wa tume huru ya uchaguzi. Shit!
 
Narudia tena kwa unyenyekevu..Nchi nyingi barani Afrika uingia kwenye machafuko kwasababu ya Uchaguzi .Pili leo hii NEC wanaweza kutupa sababu gani za kuwanyima mawakala nakala za viapo ambao ni utambulisho wa wakala.?
Je ,NEC wanaweza kutuambia ni sababu gani mawakala wa vyama wasipewe nakala za matokeo ya Uchaguzi?
Yaani mtu anaesimamia uchaguzi akifanya ndivyo sivyo basi waziri ndiye amwajibishe...aibu hii kabisa ,yaani waziri ambae ni kada wa chama kinachoshiriki uchaguzi!
Mwisho ,kuna tabia ya viongozi wanaotengeneza matatizo ili iwe chanzo chao kukaa madarakani.
July nakuja...NAIPENDA TANZANIA
 
Vyama vya upinzani Tanzania mnatuchosha hamna maamuzi mpo kuralamika lalamika tu

Haya mmeona kuna makosa solution ni IPI toeni solution huu si mda wa ngonjera
Mambo,muhimu ni kuwe na haki kwa wote,maana tunajenga nyumba moja,lkn Mkuu amesisitiza hataki mambo ya vurugu na hata vyombo pia vimetaka iwe hivyo,je? hawa ni kina nani wanakataa kutii Sauti za Mamlaka?.
Naomba wajue hili na kuwanasihi hawa watu,anaye lalamika hakulizika ijapo vigumu kulidhisha wote lkn hili linaumuhimu wa wote kuridhika maaana ndio ukweli wenyewe.
 
Ni ujinga mkubwa kwa NEC kuogopa uchaguzi huru na wahaki. Hapo anaogopwa Lissu.
 
Miaka yote mlishiriki na mkapata ubunge kwa kanuni hizi hizi
Walipata wabunge wachache kadri ccm ilivyotaka lkn safari hii hawataki Chadema wapate hata mbunge mmoja...!!!
 
Magufuli naona anaiandaa hii nchi tayari kwa vikwazo vinavyoenda kuua kabisa uchumi huu ulioshaanza kuporomoka.
 
Mwenyekiti wa Tume asijisahau , cheo ni dhamana ya muda mfupi sana , shetani hana rafiki , asije kumlilia mtu
 
Mambo,muhimu ni kuwe na haki kwa wote,maana tunajenga nyumba moja,lkn Mkuu amesisitiza hataki mambo ya vurugu na hata vyombo pia vimetaka iwe hivyo,je? hawa ni kina nani wanakataa kutii Sauti za Mamlaka?.
Naomba wajue hili na kuwanasihi hawa watu,anaye lalamika hakulizika ijapo vigumu kulidhisha wote lkn hili linaumuhimu wa wote kuridhika maaana ndio ukweli wenyewe.
unataka maridhiano na mtu asiyeitaji maridhiano

Kama umewahi kucheza mpira unaweza jiuliza kipi huwa kinatokea kwenye fainali mmefungwa alafu bado dakika kumi mpira uishe galfa unashangaa refa anauweka mpira kwapani, huwa kipi kinatokea
 
Back
Top Bottom