Elections 2015 Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) yafuta Matokeo yote ya Uchaguzi Mkuu

Matokeo yaliyofutwa ni URAISI WA ZANZIBAR na WAWAKILISHI.

Matatizo ni KARATASI ZA URAISI ZANZIBAR sio BARA!!! ..hivi jamani watu wa UKAWA kwanini mnataka kuleta vurugu ??

Tatizo ni nini hasaa?? Vimetumika vktuo hivyo hivyo na wasimamizi ndio hao hao na wapiga kura ni hao hao...yakibatilika yabatilike kote
 
uchaguzi zanzibar haukuwa huru na haki na kuna kura za muungano kwenye same ballot boxes, so tunaamini kura za bara pia hazikusimamiwa kwa uhuru na haki.
either raisi wa muungano asitangazwe mpaka zenji warudie au na huku matokeo yafutwe.

Zanzibar ni kama Jimbo, wao kama wamevuruga, sio Tanzania nzima warudi.

Sijui kwanini ZEC hawaelezi vizuri, naona watu wa Bara wanashindwa kutatua chemsha bongo/brain teaser ya kilichotokea.
 
Tutalumbana sana hapa lakini cha msingi ni Watanzania wapenda nchi yao kuchukua hatua kivitendo za kuinusuru. Mwalimu aliacha ameyaongea yote haya na sisi tumeyapuuza lakini hata pale tulipoletewa mawazo mazuri kutoka kwa wananchi juu ya katiba mpya ulevi wa madaraka ukatupotosha.
Nakumbuka ZZK akikumbusha kuwa KATIBA NI MUAFAKA WA KITAIFA na inaweza kutengenezwa vizuri wakati kuna amani. Viongozi wa ccm hawakuwa hata na maona ya miaka miwili mbele wakapuuza wakidhani amani ya Tanzania iliumbwa na Mungu kana kwamba hizo Sierra Leone, Libya, Congo, Sudan hazikuumbwa na Mungu huyo huyo.
Cha kushangaza watu bila hata kuihurumia nchi yao wanapofushwa na madaraka na kuufuta uchaguzi halali bila kutangaza hata matokeo yenyewe!!???

Mwenye video clip ya Mh. Mnyika akieleza haya mambo anaweza kutusaidia:
"...tumnefika hapa sababu ya udhaifu wa serikali
...tumefka hapa sababu ya udhaifu wa JK"

Then mkumbuke Mwalimu:
"...CCM imara ....."
 
Mbona bara hawafuti, kwao wao hawakupiga kura za rais wa muungano?
 
Zilizofutwa ni Matokeo Ya Urais na Sio Ya Wabunge, madiwani wala Wawakilishi. Kwa hiyo Kura za Ubunge ziko pale pale

Ugomvi upo kwa Urais na sio kwa wabunge,, madiwani etc!
Mmetuangusha hamkumtilia kura Lowassa basi sisi hatuna tena tamaa ya kuupata Urais wa Zanzibar. Hawatupi, hawatupi, hawatupi n'go!!!!!
 

Kama Dr John Pombe Magufuli atapishana na mshindi wa pili kwa idadi ya kura CHINI YA LAKI 5 ambayo ndiyo idadi ya wapiga kura wote wa Zanzibar basi matokeo ya urais wa Muungano yatapaswa kusubiri marudio ya kura Zanzibar, lakini kama MAgufuli amemshinda mshindi wa pili kwa ZAIDI ya kura LAKI 5 basi matokeo yoyote ya Zanzibar hayawezi kuathiri MATOKEO YA URAIS WA MUUNGANO, kwa namna hiyo NSHINDI WA KURA ZA MUUNGANO ATAAPISHWA KAMA KAWAIDA.


Cha pili., NEC sio ZEC, hizi ni tume mbili tofauti, matatizo yaliyowapata ZEC sio matatizo yaliyowapata NEC, hivyo kama upande wa NEC hakukuwa na matatizo yoyote basi uchaguzi wa MUUNGANO KWA UPANDE WA ZANZIBAR UTAENDELEA KUTAMBULIWA, ni ule tu wa SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR ndio utakaorudiwa.
 


Tunaomba ututajie mikoa ambayo uchaguzi wa RAIS umeahirishwa??

Chaguzi nyingi mkoani zilizoahirishwa ni za UDAWANI na KATA. Lakini kila jimbo tanzania BARA wamepiga kura za RAISI. Mfano Kimara Stop Over hawajapiga kura za DIWANI. ARUSHA MJINI, LUDEWE hawajapiga kura za MBUNGE.
 
Kwa akili zako fupi unahisi mamvi angeongoza. Ndio maana muliambiwa malofa.

Wewe ni mtu asiye na akili hata kidogo. Baada ya kulishwa maharage yanayotokana na fedha za wizi huwezi hata kufikiria kidog umekuwa zuzu tu. Niambie ni nini ulikuwa umuhimu wa CCM kuwakamata vijana wa IT wa Chadema kama si kuogopa kuumbuliwa kama Maalim Seif alivyoiumbua ZEC?

Watu wengine hasara tupu. Swine.
 
Kwa hiyo na matokeo ya Lowassa na Magufuli kwa Zanzibar ni feki??Tabu Sana.
 
Maalim seif kujitangazia matokeo ni kinyume na taratibu na yeye anajua namna alivyofanya kuvuruga uchaguzi....Tume imefanya jambo jema kuepuka vurugu zanzibar.
 
Tatizo ni nini hasaa?? Vimetumika vktuo hivyo hivyo na wasimamizi ndio hao hao na wapiga kura ni hao hao...yakibatilika yabatilike kote

Mfano: Tanzania bara Jimbo la ubungo, unapewa karatasi TATU (Raisi muungano, Mbunge na Diwani) . kwa ZANZIBAR unapewa 4 (Raisi wa Muungano, Raisi wa Zanzibar, Mwakilishi na Diwani) tatizo liko kwenye hizi tatu za mwisho sio ile ya TANZANIA yote!!! TANZANIA BARA Hawana karatasi ya nne ya URAISI ZANZIBAR kwahiyo HAWARUDII.
 

Matokeo ya znz hayaathiri kura za Bara, hii ni kwa kuwa gap baina ya Hapakazitu na Safari ya matumaini ni kubwa mno, hadi sasa hapakazitu anaongoza kwa zaidi ya kura Milion Moja, hivyo hata kama waznz wote wakikpa kura safariyamatumaini haitaathiri ushindi wa hapakazitu.
 
Katiba ya Jamhuri ya Muungano rais wa Muungano anachaguliwa na wapiga kura kutoka Tanzania nzima kama kura za visiwani zimefutwa huwezi kupata uhlali wa Rais wa Muungano.

Uchaguzi wa Tanzania nzima ufutwe Mara moja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…