Tume ya ushindani kuchunguza udhamini wa GSM ligi kuu

Tume ya ushindani kuchunguza udhamini wa GSM ligi kuu

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Tume ya Ushindani wa Biashara (FCC) imesema imepokea malalamiko kutoka kwa wadau wa mpira wakiitaka kuchunguza udhamini uliofanywa na kampuni ya GSM kwa Ligi Kuu ya NBC Tanzania kama hautaathiri ushindani wa soka nchini.

Wadau hao wamewasilisha malalamiko yao kwa maandishi ndani ya tume hiyo Jumatatu ya Novemba 29, 2021 wiki hii kwa mujibu wa Mtendaji Mkuu wa FCC, William Erio wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Malalamiko hayo yamepokelewa ikiwa ni siku chache tangu kampuni ya GSM kusaini mkataba wa Sh2.1 bilioni na Shirikisho la Mpira Tanzania (TFF).

Pia hilo limefanyika ikiwa ni muda mchache tangu kampuni hiyo ambayo ni mdhamini wa Yanga SC kutangaza kuzidhamini timu za Pamba na Coastal Union ya jijini Tanga.

“Tulishaanza mchakato wakutaka kujua kama kitendo hicho hakitaathiri ushindani katika soka na majibu ya suala hili yatatolewa baada ya kujiridhisha kwa kuzingatia kanuni za ushindani na kama kweli linahusiana na ushindani,” alisema Erio.

Mwananchi
 
Good idea.

Wachunguze mbivu na mbichi zijulikane, haiwezekani wao wasaini mkataba wa kuidhamini ligi kuu, halafu wahusika ambao ni vilabu vyote vya ligi kuu vikataliwe kuujadili mkataba husika, walichofanya TFF na GSM ni utapeli mtupu.
 
Kama itaonekana huo udhamini hautakiwi itabidi wadhamini wote ambao wameingia mikataba na TFF(mfano matangazo ya mipira, kudhamini mashindano, kuidhamini timu ya Taifa) na uku wanadhamini klabu/vilabu ama wanamiliki klabu/vilabu mikataba yao na TFF isitishwe mara moja
 
Kama itaonekana huo udhamini hautakiwi itabidi wadhamini wote ambao wameingia mikataba na TFF(mfano matangazo ya mipira, kudhamini mashindano, kuidhamini timu ya Taifa) na uku wanadhamini klabu/vilabu ama wanamiliki klabu/vilabu mikataba yao na TFF isitishwe mara moja
Tatizo GSM pia ni viongozi ndani ya Yanga.Hapo ndio tatizo linapoanzia.Hersi atoke kwenye uongozi wa Yanga abakie kama mdhamini.Aachane na kujihusisha na usajili na kadhalika
 
Tatizo GSM pia ni viongozi ndani ya Yanga.Hapo ndio tatizo linapoanzia.Hersi atoke kwenye uongozi wa Yanga abakie kama mdhamini.Aachane na kujihusisha na usajili na kadhalika

Sikuelewi!

Kwani GSM ni ya Hersi?

Ebu angalia utumbo uliouandika
 
Tuna haribu soka letu wenyewe, mbona Azam ana timu anadhamini Yanga pamoja na TFF? Mambo ya hovyo kabisa

Mi nafikiri shida TFF walipopoga marufuku huu ushirikiano / mkataba kujadiliwa.. sasa watu wanashindwa kuelewa mikataba iliopita kuanzia aam bnc had tbc ilijadiliwa na tff ikatoa maelezo mgawanyo ukoje ila huu wamesema ni wao na gsm ndo wanahusika marufuku kujadili hapo watu ndo wanapiga kelele
 
Bora wafanye hivoo mana hata Mimi nilikua natilia shaka
Hukutilia shaka Azam kuidhamini ligi upande wa haki ya matangazo kwa miaka 10,na bado akasaini tena na Yanga na Simba mkataba mwingine wa zaidi ya bil 34 kwa kila mmoja kwa miaka 10?

Hukutilia shaka Azam kuidhamini ligi kuu upande wa matangazo na bado akalidhamini kombe la shirikisho ilhali na yeye bado ana timu yake huko!?
 
Bora watolewe au kama vipi warudishiwe kimiambili chao

Wameweka hela ya kisheti afu masharti kibao hawataki hata watu wahoji, huo si udwanzi
Ila ukumbuke tofauti iliyopo kati ya GSM na NBC ni milioni 400 tu.
Tena GSM yuko juu coz ni biln 2.1 two years,ilhali NBC ni biln 2.5 miaka mitatu.

So GSM ndo katoa pesa nyingi kuliko mdhamini mkuu kwa kipengele cha muda.
 
GSM kafanya kihuni Sana kujaza viongozi wa Yanga siku ya kusaini contract Kama wasemaji wake......Ni bora angetafuta watu wengine kumwakilisha.....maana hao ndio wanaoharibu kuonekana timu ya yanga itakuwa na mgongano wa maslai badala ya GSM Kama kampuni .huo ndio ukiukwaji number moja..

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Hukutilia shaka Azam kuidhamini ligi upande wa haki ya matangazo kwa miaka 10,na bado akasaini tena na Yanga na Simba mkataba mwingine wa zaidi ya bil 34 kwa kila mmoja kwa miaka 10?

Hukutilia shaka Azam kuidhamini ligi kuu upande wa matangazo na bado akalidhamini kombe la shirikisho ilhali na yeye bado ana timu yake huko!?
Kweli aisee Azam kamwaga mzigo kote uko na watu awakuhoji.
ila sasa mbona mkataba huu wa gsm na tff pamoja na kutohusishwa vilabu na kuwa siri lakini tff wameweka zuio usijadiliwe,kwanini iwe siri na usijadiliwe?
 
Hukutilia shaka Azam kuidhamini ligi upande wa haki ya matangazo kwa miaka 10,na bado akasaini tena na Yanga na Simba mkataba mwingine wa zaidi ya bil 34 kwa kila mmoja kwa miaka 10?

Hukutilia shaka Azam kuidhamini ligi kuu upande wa matangazo na bado akalidhamini kombe la shirikisho ilhali na yeye bado ana timu yake huko!?
Unaujua uongozi wa azam media na azam fc angalia uongozi wa hzo taasisi mbili na utofautishe na uongozi wa gsm na kamati za yanga.
 
Kweli aisee Azam kamwaga mzigo kote uko na watu awakuhoji.
ila sasa mbona mkataba huu wa gsm na tff pamoja na kutohusishwa vilabu na kuwa siri lakini tff wameweka zuio usijadiliwe,kwanini iwe siri na usijadiliwe?
Kitu ambacho wengi hawakielewi ni kuwa,mtu pekee mwenye uwezo wa kuuzungumzia mkataba huo ni TFF na GSM. Kuuhoji au kuujadili,majibu yake yatatolewa na hawa watu wawili.

Hata wa Azam,tumeambiwa tu. Hata ukuhoji majibu watatoa Azam na TFF.
Wengine itakua ni blaablaa tu.

Ipo mikataba mingi ambayo inaingiwa na hakuna anayehoji. Huu wa GSM na TFF ni kwakua tu kuna Yanga ndani yake.
Watu hawaangalii manufaa ya mkataba na kiasi cha fedha kilichowekwa,wao wanaangalia tu uwezekano wa Yanga kuutumia mwanya huo kupata ubingwa.

Ninauhakika,FCC watautupilia mbali huu mjadala. Hauna mashiko yoyote.
 
“Kuna tofauti kubwa kati ya AZAM FC na AZAM TV hakuna mahali popote unaweza kuona viongozi wa AZAM TV kama kina Tido Mhando, Yahya Mohamed wanajihusiha na shughuli za klabu ya Azam FC.

“Lakini upande wa GSM unamkuta Hersi, anaweza kuzungumza vyovyote lakini operations za klabu ya Yanga kwa asilimia kubwa zinaendeshwa na haohao viongozi wa GSM. Mtu mmoja anajihuisha na kusajili Yanga na hapohapo yupo katika upande wa kampuni ya GSM lazima mashaka yawepo.”

GEOFFREY LEA,Mchambuzi wa EFM.


Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom