Tume ya Warioba yaja na Rasimu ya Katiba yenye maamuzi mazito...

Tume ya Warioba yaja na Rasimu ya Katiba yenye maamuzi mazito...

Status
Not open for further replies.

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,358
Tume ya Katiba inayoongozwa na Jaji Joseph Warioba inatarajiwa kutoa Rasimu ya Katiba kuanzia kesho Jumatatu.

Taarifa za uhakika kutoka ndani ya tume hiyo zinasema wajumbe wa tume hiyo wameamua kuweka itikadi za vyama pembeni na kuibuka na rasimu ya Katiba yenye mambo mazito na makubwa.

Kati ya yaliyomo ndani ya Rasimu hiyo ni Uanzishwaji wa Serikali ya Tanganyika,Tume huru ya uchaguzi na pia kupiga marufuku wabunge kuwa mawaziri.Pia tume hiyo imependekeza umri wa kugombea urais uwe kuanzia miaka 40.

Wachambuzi wa mambo wanasema haya yatakuwa ni maamuzi magumu na mazito yamefanywa na tume na pia itakuwa imeondoa kabisa uwezekano wa Chama cha CHADEMA kuongoza watanzania kuipinga katiba hiyo kama walivyokuwa wameahidi awali.

Source: Tanzania Daima Jumapili UK. 2
 
Sidhani kama yanawekutokea Tz, tena kwa tume hii "tumbo mbele katiba nyuma"!!

Yangu macho, NAOMBEA IWE KWELI!!
 
ha ha basi tutakushukuru mzee wetu ila usisahu matokeo ya uraisi kupingwa mahakamani pliz mzee na mahakama zetu ziwe huru na zitoe haki...tutaanza kuisoma kesho
 
Sidhani kama yanawekutokea Tz, tena kwa tume hii "tumbo mbele katiba nyuma"!!

Yangu macho, NAOMBEA IWE KWELI!!

Hakika hata mimi niliposoma hiyo habari nimeshangaa lakini nikasema inawezekana kama kweli wameweka itikadi pembeni.
 
Kesho si mbali
Itakuwa nzuri ili na wale wanaodai Nchi
kule Znz waanze nao kulipia umeme
na wakajiunge OIC .
 
Aiseee! Ngoja tusubiri, Kinana kawaruhusu? Na fastjet a.k.a msaidia mateja wenye macho mlegezo, paja zenye tattoo na kiuno chembamba NA siyo akina Ngwair?
 
Laiti hiyo taarifa ingekuwa na ukweli ingeleta matumaini,Mungu ibariki Tanzania
 
Nadhani sasa badala ya chama chenu kuipinga, Chama chetu tutaongoza watz kuipinga. maana kwetu sisi Tume huru kwetu ni Kilio.
Na vipi kuhusu mahakama yetu????????
 
ha ha basi tutakushukuru mzee wetu ila usisahu matokeo ya uraisi kupingwa mahakamani pliz mzee na mahakama zetu ziwe huru na zitoe haki...tutaanza kuisoma kesho

Hayo niliyoweka ni machache tu yaliyoripotiwa na gazeti
 
Kupiga marufuku wabunge kuwa mawaziri ni kitu ambacho hakina logic. Mambo ya umri wa uraisi sio màmuzi mazito kwan lilikuwepo hata kwenye katiba ya sasa. Mambo ya msingi na mazito ni kuhusu mamlaka ya urais kama taasisi na sio mtu, watueleze matumizi ya rasilimali zetu, muundo na uendeshaji wa muungano, uhuru, haki na wajibu wa raia wetu, mipaka ya uwajibikaji katika taasisi za kiserikali, itikadi na falsafa ya taifa letu na pia muundo na muingiliano wa nguzo kuu za dola. Hatutaki porojo.
 
Kesho si mbali
Itakuwa nzuri ili na wale wanaodai Nchi
kule Znz waanze nao kulipia umeme
na wakajiunge OIC .
mkuu kulipia umeme sio issue,ni nchi ndogo sana zanzibar wakipata madaraka kamili,mambo yao yatakuwa safi sana.
 
Kupiga marufuku wabunge kuwa mawaziri ni kitu ambacho hakina logic. Mambo ya umri wa uraisi sio màmuzi mazito kwan lilikuwepo hata kwenye katiba ya sasa. Mambo ya msingi na mazito ni kuhusu mamlaka ya urais kama taasisi na sio mtu, watueleze matumizi ya rasilimali zetu, muundo na uendeshaji wa muungano, uhuru, haki na wajibu wa raia wetu, mipaka ya uwajibikaji katika taasisi za kiserikali, itikadi na falsafa ya taifa letu na pia muundo na muingiliano wa nguzo kuu za dola. Hatutaki porojo.
bora iwe hivyo hakuna mbunge kuwa waziri,halafu uteuzi wa mawaziri ufuate uwiano wa jinsi vyama vimechukua viti vingapi vya ubunge,na waidhinishwe na bunge.
 
dah... haiwezekani.. nitawaongoza nape na kinana kuipinga mpka mwisho..,
 
Wachambuzi wa mambo wanasema haya yatakuwa ni maamuzi magumu na mazito yamefanywa na tume na pia itakuwa imeondoa kabisa uwezekano wa Chama cha CHADEMA kuongoza watanzania kuipinga katiba hiyo kama walivyokuwa wameahidi awali..

Naona watu wanaandaaliwa kisaikolojia kupokea usanii mwingine wa Saccos.
 
Sidhani kama yanawekutokea Tz, tena kwa tume hii "tumbo mbele katiba nyuma"!!

Yangu macho, NAOMBEA IWE KWELI!!

wewe unamjua warioba au unamsikia anamsimamo kama jiwe atawashangaza wengi.
 
Kupiga marufuku wabunge
kuwa mawaziri ni kitu ambacho hakina logic. Mambo ya umri wa uraisi sio
màmuzi mazito kwan lilikuwepo hata kwenye katiba ya sasa. Mambo ya
msingi na mazito ni kuhusu mamlaka ya urais kama taasisi na sio mtu,
watueleze matumizi ya rasilimali zetu, muundo na uendeshaji wa muungano,
uhuru, haki na wajibu wa raia wetu, mipaka ya uwajibikaji katika
taasisi za kiserikali, itikadi na falsafa ya taifa letu na pia muundo na
muingiliano wa nguzo kuu za dola. Hatutaki porojo.

umeonyesha umahiri.....ila kwenye issue ya mawaziri kutokua wabunge unasema haina logic?.....huo ni umahiri wa kipuuzi...afu we gamba sema unajitahidi kurudisha akili kichwani
 
bora iwe hivyo hakuna mbunge kuwa waziri,halafu uteuzi wa mawaziri ufuate uwiano wa jinsi vyama vimechukua viti vingapi vya ubunge,na waidhinishwe na bunge.

Mkuu Elungata umetoa hoja nzuri sana.
 
Last edited by a moderator:
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom