TUMECHOKA: Sheria mpya zitungwe kuwabana Lecturers vyuoni wanaowalaghai kingono watoto wetu wa kike, mama zetu, wake zetu na wachumba wetu

Nikiwa mwaka wa pili lecturer moja jimama liliniambia nichague 0 au nipigiwe deshi yani Absence.....nikachagua zero nikafanya final yakaisha.
 
Basi waweke mtihani wa kitaifa

Huwa nasikitika pale lecture mwenye ngoma anapokuwa na tabia hii
 
Sheria ipi tena wakati kuna Sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa Mkuu.

Hapa tuseme tu kuwa vijana waripoti haya matukio Takukuru pindi yanapojitokeza. Ubaya ni kuwa wengi hawaripoti badala yake wanaishia kulalamika hostel tu.

Inasikitisha sana tunakuwa na wasomi ambao hawana elimu ndogo kama hii.

Ila pia Mkuu usishangae watoto wakike, siku hizi kuna wakufunzi mashoga (wanataka kuliwa na vijana wenu wakiume) niliambiwa kisa cha hivi na mwanafunzi ambaye ameshindwa kuhitimu tena mwaka huu kisa mkufunzi shoga alikuwa anamtaka.na akamdaka somo lake full suti.

Nilimshauru sana aripoti kwenye vyombo husika ila huyu dogo alikuwa mjinga mjinga, sijui jambo lao limeishia wapi ila nafahamu tu hajahitimu.
 
Nilisoma na manzi yangu. Iq yake ilikua Ni average ila sio mbovu Sana pharmacology ilimsumbua Sana mpaka lecture aliomba rushwa ya pesa au rushwa ya ngono ili amsaidie tulitoa pesa
[emoji3][emoji3]
 
Katika baadhi ya nchi kuna mitihani ya kitaifa ya vyuo ambapo wanaoratibu mitihani ni watu wengine ambao ni kama NECTA hapa kwetu. Ikiwezekana tuige hao ili kupata suluhisho la wote wawili Lecturer vicheche na mabinti vicheche. Hii itawaondolea mabinti Option ya kujilengesha wapate Marks za bure.
 
Nilisoma na manzi yangu. Iq yake ilikua Ni average ila sio mbovu Sana pharmacology ilimsumbua Sana mpaka lecture aliomba rushwa ya pesa au rushwa ya ngono ili amsaidie tulitoa pesa
[emoji3][emoji3]
Kumbe mkuu umesoma pharmacology sasa mbona gonorrhea ilikusumbua sana??

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Lecturer atamfelishaje Kama uwezo anao?

Kwani hicho chuo hakina bodi ya rufaa scipt ikasahihishwe na lecturer mwngine?

ASILIMIA kubwa
Ya wanaogongwa na lecturer Ni wale mabinti vilaza, afu huwa wanajilengesha wenyewe ili waliwe.
Na kwenye haya maisha binti akizoea kutoa rushwa ya ngono ili apate anachostahili basi hawezi kuacha hadi uzeeni. Maana hii ni rushwa kama rushwa nyingine, na wakiizoea wanakuwa addicted!
Wasome kwa bidii waache visingizio. Na kama kweli lecturers wanawasumbua washirikiane na takukuru kuwakamata hao watuhumiwa!
 
Tuache ufala kama huna Hela kaaa kimya tafuta madent wa chuo wako wengi wanazaliwa kila siku, wanawake na wanaume wapo Kwa ajili ya matumizi, kila mtenda dhambi ana mtego wake, kama hataki mshauri aweke mtego huyo mtu akamatwe narudia tena simu janja zitumike ipasavyo Acheni Tanta tantalila za kishamba, mnunulie hata mini camera ya kwenye begi au mfuko wa shati.

Kama huna pesa Kaa kimya njoo Dodoma nikugawie pisi kali ya kisandawe acha kulialia
 
Lecturer atamfelishaje Kama uwezo anao?

Kwani hicho chuo hakina bodi ya rufaa scipt ikasahihishwe na lecturer mwngine?

ASILIMIA kubwa
Ya wanaogongwa na lecturer Ni wale mabinti vilaza, afu huwa wanajilengesha wenyewe ili waliwe.
Hivi hawa wasichana huwa wanakwenda Chuo bila ya kuwa na qualifications? Maana inakuwaje yeye amepata qualifications za kuingia chuo lakini anapofika chuo anapata brain fog na hawezi kuendelea na masomo?
 
Lecturer hawezi kumfelisha mwanafunzi anayejitambua, maana mtihani mmoja unasahishwa na malectures wawili na hata booklet ni namba tu. Utajuaje huyu ni fulani?.

 

Wanawatega kwa marks au tamaa tu ya pesa? Maana ni marks itabidi alale na waalimu wote.
 

Hao ni vilaza na malaya, mwanafunzi anae jitambua Hana huo ujinga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…