Tumegundua ushirikina/nguvu za giza unaofanywa na kijana kwenye biashara

Tumegundua ushirikina/nguvu za giza unaofanywa na kijana kwenye biashara

Sasa hapo kuna shida gani? Mimi kama kazi inafanyika na hakuna hasara kama ulivyosema hayo mengine sio shida zangu.

Halafu ulitakiwa kujiongeza kwanini dogo anasema ataongea na boss wake, pengine ni mpango kazi wao huo wewe unaleta ujuaji.
Usikute dogo alikuwa anaporwa na kina chuma ulete na boss anakata hela ilio pungua. Dogo kaona ajiongeze nae kwa sangoma, ila dini hairuhusu ingawa mwana anapiga kazi balaaa😂😂
 
Usikute dogo alikuwa anaporwa na kina chuma ulete na boss anakata hela ilio pungua. Dogo kaona ajiongeze nae kwa sangoma, ila dini hairuhusu ingawa mwana anapiga kazi balaaa😂😂
Kigezo cha uvumilivu ni kwavile anapiga kazi....🤣🤣biashara ngumu sana, unawez kumsalit anaekupa pumz
 
Acha atimize jadi.
Jadi haina ugomvi nawe kwann usumbue mtu
 
Nyoya na kitu cheusi vilikua viashiria vya nguvu za giza. Labda angekubali kusema vinamaanisha nn
Mkuu, mimi naona wewe ndiwe mwenye imani za kishirikina. Unyoya na kitu cheusi ni vitu vya kawaida tu. Huenda anavitumia kuchezea na aliona aibu kusema mbele yako maana angeonekana mtu mzima mwenye michezo ya kitoto.

Halafu unasema ulienda 'kujifunza biashara', sasa umeenda umeyakuta hayo madogo umeyafungulia uzi. Je, ukioneshwa na misukule yake inayovuta wateja?

Hadi hapo umefeli mafunzo. Na huenda huyo nduguyo alipanga njama na kijana ili waone kama una kifua wakupe siri nyingine au la.
 
Wasalaam
Wiki hii mwanzoni baada ya kutoka kwenye mizunguko ya kusaka tonge, niliongea na ndugu yangu mfanyabiashara nikaomba wakati anafunga hesabu nifike kujifunza mambo mawili matatu.

Ilikuwa mida ya saa 2 usiku Baada ya kufika ilipo biashara tulisalimiana vizuri tu na kijana anaepiga kazi pale. Baada ya kucheki mahesabu ambayo ndugu yangu anafanya kila akifika, tukagundua kuna upotevu wa pesa lakini sii pesa nyingi(Tsh2500).

Baada ya kumuuliza kama alitumia, yeye hakuwa na majibu imekuaje haionekani. Baada ya kucheki stock tukaona kuna bidhaa zimeisha inabidi mzigo ununuliwe mwingine, akaandika lists.

Ghafla muda amekaa kuandika list ya vitu vya kununua akaona kuna unyoya kama wa jogoo ule mkubwa umebanwa kwa kificho na gundi(solotape) kwenye droo analotunzia cash. Ikabidi tuhoji kwanini ameweka hapo, lakini bahati mbaya hakutupa majibu alisema atamwambia ndugu yangu maana yake kwa siku nyingine.

Muda huo huo mteja alikuja kununua kitu, pesa ilivyowekwa kwenye droo(alivuta droo) tukashangaa kuna kitu cha mviringo cheusi na muda tumekiona akakiwahi na kukishkilia mkononi. Kumuuliza kwanini kuna hivyo vitu jibu lake ni moja atamwambia ndugu yangu maana ya hivyo vitu siku nyingine.

Tuliondoka pale bila majibu sahihi, lakini ndugu yangu licha ya kukasirika anashauri kwasababu anapiga kazi vizuri na amepiga hiyo kazi muda mrefu atamvumilia huku akimfuatilia kwa karibu zaidi(mpaka sasa anapiga kazi).

Vipi maoni yako kwa hayo matukio? Kama faida unaipata, utamfukuza kazi? Una uzoefu wowote katika hili?

Ungemshauri nini kama ni ndugu yako? Wenye biashara halafu mmeajiri chukua tahadhari.

NB: Biashara ni ya vinywaji na uwakala
Umesema umegundua lkn sijaona uliposema ulichokigundua.
 
Wasalaam
Wiki hii mwanzoni baada ya kutoka kwenye mizunguko ya kusaka tonge, niliongea na ndugu yangu mfanyabiashara nikaomba wakati anafunga hesabu nifike kujifunza mambo mawili matatu.

Ilikuwa mida ya saa 2 usiku Baada ya kufika ilipo biashara tulisalimiana vizuri tu na kijana anaepiga kazi pale. Baada ya kucheki mahesabu ambayo ndugu yangu anafanya kila akifika, tukagundua kuna upotevu wa pesa lakini sii pesa nyingi(Tsh2500).

Baada ya kumuuliza kama alitumia, yeye hakuwa na majibu imekuaje haionekani. Baada ya kucheki stock tukaona kuna bidhaa zimeisha inabidi mzigo ununuliwe mwingine, akaandika lists.

Ghafla muda amekaa kuandika list ya vitu vya kununua akaona kuna unyoya kama wa jogoo ule mkubwa umebanwa kwa kificho na gundi(solotape) kwenye droo analotunzia cash. Ikabidi tuhoji kwanini ameweka hapo, lakini bahati mbaya hakutupa majibu alisema atamwambia ndugu yangu maana yake kwa siku nyingine.

Muda huo huo mteja alikuja kununua kitu, pesa ilivyowekwa kwenye droo(alivuta droo) tukashangaa kuna kitu cha mviringo cheusi na muda tumekiona akakiwahi na kukishkilia mkononi. Kumuuliza kwanini kuna hivyo vitu jibu lake ni moja atamwambia ndugu yangu maana ya hivyo vitu siku nyingine.

Tuliondoka pale bila majibu sahihi, lakini ndugu yangu licha ya kukasirika anashauri kwasababu anapiga kazi vizuri na amepiga hiyo kazi muda mrefu atamvumilia huku akimfuatilia kwa karibu zaidi(mpaka sasa anapiga kazi).

Vipi maoni yako kwa hayo matukio? Kama faida unaipata, utamfukuza kazi? Una uzoefu wowote katika hili?

Ungemshauri nini kama ni ndugu yako? Wenye biashara halafu mmeajiri chukua tahadhari.

NB: Biashara ni ya vinywaji na uwakala
Kiherehere tu, mambo ya watu unayaleta huku sisi tukusaidie nini sasa? Hakika nchi hii tuna uhaba wa vijana! Kaka kama binti!
 
Binafsi siwezi kuvumilia ushirikina kwenye eneo langu la makazi au biashara.Muda huu huyo dogo angekuwa kwao Ifenkenya huko.
Bado yupo, lkn kwa vile sii jambo langu kufanyia maamuzi. Nipo nimetulia tuu
 
Kiherehere tu, mambo ya watu unayaleta huku sisi tukusaidie nini sasa? Hakika nchi hii tuna uhaba wa vijana! Kaka kama binti!
Kupitia mambo ya watu unaweza kujifunza. Huna adabu😡
 
Mkuu, mimi naona wewe ndiwe mwenye imani za kishirikina. Unyoya na kitu cheusi ni vitu vya kawaida tu. Huenda anavitumia kuchezea na aliona aibu kusema mbele yako maana angeonekana mtu mzima mwenye michezo ya kitoto.

Halafu unasema ulienda 'kujifunza biashara', sasa umeenda umeyakuta hayo madogo umeyafungulia uzi. Je, ukioneshwa na misukule yake inayovuta wateja?

Hadi hapo umefeli mafunzo. Na huenda huyo nduguyo alipanga njama na kijana ili waone kama una kifua wakupe siri nyingine au la.
umewaza mbali saana, kijana kabisa yule(20s) sio mtoto useme anafanya michezo. Lakini nisikukatalie inawezekana kuna jambo, muda utanipa vya kujifunza
 
Tulia kijana, huko madukani kwetu ni misukule ndio inahudumia wateja....karibu dukani kwangu, karibu sana.
Utanikosa...bora nije kama sijui. Ukifunguka sitii mguu
 
Back
Top Bottom