Tumejifunza nini kama Taifa kuhusiana na uzushi kuhusu afya ya Rais Magufuli?

Tumejifunza nini kama Taifa kuhusiana na uzushi kuhusu afya ya Rais Magufuli?

Baba pole sana kwa majukumu mazito ya kuliongoza Taifa hili, na pole sana kwa Uvushi na uvumi kuhusu Uhai na afya yako.
Mtego huu umewanasa wapinzani, wanaccm na wasio na vyama na umeacha funzo kubwa sana kwetu kama Taifa .
Mimi mwana team yako nakuomba tu uwasamehe wote maana hawakujua walitendalo
Pia nakuomba uwasamehe na usilipize kisasi maana Biblia Takatifu inatamka 'Kisasi ni cha Bwana' Warumi 12:19.
Ingawa Kuna maamuzi utafanya katika nafasi Fulani Fulani, lakini tenda kwa utulivu mkubwa tena pale inapobidi.
Kwingineko unaweza kupotezea ili wajifunze zaidi na kubadilika.
Nakuombea afya njema na nguvu, usikatishwe Tamaa na haya yaliyotokea.
Mtego huu, umekudhihirishia marafiki wa kweli na wanafiki hivyo usiutumie kuadhibu Bali kuboresha na kuimarisha palipo nyufa. Mwenyezi Mungu akubariki sana
 
  • Thanks
Reactions: nao
Nilichojifunza ni upendo wa ajabu walionao watanzania hasa vijana juu ya Jembe letu JPM, maana walikuwa ktk khali ya taharuki uku wakianza kmsifia JPM na kuanza kumwombea kwa Mola,hakika Watu wanamkubali sana jembe letu.

Mimi binafsi naomba Mungu azidi kumpa Afya njema Raisi wetu mpendwa.

Amina,Mwisho

Watanzania tupuuze maneno ya uzushi yanayoletwa na vizandiki na wajinga juu ya mstakabali wa nchi yetu.
" wazushi kanyaga"
 
Wapinzani wamewekeza Sana kwenye mitandao ya kijamii, ukweli ni kwamba watanzania wengi wanampenda magufuli kuliko wachache wa kwenye mitandao,
Eti wanamfundisha raisi namna ya kufanya kazi,
Kumbukeni watu kufanya maovu duniani haimaanishi Mungu Yuko wrong.
 
Nimejifunza kwamba utamaduni wa Watanzania kumstahi rais na kumuheshimu sana, siyo tu unaisha, bali unaelekea kwenye utamaduni wa ajabu wa kumtakia mtu, tena rais, kifo.

Hii ni tabia mbaya kwa upande wa wananchi wenye mawazo hayo.

Lakini tabia mbaya hii imepaliliwa na kutiliwa mbolea na ubabe wa rais Magufuli.

Watu waliwakejeli Kikwete na Mwinyi kwa udhaifu wao, lakini haikufikia watu wengi hivi kusheherekea uvumi wa kifo cha rais.
Wengi kwa kipimo kipi chief?
 
Au ilikuwa ni drill ikilenga kuangalia kiwango cha usiri huko jumba jeupe kwa sasa na kuona mapokeo ya watu kama taarifa ingekuwa ya kweli. Ila kiukweli kupitia mitandao idadi kubwa ya watu walionyesha kufurahia taarifa ya awali. Inasikitisha sana.
Sasa katambua kuwa hata CCM wengi hawampendi
 
ccm wameshaturoga,hata wafanye upumbavu vipi tutawaunga mkono na wapinzani hata wakifanya jema gani hawawezi toboa hadi hapo watanzania wengi watapopata elimu zaidi ya ile ya kuvukia barabara
Sasa hata CCM wakifanya ujinga wao huwasingizia wapinzani ambao hawapo huru wamefungwa miguu na mikono
 
Mimi nilichojifunza ni kuwa serikali ya sasa imeanza kubadilika kwenye nyanja ya mawasiliano kwa umma hasa namna ya kukabiliana na tuhuma na uzushi wa kwenye mitandao ya kijamii.

Kwa jinsi ambavyo serikali/Ikulu imekabiliana na uzushi uliofanyika kwa muda wa siku tatu kuhusu afya ya Rais Magufuli imeonyesha mabadiliko makubwa sana!

Nakumbuka wakati Rais Magufuli anaingia madarakani alikuwa anapenda kujibu kwa maneno kila tuhuma na uzushi uliohusu yeye au serikali yake bila kujua kwa kufanya hivyo alikuwa anawapa umaarufu wale ambao walikuwa wanatoa uzushi au tuhuma.

Kujibu kila uzushi na tuhuma kwa maneno ndio kulimpa umaarufu Mwana Mama aitwaye Mange Kimambi ambaye alijikuta akipata wafuasi zaidi ya milioni 1.2 kutoka laki 300000.

Kanuni moja ya kukabiliana na uzushi ni kuupuuza na kama ukiona bado unaendelea basi unachofanya ni kuonyesha ukweli kwa vitendo katika muda mwafaka kwa sababu uzushi ukiachwa kwa muda mrefu uendelee kuwepo huanza kuaminisha jamii.

Uzushi kuhusu afya ya Rais Magufuli imejibiwa kwa muda mwafaka lakini kikubwa zaidi njia iliyotumika katika kujibu imeondoa imani (credibility) yote ya yule aliyeuanzisha na kuushupalia lakini vile vile waliouamini wameonekana ni wajinga au wapumbavu.

Kitu kingine nilichojifunza ni baada ya kuona baadhi ya viongozi wakuu wa vyama vya upinzani kama Zitto Kabwe, Dkt Vicent Mashinji na Godbless Lema wakiamini uzushi kuhusu afya ya Rais Magufuli ni kuwa viongozi wa vyama vya upinzani hawajui linaloendelea Ikulu. Kwa maana nyingine, siri za Ikulu kwa sasa hazitoki kwa urahisi. Fikiria viongozi wa vyama vikuu vya upinzani hawajui hata alipo Rais wa nchi achilia mbali afya yake! Yaani Zitto Kabwe wa leo hajui kinachoendelea Ikulu!

Nimejifunza pia kama wananchi wengi hawataelimishwa kuhusu matumizi ya mitandao ya kijamii kuna uwezekano ''mpumbavu'' fulani kutunga uzushi wa suala fulani linalogusa hisia za wengi na wengi wakaamini na kufanya jambo ambalo linaweza kuleta madhara makubwa kwa taifa.

Mwisho kabisa nimejifunza kuwa inatakiwa kwanza kuchukua muda kabla ya kuamini kile ambacho kimeandikwa kwenye mitandao ya kijamii kwa sababu ukweli hukawia kufika.

Nimalizie kwa kuandika, Nimeamini Uongo hupanda kwa lifti. Ukweli hupanda kwa ngazi ili kumfikia mlengwa!
yote kwa yote, kuna kitu hakiko sawa mahali.

tukumbuke tu ya wahenga wetu..... mficha uchi hazai na mficha maradhi kifo humuumbua!
 
Kuuliza alipo Rais siyo ujinga na hopeless ni nyie mlioficha taarifa kisha mkaanza kuhaha mitandaoni huku mkuwasingizia uongo wapinzani kuwa wameshangilia wakati CCM wapinzani wa ndani ya CCM hasa watumishi wa umma waathirika wa kukosa nyongeza za mishahara ndiyo wameshangilia Sana, acheni kuwapakazia uzushi wapinzani huko CCM kwenyewe hampendani, kama kweli mnampenda magufuli Mbona hamkwitisha maandamano ya Amani kumuombea?
Waliuliza kwani alipotea siku ngapi? Ni mjinga mmoja aliwalisha ujinga wake wote wakaamini na ndiyo mwanzo wa kuulizia. Amewapitia kweli kweli na ni aibu kubwa.
 
Nimejifunza kuwa hii serikali imewadhuru wengi mno hadi hao watu wamejawa na roho ya kisasi.
 
Hakuna sehem nimekubali ya kigogo
Mi ni insider mwenyewe zaid ya kigogo,
Habari baadhi kigogo anazipata kwa wenye level ya kwangu hivo sina cha kupata kwa kigogo, labda mi nimpe kigogo


Kama inside, kilitokea maana nilikuona ukipuyanga sana
 
Kwani mkulu mwenyewe yuko wapi kipenzi cha watu?si ajitokeze tu awambie wanangu nipo.
 
Nenda Youtube utaona tukio lote la kuapishwa leo Jumapili 20/10/2019 ndiyo maana wanasaccos wako kimyaa kama wamenyeshewa mvua ya mawe.
Nani yupo kimya? Kwani wapinzani ndiyo waliwatuma CCM kwenda kumtupia Moshi wa kichawi huko Ruangwa?
 
Aaaa ujerumani sasa amerudi?
Mkuu mbona una conclude kwamba Rais ni mgonjwa, umejuaje? Kigogo kadanganya watu hadi kufikia kutaja chumba ambacho ati Mh Rais alilazwa huko Ujeremani! Bado unasema Kigogo siyo muongo kwa 100%!! Ajabu
 
Back
Top Bottom