Tumejifunza nini kama Taifa kuhusiana na uzushi kuhusu afya ya Rais Magufuli?

Tumejifunza nini kama Taifa kuhusiana na uzushi kuhusu afya ya Rais Magufuli?

*UZUSHI DHIDI YA RAIS MAGUFULI UMETUACHIA MAFUNZO MENGI.*

Uzushi ulioshadadiwa na baadhi ya watu wakiwemo wanasiasa kuwa Rais Magufuli yupo hoi taabani ama amefariki dunia ni aibu nyingine kubwa.

Imesikitisha zaidi kwamba hata viongozi wakubwa wenye dhamana za uongozi waliingia katika upuuzi huu. Na wala sio jambo la kuficha kiongozi kijana kama Zitto Kabwe kushabikia upuuzi huu ni aibu kubwa kwake na ni kuwadhalilisha wananchi wa Kigoma Mjini waliomchagua kuwa Mbunge, ni aibu kwa familia yake, wanachama wa chama chake cha ACT na wanasiasa wa upinzani ambao wamekuwa wakishirikiana nae katika upuuzi kama huu.

Zitto ameandika sana kwenye mitandao akishabikia upuuzi huu, tena akipost picha ya Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan akikagua gwaride kwamba huyo ndiye Rais wa Tanzania baada ya Magufuli kufa. SHAME
Hata kama ameomba radhi lakini haiondoi kuwa yeye ni mpuuzi.

Zitto na wenzake akina Godbless Lema wa CHADEMA na vijana wao akina Yeriko na wengi wakaona wamepata pa kufanya majigambo ya siasa.

Nimejifunza nini?

1. Watanzania wengi wanampenda sana Rais Magufuli. Hapa mtaani kwangu baada ya Rais Magufuli kutokea kwenye TV mubashara akiwaapisha viongozi, kuliibuka shangwe kana kwamba Yanga au Simba imefungwa bao. Lakini pia katika mitandao ya kijamii unaweza kuona jinsi Watanzania wengi walivyofurahi baada ya kuthibitika taarifa za kuwa Rais Magufuli yupo hoi na kakimbizwa nje ya nchi hazina ukweli.

2.Tuna wanasiasa wa upinzani wa hovyo nchi hii haijapata kutokea. Wamekosa hoja za msingi ili wawe mbadala wa CCM na wamebaki kuokoteza uvumi na uzushi usio na mashiko. PUMBAFU KABISA.

3. Watanzania wamewajua wasioitakia heri nchi yao. Makatili na wenye uchu wa madaraka.

4. Huyo Kigogo wa kwenye Twitter amegeuka kuwa Kipimbi, muongo, mzushi, mchanganishi na hafai. Anaelezwa kuwa ni Zitto Kabwe kwa hivyo ndivyo thamani yake ilivyoanguka na wengi sasa wamejua kuwa ni mpuuzi.

5. Tuna Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ambayo imekosa maarifa kabisa. Haiwezekani watu wanacheza na mitandao, wanayumbisha nchi na TCRA imekaa kimya tu. Wameshindwa hata kukemea tu. Nchi nyingine TCRA zao zinakuwa na ubunifu wa hali ya juu wa kuhakikisha hakuna loopholes za watu kutumia mitandao kupotosha ukweli na kuvuruga amani na utulivu. Ni ama akaunti zao zinafungwa ama wanatumia sheria za mitandao walizonazo kuwadhibiti. Lakini hapa kwetu ndio kwanza wapotoshaji akaunti zao zinapata verification na wanatamba wanavyotaka.

Makamu wa Rais waliyekuwa wanamtangaza kuwa anajiandaa kuingia Ikulu kwa zuria jekundu kaishia kugawiwa sambusa na JPM. Nae siku nyingine ajifunze kuwakemea watu wanaomgombanisha na Mkuu wa Nchi. Vinginevyo kwa uzoefu wa nchi nyingine mambo kama haya husababisha mtafaruku mkubwa kwa sababu huaminika wanaomchafua Rais wanatumwa na Makamu wake ambaye amepewa mpenyo wa kuwa Rais pale Rais aliyopo madarakani anapofariki dunia kwa mujibu wa Katiba.

Mama Samia Suluhu Hassan usikubali upuuzi huu wa akina Zitto Kabwe, usipoyaamini maneno yangu ipo siku utanikumbuka.

Mwisho, naungana na Watanzania wote kufurahia kushindwa kwa akina Zitto Kabwe na genge lake la akina Kigogo. WAMESHINDWA, WAMELEGEA NA WAMETEPETA.

Tuchape kazi Watanzania, kupata mtu wa aina ya Dk John Pombe Magufuli kwenye kitu cha Urais sio rahisi, ndio maana huyu tuliyenae anasifiwa kila mahali. Tushtuke jamani. Tumuombee afya njema na mafanikio katika jukumu tulilompa. Ni kwa faida yetu sisi.

Asalaam Aleikhum

Salim Said Makate
Dar es salaam
20 Oktoba, 2019
 
Zitto ana roho ya kishetani

Zitto ni Kiongozi ni mbunge anashabikia kifo cha kiongozi wa Nchi

Na bado kuna watu wanamwamini ati anaipigania nchini?

N
 
Lissu na kauli ya majuzi meko anazungumza kuhusu mbunge aliepewa jimbo lake unaizungumziaje
 
Hakuna sehemu ikulu walitangaza kama Rais ana homa au mafua, sasa watu kuanza kushabikia habari ambazo ni za uzushi ambazo zinaweza kukuletea madhara si kujibebesha gunia la misumali. Kesho mtu akitiwa nguvuni utasikia kaonewa, matatizo mengine tunajiftia wenyewe
Mkuu;
Nimekuelewa! Asante sana.
 
Kuna mengi ya kujifunza
1. Viongozi wa vyama vya upinzani hawana mifumo dhabiti ya intelijensia ambayo ingetoa ukweli kabla kutoa kauli zao.
2. Uzushi kama huu unaadhiri hali ya usalama na mwenendo wa biashara hasa soko la hisa.
3. Baadhi ya watumiaji wa mitandao ni wepesi kusambaza uzushi bila kutafuta ukweli wa jambo husika. Wengine hupata fursa kueneza mawazo hasi ya kisiasa au kiuchumi.
4. Vyombo vya habari vya ndani na nje havikushadidia uvumi huu.
5. Sheria ya habari na uandishi wa habari imezingatiwa isipokuwa mitandao ya kijamii.
Mkuu;
Sina zaidi ya kuongeza kwa ulichokiandika kwa sababu mawazo yangu umeyaweka kwenye mchango huu.
 
Ni kweli Ikulu sasa hivi wamefanikiwa kwa asilimia kubwa kudhibiti uvujaji wa siri tofauti na kipindi cha nyuma! Hii imemdhoofisha sana Zitto kisiasa na kumfanya haonekane kituko!!
Mkuu;
Kuna kipindi pia aliwahi kusema Rais Magufuli ameenda China lakini siku hiyo hiyo Rais Magufuli akajitokeza kwenye hafla Ikulu.

Hili tukio pia limezidi kuonyesha kuwa hana habari ya kinachoendelea Ikulu!
 
Nlichoelewa hapo ni wewe kuwaponda wapinzani tu!
Hamjajifunza!??????
 
We kwa akili zako meco ulomuona akiongea leo ni yule wa kawaida? Hujaona alivyo mpole.
Ukweli ni kuwa anaumwa ila hajafariki. Ila kwa jinsi ilivyoonekana mtandaoni ni kuwa hapendwi kabisaaaaa, hata ajifariji namna gani nguvu ilokuwa mtandaoni inaonyesha waz kuwa hapendwi,
OVER
Mkuu;
Unapima kupendwa kwa Rais ukitumia mitandao tena kwa watu ambao wanapiga kelele?
 
Mm nimejifunza kwamba wapinzani wa Tanzania ni wapumbavu tu...

Na kwa hatua hii hakuna mbadala wa CCM
Unakosea kabisa kuwatwisha wapinzani zigo la upumbavu kwani wapo wana ccm wengi tu walioshabikia uzushi huu. Kikubwa kilichojidhihirisha ni kuwa umoja wetu kama Taifa haupo tena.
 
Nimegundua uwepo wa manyumbu mengi sana!

Kutoka ushabiki wa hadithi uchwara za ngono mpaka upumbavu wa kuzusha na kushadadia vifo.

Eti wenyewe wanajiita 'mabaharia'!

PUMBAVU! Nyumbu wakubwa!

Washughulikiwe na hao mabavicha wenzao wasio na ubongo!
 
Nimegundua uwepo wa manyumbu mengi sana!

Kutoka ushabiki wa hadithi uchwara za ngono mpaka upumbavu wa kuzusha na kushadadida vifo.

Eti wenyewe wanajiita 'mabaharia'!

PUMBAVU! Nyumbu wakubwa!

Washughulikiwe na hao mabavicha wenzao wasio na ubongo!

Hahahaa!

Jomba naona hao ‘mabaharia’ wanakuboa sana.

Anywho, kwa kiasi kikubwa sana siku hizi humu hakuna mijadala ya maana.

Mingi iliyopo ni ya kijinga kijinga tu.

Ndo maana baadhi yetu tumepunguza hata uwepo na ushiriki wetu humu....
 
"Man does not live by bread alone, but also by the flesh of good lambs".

Friedrich Nietzche - "Thus Spoke Zarathustra". 1885.

kwani umeona nime ku 'quote' kwa lugha hiyo?Jibu hoja ,'imeandikwa wapi?"
Hata haina shida,ukiaminicho sio kila mtu anakiamini.Siamini mambo mengi ikiwapo biblia na quran,najua huamini pia.Kwanini unataka niamini maneno ya mtu mmoja huyo uliye mnukuu?
 
kwani umeona nime ku 'quote' kwa lugha hiyo?Jibu hoja ,'imeandikwa wapi?"
Nimekujibu. Nimekupa mpaka jina la kitabu na muandishi.

Kama hujui kusoma hilo ni tatizo lako, si tatizo langu.

Yani ujinga wako mwenyewe unataka kunipa kazi mimi ya kukurudisha shule?
 
Magafuli anatakiwa kujifunza kuwa humble na binadamu wenzake. Ukiona binadamu wenzako wanakuombea kifo ujue kuna mahali unawakwaza.

Kuwa humble na binadamu wenzako haimaanishi kwamba usitekeleza majukumu yako kama Raisi.

Mi nadhani aisikilize ile hotuba ya Kikwete vizur kuna kitu atajifunza.
Mkuu;
Huyu ni kiongozi mkuu wa nchi yenye wananchi zaidi ya milioni 55. Hakuna ubushi kuwa katika wananchi hao lazima kuna wengine atawakwaza tu. Kuombewa kifo haina maana anachokifanya ni makosa? Mbona hata mitume kwenye vitabu vya dini ambao walikuwa humble lakini waliombewa kifo wengine wakauwawa?

Ndio maana Marais wanapewa walinzi wenye siraha kwa sababu wanajua kuna watu wanapenda wauwawe.

Kwangu hoja eti ni ajabu kuona Rais anaombewa kifo inanishangaza sana kwa sababu sio kitu cha ajabu kutokana na nature ya kazi zake.
 
Nimekujibu. Nimekupa mpaka jina la kitabu na muandishi.

Kama hujui kusoma hilo ni tatizo lako, si tatizo langu.

Yani ujinga wako mwenyewe unataka kunipa kazi mimi ya kukurudisha shule?

kwani umeona nime ku 'quote' kwa lugha hiyo?Jibu hoja ,'imeandikwa wapi?"
Hata haina shida,ukiaminicho sio kila mtu anakiamini.Siamini mambo mengi ikiwapo biblia na quran,najua huamini pia.Kwanini unataka niamini maneno ya mtu mmoja huyo uliye mnukuu?
 
kwani umeona nime ku 'quote' kwa lugha hiyo?Jibu hoja ,'imeandikwa wapi?"
Hata haina shida,ukiaminicho sio kila mtu anakiamini.Siamini mambo mengi ikiwapo biblia na quran,najua huamini pia.Kwanini unataka niamini maneno ya mtu mmoja huyo uliye mnukuu?

Kwani wapi nimekuambia uamini?

Umebanwa na uharo wa kiakili?

Straight to ignore list.

I don't deal with stinking pussy.
 
Back
Top Bottom