Tumejifunza nini kama Taifa kuhusiana na uzushi kuhusu afya ya Rais Magufuli?

Tumejifunza nini kama Taifa kuhusiana na uzushi kuhusu afya ya Rais Magufuli?

Waliofurahia huo uzushi ni Wa vyama vyote Mkuu.kusema wapinzani ni kuficha tatizo.inasadikika wako mawaziri, wabunge Na wakuu Wa mikoa walianza kushangilia kimyakimya Na kuulizana kama makamu anafaa kwa nafasi hiyo badala ya kumuombea.hoja ya waliozusha kukamatwa siungi mkono sana, maana wako viongozi Wa upinzani wamezushiwa vingi Na wahusika wanaachwa tu...lugola uwaziri Wa mambo ya ndani umemshinda kiujumla.
 
Na huu ni ukweli usio na shaka....Kama tuliyoaminishwa na kina Zitto,Kigogo na wengineo ingekuwa ni kweli ni ukweli usiopingika Nchii ingeingia machafukoni maana wale wote walionyesha chuki ya wazi wazi Kwa Mheshimiwa Raisi sijui kama wangekuwa salama hii ingewahusisha Zitto,Membe na genge lake màana wanachi walio wengi wenye mapenzi ya dhati na Mheshimiwa Rais wangelichukulia hili tukio kama la kutengenezwa hivyo lazima wangeamua kulipiza kisasi mwisho wa siku nchi hii isingekalika
 
Acheni kukuza mambo. Namshauri huyo Waziri awapuuzilie mbali nyinyi mnaoukuza huo ujinga na huyo Musiba wenu. Kunyamaza nako ni busara pia.
 
mimi sio chadema wala sio mfuasi wa Mbowe... ila ni mwanasiasa makini sana.

Inaniuma hata Mbowe kuwa na kesi ambapo ni ama ameonewa ama mambo ya mob.

nilichomaanisha ni kwamba kuna kiwango cha viongozi wa upinzani kuto act ama kuongea kitoto....

Mbowe ni mfano hai wa aina hiyo ya kiongozi. Akiongea Mbowe unashtuka. Akiongea Zitto una ignore

Hilo la viongozi wa upinzani kuonewa liko wazi na ni kilio chetu cha muda mrefu, kwamba rais wa sasa anatumia madaraka yake kuwakomoa na kuwatesa wapinzani wake. Naona unakiri hilo sasa, sio kwamba unasimamia haki, bali ni baada ya kuona hakufurahia uvumi wa kipenzi chako. Narudia tena, hapa unampaka mafuta Mbowe kwa mgongo wa chupa kisa hakuwa mmoja ya waliofurahia huo uvumi. Ila huna lolote la maana unaloona kwa Mbowe zaidi ya hilo.
 
Nimpongeze Tundu Lisu, amekaa kimya na hata alipotaka kusema alitamka maneno ya kuomba heri ya Mhe.Rais. Kwamba ameandika kutoka moyoni au la ni Siri yake na Mwenyenzi Mungu.

Niwaombe Watanzania tusivae ukatili mkubwa kiasi hiki, kiongoz anapohisiwa kupata tatizo Taifa linakaa kimya na kumwombea mazuri ila nimeshangazwa kuona mtaani hata wale wanaccm tuliotegemea wamwombee afya njema walibadilika na kuanza kujadili Kama Makamu anafaa au la. Sisemi wanaccm wote bali nasema na wale waliofurahia uvumi uliokuwa unaendelea.

Mawazi na wakuu wa Mikoa, mmeonyesha wazi kwamba upo unafiki ndani yenu na hapendwi mtu inapendwa ajira...mlikuwa na Uhuru wa kupost na kutoa tweet za faraja lakini mlikaa kimya na baadhi yenu mliwaza zaidi kuhusu next prezdaa kuliko kufuatilia afya ya aliyepo. Baada ya kutambua kwamba chuma kipo imara mkaondoka kabisa kwenye imani zenu za dini na kuanza kutengeneza posts za matusi na video zisizo na stahaa mkiamini kuwa maradhi na kifo vinaletwa na Binadamu. Kumbukeni na kaeni mkijua siku zote mtu apatwapo na matatizo au mpendwa wako anapopakaziwa kuwa na matatizo ukabaini huu buheri wa afya ni dhambi kuwashambulia wanaopakaza, yakupasa kumtukuza Mungu.

TBC, ninyi Ni chombo Cha Taifa na kinapaswa kusimama Kama chombo Cha Taifa achaneni na siasa na kujiendesha kishabiki...nyimbo ya Gozbeth haikupaswa kupigwa kwa wakati mliopiga...vipindi vyenu kwa siku tatu havikupaswa kupangiliwa mlivyovipangilia....tambueni wajibu wenu.

Kwa watawala, napenda kuwaomba mjifunze kitu kwenye tukio hili. HAKI IMEONDOKA, UHURU UMEONDOKA,USAWA UMEONDOKA, UBINAFSI UMETAWALA, CHUKI IMETAWALA. TAIFA LETU HALIPASWI KUSHANGILIA MABAYA YAWAPATAYO KIONGOZI WAO, TUJITAFAKARI MAANA IPO SIKU TUTASAIDIANA KWENYE SHIDA KUTOKANA NA VYAMA VYETU.

ADUI WA TANZANIA APASWI KUWA WATANZANIA BALI WATANZANIA WANAPASWA KUWA WALINZI WA TANZANIA.
Tena wewe ndio.mnafiki mkubwa, huyo aliyezomewa, kuchekwa na kidhihakiwa akiwa anaumwa ndio chanzo na injinia wa maovu yote haya Bado anayo fursa ya kubadilika hivi Viongozi wa afrika lazima.watawale kwa mkono wa chuma?? Kwanino hawajifunzi mambo mema kwa viongozi wengine waliofnikiwa kama Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Italia, Na kwingineko??

Ukweli ni kuwa Watanzania tulivumilia sana tukadharauliwa sana sasa hapo tulipofika haturudi nyuma. Ni kazi sana. Watanzania hatuna bunduki wala Bomu lakini Macho, masikio, midomo na vifaa vya kuposti tunavyo.

Kifupi tu awe alikuwa anaumwa au la hii kwake ni Adhabu kubwa.
 
Kauli zile za kumuombea mabaya Rais hazikuwa nzuri kabisa. Lakini twende mbele na kurudi nyuma, huyu bwana ameleta maumivu makubwa kwa watu wengi sana kuliko wenzake wote waliokaa miaka kumi kumi na hata yule wa miaka ishirini na NNE.
Sasa mlitegemea kwenye kundi la wenye maumivu makubwa mioyoni ukileta uvumi watu wata kaa chini na kuangua kilio? Hapana, watazungusha round ya kinywaji huku wakijipongeza kimya kimya.
Ila la ajabu ni kuwa kuna kundi la wasaidizi wake walikuwa wanatumiana SMS ambazo kuwezi kuamini zimeandikwa na wao! Kwa nini hata hao?
 
Tarehe 19 na tarehe 20 October 2019 ni siku ambazo wengi wa watanzania hatutakaa tukazisahau maishani mwao.

Tulivunjwa miyoyo,tulikosa matumaini na wengine walitamani kuikimbia nchi aidha kwa kukosa matumaini au kwa kuhofia usalama wao.

Rais anapokuwa amekufa mazingira ya kutatanisha hali hiyo huleta vita ndani ya nchi.Mambo haya yalitokea nchini Rwanda na Burundi ,na nchi nyengine.

Watanzania wengi walikua wanafuatilia ziara ya Rais. Walikuwa wakifurahia sana gafla wanaambiwa na wapinzani eti amekufa tena wapinzani hao wanafurahia kifo hicho.kwa maana nyengine walikuwa wamepanga kifo chicho.

Niseme kuwa Mungu amewatuliza watazania vinginevo yaliyotokea Burundi na Rwanda yangeweza kutokea baada ya kuona watu wanashangilia mabaya juu ya rais.

Wako watu walianzisha au kushangilia mabaya hayo.wanajukikana na wengine wametajwa Leo na Musiba.yako madhara makubwa wamesababisha kutoka na uzushi huo.

Vyombo vya Dora viwasake kote waliko wawekwe ndani mpaka rais atakapotoka madarakani.Hii itakuwa afya kwa taifa letu la Leo na la kesho kwa sababu watu hawa wanavuruga nchi.

Najua wakikamatwa mataifa ya nje yatapiga makelele kama kawaida yao.lakini potelea mbali.kwanza in usalama kwao.

Waziri mwenye dhamana chukua hatua LA sivyo watanzania wengi watawaza mengi juu yako!!
Mkuu, ebu fanya kuscreenshot popote na yeyote alie andika neno KIFO CHA RAIS
 
Jana alikuwa mpole, mnyenyekevu, asiye na mambo mengi, mwenye hekima na busara tele; Ametoa maagizo kwa msisitizo na bila vile vitisho vyake tulivyo vizoea, nk.

Akiendelea na aina ile ya kutoa hotuba, huku akiguswa na kuonesha kuyajali makundi yote kwenye jamii likiwemo kundi lililotengwa la watumishi wa umma; huenda mbele ya safari akarudisha imani kwa hayo makundi yote muhimu kwenye jamii.
Kweli hili la watumishi wa umma inabidi alipe uzito unaostahili. Wanalalamika kutopanda madaraka ya kiutumishi, kutopata increments zitokanazo na OPRAS, kutopewa posho za uhamisho hasa kwa waalimu. Na kubwa kuliko yote kukaripiwa na wanasiasa wakiwa kazini.
 
Yani uvunjike moyo kwa mtu asiyekupa chakula!!!?what the hell!?

Kwani hatakufa huyo mtu wenu?

Acha fikra finyu.The niga is not a God,he is going to die one day,any day.

Acheni kumpa u-Mungu.
 
Mpaka sasa hivi hakuna taarifa rasmi iliyotolewa na serikali kuhusu afya ya JPM kuwa alikuwa anaumwa! Huu uvumi uliletwa na kigogo2014 na kusambaa kwenye mitandao ya kijamii. Rais wetu ni mzima wa Afya na tunamuomba Mungu aendelelee kumlinda.
Kweli hakuna taarifa rasmi lakini kuna kizazi cha mawaziri ambao hufanya kazi kupitia Twitter kama HKigwangalla, HBashe, UMwalimu wametnibitisha kupitia akaunti zao kuwa JPM alikuwa anaumwa ila sasa amepona. Wanasema Chuma kimerudi!!
 
Tarehe 19 na tarehe 20 October 2019 ni siku ambazo wengi wa watanzania hatutakaa tukazisahau maishani mwao.

Tulivunjwa miyoyo,tulikosa matumaini na wengine walitamani kuikimbia nchi aidha kwa kukosa matumaini au kwa kuhofia usalama wao.

Rais anapokuwa amekufa mazingira ya kutatanisha hali hiyo huleta vita ndani ya nchi.Mambo haya yalitokea nchini Rwanda na Burundi ,na nchi nyengine.

Watanzania wengi walikua wanafuatilia ziara ya Rais. Walikuwa wakifurahia sana gafla wanaambiwa na wapinzani eti amekufa tena wapinzani hao wanafurahia kifo hicho.kwa maana nyengine walikuwa wamepanga kifo chicho.

Niseme kuwa Mungu amewatuliza watazania vinginevo yaliyotokea Burundi na Rwanda yangeweza kutokea baada ya kuona watu wanashangilia mabaya juu ya rais.

Wako watu walianzisha au kushangilia mabaya hayo.wanajukikana na wengine wametajwa Leo na Musiba.yako madhara makubwa wamesababisha kutoka na uzushi huo.

Vyombo vya Dora viwasake kote waliko wawekwe ndani mpaka rais atakapotoka madarakani.Hii itakuwa afya kwa taifa letu la Leo na la kesho kwa sababu watu hawa wanavuruga nchi.

Najua wakikamatwa mataifa ya nje yatapiga makelele kama kawaida yao.lakini potelea mbali.kwanza in usalama kwao.

Waziri mwenye dhamana chukua hatua LA sivyo watanzania wengi watawaza mengi juu yako!!
Mkuu tumia akili kidogo ulizo nazo . hata huko CCM kuna watu hawamkubali huyo rais ushaidi upo. Si unakumbuka zile clips hapa juzi kati ?
 
Nchi imejaa usiri. Ikulu haijatangaza rais anaumwa. Unataka mawaziri wa tweet pole watumbuliwe?

Ikulu inaficha rais anaumwa halafu unataka mawaziri wa tweet pole?

Hiyo nchi iliyojaa chuki anayeiongoza ni nani? Unamsikiliza kauli zake?

Sitetei kauli za kuombea mtu kifo. Si za kistaarabu na hazina maadili.

Lakini, kiongozi mkuu wa nchi anaonesha mfano gani kwa nchi? Anajenga Umoja wa Taifa au anaubomoa kwa kauli zake
He Who Digieth tha Pit shali fall in it himself
 
Ufupi wa akili yako ni pale unapofikiri kila anaye muombea mabaya Rais Maghufuli ni mpinzani na siyo CCM . hebu nikuulize swali , zile clips zilizo wahusisha makambas , kinana , nape nk hao nao ni chadema ? Tumieni kidogo basi hizo akili zenu . anaweza hata akawa ni m CCM mwenzenu alozusha huo uzushi
Niliposema wapinzani sikumaanisha CHADEMA, ACT WAZALENDO, TLP nk. Nilimaanisha watu wenye mtizamo tofauti na anachokisimamia Mh. Rais.

Martin Luther King na Yohane Kalvini, waliasisi uprotestant kutokana na tapo toka Roman katoliki ijapokua wote wanatumia Bibilia na wote wakimuamini Yesu kuwa BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YAO.

Yawezekana una degree(s) lakini ikawa ya medicine, engeneering, geology nk, hivyo ufahamu wako katika lugha ya kiswahili ukawa finyu na hii haitamaanisha kwamba wewe si msomi au huna akili.
 
Kauli zile za kumuombea mabaya Rais hazikuwa nzuri kabisa. Lakini twende mbele na kurudi nyuma, huyu bwana ameleta maumivu makubwa kwa watu wengi sana kuliko wenzake wote waliokaa miaka kumi kumi na hata yule wa miaka ishirini na NNE.
Sasa mlitegemea kwenye kundi la wenye maumivu makubwa mioyoni ukileta uvumi watu wata kaa chini na kuangua kilio? Hapana, watazungusha round ya kinywaji huku wakijipongeza kimya kimya.
Ila la ajabu ni kuwa kuna kundi la wasaidizi wake walikuwa wanatumiana SMS ambazo kuwezi kuamini zimeandikwa na wao! Kwa nini hata hao?
uko sahihi sana Mr mkongwe we nimzoefu kweli.

jamaa ameumiza wengi na ashukuru kwamba hakufa, yaani hata wale tulikaa kimya tisubiri kwanza akidanja tufanye sherehe kabisa.
 
Back
Top Bottom